Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Muko na Lazima ya “Uvumilivu”

Muko na Lazima ya “Uvumilivu”

KISHA Anita * kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, bwana yake alimupinga sana. Dada Anita anasema hivi: “Alinizuia kuenda kwenye mikutano na alinikataza hata kutaja jina la Mungu. Kusema tu jina la Yehova kulifanya bwana yangu akasirike sana.”

Kufundisha watoto wake juu ya Yehova kulimuletea pia dada Anita mateso makali. Anasema hivi: “Nilikatazwa kumuabudu Yehova katika nyumba yangu. Singeweza kujifunza na watoto wangu waziwazi, wala kuwapeleka kwenye mikutano.”

Mambo yenye ilimufikia dada Anita, inaonyesha kwamba upinzani kutoka kwa watu wa familia unaweza kutia uaminifu wa Mukristo katika jaribu kubwa. Tena, mambo kama vile ugonjwa wa kukawia, kufiwa na mutoto, kufiwa na bibi ao bwana, ao mutu wa familia kuacha kumutumikia Yehova, inaweza kujaribu uaminifu wetu. Lakini, ni nini inaweza kumusaidia Mukristo aendelee kuwa mwaminifu kwa Yehova?

Unaweza kufanya nini ikiwa unapambana na majaribu kama hayo? Mutume Paulo alisema hivi: ‘Munahitaji kuwa na uvumilivu.’ (Ebr. 10:36) Lakini, ni nini inaweza kukusaidia uvumilie?

UMUTEGEMEE YEHOVA KATIKA SALA

Njia moja kubwa ya kutusaidia kupata nguvu ya kuvumilia majaribu, ni kumutegemea Mungu katika sala. Tuchunguze mufano moja. Siku ya Kwanza fulani kisha muchana, familia ya dada Ana ilipatwa na musiba. Bwana yake mwenye aliishi pamoja naye kwa miaka 30, alikufa kifo cha kushitukia. Dada Ana anasema hivi: “Tangu alienda kwenye kazi hajarudia nyumbani, na alikuwa tu na miaka 52.”

Ni nini ilimusaidia dada Ana avumilie? Alikuwa anaenda kwenye kazi, na kazi hiyo ilimusaidia kwa sababu ilimuomba afikiri sana. Hata hivyo, haikumaliza huzuni yake. Dada huyo anasema hivi: “Nilimufungulia Yehova moyo wangu, na nilimuomba anisaidie kuvumilia hali hiyo.” Yehova alijibia sala zake? Iko hakika kwamba Yehova alijibu sala hizo. Anasema hivi: “Amani yenye Yehova mwenyewe anaweza kutoa, ilinituliza na kulinda akili yangu. Niko hakika kwamba, wakati unaokuja, Yehova atamufufua bwana yangu.”—Flp. 4:6, 7.

‘Musikiaji wa sala’ ameahidi kwamba atasaidia watumishi wake ili waendelee kuwa waaminifu kwake. (Zab. 65:2) Hauone kwamba ahadi hiyo inatia imani nguvu? Hauone kwamba inaweza kukusaidia wewe pia kuvumilia?

MIKUTANO YA KIKRISTO INATUPATIA NGUVU YA KUVUMILIA

Tangu zamani, Yehova anategemeza watu wake kupitia kutaniko la Kikristo. Kwa mufano, wakati ndugu na dada wa kutaniko la Thesalonike walipata mateso makali, mutume Paulo aliwatia moyo ‘waendelee kufarijiana na kujengana, kama vile [walikuwa] wanafanya.’ (1 Tes. 2:14; 5:11) Kusaidiana na kukusanyika pamoja, kuliwapatia Wakristo Wathesalonike nguvu ya kuvumilia majaribu ya imani yao. Mufano wao muzuri wa uvumilivu unaonyesha jambo lenye tunapaswa kufanya leo ili tuweze kuvumilia.

Kufanya urafiki wa sana pamoja na ndugu na dada katika kutaniko, kunaweza kutusaidia tushiriki “mambo ambayo ni ya kujengana.” (Rom. 14:19) Ni lazima sana kufanya hivyo, zaidi sana katika nyakati hizi za taabu. Mutume Paulo alipata magumu mengi, na Yehova alimupatia nguvu ya kuvumilia. Wakati fulani, Mungu alimupatia nguvu ya kuvumilia kupitia Wakristo wenzake. Kwa mufano, wakati alituma salamu zake kwa ndugu na dada katika kutaniko la Kolosai, mutume Paulo alisema hivi juu yao: ‘Wamekuwa musaada wenye kunitia nguvu.’ (Kol. 4:10, 11) Walimupenda sana mutume Paulo, na hilo liliwachochea wamufariji na kumutia moyo wakati wa magumu. Pengine wewe pia umekwisha kutiwa moyo na ndugu na dada katika kutaniko.

MUSAADA WA WAZEE

Wazee katika kutaniko la Kikristo, ni njia ingine yenye Mungu anatumia ili kutusaidia kuvumilia. Wanaume hao wenye kukomaa kiroho wanaweza kuwa ‘kama mahali pa kujificha kutokana na upepo na mahali pa kujificha kutokana na zoruba ya mvua, kama vijito vya maji katika inchi isiyo na maji, kama kivuli cha mwamba muzito katika inchi iliyochoka.’ (Isa. 32:2) Kujua kwamba wazee wako tayari kutusaidia kunatufariji sana! Umekwisha kufaidika na mupango huo wenye upendo? Wazee wanaweza kukusaidia ili ukuwe na nguvu ya kuvumilia.

Bila shaka, wazee hawawezi kufanya muujiza ili kumaliza magumu yetu. Wao pia ni wanadamu wasiokamilika, na wako na ‘uzaifu uleule kama [sisi].’ (Mdo. 14:15) Hata hivyo, sala zenye wanatoa kwa ajili yetu zinaweza kutusaidia sana. (Yak. 5:14, 15) Ndugu mumoja katika inchi ya Italia alipambana na ugonjwa wa misuli (dystrophie musculaire). Alisema hivi: “Niliweza kuvumilia kwa sababu wazee walinionyesha upendo na kunitembelea kila mara.” Je, unaweza kufaidika kabisa na mupango wenye upendo wa Yehova, ni kusema, wazee wa kutaniko?

UENDELEE KUWA NA PROGRAMU NZURI YA KIROHO

Kuna mambo mengine yenye tunaweza kufanya ili tuweze kuvumilia. Jambo moja ni kuendelea kuwa na programu nzuri ya kiroho. Tuone mufano wa John, ndugu mwenye kuwa na miaka 39; aliambiwa na muganga kwamba iko na ugonjwa wa kansere. Anasema hivi: “Nilijisikia mubaya sana kwa sababu nilikuwa ningali kijana.” Wakati huo, mutoto wake mwanaume alikuwa tu na miaka tatu. John anasema hivi: “Kwa sababu ya ugonjwa huo, bibi yangu alilazimika kunihangaikia mimi na mutoto wetu, na kunisaidia kuenda kuonana na muganga.” Matunzo yenye John alikuwa anapata, ilimufanya achoke sana na akuwe karibu kutapika. Magumu yake haikuishia pale. Baba yake alipata ugonjwa wenye hauwezi kupona; kwa hiyo, iliomba kumushugulikia.

Namna gani John na familia yake waliweza kuvumilia hali hiyo ngumu? Anasema hivi: “Hata kama nilikuwa mwenye kuchoka, nilijikaza ili familia yetu iendelee kuwa na programu nzuri ya kiroho. Tulihuzuria mikutano yote, tulihubiri kila juma, na tulifanya ibada ya familia kwa ukawaida hata wakati ilikuwa vigumu kufanya hivyo.” Bila shaka, John alielewa kwamba, ili kuvumilia kila jaribu, ni jambo la lazima kuendelea kuwa na programu nzuri ya kiroho. Je, anaweza kutolea watu wenye kupambana na majaribu shauri fulani? Anasema hivi: “Kwanza nilihuzunika na nilikuwa na wasiwasi, kisha nilitulia kabisa. Nilijua kwamba Yehova alinipenda na alinipatia nguvu yenye nilikuwa nayo lazima. Yehova anaweza kukupatia nguvu, kama vile alinipatia mimi.”

Tuko hakika kwamba, Mungu anaweza kutusaidia tuvumilie majaribu na hali zingine zenye tunapambana nazo leo na za wakati unaokuja. Kwa hiyo, tumutegemee Yehova katika sala, tufanye urafiki wa sana pamoja na ndugu na dada katika kutaniko, tutafute musaada wa wazee wa kutaniko, na tuendelee kuwa na programu nzuri ya kiroho. Kwa kufanya hivyo, tutatenda kupatana na maneno haya ya mutume Paulo: ‘Munahitaji kuwa na uvumilivu.’

^ fu. 2 Majina fulani imebadilishwa.