Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Muti Ukikatwa, Unaweza Kuchipuka Tena?

Muti Ukikatwa, Unaweza Kuchipuka Tena?

UKILINGANISHA muti wa muzeituni wenye kuzeeka na muti wa mwerezi mukubwa wa Lebanoni, muzeituni unaweza kuonekana kuwa mudogo sana. Hata hivyo, muzeituni uko na uwezo wa ajabu wa kuishi kwa muda murefu sana. Inasemekana kwamba mizeituni fulani imeishi miaka 1000. Muti wa muzeituni unatuma mizizi yake mbali sana katika udongo; kwa hiyo, muti huo uko na uwezo wa kuchipuka tena hata kama umekwisha kukatwa. Kadiri mizizi yake inaendelea kuishi, muti huo utachipuka tena.

Muzee wa ukoo Ayubu alikuwa hakika kwamba hata kama angekufa, angeweza kuishi tena. (Ayu. 14:13-15) Pengine alitumia mufano wa muti wa muzeituni ili kuonyesha kama anaamini kabisa kwamba Mungu iko na uwezo wa kumufufua. Ayubu alisema hivi: ‘Kwa ajili ya muti kuna tumaini, ukikatwa, utachipuka tena.’ Wakati mvua inaanza kunyesha na kumaliza kipwa kali, shina la muzeituni lenye kukauka linaweza kuotesha sehemu fulani kupitia mizizi yake na kutoa ‘matawi kama mumea mupya.’ —Ayu. 14:7-9.

Kama vile tu mulimaji anatamani sana kuona muzeituni uliokatwa unachipuka tena, Yehova Mungu pia anatamani sana kuwafufua watumishi wake na watu wengine wengi. (Mt. 22:31, 32; Yoh. 5:28, 29; Mdo. 24:15) Itakuwa furaha kubwa sana wakati tutakaribisha watu hao na kuona namna wanafurahia tena maisha!