Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Japani Inapewa Zawadi Nzuri Sana

Japani Inapewa Zawadi Nzuri Sana

KWENYE mukutano mumoja wa pekee wenye ulifanyika katika muji wa Nagoya, Japani, tarehe 28 Mwezi wa 4, 2013, ndugu Anthony Morris wa Baraza Linaloongoza alitoa tangazo moja lenye wahuzuriaji hawakutazamia. Aliwatangazia kutolewa kwa kitabu kipya chenye kichwa Biblia—Injili Kulingana na Mathayo, katika luga ya Kijapani. Watu zaidi ya 210 000 wenye walikuwa mahali hapo na wenye walifuata mukutano huo kupitia Internete, walipiga mikono kwa muda murefu.

Kitabu hicho cha pekee sana chenye kurasa 128, kilichukuliwa katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya luga ya Kijapani. Ndugu Morris alisema kwamba kusudi la kitabu hicho ni “kutimiza mahitaji ya mahubiri katika Japani.” Kitabu hicho kimeandikwa namna gani? Sababu gani kimechapishwa? Watu walikipokea namna gani?

NAMNA KIMEANDIKWA

Namna kitabu hicho cha Mathayo kimeandikwa ilishangaza sana watu wenye walihuzuria mukutano huo wa pekee. Luga ya Kijapani inaweza kuandikwa kutoka juu kuenda chini, ao kutoka kushoto kuenda kuume; vichapo vingi vya Kijapani vimeandikwa kutoka kushoto kuenda kuume. Hata vichapo vyetu vya hivi karibuni vimeandikwa kwa namna hiyo. Lakini maandishi yenye kuwa katika kitabu hicho kipya imeandikwa kutoka juu kuenda chini. Hiyo ni namna ya kuandika yenye inatumiwa sana katika Magazeti na vitabu vingi vya Kijapani. Watu wengi wenye wanasoma Kijapani wanaona kwamba ni mwepesi zaidi kusoma maandishi yenye kuandikwa kwa namna hiyo. Tena katika kitabu hicho, vichwa vidogo-vidogo vimeandikwa mahali mbalimbali katikati ya kurasa, na hilo linasaidia musomaji aone mara moja mambo makubwa.

Namna kitabu cha Mathayo kimeandikwa imesaidia sana ndugu na dada wa Japani. Dada mumoja mwenye kuwa na miaka zaidi ya 80 alisema hivi: “Nilikuwa nimesoma kitabu cha Mathayo mara nyingi, lakini sasa maandishi ya kutoka juu kuenda chini, na vichwa vidogo-vidogo vyenye kuwa katikati ya kurasa vimenisaidia kuelewa vizuri Mahubiri ya Yesu ya Mulimani.” Dada mwengine mwenye kuwa na miaka 30 aliandika hivi: “Nilisoma kitabu cha Mathayo tangu mwanzo mupaka mwisho bila kupumuzika. Ninazoea kusoma maandishi ya kutoka kushoto kuenda kuume, lakini Wajapani wengi wanapenda kusoma maandishi ya kutoka juu kuenda chini.”

KIMECHAPISHWA KWA AJILI YA MAHUBIRI KATIKA JAPANI

Namna gani kitabu hicho kimoja tu cha Biblia kitatimiza mahitaji ya mahubiri katika Japani? Wajapani wengi hawajue mambo mengi juu ya Biblia, lakini wanapenda kuisoma. Wale wenye hawajaona Biblia hata siku moja, watapata nafasi ya kusoma kitabu cha Mathayo, ambacho ni sehemu ya Biblia.

Sababu gani ni kitabu cha Mathayo ndicho kilichaguliwa? Wakati Wajapani wengi wanasikia neno “Biblia,” mara moja wanamukumbuka Yesu Kristo. Kwa hiyo, kitabu cha Mathayo kilichaguliwa kwa sababu kinatoa maelezo juu ya kizazi cha Yesu na kuzaliwa kwake, Mahubiri yake ya Mulimani yenye kujulikana sana, na juu ya unabii wake wa maana sana juu ya siku za mwisho. Wajapani wengi watafurahia sana habari hizo.

Wahubiri wa Ufalme katika Japani wameanza kutolea watu kitabu hicho kwa bidii katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, na wakati wanarudilia watu wenye kupendezwa. Dada mumoja aliandika hivi: “Sasa ninapata nafasi nyingi za kutolea watu Neno la Mungu katika eneo letu. Kwa mufano, niliweza kutolea mutu kitabu cha Mathayo mangaribi ileile kisha tu mukutano wa pekee!”

WATU WALIKIPOKEA NAMNA GANI?

Wahubiri wanafanya nini ili kutolea watu kitabu cha Mathayo? Watu wengi katika Japani wanazoea kutumia maneno kama vile “lango jembamba,” ‘kutupa lulu mbele ya nguruwe,’ na ‘musihangaike kamwe juu ya kesho.’ (Mt. 6:34; 7:6, 13) Wanashangaa sana wakati wanajua kwamba ni Yesu Kristo ndiye alisema maneno hayo. Wakati wanaona maneno hayo katika Injili ya Mathayo, wengi wanasema hivi: “Nilikuwa na hamu kabisa ya kusoma Biblia, hata mara moja tu.”

Wakati wahubiri wanarudilia wale wenye walikubali kitabu cha Mathayo, mara nyingi wanawaambia kwamba walikisoma chote bila kukawia, ao kwamba walisoma sehemu fulani. Mwanaume fulani mwenye kuwa na miaka zaidi ya 60 alimuambia muhubiri mumoja hivi: “Nilisoma kitabu hicho mara nyingi na nilifarijika. Tafazali, unifundishe mengi zaidi juu ya Biblia.”

Wahubiri wako wanatolea watu kitabu cha Mathayo wakati wanahubiri mahali pa watu wengi. Dada mumoja alikuwa anahubiri mahali pa watu wengi. Wakati huo, alitolea mwanamuke fulani kitabu cha Mathayo na akamupatia adresi yake ya Internete. Kisha saa moja, mwanamuke huyo alimuandikia kupitia Internete ili kumuambia kwamba amesoma sehemu fulani ya kitabu hicho na kwamba anapenda kujua mengi zaidi. Kisha juma moja, mwanamuke huyo alianza kujifunza Biblia, na bila kukawia, akaanza kuhuzuria mikutano.

Vitabu Biblia—Injili Kulingana na Mathayo zaidi ya 1 600 000 vimetumwa katika makutaniko mbalimbali ya Japani, na kila mwezi wahubiri wanatolea watu maelfu ya kitabu hicho. Maneno ya utangulizi ya kitabu hicho inaonyesha tamaa ya wachapishaji wake. Inasema hivi: “Tunatumaini kwa moyo wote kwamba, kusoma kitabu hiki kutakufanya upendezwe zaidi na Biblia.”