Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unaelewa “Maana”?

Unaelewa “Maana”?

“Ndipo akafungua akili zao ili kuifahamu [ao kuielewa] maana ya Maandiko.”LU. 24:45.

1, 2. Kwenye siku ya kufufuliwa kwake, namna gani Yesu alitia moyo wanafunzi wake?

NI SIKU ya kufufuliwa kwa Yesu. Wanafunzi wake wawili wanasafiri kuenda katika kijiji kimoja kwenye kilometre 11 hivi kutoka Yerusalemu. Hawakujua kwamba Yesu alikuwa amefufuliwa; kwa hiyo, walikuwa wenye kuhuzunika sana kwa sababu ya mambo yenye ilitoka tu kufanyika. Mara moja, Yesu akawatokea na akaanza kutembea pamoja nao na kuwatia moyo. Namna gani aliwatia moyo? ‘Akaanzia Musa na Manabii wote, akawafasiria mambo yanayomuhusu yeye mwenyewe katika Maandiko yote.’ (Lu. 24:13-15, 27) Kisha tu kufanya hivyo, mioyo yao ilianza kuwaka kwa sababu ‘aliwafungulia’ Maandiko ao aliyafasiria waziwazi.—Lu. 24:32.

2 Mangaribi hiyohiyo, wanafunzi hao wawili walirudia Yerusalemu. Wakati walikuta mitume, walianza kuwaelezea mambo yenye walikuwa wamejionea. Wakati walikuwa wanaeleza, Yesu akawatokea wote. Hata hivyo, mitume wake waliogopa sana. Wakakuwa na mashaka katika mioyo yao. Namna gani Yesu aliwatia moyo? Biblia inasema hivi: “Akafungua akili zao ili kuifahamu [ao kuielewa] maana ya Maandiko.”—Lu. 24:45.

3. Tunaweza kukutana na magumu gani, na ni nini inaweza kutusaidia tukuwe na maoni mazuri juu ya kazi yetu ya kuhubiri?

3 Kama wanafunzi hao wa Yesu, sisi pia tunaweza kuhuzunika wakati fulani.  Pengine tunafanya mengi katika kazi ya Bwana, lakini tunavunjika moyo kwa sababu hatuone matokeo. (1 Kor. 15:58) Ao inawezekana kwamba wale wenye tunajifunza nao Biblia hawafanye kabisa maendeleo. Wengine kati yao wanaweza hata kukataa kumutumikia Yehova. Tunaweza kufanya nini ili tukuwe na maoni mazuri juu ya kazi yetu ya kuhubiri? Jambo moja lenye linaweza kutusaidia ni kuelewa maana ya mifano yenye Yesu alitumia ambayo inapatikana katika Maandiko Matakatifu. Tuchunguze sasa mifano tatu kati ya hiyo na tuone mambo yenye mifano hiyo inaweza kutufundisha.

MUFANO WA MUPANDAJI MWENYE KULALA USINGIZI

4. Mufano wa Yesu wa mupandaji mwenye kulala usingizi unamaanisha nini?

4 Soma Marko 4:26-29. Mufano wa Yesu wa mupandaji mwenye kulala usingizi unamaanisha nini? Mwanaume mwenye kuzungumuziwa katika mufano huo anafananisha kila muhubiri wa Ufalme. Mbegu inafananisha ujumbe wa Ufalme wenye tunahubiria watu wenye mioyo mizuri. Kwa kawaida, mupandaji ‘analala usingizi usiku na anaamuka muchana.’ Kipindi cha kukomaa kinachukua muda fulani, ni kusema, kuanzia wakati wa kupanda mupaka wakati wa kuvuna. Katika kipindi hicho mbegu ‘inaota na kukomaa na kuwa ndefu.’ Mbegu inaota na kukomaa ‘yenyewe’ hatua kwa hatua. Vilevile, kukomaa kwa njia ya kiroho kunafanyika hatua kwa hatua. Wakati mutu anafanya maendeleo mupaka anachochewa kumutumikia Mungu, anazaa matunda, ni kusema, anajitoa kwa Yehova katika sala na anabatizwa.

5. Sababu gani Yesu alitumia mufano wa mupandaji mwenye kulala usingizi?

5 Sababu gani Yesu alitumia mufano huo? Alipenda kutusaidia tuelewe kwamba ni Yehova ndiye anafanya kweli ikomae katika mioyo ya watu wenye “mwelekeo unaofaa.” (Mdo. 13:48; 1 Kor. 3:7) Tunapanda mbegu na kuimwangia maji, lakini hatuna mamlaka ya kufanya mbegu hiyo ikomae. Hatuwezi kuikaza ao kuifanya ikomae mbio sana. Kama mwanaume mwenye kuzungumuziwa katika mufano huo, hatujue namna mbegu inaota na kukomaa. Mara nyingi inakomaa bila sisi kujionea, wakati tunaendelea na maisha yetu ya kila siku. Lakini kisha muda fulani, mbegu ya Ufalme inaweza kuzaa matunda. Kisha, mwanafunzi mupya anajiunga na sisi katika kazi ya mavuno, na tunafaidika na musaada wake.—Yoh. 4:36-38.

6. Tunapaswa kutambua nini kuhusiana na maendeleo ya kiroho ya mwanafunzi wa Biblia?

6 Mufano huo unaweza kutufundisha nini? Kwanza, tunapaswa kutambua kwamba hatuwezi kumulazimisha mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. Unyenyekevu utatusaidia tusitafute kumukaza mwanafunzi wa Biblia abatizwe. Tunajikaza kumusaidia mwanafunzi, lakini tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kukubali kwamba ni yeye mwenyewe ndiye anapaswa kuamua kujitoa kwa Yehova katika sala. Mutu anapaswa kuchochewa na upendo wakati anaamua kujitoa kwa Mungu katika sala, na anafanya hivyo kwa kujipendea. Ni jambo hilo tu ndilo Yehova anakubali.—Zab. 51:12; 54:6; 110:3.

7, 8. (a) Tunajifunza tena nini katika mufano wa Yesu wa mupandaji mwenye kulala usingizi? Toa mufano. (b) Mufano huo unatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

7 Pili, mambo yenye tunajifunza katika mufano huo yatatusaidia tusivunjike moyo ikiwa mwanzoni hatupate matokeo katika kazi yetu ya kuhubiri. Ni lazima tuonyeshe uvumilivu. (Yak. 5:7, 8) Ikiwa sisi tulifanya yetu yote ili kusaidia mwanafunzi, lakini hafanye maendeleo, tujue kwamba hilo halimaanishe kwamba sisi hatujue kufundisha. Yehova anafanya mbegu ya kweli izae matunda katika moyo munyenyekevu wenye utakuwa tayari kufanya mabadiliko. (Mt. 13:23) Kwa hiyo hatupaswe kusema  kwamba kazi yetu ya kuhubiri ni ya muzuri ao hapana kwa sababu tu ya matokeo. Yehova haone kwamba tumeshindwa kwa sababu wale wenye tunajifunza nao wamekataa kufanya maendeleo. Lakini, anaona bidii yetu kuwa ya lazima sana iwe tunapata matokeo mazuri ao hapana.—Soma Luka 10:17-20; 1 Wakorintho 3:8.

8 Tatu, mara nyingi hatutambue mabadiliko yenye kufanyika katika moyo wa mutu. Kwa mufano, mwanaume mumoja na bibi yake walikuja kumuona misionere mumoja mwenye alikuwa anajifunza nao na kumwambia kama wanapenda kuwa wahubiri wasiobatizwa. Misionere huyo aliwakumbusha kwamba ikiwa wanataka kuwa wahubiri, walipaswa kuacha kuvuta tumbako. Lakini alishangaa sana wakati mwanaume huyo na bibi yake walimuambia kwamba waliacha kuvuta tumbako kumepita miezi mingi. Sababu gani waliacha? Walitambua kwamba, ikiwa wangeendelea kuvuta, Yehova angewaona na kwamba anachukia unafiki. Mioyo yao iliwachochea kuchagua kati ya kuvuta mbele ya misionere huyo ao kuachana kabisa na tumbako. Upendo wao kwa Yehova uliwasaidia wachukue uamuzi muzuri. Walifanya maendeleo ya kiroho, hata kama misionere huyo hakuwa anaona mabadiliko yenye ilikuwa inafanyika katika mioyo yao.

MUFANO WA WAVU

9. Mufano wa wavu unamaanisha nini?

9 Soma Mathayo 13:47-50. Mufano wa Yesu wa wavu unamaanisha nini? Yesu alifananisha kazi ya kuhubiria watu wote ujumbe wa Ufalme na kazi ya kushusha wavu mukubwa katika bahari. Kama vile wavu unachukua “samaki [wengi] wa kila aina,” kazi yetu ya kuhubiri inaleta mamilioni ya watu wa kila namna. (Isa. 60:5) Hesabu ya watu wenye wanakuja kwenye mikusanyiko na kwenye Ukumbusho kila mwaka inaonyesha jambo hilo. Wamoja kati ya samaki hao wa mufano ni “wazuri” na wanakusanywa katika kutaniko la Kikristo. Lakini wengine ni “wasiofaa;” si wote wenye wanakusanywa ndio wanakubaliwa na Yehova.

Kisha kusoma andiko la Mathayo 13:47-50 . . .

10. Sababu gani Yesu alitumia mufano wa wavu?

10 Sababu gani Yesu alitumia mufano huo? Kazi ya kutenganisha samaki haifananishe hukumu ya mwisho yenye itafanyika wakati wa ziki kubwa. Lakini inafananisha mambo yenye inafanyika katika siku za mwisho za ulimwengu huu. Yesu alionyesha kwamba si wote ambao wanavutiwa na kweli ndio wanaamua kumutumikia Yehova. Wengi wamekuja kwenye mikutano yetu. Wengine wamekubali tujifunze nao Biblia lakini hawako tayari kutoa ahadi ya kumutumikia Yehova. (1 Fal. 18:21) Lakini wengine hawakuje tena kwenye mikutano yetu. Vijana fulani walizaliwa katika familia za Kikristo lakini hawakukomalisha upendo wao kwa Yehova. Iwe mambo yako namna gani, Yesu alikazia kwamba kila mutu anapaswa kuchukua uamuzi wake mwenyewe. Yehova anaona wale wenye wanachukua uamuzi wa kumutumikia kuwa “vitu vyenye kutamanika vya mataifa yote.”—Hag. 2:7.

. . . fikiria maana yake leo

11, 12. (a) Namna gani tunaweza kufaidika na mufano wa wavu? (b) Mufano huo unatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

11 Namna gani tunaweza kufaidika na mufano wa Yesu wa wavu? Kuelewa mufano huo kunatusaidia tusivunjike moyo sana ikiwa mwanafunzi wa Biblia ao mutoto wetu anakataa kumutumikia Yehova. Jambo hilo linaweza kutokea hata kama tulifanya yetu yote ili kumusaidia. Kukubali kujifunza Biblia ao kuzaliwa katika familia ya Kikristo hakumaanishe kwamba mutu atakubali mara moja kufanya urafiki pamoja na Yehova. Wale wote wenye wanakataa  utawala wa Yehova, mwishowe hawatakubaliwa kubaki katikati ya watu wa Mungu.

Watu fulani wenye kuvutiwa na kweli watachagua kumutumikia Yehova(Ona fungu la 9 mupaka 12)

12 Tunaweza kusema kwamba wale wenye wameacha kweli hawataruhusiwa tena kurudia katika kutaniko? Ao ikiwa mutu fulani anakosa kujitoa kwa Yehova, hilo linamaanisha kwamba ataendelea kuonwa kuwa ‘asiyefaa’? Hapana. Watu kama hao wangali na nafasi ya kuamua kumutumikia Yehova mbele ziki kubwa ianze. Ni kama vile Yehova anawaambia hivi: ‘Murudi kwangu, nami nitarudi kwenu.’ (Mal. 3:7) Mufano mwengine wenye Yesu alitoa wa mwana mupotevu unakazia jambo hilo.—Soma Luka 15:11-32.

MUFANO WA MWANA MUPOTEVU

13. Mufano wa mwana mupotevu unamaanisha nini?

13 Mufano wa Yesu wa mwana mupotevu unamaanisha nini? Baba mwenye huruma katika mufano huo anafananisha Yehova, Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo. Mutoto mwenye anaomba sehemu yake ya mali na kisha anaitumia ovyovyo anafananisha wale wenye wameacha kutaniko. Watu hao wanakuwa kama wamesafiri mupaka ‘inchi ya mbali,’ ni kusema, ulimwengu wa Shetani ambao umetengwa na Yehova. (Efe. 4:18; Kol. 1:21) Wamoja kati yao wanarudiwa na akili na wanajikaza sana ili kurudi katika tengenezo la Yehova. Baba yetu mwenye kusamehe amekaribisha kwa uchangamufu watu hao wanyenyekevu ambao wametubu.—Isa. 44:22; 1 Pet. 2:25.

14. Sababu gani Yesu alitumia mufano wa mwana mupotevu?

14 Sababu gani Yesu alitumia mufano huo? Yesu alitumia mufano huo wenye kuvutia ili kuonyesha kwamba Yehova anapenda wale wenye wameacha kutaniko warudi Kwake. Baba mwenye kuzungumuziwa katika mufano huo aliendelea kutumaini kwamba mutoto wake atarudi. Wakati aliona mutoto wake anakuja, baba huyo alikimbia mbio ili kumukaribisha, hata kama ‘alikuwa angali mbali.’ Mufano huo unatia kabisa moyo wale wenye wameacha kweli wamurudilie Yehova bila kukawia. Wanaweza kuwa wamechoka sana kiroho; kwa hiyo, wanaweza kuwa na haya na kuona kuwa ni vigumu kurudia katika kutaniko. Lakini bidii yao haiko ya bure; hata mbinguni kutakuwa furaha kubwa wakati watarudi.—Lu. 15:7.

15, 16. (a) Mufano wa Yesu wa mwana mupotevu unatufundisha nini? Toa mifano fulani. (b) Mufano huo unatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu?

15 Namna gani tunaweza kufaidika na mufano wa mwana mupotevu?  Tunapaswa kumuiga Yehova. Hatupaswe hata kidogo kuwa ‘waadilifu kupita kiasi’ kwa kukataa kukaribisha watenda-zambi wenye wametubu. Kukataa kuwakaribisha kunaweza kutuingiza katika hatari ya kiroho. (Mhu. 7:16) Kuna jambo lingine lenye tunaweza kujifunza katika mufano huo. Tunapaswa kuona mutu mwenye ameacha kutaniko kama “kondoo aliyepotea,” wala si kama kondoo mwenye hawezi kurudia. (Zab. 119:176) Ikiwa tunakutana na mutu mwenye ameacha kutaniko, tutakuwa tayari kumusaidia arudie? Tutakuwa tayari kujulisha wazee ili wamupatie musaada unaofaa? Tukifanya hivyo, tutaonyesha kwamba tunatumia vizuri mambo yenye tumejifunza katika mufano wa Yesu wa mwana mupotevu.

16 Ona namna watu fulani wenye walikuwa wameacha tengenezo wanaeleza namna wamefaidika na rehema ya Yehova, na namna ndugu na dada katika kutaniko waliwasaidia na kuwaonyesha upendo. Ndugu mumoja mwenye alikuwa ametengwa na kutaniko kwa muda wa miaka 25 anasema hivi: “Furaha yenye nilipata kisha kurudishwa iliendelea kuongezeka kwa sababu Yehova alinitolea ‘majira ya kuburudisha.’ (Mdo. 3:19) Kila mutu katika kutaniko ananisaidia na kunionyesha upendo! Sasa niko na familia nzuri ya kiroho.” Dada mumoja kijana mwenye aliacha tengenezo kwa muda wa miaka 5 anasema hivi: “Ninashindwa kueleza namna nilijisikia wakati niliona ndugu na dada wananionyesha waziwazi upendo wenye Yesu alifundisha. Ni pendeleo kubwa sana kuwa katika tengenezo la Yehova!”

17, 18. (a) Mifano tatu yenye tumechunguza imetufundisha mambo gani ya lazima? (b) Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

17 Mifano tatu yenye tumechunguza inatufundisha mambo gani ya lazima? Kwanza, tunapaswa kutambua kwamba hatuna uwezo wa kufanya mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. Ni Yehova ndiye ana uwezo huo. Pili, hatuwezi kutazamia kwamba watu wote wenye kukusanyika na sisi ao wenye tunajifunza nao Biblia watakubali kumutumikia Yehova. Tatu, hata kama ndugu na dada fulani wanaweza kukataa kweli na wanamuacha Yehova, hatupaswe kuvunjika moyo na kufikiri kwamba hawawezi tena kurudia. Na ikiwa wanarudia, tunapaswa kumuiga Yehova kwa kuwakaribisha kwa uchangamufu.

18 Kila mumoja wetu anatiwa moyo kuendelea kutafuta ujuzi, uelewaji, na hekima. Wakati tunasoma mifano yenye Yesu alitumia, tutafute kuelewa maana ya mifano hiyo, sababu gani iliandikwa katika Biblia, namna gani tunaweza kutumikisha mambo yenye tumejifunza, na mifano hiyo inatufundisha nini juu ya Yehova na juu ya Yesu. Tukifanya hivyo tutaonyesha kwamba tunaelewa maana ya maneno ya Yesu.