Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunaweza Kuendelea Kuwa na Mwenendo Safi

Tunaweza Kuendelea Kuwa na Mwenendo Safi

‘Musafishe mikono yenu, . . . na mutakase mioyo yenu.’—YAK. 4:8.

1. Watu wa ulimwengu wako na maoni gani kuhusu mwenendo safi?

TUNAISHI katikati ya watu wa ulimwengu wenye kuwa na mwenendo muchafu. Kwa mufano, watu wengi hawaone kwamba ni mubaya mwanaume kulala na mwanaume ao mwanamuke kulala na mwanamuke; tena, hawaone kwamba ni mubaya kulala na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yake. Mambo hayo yanaonyeshwa wazi katika filme, vitabu, nyimbo, matangazo, na katika mambo ya kujifurahisha. (Zab. 12:8) Kwa sababu mwenendo mubaya umeenea sana katika ulimwengu, mutu anaweza kujiuliza hivi: ‘Je, inawezekana kabisa kuendelea kuwa na mwenendo safi?’ Bila shaka jibu ni ndiyo. Yehova anaweza kuwasaidia Wakristo wa kweli waendelee kuwa na mwenendo safi.—Soma 1 Wathesalonike 4:3-5.

2, 3. (a) Sababu gani tunapaswa kupiganisha tamaa mbaya? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Hata hivyo, tunapaswa kwanza kujua kwamba, ili kuendelea kuwa na mwenendo safi, tunapaswa kuepuka kuwa na tamaa mbaya. Kama vile chambo kwenye ndoano kinaweza kuvutia samaki, vilevile, ikiwa Mukristo hazuie bila kukawia mawazo na tamaa mbaya, inaweza kukomaa na kumufanya aangukie katika mutego. Mawazo na tamaa mbaya vinaweza kuvutia mwili wetu wenye zambi na kutuchochea kufanya mambo mabaya. Kisha, tamaa mbaya inaweza kukomaa sana, na ikiwa nafasi inajitokeza, tunaweza kufanya zambi. Ndiyo, ‘tamaa . . . inazaa zambi.’—Soma Yakobo 1:14, 15.

3 Ni vizuri kufikiria namna tamaa ya muda mufupi tu inaweza kukomaa na kuzaa zambi nzito. Lakini, tunatiwa moyo kujua kwamba, ikiwa haturuhusu tamaa mbaya ikomae ndani ya moyo wetu, hilo litatusaidia tusiangukie katika zambi ya uasherati na kupatwa na matokeo mabaya! (Gal. 5:16) Tuzungumuzie sasa njia tatu zenye zitatusaidia kupambana na tamaa mbaya: urafiki wetu pamoja na Yehova, mashauri ya Neno lake, na musaada wa Wakristo wenye kukoma kiroho.

‘MUMUKARIBIE MUNGU’

4. Sababu gani ni jambo la lazima tumukaribie Yehova?

4 Biblia inashauria hivi wale wenye wanapenda ‘kumukaribia Mungu’: ‘Musafishe mikono yenu, . . . na mutakase mioyo yenu.’ (Yak. 4:8) Wakati tunaona urafiki wetu pamoja na Yehova kuwa wa lazima sana, tutajikaza kumupendeza katika kila hali ya maisha yetu, na katika mawazo yetu pia. Tunapenda tukuwe na ‘moyo’ safi kwa kuendelea kukaza akili yetu juu ya mambo yenye kuwa safi, mazuri, na yenye kustahili sifa. (Zab. 24:3, 4; 51:6; Flp. 4:8) Jambo la kufurahisha ni hili: Yehova anajua kwamba hatukamilike na kwamba tunaweza kuanza kufikiria mambo mabaya. Lakini tunajua kwamba Yehova anahuzunika wakati tunaendelea kufikiria mambo mabaya kuliko kufanya nguvu yetu yote ili kuachana nayo. (Mwa. 6:5, 6) Kufikiria jambo hilo kunatusaidia tuazimie zaidi kuendelea kuwa na mawazo safi.

5, 6. Namna gani sala inaweza kutusaidia kupiganisha tamaa mbaya?

5 Tunaonyesha kwamba tunamutegemea kabisa Yehova kwa kuendelea kumuomba atusaidie kupiganisha mawazo mabaya. Wakati tunamukaribia Yehova katika sala, yeye pia anatukaribia. Iko tayari kutupatia roho yake takatifu, na roho hiyo inatusaidia tuazimie kupiganisha mawazo mabaya na kuendelea kuwa na mwenendo safi. Kwa hiyo, tumuonyeshe Mungu kwamba tunatamani sana kumufurahisha kupitia kutafakari kwa moyo wetu, ni kusema, kupitia mambo yenye tunafikiria. (Zab. 19:14) Je, tunamuomba Yehova kwa unyenyekevu achunguze moyo wetu ili kuona ikiwa umeanza kuwa na “njia” yoyote mbaya, ni kusema, tamaa mbaya ao mawazo mabaya yenye inaweza kutuingiza katika zambi? (Zab. 139:23, 24) Wakati tunapambana na jaribu fulani, je, kila mara tunamuomba atusaidie tuendelee kuwa waaminifu?—Mt. 6:13.

6 Mbele ya kumujua Yehova, inawezekana tulikuwa tunapenda mambo yenye anachukia, na inawezekana tunaendelea kupambana na mawazo hayo mabaya. Hata hivyo, Yehova anaweza kutusaidia tufanye mabadiliko yenye inaombwa ili tuendelee kumutumikia kwa njia yenye kukubalika. Mufalme Daudi alielewa jambo hilo. Kisha kufanya uzinifu na Bath-sheba, alimuomba Yehova hivi: ‘Uumbe moyo safi ndani yangu, . . . na uweke ndani yangu roho mupya, iliyo imara.’ (Zab. 51:10, 12) Zambi inaweza kuchochea sana mwili wetu wenye haukamilike, lakini Yehova anaweza kutia ndani yetu roho yenye kupenda, ni kusema, tamaa ya kumutii. Hata kama tamaa mbaya imeingia sana katika moyo wetu na kujaribu kutuzuia tukuwe na mawazo safi, Yehova anaweza kuongoza hatua zetu ili tutii amri zake na tuweze kuishi kulingana na amri hizo. Anaweza kuzuia jambo lolote lenye kuumiza liendelee kuwa na mizizi katika moyo wetu.—Zab. 119:133.

Ikiwa tamaa mbaya inaanza kuwa na mizizi katika moyo wetu, tunapaswa kuiondoa (Ona fungu la 6)

‘MUKUWE WATENDAJI WA NENO’

7. Namna gani Neno la Mungu linaweza kutusaidia tuepuke kuwa na mawazo mabaya?

7 Yehova anaweza kujibia sala zetu kupitia Neno lake Biblia. Hekima yenye kupatikana katika Neno la Mungu “kwanza kabisa ni safi kiadili.” (Yak. 3:17) Kusoma Biblia kila siku na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma kunaweza kutusaidia tuepuke kuwa na mawazo mabaya. (Zab. 19:7, 11; 119:9, 11) Tena, Biblia ina mifano na mashauri yenye kufaa yenye inaweza kutusaidia tuepuke kuwa na tamaa mbaya.

8, 9. (a) Namna gani kijana mumoja alifikia kufanya uasherati na mwanamuke kahaba? (b) Mufano wenye kupatikana katika Methali sura ya 7 unaweza kutusaidia kuepuka hali gani?

8 Tunasoma hivi kwenye Methali 5:8: ‘Itenge njia yako mbali naye [mwanamuke kahaba], wala usiukaribie mulango wa nyumba yake.’ Methali sura ya 7 inaonyesha hatari ya kuzarau shauri hilo; sura hiyo inazungumuzia kijana mwanaume mwenye alikuwa anapita pembeni ya nyumba ya mwanamuke kahaba. Usiku umefika. Kwenye pembe ya njia, mwanamuke fulani mwenye kuvaa mubaya anamukaribia. Mwanamuke huyo anamukamata na kumubusu (kumupatia baiser). Maneno ya mwanamuke huyo inaamusha tamaa mbaya ndani ya kijana huyo, na anashindwa kujizuia. Wanafanya uasherati. Inaonekana kwamba kijana huyo hakupanga kufanya uasherati. Kijana huyo hana uzoefu na anakosa utambuzi. Hata hivyo, anapaswa kupatwa na matokeo mabaya ya matendo yake. Jambo hilo halingemupata ikiwa angeepuka kupita pembeni ya nyumba ya mwanamuke huyo!—Met. 7:6-27.

9 Je, wakati fulani, sisi pia tunakosa utambuzi, pengine kwa kujitia katika hali zenye zinaweza kuamusha tamaa mbaya ndani yetu? Kwa mufano, wakati wa usiku, programu fulani za televizyo zinaweza kuwa na vipindi mbalimbali vyenye kuonyesha mambo machafu. Je, kuna hatari fulani ikiwa mutu anabadilisha-badilisha programu za televizyo ili tu kuona mambo yenye kuonyeshwa? Ao, pengine, bila kutazamia tunaweza kufungua adresi za Internete zenye kuwa na mambo ya pornografia, ao mambo mengine ya uasherati na programu hizo zinaweza kutuingiza katika jaribu. Katika hali kama hizo, mambo yenye tunatazama inaweza kutokeza tamaa mbaya ndani yetu, na hilo linaweza kufanya tukose kumutii Yehova.

10. Sababu gani ni hatari kuchezeana kimapenzi? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

10 Biblia inatusaidia tena katika njia ingine; inatutolea mashauri juu ya namna wanaume na wanawake wanapaswa kutendeana. (Soma 1 Timotheo 5:2.) Mashauri hayo inatusaidia tuepuke kuwachezea wengine kimapenzi. Watu fulani wanaweza kuona kwamba haiko mubaya kutumia ishara za mwili, za uso, na kuangalia mutu mwengine kwa njia yenye inaamusha mapenzi. Wanafikiri kwamba kufanya hivyo ni tofauti na kufanya kitendo cha ndoa. Lakini, kuchezeana kimapenzi kunaweza kuamusha tamaa mbaya, na tamaa hiyo inaweza kutuingiza katika zambi ya uasherati. Kwa kuwa jambo hilo limekwisha kutokea, linaweza kutokea tena.

11. Yosefu alituachia mufano gani muzuri?

11 Yosefu alituachia mufano muzuri. Wakati bibi ya Potifa, mukubwa wake wa kazi, alijaribu kumushawishi, Yosefu alikataa kabisa. Lakini, bibi ya Potifa hakuchoka. Kila siku alikuwa anamuambia aendelee kuwa pamoja naye. (Mwa. 39:7, 8, 10) Kulingana na mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia, ni kama vile bibi ya Potifa alikuwa anasema hivi: “‘Tukibaki sisi wawili kwa muda mufupi tu,’ natumaini kwamba [Yosefu] atachukua hatua ya kwanza.” Hata hivyo, Yosefu aliazimia kabisa kukataa vishawishi vya mwanamuke huyo. Alikataa bibi ya Potifa amuchezee kimapenzi, naye aliepuka kumuchezea kimapenzi; kufanya hivyo, kulimusaidia asikuwe na tamaa mbaya. Wakati bibi ya Potifa alijaribu kumukaza alale naye, Yosefu alikataa mara moja. ‘Akaliacha vazi lake mukononi mwake, akakimbia na kwenda inje.’—Mwa. 39:12.

12. Ni nini inaonyesha kwamba mambo yenye tunaangalia inaweza kudanganya moyo wetu?

12 Biblia inatuonya pia kwamba mambo yenye tunaangalia inaweza kudanganya moyo wetu. Macho yenye kuendelea kuangalia inaweza kuamusha ao kukomalisha tamaa ya kufanya uasherati. Yesu alionya kwamba ‘kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.’ (Mt. 5:28) Kumbuka mambo yenye ilimupata Mufalme Daudi. Wakati alikuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba yake, ‘alimuona mwanamuke akioga.’ (2 Sam. 11:2) Kuliko kuangalia mahali pengine, Daudi aliendelea kumuangalia na kufikiri juu yake. Hilo lilimufanya atamani bibi ya mwanaume mwenzake na kuchukua mipango ya kufanya uzinifu naye.

13. Sababu gani tunapaswa ‘kufanya agano pamoja na macho yetu,’ na namna gani tunaweza kufanya hivyo?

13 Ili tupiganishe mawazo mabaya, tunapaswa ‘kufanya agano pamoja na macho yetu,’ kama vile mwanaume mwaminifu Ayubu alifanya. (Ayu. 31:1, 7, 9) Tunapaswa kuazimia kuzuia macho yetu ili tuepuke kutamani mutu mwenye tunaangalia. Pia, tunapaswa kuepuka kuangalia picha zenye kuonyesha mambo ya uasherati kwenye ordinatere, kwenye vibao vya matangazo, kwenye jalada za magazeti ya ulimwengu, ao nafasi zingine.

14. Tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kuwa na mwenendo safi?

14 Ikiwa mambo yote yenye tumezungumuzia imekusaidia utambue nafasi kwenye unapaswa kufanya mabadiliko fulani ili upiganishe tamaa mbaya, tenda bila kukawia. Ukuwe tayari kukubali mashauri ya Neno la Mungu; kufanya hivyo, kunaweza kukusaidia uepuke kufanya zambi, na kunaweza kukusaidia uendelee kuwa na mwenendo safi.—Soma Yakobo 1:21-25.

“UWAITE KWAKO WANAUME WAZEE”

15. Ikiwa tunapiganisha tamaa mbaya, sababu gani ni lazima tuombe musaada?

15 Ikiwa tunapiganisha tamaa mbaya za kufanya uasherati, Wakristo wenzetu ni njia ingine yenye Yehova anatumia ili kutusaidia. Bila shaka, inaweza kuwa vigumu kuambia watu wengine mambo yetu ya siri. Lakini kutafuta musaada wa Wakristo wenye kukomaa kiroho, kunaweza kutusaidia tuepuke kuwa na tamaa mbaya. (Met. 18:1; Ebr. 3:12, 13) Kumuelezea Mukristo mwenye kukomaa kiroho uzaifu wetu, kunaweza kutusaidia tutambue mambo yenye inaweza kututia katika hatari. Kufanya hivyo kutatusaidia tufanye mabadiliko ili tubaki katika upendo wa Yehova.

16, 17. (a) Namna gani wazee wanaweza kusaidia wale wenye kupiganisha tamaa mbaya? Toa mufano. (b) Sababu gani wale wenye kuwa na tabia ya kuangalia pornografia wanapaswa kuomba musaada bila kukawia?

16 Wazee wanastahili kabisa kutusaidia. (Soma Yakobo 5:13-15.) Katika inchi ya Brazili, kijana mumoja mwanaume alipiganisha tamaa mbaya kwa muda wa miaka mingi. Anasema hivi: “Nilijua kwamba mawazo yangu haikumupendeza Yehova, lakini nilisikia haya sana kuwaelezea wengine namna nilikuwa ninajisikia.” Jambo la kupendeza ni kwamba, katika kutaniko lake, muzee mumoja alitambua kwamba kijana huyo alikuwa na lazima ya musaada, na kwa hiyo alimutia moyo aombe musaada wa wazee. Kijana huyo anakumbuka: “Nilishangaa kuona wazee wananitendea kwa wema, walikuwa wema sana na walinielewa vizuri kabisa kuliko namna niliwazia. Walinisikiliza kwa uangalifu. Walitumia Biblia ili kunionyesha kwamba Yehova ananipenda, na walisali pamoja na mimi. Hilo lilinisaidia nikuwe tayari kukubali mashauri ya Biblia yenye walinitolea.” Kisha kufanya maendeleo ya kiroho, anasema hivi: “Sasa ninaelewa kwamba, ni vizuri kuomba musaada kuliko kujaribu kubeba mizigo yetu sisi wenyewe.”

17 Ikiwa mutu iko na tabia mubaya ya kuangalia pornografia, anapaswa kuomba musaada. Ikiwa mutu huyo anakawia kuomba musaada, hilo litamufanya akuwe na tamaa mbaya, na tamaa hiyo ‘itakomaa na kuzaa zambi’ yenye itaumiza wengine na kuchafua jina la Yehova. Tamaa ya kumupendeza Yehova na kubakia katika kutaniko la Kikristo imechochea watumishi wake wengi wakubali musaada wake wenye upendo.—Yak. 1:15; Zab. 141:5; Ebr. 12:5, 6.

AZIMIA KUENDELEA KUWA NA MWENENDO SAFI!

18. Umeazimia kufanya nini?

18 Ulimwengu wa Shetani unaendelea kuharibika sana. Lakini, watumishi wa Yehova wanatumia nguvu zao zote ili kuendelea kuwa na mawazo safi na kushikamana na kanuni zake za mwenendo safi za hali ya juu. Jambo hilo linamufurahisha sana Yehova! Kwa hiyo, kila mumoja wetu aazimie kubakia karibu na Yehova na kukubali muongozo wenye anatutolea kupitia Neno lake na kutaniko la Kikristo. Kuendelea kuwa na mwenendo safi kunatusaidia tukuwe na furaha na amani ya moyo. (Zab. 119:5, 6) Kisha Shetani kuharibiwa, tutakuwa na pendeleo la kuishi milele katika dunia mupya yenye kuwa safi.