Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Gogu wa Magogu mwenye kuzungumuziwa katika kitabu cha Ezekieli ni nani?

Mafasirio hayo ilikuwa inategemea kitabu cha Ufunuo chenye kuonyesha kwamba Shetani Ibilisi ndiye anaongoza mashambulizi juu ya watumishi wa Mungu katika dunia yote. (Ufu. 12:1-17) Kwa hiyo, tulifikiri kwamba Gogu ni jina lingine la Shetani.

Hata hivyo, mafasirio hayo ilitokeza maulizo fulani ya maana. Sababu gani? Fikiria jambo hili: Wakati anazungumuzia kuharibiwa kwa Gogu, Yehova anasema hivi: ‘Nitakutoa ukuwe chakula cha ndege wenye kuwinda, na ndege wa kila namna ya bawa, na wanyama wa mwituni [pori].’ (Eze. 39:4) Kisha Yehova anaongeza hivi: ‘Katika siku hiyo, nitamupa Gogu mahali huko, kaburi katika Israeli . . . Nao watalazimika kumuzika Gogu na umati wake wote huko.’ (Eze. 39:11) Lakini, namna gani kiumbe wa kiroho anaweza kukuliwa na “ndege wa kila namna ya bawa na wanyama wa mwituni”? Namna gani Shetani anaweza kupewa “kaburi” ao nafasi ya kuzikwa hapa duniani? Biblia inasema waziwazi kwamba Shetani atatupwa katika abiso kwa miaka 1 000. Lakini haiseme kwamba atakuliwa ao kuzikwa.—Ufu. 20:1, 2.

Biblia inasema kwamba kisha miaka 1 000, Shetani atafunguliwa kutoka katika abiso, na ‘ataenda kupotosha [kudanganya] yale mataifa yaliyo katika pembe ine za dunia, Gogu na Magogu, kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita.’ (Ufu. 20:8) Ikiwa Shetani ndiye Gogu, namna gani anaweza kujidanganya yeye mwenyewe? Kwa hiyo, “Gogu” mwenye kuzungumuziwa katika kitabu cha Ezekieli na katika kitabu cha Ufunuo haiko Shetani.

Kwa hiyo, Gogu wa Magogu ni nani? Ili kujibu ulizo hilo, ni lazima tuchunguze Maandiko ili tujue ni nani mwenye anashambulia watumishi wa Mungu. Biblia inazungumuzia shambulizi la ‘Gogu wa Magogu.’ Lakini pia, inazungumuzia shambulizi la ‘mufalme wa kaskazini’ na shambulizi la “wafalme wa dunia.” (Eze. 38:2, 10-13; Dan. 11:40, 44, 45; Ufu. 17:14; 19:19) Mashambulizi hayo inatofautiana? Jibu ni hapana. Bila shaka Biblia inatumia majina hayo ili kuzungumuzia shambulizi lilelile. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu Biblia inatuambia kwamba mataifa yote ya dunia itajiunga pamoja ili kufanya shambulizi hilo la mwisho lenye litatokeza vita ya Har-Magedoni.—Ufu. 16:14, 16.

Wakati tunalinganisha Maandiko hayo yote yenye kuzungumuzia shambulizi la mwisho juu ya watumishi wa Mungu, tunaelewa muzuri kwamba Gogu wa Magogu haiko Shetani, lakini ni muungano wa mataifa. Je, muungano huo wa mataifa ndio utakuwa ‘mufalme wa kaskazini’? Hatuwezi kuhakikisha jambo hilo. Lakini inaonekana kwamba mawazo hayo inapatana na maneno yenye Yehova anasema juu ya Gogu. Yehova anasema hivi: ‘Na wewe hakika utakuja kutoka mahali pako, kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini, wewe na vikundi vingi vya watu pamoja na wewe, hao wote wakiwa wamepanda farasi, kutaniko kubwa, naam, jeshi kubwa sana.’—Eze. 38:6, 15.

Vilevile, nabii Danieli mwenye aliishi wakati moja na nabii Ezekieli, alisema hivi juu ya mufalme wa kaskazini: ‘Kutakuwa habari ambazo zitamusumbua, kutoka upande wa mashariki na kutoka kaskazini, naye ataenda kwa gazabu [hasira] kubwa ili kuangamiza na kuharibu wengi. Naye atasimamisha mahema yake makubwa kati ya ile bahari kubwa na mulima mutakatifu wa lile Pambo; naye ataenda mupaka mwisho wake, wala hatakuwa na wa kumusaidia.’ (Dan. 11:44, 45) Maneno hayo inafanana kabisa na maneno yenye kitabu cha Ezekieli kinasema juu ya mambo yenye Gogu atafanya.—Eze. 38:8-12, 16.

Shambulizi hilo litatokeza nini? Nabii Danieli anatuambia hivi: ‘Mikaeli [Yesu Kristo] atasimama wakati huo [kwenye Har-Magedoni], ule mukubwa anayesimama [tangu mwaka wa 1914] kwa ajili ya wana wa watu wako. Na kutakuwa na wakati wa taabu [ziki kubwa] ambayo haijapata kutokea tangu kuwapo kwa taifa lolote mupaka wakati huo. Na wakati huo watu wako wataponyoka, kila mumoja anayepatikana ameandikwa katika kile kitabu.’ (Dan. 12:1) Jambo hilo lenye Yesu mujumbe wa Mungu atafanya, linazungumuziwa pia kwenye Ufunuo 19:11-21.

Lakini, ni nani ndiye “Gogu na Magogu” mwenye kuzungumuziwa katika Ufunuo 20:8? Jina hilo linaonyesha wale wote wenye watamupinga Yehova na kushambulia watu wake mwishoni mwa miaka 1000. Wataonyesha chuki kama ‘Gogu wa Magogu,’ ni kusema, mataifa yote yenye itashambulia watumishi wa Mungu mbele ya ziki kubwa kumalizika. Vikundi vyote viwili vitapatwa na hukumu ileile, ni kusema, kifo cha milele! (Ufu. 19:20, 21; 20:9) Kwa hiyo, ni jambo lenye kufaa kusema kwamba “Gogu na Magogu” mwenye kuzungumuziwa katika andiko hilo la Ufunuo, ni wale wote wenye watakuwa waasi mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu Moja.

Kwa sababu tunajifunza Neno la Mungu kwa bidii, tunangojea kwa hamu kuona hivi karibuni ni nani mwenye atakuwa “mufalme wa kaskazini.” Lakini, iwe ni nani ataongoza muungano huo wa mataifa, tuko hakika na mambo mbili: (1) Gogu wa Magogu na majeshi yake watashindwa na kuharibiwa; na (2) Yesu Kristo, Mufalme wetu mwenye kutawala, atawaokoa watumishi wa Mungu, na kuwaingiza katika dunia mupya yenye amani na usalama wa kweli.—Ufu. 7:14-17.