Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anaongoza Kazi Yetu ya Kufundisha Katika Dunia Yote

Yehova Anaongoza Kazi Yetu ya Kufundisha Katika Dunia Yote

“Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.”​—ISA. 48:17.

1. Wakristo wa wakati wetu wamepambana na magumu gani katika kazi ya kuhubiri?

WANAFUNZI wa Biblia * walianza kuhubiri habari njema kumepita sasa miaka zaidi ya 130; wakati huo walipata magumu mengi. Kama vile tu Wakristo wa kwanza-kwanza, Wanafunzi hao wa Biblia walikuwa wanahubiri ujumbe wenye watu wengi hawakufurahia. Walikuwa wachache, na watu wengi katika ulimwengu waliwaona kuwa watu wasio na elimu ya kutosha. Kisha muda fulani walipaswa kupambana na “hasira kali” ya Shetani Ibilisi. (Ufu. 12:12) Pia, kazi yao ya kuhubiri ilipaswa kufanyika katika “siku za mwisho,” ambazo ni “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.”​—2 Tim. 3:1.

2. Yehova amefanya nini ili kutusaidia tuweze kuhubiri?

2 Hata hivyo, Yehova alikusudia kwamba watumishi wake watangaze habari njema katika dunia yote, na hakuna kitu kinaweza kumuzuia atimize kusudi lake. Kama vile aliokoa Waisraeli wa zamani kutoka Babiloni, Yehova ameokoa watumishi wake wa wakati wetu kutoka katika ‘Babiloni Mukubwa,’ ni kusema, dini zote za uongo. (Ufu. 18:1-4) Ametufundisha kwa faida yetu wenyewe; ametubariki kwa kutusaidia tuishi kwa amani, na ametusaidia ili tuweze kufundisha wengine. (Soma Isaya 48:16-18.) Hilo halimaanishe kwamba Yehova anatumia uwezo wake wa kujua wakati unaokuja ili ajue na kuongoza mambo ya hapa duniani kusudi tu kazi ya kuhubiri habari njema isonge mbele. Hali fulani katika ulimwengu zimetusaidia ili tuweze kufanya kazi ya kutoa ushahidi. Hata hivyo, ni Yehova tu ndiye ametusaidia ili tuweze kuvumilia mateso, na matatizo mengine yenye inafanya ikuwe vigumu kufanya kazi yetu ya kuhubiri katika ulimwengu huu wenye kutawaliwa na Shetani.​—Isa. 41:13; 1 Yoh. 5:19.

3. Namna gani “ujuzi wa kweli” umekuwa mwingi?

3 Nabii Danieli aliongozwa na roho takatifu ya Yehova ili aandike kwamba katika siku za mwisho “ujuzi wa kweli” utakuwa mwingi. (Soma Danieli 12:4.) Yehova alisaidia Wanafunzi wa Biblia waelewe kweli za musingi za Biblia, hata kama kwa muda murefu, mafundisho ya dini za uongo ilikuwa imezuia watu kujua kweli hizo. Yehova anatumia sasa watumishi wake ili kujulisha watu wengine kweli hizo katika dunia yote. Leo, tunajionea namna unabii wa Danieli unatimia. Watu karibu milioni 8 wamekubali kweli ya Biblia, na wanatangaza kweli hiyo katika dunia yote. Ni mambo gani imetusaidia ili tuweze kufanya kazi hiyo katika dunia yote?

KAZI YA KUTAFSIRI BIBLIA

4. Katika miaka ya 1800, Biblia ilitafsiriwa kwa kiasi gani?

4 Leo watu wengi wanaweza kupata Biblia; na hilo ni jambo moja lenye limetusaidia ili tuweze kutangaza habari njema. Kwa miaka mingi, viongozi wa dini zenye kujiita kuwa za Kikristo, walikataza kabisa watu kusoma Biblia, na walifikia hata kuua watu fulani wenye waliitafsiri. Hata hivyo, katika miaka ya 1 800, mashirika fulani ilitafsiri na kuchapisha Biblia, yote nzima ao sehemu, katika luga 400 hivi. Kufikia mwanzo wa miaka ya 1 900, watu wengi walikuwa na Biblia, lakini hawakuwa na ujuzi wa kweli wa mafundisho ya Neno la Mungu.

5. Ni kazi gani Mashahidi wa Yehova wamefanya ili kutafsiri Biblia?

5 Wanafunzi wa Biblia walijua kwamba walipaswa kuhubiri; kwa hiyo, bila kuchoka, walijulisha watu mambo yenye Biblia inafundisha. Zaidi ya hilo, watu wa Yehova walitumia tafsiri mbalimbali za Biblia na walizigawanyia watu wengine. Kuanzia mwaka wa 1950, wamechapisha Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, yote nzima ao sehemu, katika luga zaidi ya 120. Katika mwaka wa 2013, kumetolewa chapa mupya ya Biblia hiyo katika Kiingereza. Itakuwa mwepesi zaidi kuitafsiri katika luga zingine. Biblia yenye kuwa mwepesi kusoma na mwepesi kuelewa, inatusaidia kutimiza kazi yetu ya kuhubiri.

NYAKATI ZA AMANI

6, 7. (a) Vita imeenea kwa kiasi gani katika ulimwengu? (b) Namna gani amani ya kadiri imesaidia kazi yetu ya kuhubiri katika inchi nyingi?

6 Pengine unajiuliza hivi: ‘Kumekuwa amani gani katika ulimwengu?’ Kwa mufano, katika miaka ya 1900, vita imeua mamilioni ya watu, zaidi sana wakati wa vita ya kwanza na ya pili ya ulimwengu. Lakini kwenye mukusanyiko mumoja wenye ulifanyika katika mwaka wa 1942, wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, ndugu Nathan Knorr, mwenye alikuwa anaongoza kazi ya Mashahidi wa Yehova, alitoa hotuba yenye kichwa “Amani​—Je, Inaweza Kudumu?” Katika hotuba hiyo, ndugu Nathan Knorr alizungumuzia unabii wenye kupatikana katika Ufunuo sura ya 17, ili kuonyesha kwamba, Vita ya Pili ya Ulimwengu haitaendelea mupaka Har-magedoni, lakini kwamba kisha vita hiyo kutakuwa kipindi cha amani.​—Ufu. 17:3, 11.

7 Hilo halimaanishe kwamba kisha Vita ya Pili ya Ulimwengu kulikuwa amani katika sehemu zote za dunia. Ripoti moja inasema kwamba, tangu mwaka wa 1946 mupaka 2013 kumekuwa vipindi 331 vya vita. Mamilioni ya watu wamekufa katika vita hizo. Lakini katika miaka hiyo, kumekuwa amani ya kadiri katika inchi nyingi, na Mashahidi wa Yehova wametumia hali hiyo ya amani ili kuhubiri habari njema. Wamepata matokeo gani? Katika mwaka wa 1944, hesabu ya wahubiri katika dunia yote ilikuwa chini ya 110 000. Lakini leo, kuna wahubiri milioni 8 hivi! (Soma Isaya 60:22.) Bila shaka, katika nyakati za amani, tunaweza kuhubiria watu wengi zaidi habari njema.

MAENDELEO KATIKA NAMNA YA KUSAFIRI

8, 9. Kumekuwa maendeleo gani katika namna ya kusafiri, na namna gani maendeleo hayo yametusaidia katika kazi ya kuhubiri?

8 Maendeleo yenye imefanyika katika namna ya kusafiri imetusaidia sana ili tuweze kufanya kazi ya kuhubiri. Katika mwaka wa 1900 kulikuwa kumepita miaka 21 hivi tangu gazeti Munara wa Mulinzi lilianza kuchapishwa. Wakati huo, kulikuwa motokari karibu 8 000 tu katika États-Unis, na barabara nzuri zilikuwa chache. Leo, katika dunia yote kuna motokari zaidi ya miliare moja na nusu, na kuna barabara nyingi nzuri katika maeneo mengi. Motokari na barabara nzuri vinasaidia wahubiri wengi kuhubiria watu wenye kupatikana katika maeneo ya mbali. Hata kama hatuna motokari ao barabara nzuri, na tunalazimika kutembea kwa miguu, tunafanya yote yenye tunaweza ili kufanya wanafunzi.​—Mt. 28:19, 20.

9 Kuna namna zingine za kusafiri zenye zimetusaidia sana katika kazi yetu. Tunatumia motokari za kubeba mizigo, mashua, na treni (train) ili tuweze kupeleka vichapo katika maeneo ya mbali. Waangalizi wenye kusafiri, ndugu wa Halmashauri za Tawi, wamisionere, na watumishi wengine wa Yehova wanatumia avion ili waweze kusafiri haraka wakati wanaenda kwenye mikusanyiko ao kutimiza migao mingine ya kiteokrasi. Zaidi ya hilo, ndugu wa Baraza Linaloongoza na ndugu wengine wenye wanatumika kwenye makao yetu makubwa wanatumia avion wakati wanaenda katika inchi mbalimbali ili kutia moyo na kufundisha Wakristo wenzao. Kwa njia hiyo, maendeleo katika namna ya kusafiri inasaidia watu wa Yehova wakuwe na umoja.​—Zab. 133:1-3.

NAMNA LUGA IMETUSAIDIA

10. Sababu gani tunaweza kusema kwamba Kiingereza ndio luga yenye watu wengi zaidi wanazungumuza?

10 Wakati wa mitume, watu wengi walikuwa wanazungumuza Kigiriki cha kawaida, ao Koine, katika maeneo yenye ilikuwa chini ya Utawala wa Roma. Leo pia, ni luga yenye watu wengi zaidi wanazungumuza? Watu wengi wanaweza kusema kwamba luga hiyo ni Kiingereza. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Katika dunia yote, karibu mutu mumoja kati ya watu ine, anasema ao kusikia Kiingereza.” (English as a Global Language) Kiingereza ndio luga yenye watu wengi zaidi wanajifunza katika dunia. Watu wa inchi nyingi wanatumia luga hiyo ili kuzungumuzia mambo ya biashara, politike, sayansi, ao teknolojia.

11. Namna gani luga ya Kiingereza imesaidia ili ibada safi isonge mbele?

11 Kwa sababu watu wengi katika dunia wanatumia Kiingereza, hilo limesaidia ibada safi isonge mbele. Kwa miaka mingi, gazeti Munara wa Mulinzi na vichapo vyetu vingine, vilikuwa vinachapishwa kwanza katika Kiingereza. Kwenye makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova, Kiingereza ndio luga yenye kutumiwa. Na hiyo ndio luga yenye kutumiwa ili kufundisha wanafunzi kwenye Kituo cha Mafundisho cha Mashahidi wa Yehova cha Patterson, New York, États-Unis.

12. Tumetafsiri vichapo vyetu katika luga ngapi, na namna gani maendeleo katika mambo ya ordinatere imetusaidia?

12 Tuko na pendeleo la kuhubiria watu wa mataifa yote habari njema ya Ufalme. Kwa hiyo, tumetafsiri vichapo vyetu katika luga 700 hivi. Leo kumefanyika maendeleo katika mambo ya ordinatere. Kwa mufano, programe za ordinatere, kama vile ile inayoitwa MEPS, zimetusaidia sana katika kazi ya kutafsiri. Mambo hayo imetusaidia ili tuweze kuhubiria watu wengi zaidi, na inatusaidia ili tuendelee kuwa na umoja katika dunia yote. Lakini jambo lenye linatuunganisha zaidi ni ile ‘luga safi,’ ni kusema, kweli ya Neno la Mungu, ambayo ni luga ya maana zaidi.​—Soma Sefania 3:9.

NAMNA SHERIA ZIMETUSAIDIA

13, 14. Namna gani sheria na tribinali katika inchi mbalimbali zimetusaidia?

13 Katika habari yenye ilitangulia, tuliona kwamba sheria yenye ilitumiwa katika utawala wote wa Roma ilisaidia Wakristo wa kwanza-kwanza ili waweze kuhubiri. Leo pia, sheria zinasaidia sana Wakristo wa wakati wetu. Kwa mufano, makao yetu makubwa inapatikana katika États-Unis. Sheria ya inchi hiyo inatolea watu uhuru wa kuabudu, kusema, na wa kufanya mikusanyiko. Hilo limepatia ndugu na dada wa États-Unis uhuru wa kufanya mikutano na kuzungumuzia waziwazi habari za Biblia, na kuelezea wengine mambo yenye wanajifunza. Hata hivyo, iliomba Mashahidi wa Yehova waende kwenye tribinali ili wapate uhuru wa kutumia haki zao zingine. (Flp. 1:7) Wakati tribinali fulani za États-Unis zilikataa kuwapatia haki zao, mara nyingi walienda kwenye tribinali kubwa zaidi, na tribinali hizo ziliunga mukono haki yao ya kuwa watangazaji wa Ufalme.

14 Pia katika inchi zingine tribinali mbalimbali zimeunga mukono uhuru wetu wa kuabudu na kuhubiria wengine habari njema. Katika inchi fulani, tribinali zilikataa kutupatia haki zetu, lakini tukaenda kwenye tribinali za kimataifa. Kwa mufano, katika Mwezi wa 6, 2014, tulipata ushindi katika visa 57 kwenye Tribinali ya Haki za Kibinadamu ya Ulaya, na maamuzi yenye Tribinali hiyo ilichukua kwa ajili yetu inatumika katika inchi zote zenye kufanyiza Baraza la Ulaya. Hata kama ‘tunachukiwa na mataifa yote,’ tribinali katika inchi nyingi zimeamua kwamba tuko na haki ya kufanya ibada.​—Mt. 24:9.

NAMNA MAENDELEO KATIKA TEKNOLOJIA IMETUSAIDIA

Tunatolea watu vichapo vyetu katika dunia yote

15. Kumefanyika maendeleo gani katika namna ya kuchapisha, na namna gani maendeleo hayo imetusaidia?

15 Maendeleo mengi imefanyika katika namna ya kuchapisha vichapo, na hilo limesaidia sana kazi ya kuhubiri katika dunia yote. Katika mwaka wa 1450 hivi, Johannes Gutenberg alitengeneza mashini ya kuchapisha, na watu walitumia mashini kama hiyo kwa miaka mingi. Lakini katika miaka 200 hivi yenye imepita, kumefanyika maendeleo makubwa sana katika namna ya kuchapisha. Kumekuwa sasa mashini kubwa-kubwa za kuchapisha zenye kutumika haraka sana, na tena za hali ya juu zaidi. Makaratasi na kazi ya kutengeneza vitabu haiombe tena feza nyingi kama zamani. Kumekuwa pia aina mupya za kuchapisha, na hilo limefanya kazi hiyo ikuwe haraka zaidi, na limefanya picha zikuwe zenye kuvutia zaidi. Hilo limekuwa na matokeo gani juu ya kazi yetu? Fikiria jambo hili: Gazeti la kwanza la Munara wa Mulinzi, lilitolewa katika Mwezi wa 7, 1879. Wakati huo, ni magazeti 6 000 ndio ilichapishwa. Haikuwa na picha hata moja, na ilitolewa tu katika luga ya Kiingereza. Leo kumepita sasa miaka 136. Kwa kila gazeti Munara wa Mulinzi tunachapisha magazeti zaidi ya milioni 50, na inagawanyiwa watu katika dunia yote. Gazeti hilo limekuwa na picha nzuri zenye kuwa na rangi ya kupendeza, na linapatikana katika luga zaidi ya 200.

16. Ni mambo gani imesaidia kazi yetu ya kuhubiri katika dunia yote? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

16 Fikiria vyombo fulani vyenye vimetengenezwa katika miaka 200 yenye imepita, ambavyo watu wa Mungu wametumia katika kazi ya kuhubiri habari njema. Tumekwisha kutaja treni, motokari, na avion. Lakini kumekuwa pia kinga, mashini za kuandika, mashini za kufanya maandishi ya vipofu, telegrafe, telefone, vyombo vya kupiga picha, vyombo vya kurekodi sauti na video, radio, televizyo, filme ya picha zenye kutikisika, ordinatere, na Internete. Vyombo hivyo vyote vimetusaidia katika njia nyingi ili tuweze kutimiza kazi yetu ya kufanya wanafunzi. Biblia ilitabiri kwamba watu wa Yehova ‘watanyonya maziwa ya mataifa.’ Kwa hiyo, ili tuweze kuchapisha Biblia na vichapo vingine katika luga nyingi, tunatumia kwa hekima vitu vya mataifa kama vile teknolojia ya leo.​—Soma Isaya 60:16.

17. (a) Tuko hakika juu ya jambo gani? (b) Sababu gani Yehova ametupatia pendeleo la kuwa “wafanyakazi” pamoja naye?

17 Tuko kabisa hakika kwamba Yehova anatubariki. Ni wazi kwamba Yehova hategemee musaada wetu ili aweze kutimiza kusudi lake. Lakini Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, ametupatia pendeleo la kuwa “wafanyakazi” pamoja naye, na hilo linatupatia nafasi ya kuonyesha upendo wetu kwake na kwa jirani yetu. (1 Kor. 3:9; Mk. 12:28-31) Tutumie basi kila nafasi yenye tunapata ili kuhubiri habari njema ya Ufalme, ambayo ni kazi ya maana zaidi yenye inafanyika hapa duniani. Kwa hiyo, tuendelee kuonyesha shukrani yetu kwa Yehova kwa sababu anaongoza na anabariki kazi yetu ya kufundisha katika dunia yote.

^ fu. 1 Wanafunzi wa Biblia walianza kuitwa Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa 1931.​—Isa. 43:10.