Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani Kutengwa na Kutaniko ni Mupango Wenye Upendo?

Sababu Gani Kutengwa na Kutaniko ni Mupango Wenye Upendo?

NDUGU Julian anakumbuka hivi: “Wakati nilisikia kwamba mutoto wangu ametengwa na kutaniko, nilijisikia kwamba maisha yangu imefikia mwisho. Yeye ndiye alikuwa mutoto wangu wa kwanza, na alikuwa rafiki yangu wa sana; tulifanya mambo mengi pamoja. Alikuwa mufano muzuri, lakini bila kutazamia akaanza mara moja kujiendesha mubaya. Bibi yangu alikuwa analia kila mara, na sikuweza kumufariji. Tuliendelea kujiuliza ikiwa kwa kadiri fulani tulishindwa kutimiza daraka letu la kuwa wazazi.”

Sababu gani tunaweza kusema kwamba kutenga Mukristo na kutaniko ni mupango wenye upendo hata kama jambo hilo linaleta huzuni nyingi? Biblia inatoa sababu gani zenye kufanya uamuzi mukali kama huo uchukuliwe? Ni mambo gani inaweza kumufanya Mukristo atengwe na kutaniko?

MAMBO MAWILI YENYE KUFANYA MUKRISTO ATENGWE NA KUTANIKO

Kuna mambo mawili yenye inapaswa kufanyika ili Shahidi wa Yehova afikie kutengwa na kutaniko. Jambo la kwanza, Shahidi mwenye kubatizwa anafanya zambi nzito. Jambo la pili, Shahidi huyo anakataa kutubu zambi yake.

Hata kama Yehova hatazamie ukamilifu kwetu, ametupatia kanuni za utakatifu zenye tunapaswa kutii. Kwa mufano, Yehova anatuambia tuepuke kabisa zambi nzito kama vile, uasherati, ibada ya sanamu, wizi, kuwa munyanganyi, kuua, na kuzungumuza na mashetani.—1 Kor. 6:9, 10; Ufu. 21:8.

Hauone kwamba kanuni za Yehova juu ya mwenendo safi ni zenye kufaa na kwamba zinatulinda? Bila shaka, sisi wote tunapenda kuishi pamoja na watu wenye kupenda amani, watu wenye kuwa na mwenendo muzuri na wenye tunaweza kutumainia. Tunapata watu kama hao katikati ya ndugu na dada zetu wa kiroho, kwa sababu wakati tunajitoa kwa Mungu tunatoa ahadi kwamba tutaishi kulingana na muongozo wake wenye kutolewa katika Neno lake.

Itakuwa namna gani ikiwa Mukristo mwenye kubatizwa anafanya zambi nzito kwa sababu ya uzaifu? Zamani, watumishi waaminifu wa Yehova walifanya zambi nzito, lakini Yehova hakuwakataa kabisa. Mufalme Daudi ni mumoja kati ya watumishi hao. Mufalme Daudi alifanya uzinifu na akaua, lakini, nabii Nathani alimuambia hivi: ‘Yehova . . . anasamehe zambi yako.’—2 Sam. 12:13.

Mungu alimusamehe Mufalme Daudi kwa sababu alitubu kwelikweli. (Zab. 32:1-5) Leo pia, mutumishi wa Yehova anaweza kutengwa na kutaniko ikiwa tu anakataa kutubu zambi yake, ao ikiwa anaendelea kufanya mambo mabaya. (Mdo. 3:19; 26:20) Ikiwa wazee wenye kuwa katika halmashauri ya hukumu hawaone kabisa kwamba mutu huyo ametubu kwelikweli, wanapaswa kumutenga na kutaniko.

Mwanzoni tunaweza kuona kwamba uamuzi wa kumutenga mukosaji huyo mwenye alikataa kutubu ni mukali ao wa bila huruma, zaidi sana ikiwa mutu huyo ni wa jamaa yetu ao ni rafiki yetu. Hata hivyo, Neno la Yehova linatutolea sababu nzuri zenye kutufanya tukubali kwamba uamuzi kama huo ni wenye upendo.

FAIDA YA KUTENGA MUKOSAJI

Yesu alisema kwamba hekima inaonyeshwa kuwa yenye haki kwa matokeo yake. (Mt. 11:19) Uamuzi wenye hekima wa kumutenga mukosaji mwenye alikataa kutubu unakuwa na matokeo mazuri. Tuzungumuzie mambo tatu:

Kutenga wakosaji kunaletea jina la Yehova heshima. Kwa sababu tunaitwa kwa jina la Yehova, bila shaka matendo yetu inaweza kuwa na matokeo mazuri ao mabaya juu ya jina lake. (Isa. 43:10) Kama vile mwenendo wa mutoto unaweza kuheshimisha ao kuchafua jina la wazazi wake, mwenendo muzuri ao mwenendo mubaya wa watu wenye kuitwa kwa jina la Yehova, unaweza kufanya kwa kadiri fulani watu wakuwe na maoni mazuri ao mabaya juu ya Yehova. Jina nzuri la Mungu linatukuzwa wakati watu wenye kuitwa kwa jina lake wanatii kanuni zake za mwenendo safi. Kwa kadiri fulani, hali ilikuwa hivyo katika siku za Ezekieli, wakati watu wa mataifa walipatanisha sana jina la Yehova na Wayahudi.—Eze. 36:19-23.

Tunaweza kuchafua jina takatifu la Mungu ikiwa tunafanya matendo machafu. Mutume Petro aliwashauria Wakristo hivi: “Kama watoto watiifu, acheni kufanyizwa kulingana na tamaa mulizokuwa nazo hapo zamani katika hali yenu ya kutojua, bali, kwa kupatana na Mutakatifu aliyewaita, ninyi wenyewe pia iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote kwa sababu imeandikwa: ‘Mukuwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mutakatifu.’” (1 Pet. 1:14-16) Mwenendo wenye kuwa safi, na mutakatifu unaletea jina la Mungu heshima.

Hata hivyo, ikiwa Shahidi wa Yehova anafanya matendo mabaya, rafiki zake na wale wenye kumujua wanaweza kujua jambo hilo. Kutengwa na kutaniko kunaonyesha kwamba Yehova iko na watu wenye kuwa safi na wenye kufuata kabisa muongozo wa Maandiko ili kuchunga utakatifu huo. Katika inchi ya Uswisi, mwanaume mumoja alifika kwenye Jumba la Ufalme na kusema kwamba anapenda aanze kukusanyika. Dada yake alikuwa ametengwa na kutaniko kwa sababu ya uasherati. Akasema kwamba anapenda kujiunga na tengenezo lenye “haliruhusu mwenendo mubaya.”

Kutengwa na kutaniko kunalinda usafi wa kutaniko la Kikristo. Mutume Paulo aliwaonya Wakristo wa Korintho kuhusu hatari ya kuwaacha watu wenye kufanya zambi kimakusudi wabakie katika kutaniko. Alilinganisha uvutano mubaya wa watu kama hao na ule wa chachu yenye kuvimbisha tonge lote. Akawaonyesha kwamba ‘chachu kidogo inachachisha tonge lote.’ Kwa hiyo, aliwashauria hivi: ‘Muondoe ule mutu muovu kati yenu.’—1 Kor. 5:6, 11-13.

Inawezekana, ‘mutu muovu’ ambaye Paulo anazungumuzia alifanya kimakusudi uasherati wenye ulijulikana na watu. Na Wakristo fulani katika kutaniko walikuwa hata wameanza kutetea mwenendo wake. (1 Kor. 5:1, 2) Ikiwa zambi nzito kama hiyo ingeachiliwa, Wakristo wengine wangechochewa kufuata mwenendo muchafu wenye watu wa muji wa Korintho walizoea kufanya. Kuachilia zambi zenye kufanywa kimakusudi kunachochea watu wakuwe na tabia ya kuzarau kanuni za Mungu. (Mhu. 8:11) Zaidi ya hilo, wakosaji wenye wanakataa kutubu, wanaweza kuwa “miamba [majiwe makubwa] iliyofichwa chini ya maji” na kuharibu imani ya wengine katika kutaniko.—Yuda 4, 12.

Kutengwa na kutaniko kunaweza kumusaidia mukosaji arudiwe na ufahamu. Siku moja Yesu alizungumuzia mufano wa kijana mumoja mwenye aliacha nyumba ya baba yake na kutumia uriti wake wote katika mwenendo mubaya. Mwana mupotevu huyo alielewa kwamba maisha yenye alipitisha inje ya nyumba ya baba yake ilikuwa bila faida na mabaya sana. Mwishowe mwana huyo alirudiwa na ufahamu, akatubu, na akarudi katika familia yao. (Lu. 15:11-24) Maelezo ya Yesu kuhusu baba mwenye upendo mwenye alifurahi wakati mutoto wake alirudia, yanatusaidia kuelewa namna Yehova anajisikia wakati mukosaji anarudia katika kutaniko. Yehova anatuhakikishia hivi: ‘Ninapendezwa, si na kifo cha muovu, bali kwamba mutu muovu ageuke na kuiacha njia yake na kwa kweli aendelee kuishi.’—Eze. 33:11.

Vilevile, wale wenye wametengwa na kutaniko la Kikristo, ni kusema, familia yao ya kiroho, wanaweza kufikia kutambua kwamba wamepoteza mambo ya maana sana. Wakati wanapata matokeo mabaya ya zambi zao na kukumbuka maisha ya furaha yenye walikuwa nayo wakati walikuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova na watu wake, mambo hayo yanaweza kuwafanya warudiwe na ufahamu.

Inaomba kuwa na upendo na kuazimia kabisa ili kufikia hatua hiyo. Mutunga-zaburi Daudi alisema hivi: ‘Mwadilifu [mwenye haki] akinipiga, zingekuwa fazili zenye upendo; naye akinikaripia, hiyo ingekuwa mafuta juu ya kichwa.’ (Zab. 141:5) Kwa mufano: Wazia ni wakati wa baridi kali, mutu mwenye kusafiri anajisikia mwenye kuchoka sana katika njia. Baridi inakuwa nyingi katika mwili na anaanza kusinzia. Mutu huyo atakufa ikiwa anasinzilia katika teluji (neige). Wakati wanangojea watu wa kumuokoa, mara kwa mara wenzake watamupiga-piga kwenye uso ili asisinzie. Kufanya hivyo kunaweza kumuumiza, lakini kunaweza kuokoa uzima wake. Vilevile, Mufalme Daudi alitambua kwamba mutu mwadilifu anaweza kumupatia karipio lenye kuumiza, lakini kwa faida yake.

Katika hali nyingi, kutengwa na kutaniko ni nizamu yenye mukosaji anastahili. Kisha karibu miaka kumi hivi, mutoto wa ndugu Julian mwenye tumezungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii, alisafisha maisha yake, akarudia katika kutaniko, na sasa yeye ni muzee wa kutaniko. Anasema hivi: “Kutengwa na kutaniko kulinilazimisha nipambane na matokeo mabaya ya mwenendo wangu. Hiyo ndiyo nizamu nilipaswa kupewa.”—Ebr. 12:7-11.

NAMNA YA KUTENDEA WATENGWA KWA UPENDO

Kwa kweli, kutengwa na kutaniko ni musiba wa kiroho, lakini hatupaswe kuona musiba huo kuwa mubaya sana. Sisi wote tuko na daraka la kuhakikisha kwamba kutengwa na kutaniko kunatimiza kusudi lake.

Wazee wanajikaza sana ili kusaidia watengwa wenye kutubu wamurudilie Yehova

Wazee wenye kuwa na daraka lenye kuhuzunisha la kujulisha uamuzi wa kutengwa, wanajikaza kumuiga Yehova, Mungu mwenye upendo. Wakati wanamujulisha mukosaji kwamba ametengwa, wanamuelezea waziwazi kwa upendo hatua zenye anapaswa kufanya ili arudishwe katika kutaniko. Ili kuwakumbusha watengwa kuhusu namna wanaweza kumurudilia Yehova, wazee wanawatembelea wakati fulani wale wenye kuonyesha alama za kufanya mabadiliko ili kuwatolea mapendekezo kuhusu namna wanaweza kubadilisha mwenendo wao. *

Watu wa familia wanaweza kuonyesha kwamba wanapenda kutaniko na mukosaji wakati wanaheshimu uamuzi wa kutengwa na kutaniko. Ndugu Julian anaeleza hivi: “Niliendelea kumuona kama mutoto wangu, lakini mwenendo wake ulitia mupaka kati yangu na yeye.”

Ndugu na dada wote katika Kutaniko wanaweza kuonyesha upendo wenye kutegemea kanuni za Biblia kwa kuepuka kujiunga na kuzungumuza na mutu mwenye ametengwa na kutaniko. (1 Kor. 5:11; 2 Yoh. 10, 11) Kwa kufanya hivyo, wanaonyesha kwamba wanaunga mukono nizamu ao malipizi yenye Yehova amemupatia kupitia wazee wa kutaniko. Zaidi ya hilo, wanaweza kuonyesha kwamba wanapenda watu wenye kuhuzunika sana wa familia ya mutu mwenye ametengwa, kwa kuwategemeza ili wasijisikie kwamba wao pia wametengwa na kutaniko.—Rom. 12:13, 15.

Katika maneno yake ya kumalizia, ndugu Julian anasema hivi: “Kutengwa na kutaniko ni mupango wa lazima kwetu kwa sababu unatusaidia kuishi kulingana na kanuni za Yehova. Hata kama mupango wa kutengwa na kutaniko unaleta huzuni, mwishowe unakuwa na matokeo mazuri. Ikiwa singeonyesha kwamba ninachukia mwenendo mubaya wa mutoto wangu, hangeweza hata kidogo kubadilisha mwenendo wake.”

^ fu. 24 Ona Munara wa Mulinzi, wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 1991, ukurasa wa 21-23.