Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Umesoma kwa uangalifu habari za hivi karibuni katika Munara wa Mulinzi? Ikiwa ni hivyo, jaribu kujibu maulizo haya:

Wakristo wanapaswa kusali kwa Yesu Kristo?

Hapana. Yesu mwenyewe alifundisha kwamba tunapaswa kusali kwa Yehova, na alituachia mufano kwa kusali kwa Baba yake. (Mt. 6:6-9; Yoh. 11:41; 16:23) Ndiyo sababu wafuasi wake wa kwanza walikuwa wanasali kwa Mungu, lakini hawakusali kwa Yesu. (Mdo. 4:24, 30; Kol. 1:3)—1/1, ukurasa wa 14.

Ni mambo gani tunaweza kufanya ili kujitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho wa kila mwaka wa kifo cha Yesu?

Jambo moja lenye tunaweza kufanya, ni kufuata programu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho. Tunaweza pia kujikaza ili kuongeza bidii yetu katika kazi ya kuhubiri wakati huo. Tena tunaweza kusali na kufikiri sana juu ya tumaini lenye Mungu ametupatia.—15/1, ukurasa wa 14-16.

Namna gani maneno ya Yosefu ilitimia kisha wafungwa wawili Wamisri kumuelezea ndoto zao zenye kuwa ngumu kueleweka?

Yosefu aliambia mukubwa wa watumishi wa kumupatia Farao kinywaji kwamba atarudishwa katika kazi yake. Lakini ule mukubwa wa watumishi wa kumupatia Farao mukate, aliambiwa kwamba atauawa na kutundikwa kwenye muti. Maneno ya Yosefu kuhusu ndoto hizo mbili ilitimia. (Mwa. 40:1-22)—1/2, ukurasa wa 12-14.

Ni zawadi gani nzuri ndugu na dada wa Japani walipokea?

Walipokea kijitabu chenye kuwa na kitabu cha Mathayo chenye kilichukuliwa katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Ndugu na dada wanatolea watu kijitabu hicho katika mahubiri, na watu wengi wenye hawajue mambo mengi juu ya Biblia wanakikubali.—15/2, ukurasa wa 3.

Wakati wa mitume, ni hali gani zilisaidia kueneza habari njema katika maeneo mengi?

Kwa sababu kulikuwa Amani ya Roma, kulikuwa tu vita vidogo-vidogo. Wanafunzi wa wakati wa mitume wangeweza kusafiri kwa kutumia barabara zenye kutengenezwa muzuri. Kwa sababu luga ya Kigiriki ilizungumuzwa na watu wengi, ilikuwa mwepesi kuhubiria watu, hata Wayahudi wenye walipatikana katika utawala wote wa Roma. Tena, wanafunzi wangeweza kutumia sheria ya Roma ili kutetea habari njema.—15/2, ukurasa wa 20-23.

Sababu gani Wakristo wa kweli hawafanye Sikukuu ya Pasaka?

Yesu aliamuru wafuasi wake wakumbuke kifo chake, lakini hakuwaambia wakumbuke ufufuo wake. (Lu. 22:19, 20)—1/3, ukurasa wa 8.

Katika miaka ya hivi karibuni, sababu gani hatuzoee tena kutumia vifananishi na vifananishwa katika vichapo vyetu?

Biblia inaonyesha kwamba watu fulani walifananisha jambo fulani kubwa la wakati unaokuja. Tunapata mufano mumoja katika andiko la Wagalatia 4:21-31. Lakini ni muzuri zaidi kuepuka kuwazia-wazia ao kutumia vifananishwa ili kufasiria habari fulani ya Biblia. Hata hivyo, tunaweza kujifunza mambo mengi kupitia watu na matukio yenye kuzungumuziwa katika Biblia. (Rom. 15:4)—15/3, ukurasa wa 17-18.

Sababu gani tunapaswa kukazia uangalifu zaidi kipande cha karatasi ya mafunjo (papyrus) chenye kiliokotwa kwenye uchafu katika Misri?

Katika miaka 100 yenye imepita, kipande fulani cha karatasi ya mafunjo kiliokotwa na kilikuwa na sehemu fulani za Injili ya Yohana. Inawezekana ni cha miaka fulani kisha mutume Yohana kuandika kitabu chake, na kinahakikisha kwamba Biblia ni yenye kutegemeka.—1/4, ukurasa wa 10-11.

Sababu gani kutenga Mukristo mwenye anakataa kutubu ni mupango wenye upendo?

Biblia inazungumuzia uamuzi wa kumutenga Mukristo na kutaniko. Huo ni uamuzi muzito, lakini unaleta faida. (1 Kor. 5:11-13) Unafanya jina la Mungu liheshimiwe, unalinda usafi wa kutaniko, na unamusaidia mukosaji arudiwe na ufahamu.—15/4, ukurasa wa 29-30.