Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Urafiki Wako Pamoja na Yehova Ni wa Kweli Kabisa?

Urafiki Wako Pamoja na Yehova Ni wa Kweli Kabisa?

‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ YAK. 4:8.

1. Sababu gani urafiki wetu pamoja na Yehova unapaswa kuendelea kuwa wenye nguvu?

WEWE ni Shahidi wa Yehova mwenye kubatizwa? Ikiwa jibu ni ndiyo, uko na kitu cha bei sana, ni kusema, urafiki wako pamoja na Mungu. Hata hivyo, urafiki huo unashambuliwa na mikazo ya ulimwengu wa Shetani na kutokamilika kwetu. Wakristo wote wanapambana na hali hizo. Kwa hiyo, urafiki wetu pamoja na Yehova unapaswa kuwa wenye nguvu zaidi.

2. (a) Urafiki ni nini? (Ona maelezo ya chini.) (b) Namna gani tunaweza kufanya urafiki wetu pamoja na Yehova ukuwe wenye nguvu zaidi?

2 Urafiki wako pamoja na Yehova ni wa kweli kabisa? Unapenda urafiki huo ukuwe wenye nguvu zaidi? Andiko la Yakobo 4:8 linaonyesha namna unaweza kufanya hivyo. Linasema hivi: ‘Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia ninyi.’ Andiko hilo linaonyesha hatua mbili zenye zinaomba kufanywa. * Wakati tunachukua hatua ya kumukaribia Mungu, yeye pia anachukua hatua ya kutukaribia. Wakati hatua hizo mbili zinafanywa kwa ukawaida, hilo linafanya hatua kwa hatua urafiki wetu pamoja na Yehova ukuwe wenye nguvu. Kwa hiyo, urafiki wetu pamoja naye utakuwa wa kweli kabisa. Kama Yesu, tutakuwa na uhakika huu: ‘Yule aliyenituma ni halisi [wa kweli] . . . Mimi ninamujua.’ (Yoh. 7:28, 29) Lakini, ni hatua gani unaweza kufanya ili umukaribie Yehova?

Namna gani unaweza kuzungumuza na Mungu? (Ona fungu la3)

3. Namna gani unaweza kuzungumuza na Yehova?

3 Ili kumukaribia Yehova, ni jambo la lazima sana kuzungumuza naye kwa ukawaida. Namna gani unaweza kuzungumuza na Mungu? Unatumia njia gani ili kuzungumuza na rafiki mwenye anaishi mbali sana? Pengine, kila mara munaandikiana ao kuzungumuza kwenye telefone. Unazungumuza na Yehova wakati unasali kwa ukawaida. (Soma Zaburi 142:2.) Wewe pia unamupatia Yehova nafasi ya kuzungumuza na wewe, wakati unasoma Neno lake na kufikiri sana juu ya Neno hilo kwa ukawaida. (Soma Isaya 30:20, 21.) Tuchunguze sasa namna gani kuzungumuza na Yehova kunaweza kufanya urafiki wetu pamoja naye ukuwe wenye nguvu zaidi, na ukuwe wa kweli kabisa.

YEHOVA ANAZUNGUMUZA NA WEWE KUPITIA FUNZO LAKO LA BIBLIA

4, 5. Namna gani Yehova anazungumuza na wewe kupitia Neno lake? Toa mufano.

4 Bila shaka, uko hakika kwamba Biblia iko na ujumbe wa Mungu kwa ajili ya wanadamu wote. Lakini, Biblia iko pia na ujumbe wenye kuonyesha namna wewe unaweza kumukaribia Yehova? Ndiyo. Namna gani? Wakati unasoma na kujifunza Biblia kwa ukawaida, ufikirie namna unajisikia kuhusu mambo yenye unasoma na ufikirie pia namna unaweza kutumikisha mambo yenye unajifunza katika hali mbalimbali za maisha yako. Wakati unafanya hivyo, unamuacha Yehova azungumuze na wewe kupitia Neno lake. Kwa hiyo, hilo litakusaidia umukaribie zaidi.—Ebr. 4:12; Yak. 1:23-25.

5 Kwa mufano, soma na ufikiri sana juu ya maneno ya Yesu yenye kutuonya ‘tuache kujiwekea hazina duniani.’ Ikiwa unaona kwamba tayari unatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza katika maisha yako, utajisikia kwamba unamupendeza Yehova. Lakini, ikiwa unatambua kwamba ni lazima ufanye maisha yako kuwa mepesi ili ukazie uangalifu zaidi faida za Ufalme, Yehova amekusaidia ujue mbele ya wakati jambo lenye unaweza kufanya ili umukaribie.—Mt. 6:19, 20.

6, 7. (a) Kujifunza Biblia kunakuwa na matokeo gani juu ya upendo wetu kwa Yehova na juu ya upendo wake kwetu? (b) Tunapaswa kuwa na kusudi gani kubwa wakati tunajifunza Biblia?

6 Kujifunza Biblia kunatusaidia kujua jambo lenye tunaweza kufanya ili tuendelee kiroho, lakini pia kunatusaidia katika mambo mengine. Kunatusaidia tufurahie zaidi njia za Yehova zenye kuvutia, na hilo linatuchochea tumupende tena zaidi. Na wakati upendo wetu kwa Yehova unakomaa, yeye pia anatupenda zaidi; na hilo linafanya urafiki wetu pamoja naye ukuwe wenye nguvu zaidi.—Soma 1 Wakorintho 8:3.

7 Lakini, ili tumukaribie Yehova, ni lazima tujue sababu gani tunajifunza Neno lake. Andiko la Yohana 17:3 linasema hivi: ‘Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’ Wakati tunasoma Biblia tunaweza kujifunza mambo mengi mapya na yenye kufurahisha, lakini kusudi letu kubwa linapaswa kuwa kufikia ‘kumujua’ Yehova muzuri zaidi kuwa mutu wa kweli kabisa.—Soma Kutoka 33:13; Zab. 25:4.

8. (a) Kulingana na andiko la 2 Wafalme 15:1-5, watu fulani wanaweza kufikiri nini kuhusu namna Yehova alimutendea Mufalme Azaria? (b) Namna gani kumujua Yehova vizuri kunatusaidia tusikuwe na mashaka kuhusu njia zake?

8 Wakati tunafikia kuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova, hatutavurugika sana ikiwa habari fulani zenye kuzungumuziwa katika Biblia hazituelezee sababu gani Yehova alitenda kwa njia fulani. Kwa mufano, unawaza nini kuhusu namna Yehova alimutendea Mufalme Azaria wa Yuda? (2 Fal. 15:1-5) Ujue kwamba, hata kama ‘watu walikuwa bado wanatoa zabihu na kufukiza moshi wa zabihu katika mahali pa juu,’ Mufalme Azaria mwenyewe ‘aliendelea kufanya yaliyokuwa manyoofu [mazuri] machoni pa Yehova.’ Lakini, ‘Yehova alimuletea mufalme pigo, naye akaendelea kuwa mwenye ukoma mupaka siku ya kufa kwake.’ Sababu gani? Habari hiyo haiseme jambo lolote. Jambo hilo linapaswa kutuvuruga ao kutufanya tuanze kufikiri kwamba Yehova alimupatia Mufalme Azaria malipizi bila sababu? Ikiwa tunajua vizuri njia za Yehova, hatutavurugika na kujiuliza maulizo mengi. Njia moja ni kwamba sikuzote Yehova analeta malipizi “kwa kiwango [kipimo] kinachofaa.” (Yer. 30:11) Kujua njia hizo, kunatusadikisha kwamba, hata kama hatujue sababu gani Yehova alimupatia Mufalme Azaria malipizi, tunaweza kuwa hakika kwamba hukumu Yake ilikuwa ya haki.

9. Ni nini inatusaidia kuelewa vizuri sababu gani Yehova alimupiga Mufalme Azaria kwa ugonjwa wa ukoma?

9 Hata hivyo, kitabu kingine cha Biblia kinatoa maelezo mengine kuhusu Mufalme Azaria. Mufalme Azaria aliitwa pia Mufalme Uzia. (2 Fal. 15:7, 32) Maelezo mengine juu ya Mufalme Azaria inapatikana katika kitabu cha 2 Mambo ya Nyakati 26:3-5, 16-21, na inaonyesha kwamba, hata kama wakati fulani Uzia alifanya mambo yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, baadaye katika maisha yake ‘moyo wake ulikuwa na majivuno hata kufikia hatua ya kusababisha uharibifu [wake mwenyewe].’ Kwa sababu ya kimbelembele, alijaribu kufanya kazi yenye ilipaswa kufanywa na makuhani tu. Makuhani 81 walimuambia kwamba hakuruhusiwa kufanya kazi hiyo na walijikaza kumukataza. Uzia alitenda namna gani? Alionyesha kwamba alikuwa amekuwa mwenye kiburi sana. ‘Alikuwa na gazabu [hasira]’ juu ya makuhani. Ndiyo sababu Yehova alimupiga kwa ugonjwa wa ukoma!

10. Sababu gani hatuhitaji kila mara Yehova atufasirie kila jambo lenye anafanya, na ni nini inaweza kutusaidia kuwa hakika kabisa kwamba njia za Yehova ni za haki?

10 Tunajifunza jambo gani la lazima? Wazia kwamba Neno la Mungu halikuwa na maelezo zaidi yenye ingetusaidia kuelewa habari hiyo, kama habari zingine za Biblia zenye kuzungumuziwa kwa kifupi. Ungekuwa na mashaka juu ya haki ya Mungu? Ao ungefikiri kwamba Biblia iko na habari zaidi zenye zinakuhakikishia kwamba sikuzote Yehova anafanya yaliyo sawa, na kwamba yeye ndiye chanzo cha kanuni za mema na mabaya? (Kum. 32:4) Wakati tunafikia kumujua Yehova vizuri zaidi kuwa mutu wa kweli kabisa, tutapenda na kufurahia zaidi njia zake; na kwa hiyo, haitakuwa lazima atufasirie kila jambo lenye anafanya. Ukuwe hakika kwamba utafurahia zaidi njia za Yehova ikiwa unaendelea kujifunza na kufikiri sana juu ya Neno lake, ni kusema, njia yenye anatumia ili kuzungumuza na wewe. (Zab. 77:12, 13) Kwa hiyo, urafiki wako pamoja na Yehova utakuwa wenye nguvu zaidi, na utamuona kuwa mutu wa kweli kabisa.

WEWE UNAZUNGUMUZA NA YEHOVA KUPITIA SALA

11-13. Ni nini inaonyesha kwamba Yehova anasikiliza sala? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

11 Tunamukaribia Yehova wakati tunasali. Kupitia sala tunamusifu, tunamushukuru, na tunatafuta muongozo wake. (Zab. 32:8) Lakini, ili urafiki wako pamoja na Yehova ukuwe wa kweli, unapaswa kuwa hakika kwamba anasikiliza sala zako.

12 Watu fulani wanaamini kwamba sala inasaidia tu kutuliza akili. Wanasema kwamba sala inakusaidia tu ufikirie kwa uangalifu magumu yako na kutafuta njia za kumaliza magumu hayo. Ni kweli kwamba sala inaweza kukusaidia katika njia hizo. Lakini, namna gani unaweza kuwa hakika kwamba Yehova anasikiliza kabisa sala zako zenye kutoka moyoni?

13 Fikiria jambo hili: Wakati Yesu alikuwa mbinguni, alijionea namna Yehova alikuwa anajibia sala za watumishi Wake wenye kuwa duniani. Kisha, wakati alikuwa hapa duniani, Yesu alikuwa anatumia sala ili kuzungumuza na Baba yake wa mbinguni. Kupitia sala alimuelezea namna alijisikia. Wakati fulani, Yesu alisali hata usiku muzima. Angefanya hivyo, ikiwa alijua kwamba Yehova hakuwa kabisa anasikiliza sala zake? (Lu. 6:12; 22:40-46) Angewafundisha wanafunzi wake namna ya kusali ikiwa alijua kwamba sala inasaidia tu kutuliza akili? Bila shaka, Yesu alijua kwamba sala ni njia ya kuzungumuza kabisa na Yehova. Wakati fulani, Yesu alisali hivi: ‘Baba, ninakushukuru kwamba umenisikia. Kweli, nilijua kwamba sikuzote wewe unanisikia.’ Sisi pia tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova ni ‘musikiaji wa sala.’—Yoh. 11:41, 42; Zab. 65:2.

14, 15. (a) Tunapata faida gani wakati tunakuwa wazi katika sala zetu? (b) Namna gani sala zilimusaidia dada mumoja afanye urafiki wake pamoja na Yehova ukuwe wenye nguvu zaidi?

14 Ikiwa sala zako ziko wazi, hilo litakusaidia utambue waziwazi namna Yehova anajibia sala hizo, hata kama wakati fulani majibu hayaonekane wazi. Wakati Yehova anajibia sala zako, hilo linakusaidia umuone kuwa mutu wa kweli kabisa. Zaidi ya hilo, Yehova atakukaribia zaidi kadiri unaendelea kumuelezea kila jambo lenye kukuhangaisha katika moyo wako.

15 Tuone mufano wa dada Kathy. * Mwanzoni, hakupendezwa kabisa na kazi ya kuhubiri, hata kama alikuwa anahubiri kwa ukawaida. Anasema hivi: “Sikupenda kazi ya kuhubiri. Kusema kweli, sikuipenda kabisa. Wakati niliacha kazi yangu ya kimwili kwa sababu ya miaka, muzee mumoja aliniambia kwamba inawezekana nikuwe painia wa kawaida; alinipatia hata fomu ya kuwa painia. Nikaamua kuwa painia, lakini pia nilianza kusali kila siku ili Yehova anisaidie nipende kazi ya kuhubiri.” Yehova alijibu sala za dada huyo? Dada Kathy anasema hivi: “Huu ni mwaka wangu wa tatu katika kazi ya upainia. Kwa sababu ninapitisha wakati mwingi katika mahubiri na ninaiga mufano wa dada wengine, hilo limenisaidia kukomalisha hatua kwa hatua ufundi wangu wa kuhubiri. Sasa, ninapenda sana kazi ya kuhubiri. Jambo la maana zaidi, ni kwamba nimekuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova kuliko zamani.” Kwa kweli, sala za dada Kathy zilimusaidia aone urafiki wake pamoja na Yehova kuwa wa kweli kabisa.

FANYA HATUA YA KWANZA

16 Tunapaswa kuendelea kukomalisha urafiki wetu pamoja na Yehova katika maisha yetu yote. Ikiwa tunapenda Mungu atukaribie, tunapaswa kufanya hatua ya kwanza ili kumukaribia. Kwa hiyo, tuendelee kuzungumuza kwa ukawaida na Mungu wetu kupitia funzo la Biblia na kupitia sala. Tukifanya hivyo, urafiki wetu pamoja na Yehova utaendelea kuwa wenye nguvu zaidi na hilo litatusaidia kupambana vizuri na magumu yetu.

Tunapaswa kuendelea kukomalisha urafiki wetu pamoja na Yehova katika maisha yetu yote (Ona fungu la 16, 17)

16, 17. (a) Tunapaswa kufanya nini ili urafiki wetu pamoja na Yehova uendelee kuwa wenye nguvu zaidi? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Wakati fulani magumu yetu yanaweza kuendelea hata kama tunasali kwa bidii, na hilo linaweza kuwa tatizo kwetu. Katika nyakati kama hizo, tunaweza kuanza kukosa kumutumainia Yehova. Tunaweza kuanza kujiuliza ikiwa kwa kweli Yehova anasikiliza sala zetu ao ikiwa yeye angali rafiki yetu. Unaweza kufanya nini ikiwa umeanza kufikiri hivyo? Habari yenye kufuata itazungumuzia jambo hilo.

^ fu. 2 Urafiki ni namna watu wawili wanajisikia kuhusu kila mumoja na namna wote wawili wanatendeana. Kwa hiyo, wote wanapaswa kufanya jambo fulani ili urafiki wao uendelee kuwa wenye nguvu.

^ fu. 15 Majina fulani yamebadilishwa.