Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Amri ya Kuoa ao Kuolewa “Katika Bwana Tu”—Ingali Yenye Kufaa?

Amri ya Kuoa ao Kuolewa “Katika Bwana Tu”—Ingali Yenye Kufaa?

Sipate mutu wa kuoana naye katika kutaniko, na ninaogopa kwamba nitazeeka nikiwa pekee yangu.”

“Wanaume fulani wasio Mashahidi ni watu wazuri, wenye kuvutia, na wako na uwezo wa kufikiri vizuri. Hawapinge dini yangu, na wanaonekana kuwa wenye kuvutia zaidi kuliko ndugu fulani.”

Watumishi fulani wa Mungu wamesema maneno kama hayo wakati wanatafuta mutu wa kuoana naye. Hata hivyo, wanajua shauri la mutume Paulo la kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu.” Shauri hilo linapaswa kuongoza mwenendo wa kila Mukristo. (1 Kor. 7:39) Kwa hiyo, sababu gani wanasema maneno hayo?

SABABU YENYE INAFANYA WENGINE WAKUWE NA MASHAKA

Wakristo wenye kusema maneno hayo, wanaweza kufikiri kwamba hesabu ya dada wenye wanaweza kuolewa ni kubwa zaidi kuliko hesabu ya ndugu. Katika inchi nyingi hesabu ya dada ni kubwa kuliko hesabu ya ndugu. Tufikirie mifano mbili: Katika inchi ya Korea, kati ya Mashahidi mia moja wenye hawajaoa ao kuolewa, 57 ni dada, na 43 ni ndugu. Katika inchi ya Kolombia, ripoti inaonyesha kwamba kati ya Mashahidi mia moja, 66 ni dada, na 34 ni ndugu.

Katika inchi fulani, tatizo kubwa ni kwamba wazazi wasio Mashahidi wanaweza kuomba mali mingi (dot), na jambo hilo linazuia ndugu wenye hawana mali ya kutosha waoe. Wakati dada anafikiria mambo hayo, anaweza kuona kwamba ni vigumu kupata ndugu wa kumuoa “katika Bwana.” Kwa hiyo, anaweza kujiuliza hivi: “Ninaweza kutazamia kwamba nitapata bwana mwenye kufaa kabisa katika kutaniko?” *

NI LAZIMA KUMUTUMAINIA YEHOVA

Ikiwa umekwisha kuwa na mawazo kama hayo, ukuwe hakika kwamba Yehova anajua hali yako. Bila shaka anajua namna unajisikia kuhusu jambo hilo.—2 Nya. 6:29, 30.

Hata hivyo, katika Neno lake, Yehova ametoa muongozo wa kuoa ao kuolewa katika Bwana tu. Sababu gani? Kwa sababu anapenda watu wake wakuwe na maisha mazuri. Anapenda watumishi wake wasipatwe na maumivu yenye mutu anaweza kupata kwa sababu ya kuchukua maamuzi mabaya, lakini pia anapenda wakuwe wenye furaha. Katika siku za Nehemia Wayahudi wengi walioa wanawake wenye hawakuwa waabudu wa Yehova. Kwa hiyo, Nehemia aliwakumbusha matokeo mabaya ambayo Mufalme Sulemani alipata kwa sababu alioa wanawake wasio Waisraeli. Nehemia aliwaambia kwamba ijapokuwa Mufalme Sulemani ‘alipendwa na Mungu wake, . . . wake wa kigeni walimufanya hata yeye atende zambi.’ (Neh. 13:23-26) Ndiyo sababu Mungu amewaamuru watumishi wake waoe ao kuolewa tu na waabudu wa kweli, na kufanya hivyo ni kwa faida yao. (Zab. 19:7-10; Isa. 48:17, 18) Wakristo wa kweli wanamushukuru Mungu kwa sababu anawahangaikia kwa upendo; kwa hiyo wanategemea muongozo wake. Wanaonyesha kwamba wanamukubali Mungu kuwa Mutawala wa Ulimwengu Wote Muzima kwa kutii muongozo wake.—Met. 1:5.

Bila shaka, unataka kuepuka ‘kufungwa nira’ na mutu mwenye anaweza kukuchochea uache kumutumikia Mungu. (2 Kor. 6:14) Leo Wakristo wengi wametii muongozo huo wa Mungu ambao tangu zamani umeonekana kuwa ulinzi, na wamefikia kutambua kwamba walichukua maamuzi mazuri. Lakini Wakristo fulani wamechukua maamuzi mabaya.

AMRI HIYO INGALI YENYE KUFAA

Maggy, * dada wa Australia, anaeleza jambo lenye lilimufikia wakati alianza kufanya urafiki wa kimapenzi na kijana fulani asiye Shahidi. Anasema hivi: “Nilikosa mikutano mingi kwa sababu tu nilitaka kuwa pamoja naye. Hali yangu ya kiroho iliharibika sana.” Ratana, dada wa India alianza kufanya urafiki wa kimapenzi na mwanafunzi mwenzake mwenye alikuwa ameanza kujifunza Biblia. Lakini kisha muda fulani, mwanafunzi huyo alionyesha kwamba nia yake ilikuwa kuanza urafiki wa kimapenzi pamoja naye. Mwishowe dada huyo aliacha kweli, na akakubali kubadilisha dini ili kuolewa.

Mufano mwengine ni wa dada Ndenguè wa Cameroun. Alikuwa na miaka 19 wakati aliolewa. Mwanaume mwenye angemuoa alimuahidi kwamba atamuachia uhuru wa kufuata dini yake. Lakini juma mbili kisha ndoa yao, bwana yake alimukataza kuhuzuria mikutano. Dada huyo anasema hivi: “Nilijisikia peke yangu na nililia. Nilitambua kwamba nimeshindwa kuongoza maisha yangu. Nilijilaumu kila mara.”

Kwa kweli, si watu wote wasio Mashahidi ndio wanabadilika na kuwa wakali kuelekea bibi ao bwana yao aliye Shahidi. Lakini, hata kama hauteseke kwa sababu umeoa ao kuolewa na mutu mwenye haiko Shahidi, hauone kama hilo linaweza kuwa na matokeo fulani juu ya urafiki wako pamoja na Baba yako wa mbinguni mwenye upendo? Utajisikia namna gani wakati utajua kwamba umezarau shauri lenye Yehova alikutolea kwa faida yako? Zaidi ya yote, Yehova atajisikia namna gani juu ya uamuzi wenye umechukua?—Met. 1:33.

Ndugu na dada katika dunia yote wanaweza kushuhudia kwamba ni muzuri zaidi kuolewa “katika Bwana tu.” Wale ambao hawajaoa ao kuolewa wameazimia kufurahisha moyo wa Mungu kwa kuwa tayari kuoa ao kuolewa tu na mutu mwenye kufaa kati ya waabudu wenzao. Michiko ni dada wa Japani ambaye watu wa jamaa yake walijaribu kumukaza aolewe na mutu asiye Shahidi. Dada huyo aliendelea kuvumilia jaribu hilo. Hata hivyo, aliona namna rafiki zake fulani na wengine wenye anajuana nao wanapata watu wa kuoana nao katika kutaniko. Anasema hivi: “Niliendelea kuwa hakika kwamba kwa sababu Yehova ni ‘Mungu mwenye furaha,’ si lazima kuolewa ao kuoa ili tukuwe na furaha. Pia, ninaamini kwamba anatimiza tamaa za moyo wetu. Kwa hiyo, ikiwa tunataka kuoa ao kuolewa lakini hatupate mutu wa kuoana naye, ni vizuri zaidi tubaki bila kuoa ao kuolewa kwa sasa.” (1 Tim. 1:11) Mwishowe, Michiko aliolewa na ndugu muzuri, na ni mwenye furaha kwa sababu alingojea.

Ndugu fulani pia wamengojea ili kupata dada mwenye kufaa. Bill, ndugu wa Australia ni mumoja wao. Anasema kwamba wakati fulani alivutiwa na wanawake wasio Mashahidi. Lakini, aliepuka kabisa kuwa rafiki wao wa sana. Sababu gani? Hakupenda kufanya hatua ya kwanza ili ‘kufunga nira isio sawa’ na mutu asiyeamini. Kwa muda wa miaka fulani, alipendezwa na dada fulani, lakini dada hao hawakupendezwa naye. Bill alivumilia miaka 30 mbele apate dada mwenye kufaa. Bill anasema hivi: “Mimi sisikitike hata kidogo.” Anasema tena hivi: “Nimebarikiwa sana kwa sababu tunahubiri pamoja, tunajifunza pamoja, na tunamuabudu Yehova pamoja. Ninafurahi kujuana na rafiki za bibi yangu kwa sababu wote ni Mashahidi. Tunatumia kanuni za Biblia ili kufanya ndoa yetu ikuwe muzuri zaidi.”

WAKATI UNAMUNGOJEA YEHOVA

Wakati unategemea shauri la Yehova na kungojea mupaka upate mutu wa kuoana naye, unaweza kufanya nini? Kwanza, ni vizuri ujue sababu gani haujaoa ao kuolewa. Ikiwa unaona kwamba sababu kubwa ni kutafuta kutii amri ya Biblia ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu,” unastahili pongezi kwa sababu unaheshimu amri hiyo ya Mungu. Ukuwe hakika kwamba Yehova anafurahi kuona kwamba unaazimia kutii Neno lake. (1 Sam. 15:22; Met. 27:11) Unaweza kuendelea ‘kumimina moyo wako’ kwa Mungu katika sala. (Zab. 62:8) Kadiri unaendelea kusali kwa bidii, urafiki wako pamoja na Yehova utakuwa wenye nguvu zaidi. Zaidi ya hilo, urafiki wako pamoja na Yehova utakuwa wenye nguvu kila siku. Ukuwe hakika kwamba Aliye Juu Zaidi anapendezwa na watumishi wake wote waaminifu na kwamba uko mwenye bei kubwa machoni pake. Anahangaikia mahitaji yako na tamaa zako. Hamuahidi mutu yeyote bwana ao bibi. Lakini ikiwa kwa kweli unatamani kupata bibi ao bwana, Mungu anajua njia nzuri zaidi ya kutosheleza tamaa hiyo.—Zab. 145:16; Mt. 6:32.

Wakati fulani, unaweza kujisikia kama mutunga-zaburi Daudi, mwenye alisema hivi: “Ufanye haraka, unijibu, Ee Yehova; roho yangu imefikia mwisho. Usiufiche uso wako mbali nami.” (Zab. 143:5-7, 10) Katika hali kama hizo, umuachie Baba yako wa mbinguni wakati ili akuonyeshe anapenda ufanye nini. Unaweza kufanya hivyo kwa kuchukua wakati wa kusoma Neno lake na kutafakari sana juu ya mambo yenye unasoma. Utajua amri zake na utaona namna aliwatendea watumishi wake wa zamani. Ukimusikiliza, utakuwa hakika zaidi kwamba kumutii ni jambo la hekima.

Wale wenye hawajaoa ao kuolewa ni watu wa lazima katika kutaniko, mara nyingi wanasaidia familia na vijana

Wakati haujaoa ao kuolewa, ni mambo gani mengine unaweza kufanya ili ukuwe na furaha na upate matokeo mazuri? Unaweza kutumia wakati huo ili kukomalisha utambuzi wako wa kiroho, kuonyesha ukarimu, kuwa mufanya kazi mwenye bidii, mwenye urafiki, kushikamana na Mungu, na kuwa na sifa nzuri; kufanya hivyo kutakutayarisha kwa ajili ya maisha ya familia yenye furaha. (Mwa. 24:16-21; Rut. 1:16, 17; 2:6, 7, 11; Met. 31:10-27) Tafuta kwanza Ufalme kwa kuhubiri kwa bidii na kusaidia katika kazi zingine mbalimbali za kiroho; kufanya hivyo itakuwa ulinzi kwako. Bill, mwenye tumetaja katika habari hii, anasema hivi kuhusu wakati alikuwa na nia ya kuoa: “Ulipita haraka sana! Nilitumia wakati huo ili kufanya kazi ya upainia.”

Kwa kweli, amri ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu” ingali yenye kufaa. Kutii muongozo huo kunaweza kukusaidia umuheshimu Yehova na uendelee kutosheka. Biblia inasema hivi: ‘Mwenye furaha ni mutu anayemuogopa Yehova, ambaye amependezwa sana na amri zake. Vitu vyenye samani na utajiri viko nyumbani mwake; nao uadilifu wake unasimama milele.’ (Zab. 112:1, 3) Kwa hiyo, azimia kushikamana na amri ya Mungu ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu.”

^ fu. 7 Habari hii inazungumuzia sana maoni ya dada fulani. Hata hivyo, kanuni zenye kutumiwa zinahusu pia ndugu.

^ fu. 13 Majina fulani yamebadilishwa.