Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wazee, Munaona Namna Gani Kazi ya Kuzoeza Wengine?

Wazee, Munaona Namna Gani Kazi ya Kuzoeza Wengine?

“Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu.” MHU. 3:1.

1, 2. Waangalizi wengi wa muzunguko wameona hali gani katika makutaniko mengi?

MWANGALIZI wa muzunguko anakaribia kumaliza mukutano wake pamoja na baraza la wazee. Wakati anawaangalia, anaonyesha kwamba anawapenda sana wazee hao wenye bidii. Wamoja kati yao walikuwa wamekomaa sana, wangeweza kuwa hata na miaka ya baba yake. Lakini, jambo fulani linamuhangaisha; kwa hiyo anawauliza hivi: “Ndugu, mumefanya nini ili kuzoeza wengine wakuwe na mengi zaidi ya kufanya katika kutaniko?” Wakakumbuka kwamba wakati mwangalizi huyo alitembelea kutaniko lao wakati uliopita, aliwaomba wajikaze sana ili kuzoeza wengine. Mwishowe, muzee mumoja akasema hivi: “Kusema kweli, hatukufanya kabisa vile ulituambia.” Wazee wengine wakakubaliana naye.

2 Ikiwa uko muzee wa kutaniko, pengine wewe pia ungejibu kama muzee huyo. Katika dunia yote, waangalizi wa muzunguko wameona kwamba, katika makutaniko mengi, kuna lazima kubwa ya kuzoeza ndugu, iwe ni vijana ao wenye kukomaa, ili walichunge kundi. Lakini kufanya hivyo kuna magumu fulani. Sababu gani?

3. (a) Namna gani Maandiko yanaonyesha kwamba ni lazima kuzoeza wengine, na sababu gani kila mumoja wetu anapaswa kufikiria jambo hilo? (Ona maelezo ya chini.) (b) Sababu gani wazee fulani wanaweza kuona kwamba ni vigumu kuzoeza wengine?

3 Ikiwa wewe ni muchungaji, bila shaka umetambua kwamba ni jambo la lazima sana kuzoeza wengine. * Unajua kwamba ndugu wengi wanahitajiwa ili wasaidie makutaniko yaendelee kuwa nguvu kiroho na kuanzisha makutaniko mengine. (Soma Isaya 60:22.) Pia, unajua kwamba, Neno la Mungu linakuomba ‘uwafundishe wengine.’ (Soma 2 Timotheo 2:2.) Hata hivyo, kama wazee wenye tumezungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii, unaweza kuona kwamba ni vigumu kuzoeza wengine. Kisha kutimiza mahitaji ya familia, mambo ya kazi, madaraka mbalimbali katika kutaniko, na mambo mengine yenye inaomba kufanywa haraka, unaweza kuona kwamba hauna tena wakati wa kuzoeza wengine. Hata hivyo, tuone sababu gani ni jambo la lazima kuzoeza wengine.

UTIE KAZI YA KUZOEZA WENGINE PA NAFASI YA KWANZA

4. Toa sababu moja yenye inaweza kufanya wazee fulani waache kwanza kuzoeza wengine.

4 Sababu gani wazee fulani wanaweza kuona kwamba ni vigumu kupata wakati wa kuzoeza wengine? Wanaweza kufikiri hivi: ‘Ni jambo la lazima kuzoeza wengine, lakini haiko jambo la haraka sana kama mambo mengine ya kutaniko. Ikiwa ninaacha kwanza kuzoeza wengine, kutaniko litaendelea tu vizuri.’ Ni kweli, mambo mengi inaomba kushugulikiwa haraka. Lakini kuacha kwanza kuzoeza wengine kunaweza kuharibu hali ya kiroho ya kutaniko.

5, 6. Mufano wa mutembezaji wa motokari na namna anaona kazi ya kutunza motere, unaweza kutufundisha nini, na namna gani hilo linaweza kuhusu mazoezi yenye ndugu wanapokea katika kutaniko?

5 Fikiria mufano huu: Mutembezaji wa motokari anajua kwamba, ili motokari yake iendelee kutumika muzuri, anapaswa kubadilisha mafuta kwa ukawaida. Lakini anaweza kufikiri kwamba kubadilisha mafuta ya motere haiko jambo la haraka sana sawa vile kujaza mazuti ao esanse katika motokari. Bila shaka, ikiwa hatie mazuti ao esanse katika motokari yake, itazimika na kuacha kutembea. Anaweza kufikiri hivi: ‘Hata kama sina wakati wa kubadilisha mafuta, motokari yangu itaendelea kutembea kwa wakati fulani.’ Lakini kufanya hivyo kunaweza kuleta hatari gani? Ikiwa mutembezaji wa motokari anaendelea kusema kwamba atatunza motokari yake wakati mwingine, siku moja motokari hiyo itaharibika sana. Na ikiwa motokari hiyo inaharibika sana, atatumia wakati na feza nyingi ili kuitengeneza. Mufano huo unatufundisha nini?

6 Wazee wanafanya kazi nyingi za lazima zenye zinaombwa kushugulikiwa haraka; ikiwa hawafanye hivyo, kutaniko linaweza kuwa katika hali mbaya. Kwa hiyo, kama vile tu mutembezaji anahakikisha kwamba tanki ya motokari yake inajaa mazuti ao esanse, wazee pia wanapaswa ‘kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Flp. 1:10) Hata hivyo, wazee fulani wanahangaikia sana mambo yenye inahitaji kushugulikiwa haraka, mupaka wanafikia kukosa wakati wa kuzoeza wengine; kufanya hivyo, ni kama vile kukosa kutunza motere ya motokari. Lakini, ikiwa kila mara wazee wanaacha kwanza kuzoeza wengine, mwishowe kutaniko litakosa ndugu wenye kustahili ili kushugulikia mambo mbalimbali.

7. Tunapaswa kuona namna gani wazee wenye wanachukua wakati ili kuzoeza wengine?

7 Ndiyo sababu wazee wanapaswa kuwa waangalifu ili wasifikiri kwamba kuzoeza wengine haiko jambo la lazima sana. Wazee wenye kufikiria wakati unaokuja na kutumia wakati wao ili kuzoeza ndugu wenye hawana uzoefu mwingi ni wasimamizi-nyumba wenye hekima na ni baraka kabisa kwa kutaniko lote. (Soma 1 Petro 4:10.) Kutaniko linafaidika namna gani?

UTUMIE WAKATI KWA HEKIMA

8. (a) Sababu gani wazee wanapaswa kuzoeza wengine? (b) Wazee wenye kutumikia mahali penye kuwa lazima kubwa wako na daraka gani la haraka? (Ona kisanduku “ Daraka Kubwa Sana.”)

8 Hata wazee wenye uzoefu mwingi zaidi wanapaswa kuwa wanyenyekevu na kuelewa kwamba kadiri wanaendelea kukomaa, hawatakuwa tena na uwezo wa kutimiza kabisa mambo yenye wanafanya sasa katika kutaniko. (Mika 6:8) Pia, wanapaswa kujua kwamba “wakati na tukio lisilotazamiwa” linaweza kuleta mabadiliko ya bila kutazamia na kufanya ikuwe vigumu kwao kutimiza madaraka yao katika kutaniko. (Mhu. 9:11, 12; Yak. 4:13, 14) Wazee wenye kuhangaikia hali nzuri ya kondoo za Yehova, wanaelezea vijana Wakristo kwa wakati unaofaa mambo yenye wamejifunza kwa miaka mingi.—Soma Zaburi 71:17, 18.

9. Ni tukio gani la wakati unaokuja linafanya ikuwe jambo la lazima sana kuzoeza wengine?

9 Ni jambo gani lingine linaonyesha kwamba wazee wenye kuzoeza wengine ni baraka kwa kundi? Wanasaidia ndugu na dada katika kutaniko waendelee kuwa nguvu kiroho. Namna gani? Bidii yenye wazee wanafanya ili kuzoeza wengine inafanya ndugu wengi zaidi wakuwe tayari kusaidia kutaniko likuwe nguvu kiroho na lenye umoja tangu sasa, na zaidi sana wakati wa muvurugo mukubwa, ni kusema, wakati wa ziki kubwa. (Eze. 38:10-12; Mika 5:5, 6) Kwa hiyo, wazee wapendwa, tafazali, tunawaomba kuanzia leo mufanye kwa ukawaida kazi ya kuzoeza wengine.

10. Muzee anapaswa kufanya nini ili apate wakati wa kuzoeza wengine?

10 Bila shaka, tunaelewa kwamba munatumia wakati mwingi sana ili kushugulikia kazi mbalimbali za lazima katika kutaniko, na hilo linaweza kuwafanya mujisikie kuwa wenye kuchoka sana. Lakini, ni jambo la lazima mutumie sehemu fulani ya wakati huo ili kuzoeza wengine. (Mhu. 3:1) Kufanya hivyo ni kutumia wakati kwa hekima.

UTAYARISHE MOYO WA MWANAFUNZI

11. (a) Ni jambo gani lenye kupendeza kuhusu mapendekezo yenye wazee wa inchi mbalimbali walitoa? (b) Kulingana na Methali 15:22, sababu gani itakuwa jambo la lazima kuchunguza mapendekezo ya wazee wengine?

11 Hivi karibuni, wazee fulani wenye wamepata matokeo mazuri kwa kusaidia ndugu wakomae kiroho waliulizwa ni njia gani wanatumia ili kuzoeza wengine. * Hata kama hali zao zinaachana sana, walitoa mapendekezo yenye kufanana sana. Hilo linaonyesha nini? Linaonyesha kwamba mazoezi yenye kutegemea Biblia inahusu wanafunzi wa “kila mahali katika kila kutaniko,” kama vile ilikuwa katika siku za mutume Paulo. (1 Kor. 4:17) Katika habari hii na ile yenye kufuata, tutachunguza mapendekezo fulani ya wazee hao. (Met. 15:22) Pia, tutatumia neno “walimu” ili kuzungumuzia wale wenye kutoa mazoezi, na neno “wanafunzi” ili kuzungumuzia wale wenye kupokea mazoezi.

12. Mwalimu anapaswa kutayarisha nini, na sababu gani?

12 Mwalimu anapaswa kutayarisha moyo wa mwanafunzi mbele ya kumuzoeza. Mulimaji anapaswa kulima, ao kuregeza udongo mbele apande mbegu; vilevile, mwalimu anapaswa kutayarisha moyo wa mwanafunzi mbele ya kumufundisha ufundi mupya. Kwa hiyo, namna gani mwalimu anaweza kutayarisha moyo wa mwanafunzi? Kwa kufuata njia yenye nabii fulani wa zamani alitumia. Nabii huyo alitumia njia gani?

13-15. (a) Nabii Samweli alipewa mugawo gani? (b) Namna gani nabii Samweli alitimiza mugawo wake? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (c) Sababu gani leo wazee wanaweza kufaidika sana na habari ya Biblia kuhusu nabii Samweli?

13 Kumepita zaidi ya miaka 3000, tangu Yehova alizungumuza na Samweli, nabii mwenye kuzeeka na kumuambia hivi: ‘Karibu wakati kama huu kesho nitatuma mutu kwako kutoka katika inchi ya Benyamini. Nawe umutie mafuta akuwe kiongozi juu ya watu wangu Israeli.’ (1 Sam. 9:15, 16) Nabii Samweli alielewa kwamba daraka lake la kuongoza Waisraeli lilikuwa limefikia mwisho na kwamba Yehova amemupatia kazi ya kumutia mafuta mutu mwenye atachukua nafasi yake. Pengine nabii Samweli alijiuliza hivi: ‘Namna gani ninaweza kutayarisha mutu huyo kwa ajili ya daraka hilo?’ Alipata wazo fulani na kisha alipanga namna ya kulitimiza.

14 Siku yenye ilifuata, wakati nabii Samweli alimuona Sauli, Yehova alimuambia hivi: ‘Huyu ndiye mutu.’ Kisha, nabii Samweli alifanya kulingana na namna alikuwa amepanga. Alimualika Sauli ili wakule chakula pamoja katika chumba cha kukulia. Kisha akamupatia Sauli na mutumishi wake viti vizuri vya kuikalia na sehemu nzuri sana ya nyama na kumuambia hivi: ‘Ukule, kwa maana wamekuwekea hicho akiba mupaka wakati uliowekwa.’ Kisha, Sauli na nabii Samweli wakatembea pamoja na kuzungumuza mupaka walifika katika nyumba ya nabii Samweli. Nabii Samweli alipenda kutumia vizuri hali hiyo yenye kufaa kabisa ambayo ilitokezwa wakati wa chakula na wakati wa matembezi yenye kufurahisha. Kwa hiyo, akamuomba Sauli wapande kwenye sehemu ya juu ya nyumba yake. Katika hewa yenye baridi ya mangaribi, Samweli “akaendelea kusema na Sauli darini [sehemu ya juu ya nyumba]” mupaka wakati walienda kulala. Siku yenye ilifuata, Samweli akamutia Sauli mafuta, akamukumbatia, na kumupatia maagizo mengi zaidi. Kisha, akamuacha Sauli aende. Wakati huo, Sauli alikuwa ametayarishwa kwa ajili ya mambo yenye ilikuwa mbele yake.—1 Sam. 9:17-27; 10:1.

15 Bila shaka, kumutia mafuta mutu ili akuwe kiongozi wa taifa ni tofauti kabisa na kuzoeza ndugu ili akuwe muzee ao mutumishi wa huduma katika kutaniko. Hata hivyo, mufano wa nabii Samweli unaweza kufundisha wazee wa leo mambo mengi sana ya lazima. Tuchunguze sasa mambo mawili tu kati ya mambo hayo.

WALIMU WENYE KUWA TAYARI NA MARAFIKI WA KWELI

16. (a) Samweli alijisikia namna gani wakati Waisraeli waliomba mufalme? (b) Samweli alijisikia namna gani wakati Yehova alimuambia amutie Sauli mafuta?

16 Ukuwe tayari, lakini usisite kuzoeza wengine. Wakati nabii Samweli alisikia kwa mara ya kwanza kwamba Waisraeli walipenda wakuwe na mufalme mwanadamu, alivunjika moyo na alijisikia kuwa wamemukataa. (1 Sam. 8:4-8) Kwa hiyo, alisita kufanya jambo lenye watu walikuwa wamemuomba mupaka Yehova aliona kuwa ni lazima amuambie mara tatu kwamba asikilize sauti yao. (1 Sam. 8:7, 9, 22) Hata hivyo, Samweli hakusikia uchungu ao kumuwekea kinyongo mutu mwenye angechukua nafasi yake. Wakati Yehova alimuambia nabii Samweli amutie Sauli mafuta, nabii Samweli hakutii kwa sababu tu alipaswa kutii, lakini kwa sababu alimupenda Yehova.

17. Namna gani leo wazee wanafuata mufano wa nabii Samweli, na hilo linawaletea faida gani?

17 Leo, wazee wenye uzoefu wanafuata mufano wa nabii Samweli kwa kuzoeza wengine kwa upendo. (1 Pet. 5:2) Wazee kama hao hawakatae kuzoeza wengine kwa kuogopa kwamba wanafunzi hao watachukua mapendeleo yao fulani katika kutaniko. Walimu wazuri hawaone wanafunzi wenye kufanya maendeleo kuwa ndugu wenye kufanya mashindano pamoja nao, lakini wanawaona kama ‘wafanyakazi wenzao,’ ni kusema, zawadi ya bei sana kwa ajili ya kutaniko. (2 Kor. 1:24; Ebr. 13:16) Walimu hao wenye upendo wanafurahi sana wakati wanaona namna wanafunzi hao wanatumia uwezo wao kwa faida ya ndugu na dada katika kutaniko.—Mdo. 20:35.

18, 19. Namna gani muzee anaweza kutayarisha moyo wa mwanafunzi, na sababu gani ni jambo la lazima kutumia njia hiyo?

18 Ukuwe rafiki, lakini usikuwe mwalimu tu. Wakati nabii Samweli alikutana na Sauli, angechukua chupa ya mafuta, na kumumwangia mbio-mbio kwenye kichwa. Sauli angeenda kuwa mufalme mwenye mamlaka bila kupewa mazoezi fulani. Lakini, kwa upendo nabii Samweli alichukua wakati ili kutayarisha pole-pole moyo wa Sauli. Kisha kula pamoja chakula kitamu, kufanya matembezi yenye kufurahisha, kuongea kwa muda murefu pamoja naye, na kupumuzika vizuri, nabii Samweli aliona kwamba wakati ulikuwa umefika ili kumutia Sauli mafuta.

Ni lazima kufanya urafiki na mwanafunzi mbele ya kuanza kumuzoeza(Ona fungu la 18, 19)

19 Vilevile, leo walimu wanapaswa kuanza mazoezi kwa kuchukua wakati wa kutafuta nafasi yenye kufaa ili kufanya urafiki pamoja na mwanafunzi. Mambo mbalimbali yenye muzee anaweza kufanya ili kuwa na urafiki pamoja na mwanafunzi, inategemea hali za inchi, eneo, na tabia za watu. Lakini, iwe unaishi wapi, na hata kama uko na kazi nyingi za kufanya katika kutaniko, ikiwa unapitisha wakati pamoja na mwanafunzi, ni kama vile unamuambia hivi: “Ninakuona kuwa wa lazima.” (Soma Waroma 12:10.) Bila shaka, wanafunzi wa kila mahali watakuwa wenye shukrani sana kwa sababu munawahangaikia kwa upendo.

20, 21. (a) Mwalimu mwenye kupata matokeo mazuri anafanya nini? (b) Tutachunguza nini katika habari yenye kufuata?

20 Wazee, mukumbuke kwamba, mwalimu mwenye kupata matokeo mazuri haonyeshe tu kwamba anapenda kuzoeza mwanafunzi, lakini anaonyesha pia kwamba anamupenda mwanafunzi. (Linganisha na Yohana 5:20.) Mwanafunzi anatambua haraka sifa hiyo ya lazima ya mwalimu, na hilo linamufanya afurahie sana mazoezi yenye anapewa. Kwa hiyo, wazee wapendwa, wakati munazoeza wengine, mukuwe marafiki, lakini musikuwe walimu tu.—Met. 17:17; Yoh. 15:15.

21 Kisha kutayarisha moyo wa mwanafunzi, muzee anapaswa sasa kumufundisha ufundi mbalimbali wenye anahitaji. Muzee anapaswa kutumia njia gani? Tutachunguza njia hizo katika habari yenye kufuata.

^ fu. 3 Habari hii na ile yenye kufuata zimetayarishwa zaidi sana kwa ajili ya wazee. Hata hivyo, zinahusu wote katika kutaniko. Sababu gani? Kwa sababu zitasaidia wanaume wote wenye kubatizwa waelewe kwamba wanapaswa kuzoezwa ili wafanye mengi zaidi katika kutaniko. Ikiwa wanapata mazoezi, kila mutu katika kutaniko atafaidika.

^ fu. 11 Wazee hao wanaishi katika inchi ya Afrika ya Kusini, Australia, Bangladesh, Belgique, Brazili, États-Unis, Guiana ya Ufaransa, Japani, Korea, Meksiko, Namibia, Nigeria, Réunion, Ufaransa, na Urusi.