Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MASIMULIZI KUHUSU MAISHA YA WATU

Tumepata Kazi Yenye Kufurahisha Zaidi

Tumepata Kazi Yenye Kufurahisha Zaidi

WAKATI mimi na Gwen tulikuwa na miaka tano, tulianza kujifunza kucheza dansi. Tulikuwa hatujakutana. Lakini wakati tulikuwa tunakomaa, kila mumoja wetu alikuwa ameazimia kufanya aina ya dansi yenye kuitwa baleti ikuwe kazi yake ya maisha. Wakati tulifikia kuwa wachezaji wenye kujulikana sana, tuliacha kazi hiyo. Ni nini ilituchochea kuamua hivyo?

David: Nilizaliwa mwaka wa 1945 katika jimbo la Shropshire, Uingereza. Baba yangu alikuwa na ferme (mahali pa kulima na kufugia wanyama) katika kijiji kimoja chenye amani. Kisha kutoka kwenye masomo, nilifurahia kukulisha kuku, kukusanya mayai, na nilipenda kuchunga ngombe na kondoo. Wakati wa mapumuziko ya masomo, nilisaidia kufanya kazi ya kuvuna, wakati fulani kwa kutembeza motokari zetu za kuvuna.

Hata hivyo, nilikuwa na tamaa ingine yenye ilianza kuongoza maisha yangu. Baba yangu alitambua tamaa hiyo wakati nilikuwa ningali mutoto mudogo. Nilipenda kucheza kila wakati nilisikia sauti ya muziki. Kwa hiyo, wakati nilikuwa na miaka tano, baba yangu alimuambia mama anipeleke kwenye masomo fulani ya eneo letu ili kujifunza aina fulani ya dansi (dansi ambayo wachezaji wanavaa viatu vyenye kutoa sauti kwenye udongo). Mwalimu wangu aliona kwamba nilikuwa na uwezo wa kucheza dansi inayoitwa baleti, na kwa hiyo alinipatia mazoezi ili nijifunze dansi hiyo. Wakati nilikuwa na miaka 15, nilipewa nafasi ya kusoma kwa bure kwenye masomo yenye kuheshimiwa sana ya Royal Ballet School yenye kupatikana katika Londres. Nilikutana na Gwen kwenye masomo hayo, na tulichaguliwa ili kucheza dansi pamoja.

Gwen: Nilizaliwa katika muji mukubwa wa Londres mwaka wa 1944. Wakati nilikuwa mutoto mudogo, nilikuwa na imani kubwa katika Mungu. Nilijikaza kusoma Biblia yangu, lakini nikaona kwamba ni vigumu kuielewa. Wakati nilikuwa na miaka tano, nilienda kujifunza kucheza dansi. Kisha miaka sita, kulifanyika mashindano ya wachezaji wote wa dansi wa Uingereza, na iliahidiwa kwamba yule mwenye atapata ushindi atapewa zawadi ya kusomea kwenye masomo ya Royal Ballet School. Nilipata ushindi kwenye mashindano hayo. Masomo hayo ilipatikana White Lodge, nyumba yenye kupendeza sana ya Georgia katika Richmond Park, inje ya muji wa Londres. Kwenye masomo hayo, walimu wenye kuheshimiwa sana walinifundisha kucheza dansi ya baleti. Wakati nilikuwa na miaka 16, nilikuwa muchezaji mukubwa kwenye masomo ya Royal Ballet School katikati ya muji wa Londres, na tulikutana na David kwenye masomo hayo. Kwa miezi kidogo tu, mimi pamoja na David tulikuwa tunacheza dansi ya baleti na kuimba muziki wenye kuitwa opera katika jumba la Royal Opera House lenye kupatikana Covent Garden, katika Londres.

Kazi yetu ya kucheza dansi ya baleti ilituwezesha kusafiri katika inchi mbalimbali katika dunia yote

David: Mimi na Gwen, kazi yetu ilitupatia nafasi ya kuchezea katika majumba yenye kujulikana sana, kama vile jumba la Royal Opera House na jumba la London Festival Ballet (leo ni English National Ballet). Mwalimu wetu mumoja kwenye Royal Ballet alianzisha shirika la kimataifa katika muji wa Wuppertal, Ujerumani, na akatuchagua sisi wawili tu. Wakati wa kazi yetu ya kucheza, tulichezea katika majumba mbalimbali ya michezo katika dunia yote, na tulikuwa wenye kujulikana sana kama vile Dame Margot Fonteyn na Rudolf Nureyev. Maisha kama hayo ya kushindana ilitufanya tukuwe wenye majivuno, na tulijitoa sana katika kazi yetu ya kucheza dansi.

Gwen: Nilitumia mwili wangu na akili yangu yote ili kucheza dansi. Mimi na David tulikuwa na tamaa ya kuwa wachezaji wenye kujulikana sana. Nilifurahi sana wakati watu waliniambia nitie sinyatire yangu kwenye vitu fulani, wakati watu walinipatia maua, na wakati watu walinipigia mikono. Katika mambo ya michezo, nilizungukwa na watu wengi wenye kuwa na mwenendo mubaya, wenye kuvuta tumbaku, na wenye kunywa pombe. Nilitegemea hirizi za bahati nzuri kama wachezaji wengine katika ulimwengu.

MAISHA YETU INABADILIKA KABISA

Siku ya ndoa yetu

David: Kisha miaka mingi katika kazi ya kucheza, nilianza kuchoka kwa sababu ya kusafiri kila mara. Kwa sababu nilikomalia katika mashamba, nilianza kutamani kuishi maisha mepesi katika kijiji. Kwa hiyo katika mwaka wa 1967, niliacha kucheza na nikaanza kutumika katika ferme kubwa karibu na nyumba ya wazazi wangu. Ferme hiyo iliniwezesha kulipia nyumba ndogo katika eneo hilo. Kisha nilimuita Gwen kwenye telefone na nikamuuliza ikiwa atakubali tuoane. Alikuwa ameanza kucheza aina fulani ya dansi yenye kuitwa solo, na kazi yake ilikuwa inaenda vizuri; kwa hiyo, haikuwa mwepesi kwake kuchukua uamuzi huo. Hata hivyo, alikubali tuoane, na akakubali tuishi pamoja katika kijiji chetu, maisha yenye alikuwa hazoee.

Gwen: Ndiyo, ilikuwa vigumu kwangu kuzoea maisha ya ferme. Kazi ya kutosha maziwa ya ngombe, kukulisha nguruwe na kuku katika majira mbalimbali ilikuwa tofauti sana na maisha yenye nilizoea. David alianza kusoma kwa muda wa miezi 9 kwenye masomo fulani ili ajue njia mupya zenye zinatumiwa katika mambo ya ferme. Wakati huo, nilijisikia kabisa kuwa peke yangu kwa sababu David alikuwa anarudia usiku nyumbani. Ni wakati huo ndio Gilly, binti yetu wa kwanza alizaliwa. David aliniambia nijifunze kutembeza motokari, na siku moja, wakati nilikuwa ninatembelea muji fulani wenye ulikuwa karibu, nilimuona Gael, mwenye nilikutanaka naye wakati alikuwa anauzisha katika duka ya eneo hilo.

Maisha yetu ya kwanza-kwanza katika ferme

Gael alinialika kwake ili tukunywe chai pamoja. Tuliangalia picha za siku ya ndoa yake, na picha moja ilionyesha kikundi cha watu fulani inje ya nyumba fulani yenye kuitwa Jumba la Ufalme. Nilimuuliza ikiwa nyumba hiyo ilikuwa ya kanisa gani. Wakati aliniambia kwamba yeye na bwana yake ni Mashahidi wa Yehova, nilifurahi sana. Nilikumbuka kwamba shangazi yangu mumoja alikuwa pia Shahidi. Nilikumbuka pia kwamba baba yangu alichukizwa na kukasirika sana, na alitupa vichapo vyake kwenye yalala. Kwa kawaida baba yangu ni mupole sana; lakini nilijiuliza sababu gani alimukasirikia sana shangazi yangu mwenye alikuwa na tabia muzuri.

Mwishowe, nilifikia kujua kwamba mambo yenye shangazi yangu alikuwa anaamini ilikuwa tofauti na mafundisho ya dini zingine. Gael alinionyesha mambo yenye Biblia inafundisha kabisa. Nilishangaa sana wakati nilijua kwamba mafundisho mengi ya dini, kama vile fundisho la Utatu na fundisho la kutokufa kwa nafsi, hayapatane na mambo yenye Biblia inafundisha. (Mhu. 9:5, 10; Yoh. 14:28; 17:3) Pia, niliona kwa mara ya kwanza jina la Mungu, Yehova, katika Biblia.—Kut. 6:3.

David: Gwen aliniambia mambo yenye alikuwa anajifunza. Nilikumbuka kwamba wakati nilikuwa mutoto, baba yangu aliniambia kwamba nilipaswa kusoma Biblia. Kwa hiyo, mimi na Gwen tulikubali kujifunza Biblia pamoja na Gael na Derrick, bwana yake. Kisha miezi sita tukahamia katika muji wa Oswestry, katika jimbo la Shropshire, kwa sababu tulipata mutu mwenye angetulipa ili kutumikisha ferme yetu ndogo. Katika muji huo, dada mumoja Shahidi anayeitwa Deirdre, aliendelea kujifunza Biblia kwa uvumilivu pamoja na sisi. Mwanzoni tulifanya maendeleo ya kiroho polepole. Kazi ya kuchunga wanyama ilituchukua muda mwingi sana. Lakini, hatua kwa hatua kweli ya Biblia ilianza kuwa na mizizi katika mioyo yetu.

Gwen: Tatizo kubwa lenye nilipaswa kupiganisha ni kuachana kabisa na mambo ya uchawi. Andiko la Isaya 65:11 lilinisaidia kuelewa maoni ya Yehova juu ya “wale wanaoandaa [wanaotayarisha] meza kwa ajili ya mungu wa Bahati.” Iliniomba wakati mwingi na sala nyingi ili niachane kabisa na hirizi za bahati na za kunilinda. Wakati nilijifunza kwamba “yeyote yule anayejiinua atanyenyekezwa, na yeyote yule anayejinyenyekeza atainuliwa,” nilielewa Yehova anataka nikuwe mutu wa namna gani. (Mt. 23:12) Nilitamani kumutumikia Mungu mwenye kuhangaikia sana watu na ambaye alimutoa Mwana wake mwenye alipenda sana ili akuwe zabihu ya ukombozi. Wakati huo, binti yetu wa pili alikuwa amezaliwa, na tulifurahi sana wakati tulijifunza kwamba inawezekana familia yetu iishi milele katika paradiso duniani.

David: Wakati nilielewa namna unabii mbalimbali wa Biblia unatimia kwa njia yenye kushangaza, kama vile unabii wenye kupatikana katika kitabu cha Mathayo sura ya 24 na katika kitabu cha Danieli, nilisadiki kwamba nimepata kweli. Nilitambua kwamba katika ulimwengu huu muovu, hakuna kitu kizuri zaidi kuliko kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova. Kwa hiyo, kadiri wakati uliendelea kupita, roho yangu ya kutaka kushindana ilipunguka. Nilielewa kwamba sikukuwa mutu wa lazima sana kuliko bibi yangu na binti zangu. Andiko la Wafilipi 2:4 lilinisadikisha kwamba nilipaswa kuepuka kujifikiria sana na kuepuka kufuatilia tamaa ya kupata ferme kubwa. Lakini, nilipaswa kutia kazi ya Yehova pa nafasi ya kwanza katika maisha yangu. Kisha nikaacha kuvuta tumbako. Lakini, ilikuwa vigumu sana kwetu kupanga wakati wetu ili kufika kwenye mikutano Siku ya Posho mangaribi; kwa sababu Jumba la Ufalme lilikuwa kwenye kilometre 10, na wakati huo ndio tulipaswa kutosha maziwa ya ngombe. Hata hivyo, kwa musaada wa Gwen, hatukukosa hata mukutano moja; pia, kila Siku ya Yenga asubuhi hatukukosa kuhubiri pamoja na binti zetu kisha kutosha maziwa ya ngombe.

Watu wa jamaa yetu hawakufurahia mabadiliko yenye tulifanya. Baba ya Gwen alikataa kumusemesha kwa muda wa miaka 6. Wazazi wangu pia walijaribu kutukataza kukusanyika pamoja na Mashahidi wa Yehova.

Gwen: Yehova alitusaidia kuvumilia majaribu hayo. Na kadiri wakati uliendelea kupita, ndugu na dada wa Kutaniko la Oswestry walikuwa kama familia yetu mupya, na walitutegemeza kwa upendo wakati wa majaribu hayo. (Lu. 18:29, 30) Katika mwaka wa 1972, tulijitoa kwa Yehova na kubatizwa. Nilijiwekea muradi wa kuhubiri kwa bidii ili kusaidia watu wengi zaidi wapate kweli; kwa hiyo, nikaanza kazi ya upainia.

KAZI MUPYA YENYE KULETA BARAKA

David: Miaka yenye tulipitisha katika kazi ya ferme ilikuwa yenye kuchokesha sana; lakini tulijikaza kuwa mufano muzuri kwa binti zetu katika ibada ya Yehova. Wakati huo, tuliacha kazi ya ferme kwa sababu serikali ilipunguza bei ya mifugo. Hatukuwa na nyumba yetu wala kazi, na binti yetu wa tatu alikuwa tu na mwaka moja; kwa hiyo, tulisali ili Yehova atusaidie na kutuongoza. Ili kutimiza mahitaji ya familia, tuliamua kutumia vipawa vyetu kwa kuanza kufundisha wengine namna ya kucheza dansi. Kwa sababu tuliazimia kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu, tulipata matokeo mazuri. Tulifurahi sana kuona binti zetu wote watatu wanaanza kazi ya upainia wakati walimaliza masomo. Gwen pia alikuwa painia; kwa hiyo, kila siku alitegemeza binti zetu katika kazi ya kuhubiri.

Kisha Gilly na Denise, binti zetu wawili wa kwanza, kuolewa, tuliacha kazi yetu ya kufundisha watu kucheza dansi. Tuliandikia biro ya tawi ili kujua ni wapi tunaweza kusaidia. Biro ya tawi ilitupendekeza kutumikia katika miji fulani kusini mwa Uingereza. Kwa sababu tulibakia tu na mutoto moja, Debbie, mimi pia nilianza kazi ya upainia. Kisha miaka tano, tuliombwa kusaidia makutaniko mengine ya kaskazini mwa Uingereza. Wakati Debbie aliolewa, tulipewa pendeleo la kutumika katika kazi ya ujenzi wa kimataifa kwa muda wa miaka 10. Tulitumikia katika inchi ya Zimbabwe, Moldova, Hongrie, na katika inchi ya Côte d’Ivoire. Kisha tulirudi Uingereza ili kusaidia katika kazi ya ujenzi kwenye Beteli ya Londres. Kwa sababu nilikuwa na uzoefu katika mambo ya ferme, niliombwa kufanya kazi hiyo kwenye Beteli. Leo, tunafanya kazi ya upainia kaskazini mwa Uingereza.

Tulipata furaha kubwa sana katika kazi ya ujenzi wa kimataifa

Gwen: Kwanza, tulijitoa katika kazi ya kucheza dansi ya baleti; kazi hiyo ilikuwa yenye kufurahisha lakini ya muda mufupi. Kisha, tulijitoa kwa Yehova; hilo ndilo jambo la maana zaidi lenye tulifanya, na kufanya hivyo kumetuletea furaha kubwa na yenye kuendelea. Tunaendelea kutumika pamoja, lakini sasa tunatumia miguu yetu ili kuwa mapainia. Kusaidia watu wajifunze kweli za maana sana na zenye kuleta uzima kumetuletea furaha kubwa sana. “Barua [hizo] za pendekezo” ni nzuri zaidi kuliko kujulikana sana katika ulimwengu huu. (2 Kor. 3:1, 2) Ikiwa hatungepata kweli, leo tungeendelea kukumbuka mambo ya zamani, kama vile, picha za zamani, na programu za michezo ya kazi yetu ya zamani.

David: Kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Yehova kumekuwa na matokeo mazuri sana katika maisha yetu. Kwa mufano, kumutumikia Yehova kumenisaidia nikuwe bwana na baba muzuri. Biblia inasema kwamba Miriamu, Mufalme Daudi, na wengine, walionyesha furaha yao kupitia dansi. Kwa hiyo, sisi pamoja na wengine wengi, tunangojea kwa hamu wakati tutacheza dansi kwa furaha katika dunia mupya ya Yehova.—Kut. 15:20; 2 Sam. 6:14.