Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Wazee Wanazoeza Wengine ili Wafikie Madaraka

Namna Wazee Wanazoeza Wengine ili Wafikie Madaraka

‘Mambo uliyoyasikia kutoka kwangu . . . , uwakabizi [uwatolee] watu waaminifu.’2 TIM. 2:2.

1. (a) Tangu zamani, watumishi wa Yehova wameelewa nini kuhusu kuzoeza wengine, na sababu gani jambo hilo ni lenye kufaa leo? (b) Tutachunguza nini katika habari hii?

TANGU zamani, watumishi wa Yehova wameelewa kwamba kuzoeza wengine kunaleta matokeo mazuri. Muzee wa ukoo Abramu ‘alikusanya watu wake waliozoezwa’ ili kumukomboa Loti, na watu hao walipata matokeo mazuri. (Mwa. 14:14-16) Katika siku za Mufalme Daudi, waimbaji wa nyumba ya Mungu ‘walizoezwa nyimbo kwa Yehova’ ili kumuletea Mungu sifa. (1 Nya. 25:7) Leo, tunapigana vita ya kiroho na Shetani pamoja na wafuasi wake. (Efe. 6:11-13) Pia, tunajikaza ili kumuletea Yehova sifa. (Ebr. 13:15, 16) Kwa hiyo, kama watumishi wa Mungu wa zamani, tunapaswa kuzoezwa ili tupate matokeo mazuri. Yehova amewapatia wazee daraka la kuzoeza wengine. (2 Tim. 2:2) Wazee wenye uzoefu wanatumia njia gani ili kuzoeza ndugu wastahili kushugulikia kundi?

UMUSAIDIE MWANAFUNZI AMUPENDE YEHOVA SANA

2. Mbele ya kufundisha mwanafunzi ufundi fulani, muzee anaweza kufanya nini, na sababu gani?

2 Muzee anaweza kufananishwa na mulimaji. Mbele ya kupanda mbegu, mulimaji anaweza kuona kwamba ni lazima aongeze mbolea katika udongo ili kuufanya utoe mavuno mengi. Vilevile, mbele ya kufundisha mwanafunzi ufundi fulani, unaweza kutambua kwamba ni lazima kuzungumuzia maandiko fulani pamoja naye ili kuchochea moyo wake na kuufanya ukuwe tayari kupokea mazoezi.—1 Tim. 4:6.

3. (a) Namna gani muzee anaweza kutumia maneno ya Yesu katika Marko 12:29, 30 wakati anazungumuza na mwanafunzi? (b) Sala yenye muzee anatoa inaweza kuwa na matokeo gani juu ya mwanafunzi?

3 Ili kujua ni kwa kadiri gani kweli ya Ufalme imechochea mawazo na matendo ya mwanafunzi, unaweza kumuuliza hivi: ‘Namna gani kujitoa kwa Yehova kumebadilisha namna unatumia maisha yako?’ Ulizo hilo linaweza kusaidia kuanzisha mazungumuzo mazuri kuhusu namna tunaweza kumutumikia Yehova kwa moyo wetu wote. (Soma Marko 12:29, 30.) Pengine, kisha mazungumuzo, unaweza kusali pamoja na mwanafunzi ili kumuomba Yehova amupatie roho takatifu ili imusaidie kufaidika kabisa na mazoezi yenye anapata. Ndugu huyo atatiwa moyo sana kwa kusikia unasali kwa moyo wote kwa ajili yake!

4. (a) Ni habari gani za Biblia zinaweza kumuchochea mwanafunzi afanye maendeleo ya kiroho. (b) Wazee wana kusudi gani kubwa wakati wanazoeza wengine?

4 Wakati unaanza kuzoeza mwanafunzi, muzungumuzie habari fulani za Biblia zenye zinaweza kumusaidia aone kwamba ni lazima akuwe tayari kusaidia, mwenye kutegemeka, na munyenyekevu. (1 Fal. 19:19-21; Neh. 7:2; 13:13; Mdo. 18:24-26) Sifa hizo ni za lazima sana kwa mwanafunzi kama vile mbolea ni ya maana sana kwa udongo. Sifa hizo zitamusaidia afanye maendeleo ya kiroho mbio-mbio. Jean-Claude, muzee katika kutaniko moja la Ufaransa, anasema hivi: “Wakati ninazoeza mwanafunzi, kusudi langu kubwa ni kumusaidia akomae kiroho. Ninatafuta nafasi ya kusoma andiko fulani pamoja naye ili ‘kufungua macho’ yake na kumusaidia aone ‘mambo ya ajabu’ yenye kupatikana katika Neno la Mungu.” (Zab. 119:18) Muzee anaweza kutumia njia gani zingine ili kumusaidia mwanafunzi afanye maendeleo ya kiroho?

UTOE MAPENDEKEZO NA UONYESHE SABABU

5. (a) Sababu gani ni jambo la lazima kuzungumuza na mwanafunzi kuhusu miradi yake ya kiroho? (b) Sababu gani wazee wanapaswa kuzoeza ndugu wenye wangali vijana? (Ona maelezo ya chini.)

5 Umuulize mwanafunzi hivi: ‘Uko na miradi gani ya kiroho?’ Ikiwa hana muradi fulani wa kiroho, umusaidie ajiwekee muradi wenye kupatana na uwezo wake na wenye anaweza kufikia. Umuambie muradi fulani wa kiroho wenye ulijiwekea hapo zamani, na umuelezee kwa kuchangamuka furaha kubwa yenye ulipata wakati ulifikia muradi huo. Njia hiyo yenye kuonekana kuwa mwepesi inaleta matokeo mazuri. Victor, muzee na painia huko Afrika, anakumbuka: “Wakati nilikuwa kijana, muzee mumoja aliniuliza maulizo fulani yenye kuchaguliwa vizuri juu ya miradi yangu ya kiroho. Maulizo hayo ilinisaidia nianze kufikiri sana juu ya hali ya utumishi wangu kwa Mungu.” Wazee wenye uzoefu wanaonyesha kwamba ni lazima sana kuanza kuzoeza ndugu wakati wangali vijana, kwa kuwapatia kazi mbalimbali katika kutaniko zenye kulingana na miaka yao. Kuwazoeza wakati wangali vijana kutawasaidia wakazie akili yao juu ya miradi ya kiroho kwa sababu wakati wanaendelea kukomaa, wanakuwa na mambo mengi yenye inaweza kuwakengeusha wasifuatilie miradi yao ya kiroho.—Soma Zaburi 71:5, 17. *

Umufasirie mwanafunzi sababu gani kazi fulani inapaswa kufanywa, na umupongeze kwa bidii yenye anafanya ili kutimiza kazi hiyo (Ona fungu la 5-8)

6. Yesu alitumia njia gani nzuri ili kuwazoeza mitume wake?

6 Unaweza pia kumuchochea mwanafunzi akuwe na hamu ya kutumikia kutaniko wakati unamufasiria mambo yenye anapaswa kufanya, na sababu gani. Unamuiga Yesu, Mwalimu Mukubwa, wakati unamufasiria mwanafunzi sababu gani anapaswa kufanya kazi fulani. Kwa mufano, mbele Yesu awapatie mitume amri ya kufanya wanafunzi, alionyesha sababu gani walipaswa kutii. Aliwaambia hivi: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.” Kisha aliongeza hivi: ‘Kwa hiyo muende mukafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mt. 28:18, 19) Namna gani muzee anaweza kuiga njia yenye Yesu alitumia ili kuzoeza mitume wake?

7, 8. (a) Namna gani leo wazee wanaweza kuiga njia yenye Yesu alitumia ili kuzoeza mitume wake? (b) Sababu gani ni jambo la lazima kumupongeza mwanafunzi? (c) Ni mapendekezo gani inaweza kusaidia wazee wakati wanazoeza wengine? (Ona kisanduku “ Namna ya Kuzoeza wengine,” kwenye ukurasa wa 8.)

7 Umufasirie mwanafunzi sababu gani Maandiko inaomba kufanya kazi fulani. Kwa kufanya hivyo, unamufundisha kufikiri kulingana na kanuni za Biblia. Kwa mufano, unaomba ndugu fulani afanye kazi fulani kwenye Jumba la Ufalme; kama vile kusafisha njia yenye kuenda kwenye Jumba la Ufalme. Unaweza kuchunguza pamoja naye andiko la Tito 2:10 na kumufasiria namna mugawo wake unasaidia ‘kulipamba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu.’ Pia, umuombe mwanafunzi afikirie ndugu na dada wenye kuzeeka katika kutaniko na namna gani kutimiza mugawo wake kunaweza kuwaletea faida. Kuzungumuzia mambo hayo na mwanafunzi wakati wa mazoezi kutamusaidia afikirie sana watu kuliko kukazia sheria. Atafurahi sana kuona namna ndugu na dada katika kutaniko wanafaidika na kazi yenye anatimiza.

8 Zaidi ya hilo, ujikaze sana ili kumupongeza mwanafunzi juu ya bidii yenye anafanya ili kutumikisha mapendekezo yenye unamutolea. Sababu gani ni jambo la lazima kumupongeza mwanafunzi? Kumupongeza kwa moyo wote kutamusaidia afanye maendeleo, kama vile kumuangia mumea maji kunasaidia uchipuke.—Linganisha na Mathayo 3:17.

TATIZO LINGINE

9. (a) Katika inchi tajiri, wazee wanapata tatizo gani wakati wanazoeza wengine? (b) Sababu gani vijana fulani hawatie kazi ya Mungu pa nafasi ya kwanza katika maisha yao?

9 Katika inchi tajiri, wazee wanaweza kupambana na tatizo lingine, ni kusema, wanajiuliza namna gani wanaweza kuchochea ndugu wenye kuwa na miaka kati ya 20 na 30 ili wasaidie katika kazi mbalimbali za kutaniko. Tuliuliza wazee wenye uzoefu wa inchi karibu 20 sababu gani wanafikiri kwamba ndugu fulani vijana hawaone kuwa ni lazima wafanye mengi zaidi katika kutaniko. Muzee mumoja alijibu hivi: Wakati walikuwa wangali wanakomaa, vijana fulani hawakutiwa moyo kujiwekea miradi ya kiroho. Na vijana wengine wenye walijiwekea miradi ya kiroho, wazazi wao waliwatia moyo wafuatilie miradi ya kimwili. Kwa hiyo, hawakutia kazi ya Mungu pa nafasi ya kwanza katika maisha yao.—Mt. 10:24.

10, 11. (a) Namna gani muzee anaweza kumusaidia polepole ndugu mwenye haone kuwa ni lazima kufikia madaraka abadilishe mawazo yake? (b) Muzee anaweza kuzungumuzia Maandiko gani pamoja na ndugu huyo, na sababu gani? (Ona maelezo ya chini.)

10 Ikiwa ndugu fulani haone kuwa ni lazima kufikia madaraka katika kutaniko, itaomba muzee mwenye kumuzoeza atumike sana, na kuonyesha uvumilivu. Na mwishowe mwanafunzi huyo anaweza kufikia kubadilisha mawazo yake. Kama vile mulimaji anaweza kunyorosha polepole mimea yake kwa kutumia miti ili kuitegemeza, wazee pia wanaweza hatua kwa hatua kusaidia ndugu fulani watambue kwamba ni lazima wabadilishe mawazo yao na wafikie kukubali mapendeleo katika kutaniko. Lakini, namna gani wazee wanaweza kufanya hivyo?

11 Muzee anaweza kujiwekea wakati wa kufanya urafiki pamoja na mwanafunzi. Umusaidie atambue kwamba kutaniko linahitaji musaada wake. Kisha muda fulani, muzungumuzie pamoja na mwanafunzi maandiko fulani yenye itamusaidia afikiri juu ya kujitoa kwake kwa Yehova. (Mhu. 5:4; Isa. 6:8; Mt. 6:24, 33; Lu. 9:57-62; 1 Kor. 15:58; 2 Kor. 5:15; 13:5) Unaweza kumuuliza hivi: ‘Wakati ulijitoa kwa Yehova katika sala, ulimuahidi nini?’ Ujikaze kugusa moyo wake kwa kumuuliza hivi: ‘Unawaza Yehova alijisikia namna gani wakati ulibatizwa?’ (Met. 27:11) ‘Na Shetani alijisikia namna gani?’ (1 Pet. 5:8) Usisahau hata kidogo kwamba, Maandiko yenye kuchaguliwa vizuri inaweza kugusa sana moyo wake.—Soma Waebrania 4:12. *

WANAFUNZI, MUONYESHE KWAMBA MUKO WAAMINIFU

12, 13. (a) Elisha alitenda namna gani wakati nabii Eliya alikuwa anamuzoeza? (b) Namna gani Yehova alimubariki Elisha kwa sababu ya uaminifu wake?

12 Vijana, kutaniko liko na lazima ya musaada wenu! Lakini, ni jambo gani litawasaidia mupate matokeo mazuri? Ili kupata jibu, tuchunguze mambo fulani katika maisha ya mwanafunzi mumoja wa zamani.

13 Kumepita miaka karibu 3000, tangu nabii Eliya alimuomba kijana Elisha akuwe mutumishi wake. Elisha alikubali bila kukawia na akaanza kumutumikia kwa uaminifu nabii huyo mwenye kuzeeka, kwa kufanya kazi za hali ya chini. (2 Fal. 3:11) Kisha miaka sita hivi ya mazoezi, Elisha alitambua kwamba kazi ya Eliya ya kutoa unabii katika Israeli ilikuwa karibu kumalizika. Kwa hiyo, nabii Eliya akamuomba mwanafunzi wake mwenye alikuwa amezoezwa vizuri aache kumufuata. Lakini Elisha alimuambia hivi nabii Eliya mara tatu: “Mimi sitakuacha.” Elisha alipenda aendelee kuwa pamoja na mwalimu wake. Kwa hiyo, Yehova alimubariki Elisha kwa sababu ya uaminifu na ushikamanifu wake. Alimuwezesha aone namna nabii Eliya anachukuliwa katika zoruba kwa njia yenye kushangaza.—2 Fal. 2:1-12.

14. (a) Namna gani leo wanafunzi wanaweza kuiga mufano wa Elisha? (b) Sababu gani ni jambo la lazima sana mwanafunzi akuwe mwaminifu?

14 Namna gani leo mwanafunzi anaweza kuiga mufano wa Elisha? Kwa kukubali bila kukawia kufanya kazi, hata zile za hali ya chini. Umuone mwalimu wako kuwa rafiki yako, na umuambie kwamba unafurahia sana bidii yenye anafanya kwa ajili yako. Namna unatenda wakati anakuzoeza ni kama vile unamuambia hivi: “Mimi sitakuacha.” Zaidi ya yote, ufanye kwa uaminifu kazi yoyote yenye unapewa. Sababu gani ni jambo la lazima kufanya hivyo? Kwa sababu wazee watakuwa hakika kwamba Yehova anapenda upewe madaraka mengi zaidi katika kutaniko, wakati tu unaonyesha kwamba uko mwaminifu na mwenye kutegemeka.—Zab. 101:6; soma 2 Timotheo 2:2.

UWAHESHIMU WAZEE WENYE KUKUZOEZA

15, 16. (a) Ni katika njia gani Elisha alionyesha kwamba alimuheshimu mwalimu wake? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Namna gani Elisha alifanya manabii wenzake wamutumainie?

15 Habari ya Elisha, mwenye alichukua nafasi ya nabii Eliya, inaonyesha pia namna leo ndugu wanaweza kuonyesha kwamba wanawaheshimu wazee wenye uzoefu. Kisha nabii Eliya na Elisha kutembelea kikundi fulani cha manabii katika muji wa Yeriko, wanaume hao wawili walienda pamoja kuelekea Muto Yordani. Kwenye muto huo, ‘Eliya alichukua vazi lake rasmi, akalifunga, akapiga maji, nayo mwishowe yakagawanyika huku na huku.’ Kisha kuvuka muto kupitia udongo wenye kukauka, wanaume hao wakaendelea ‘kuzungumuza huku wakitembea.’ Ni wazi kwamba, Elisha hakufikiri hata kidogo kwamba wakati huo alikuwa amejua mambo yote. Elisha aliweka katika moyo wake kila neno mwalimu wake alimuambia mupaka wakati waliachana na nabii Eliya. Kisha Eliya akapanda katika zoruba ya upepo. Baadaye, wakati Elisha alifika kwenye Muto Yordani, akapiga maji kwa kutumia vazi la nabii Eliya, na kuita: ‘Iko wapi Yehova Mungu wa Eliya?’ Mara ingine tena, maji ikagawanyika.—2 Fal. 2:8-14.

16 Je, umetambua kwamba muujiza wa kwanza wa Elisha ulifanana kabisa na ule wa nabii Eliya? Sababu gani jambo hilo ni lenye kupendeza? Inaonekana kwamba, Elisha hakufikiri kama kwa sababu alikuwa amepewa mamlaka, alipaswa kufanya mambo vile anapenda. Kwa kufuata mufano wa nabii Eliya, Elisha alionyesha kwamba alimuheshimu mwalimu wake, na jambo hilo lilifanya manabii wenzake wamutumainie. (2 Fal. 2:15) Hata hivyo, katika miaka 60 yenye Elisha alifanya katika kazi ya kutoa unabii, Yehova alimupatia uwezo wa kufanya miujiza mingi zaidi kuliko nabii Eliya. Jambo hilo linaweza kufundisha mwanafunzi nini leo?

17. (a) Namna gani wanafunzi leo wanaweza kuiga mufano wa Elisha? (b) Kisha muda fulani, namna gani Yehova anaweza kutumia wanafunzi waaminifu?

17 Usiwaze kwamba kisha tu kupewa madaraka katika kutaniko, unapaswa kutumia madaraka hayo ili kubadilisha mambo, ni kusema, kufanya mambo kwa njia tofauti kabisa na namna ilikuwa inafanywa mbele. Ikiwa kuna lazima ya kubadilisha mambo fulani, yatabadilishwa si kwa sababu wewe unapenda, lakini kulingana na mahitaji ya kutaniko na muongozo wenye kutolewa na tengenezo la Yehova. Kupitia matendo yake, Elisha alifanya manabii wenzake wamutumainie na alionyesha kwamba alimuheshimu mwalimu wake kwa kutumia njia zenye alitumia. Wewe pia unaweza kufanya waamini wenzako wakutumainie na kuonyesha kwamba unaheshimu wazee wenye uzoefu kwa kuendelea kutumia njia zao zenye kutegemea Maandiko zenye wanatumia. (Soma 1 Wakorintho 4:17.) Hata hivyo, kadiri utaendelea kuwa na uzoefu, bila shaka utaweza kuchangia kufanya mabadiliko yenye itasaidia kutaniko liendelee kutembea pamoja na tengenezo la Yehova. Kwa hiyo, kama vile alimutendea Elisha, Yehova anaweza pia kuwasaidia ninyi wanafunzi waaminifu mufanye mambo makubwa zaidi kuliko walimu wenu.—Yoh. 14:12.

18. Sababu gani leo ni jambo la lazima sana kuzoeza ndugu katika makutaniko?

18 Tunatumaini kwamba mapendekezo yenye kupatikana katika habari hii na katika ile yenye ilitangulia ichochee zaidi wazee wajiwekee wakati wa kuzoeza wengine. Tunatumaini pia kwamba ndugu wenye kustahili watakubali kwa moyo wote mazoezi yenye wanapokea na kuitumikisha kwa hekima wakati wanashugulikia kondoo za Yehova. Kufanya hivyo, kutasaidia makutaniko katika dunia yote na kutasaidia kila mumoja wetu abaki mwaminifu katika nyakati ngumu zenye zinakuja.

^ fu. 5 Ikiwa kijana anaonyesha kwamba amekomaa kiroho, ni munyenyekevu, na anatimiza mambo mengine yenye kuombwa katika Maandiko, wazee wanaweza kumupendekeza ili akuwe mutumishi wa huduma, hata kama hajaeneza miaka 20.—1 Tim. 3:8-10, 12; ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 7, 1989, ukurasa wa 29, katika Kifaransa.

^ fu. 11 Wakati muzee anazungumuza pamoja na mwanafunzi, anaweza kutumia mapendekezo yenye kupatikana katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 2012, ukurasa wa 14-16, fungu la 8-13; na kitabu Mubaki “Katika Upendo wa Mungu,” sura ya 16, fungu la 1-3.