Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Aliwapenda Watu

Aliwapenda Watu

[Nilipenda sana] wana wa binadamu.’MET. 8:31.

1, 2. Yesu alionyesha namna gani kwamba anawapenda sana watu?

MWANA muzaliwa wa kwanza wa Mungu ndiye wa kwanza kuonyesha kwa njia kubwa zaidi hekima ya ajabu ya Yehova. Yeye alikuwa hekima yenye kufananishwa na mutu, ni kusema, “stadi [fundi] wa kazi,” mwenye alitumika pembeni ya Baba yake. Wazia furaha yenye alikuwa nayo wakati Baba yake alikuwa ‘anatayarisha mbingu’ na ‘kuweka misingi ya dunia.’ Hata hivyo, kuliko kupendezwa na viumbe vingine vyote vyenye havina uzima, Mwana muzaliwa wa kwanza wa Mungu ‘[alipenda sana] wana wa binadamu’. (Met. 8:22-31) Ndiyo, Yesu alipenda sana watu hata mbele akuje hapa duniani.

2 Kisha, ili kuhakikisha kwamba iko mwaminifu kwa Baba yake na anapenda sana “wana wa binadamu,” Muzaliwa wa Kwanza wa Mungu “alijiondolea mwenyewe hali yake” na akakuwa mwanadamu. Alifanya hivyo ili atoe “fidia [zabihu ya ukombozi] badala ya wengi.” (Flp. 2:5-8; Mt. 20:28) Yesu alipenda sana watu! Wakati alikuwa duniani, Mungu alimupatia nguvu ya kufanya miujiza yenye ilionyesha kwamba alipenda sana watu. Kwa hiyo, Yesu alionyesha mambo ya ajabu yenye atafanya hivi karibuni wakati atatawala dunia yote.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Pia, Yesu alikuja duniani ili ‘kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.’ (Lu. 4:43) Yesu alijua kwamba Ufalme huo utatakasa jina la Baba yake na kumaliza kabisa matatizo yote ya wanadamu. Ndiyo sababu wakati alikuwa anahubiri, Yesu alionyesha kabisa kwamba anahangaikia sana wanadamu. Sababu gani tunapaswa kujua jambo hilo? Kwa sababu litatusaidia kuwa na tumaini hakika kwa ajili ya wakati unaokuja. Tuchunguze basi miujiza ine ya Yesu.

‘ALIKUWA NA NGUVU ZA YEHOVA ZA KUPONYESHA’

4. Eleza jambo lenye lilitokea wakati Yesu alikutana na mwanaume mumoja mwenye ukoma.

4 Yesu alipenda zaidi kuhubiria katika eneo la Galilaya. Katika eneo hilo, aliona jambo lenye kuhuzunisha katika muji fulani. (Mk. 1:39, 40) Mbele yake kulikuwa mwanaume mumoja mwenye kuwa na ugonjwa mubaya sana, ni kusema, ugonjwa wa ukoma. Alikuwa mugonjwa sana; ndiyo sababu Luka, mwenye alikuwa muganga, alisema kwamba mutu huyo alikuwa “mwenye kujaa ukoma.” (Lu. 5:12) Luka aliandika hivi: ‘Alipomuona Yesu akajiangusha kifudifudi [akainamisha uso chini] akamuomba, akisema: Bwana, ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.’ Bila shaka, mwanaume huyo alijua kwamba Yesu alikuwa na nguvu za kumuponyesha. Lakini alipenda kujua ikiwa Yesu alitaka kufanya hivyo. Yesu alitenda namna gani wakati mwanaume huyo alimuomba kwa moyo wote amuponyeshe? Yesu alikuwa na mawazo gani wakati aliona mwanaume huyo, ambaye pengine ugonjwa wake ulikuwa umeharibu mwili wake? Je, Yesu angetenda kama Mafarisayo, wenye hawakuwa wanasikilia huruma watu wenye walikuwa na ugonjwa huo? Wewe ungetenda namna gani?

5. Wakati alimuponyesha mwanaume mumoja mwenye ukoma, ni nini ilimuchochea Yesu aseme “ninataka!”?

5 Sheria ya Musa ilisema kwamba mutu mwenye kuwa na wa ukoma alipaswa kulalamika “Si safi, si safi!” Pengine mwanaume huyo alikuwa ameacha kufanya hivyo. Yesu hakumukumbusha jambo hilo. Lakini, alihangaikia kwanza mwanaume huyo na ugonjwa wake. (Law. 13:43-46) Hatujue kabisa mambo yenye Yesu alikuwa anafikiria, lakini tunaweza kujua mawazo yenye ilikuwa katika moyo wake. Yesu alijitia pa nafasi ya mwanaume huyo, na akafanya jambo lenye lilikatazwa. Akanyoosha mukono wake, akamugusa mutu huyo mwenye ukoma, na kumuambia hivi kwa sauti yenye mamlaka na yenye upendo: “Ninataka. Takasika [ukuwe safi].” Kwa hiyo, ‘ule ukoma ukamutoka.’ (Lu. 5:13) Bila shaka, Yehova alimupatia Kristo nguvu si za kufanya tu muujiza mukubwa kama huo lakini pia ili aonyeshe kwamba aliwapenda sana watu.—Lu. 5:17.

6. Ni mambo gani ya lazima yenye tunajifunza juu ya miujiza yenye Yesu alifanya, na miujiza hiyo inaonyesha nini?

6 Mungu alimupatia Yesu Kristo nguvu za kufanya miujiza mbalimbali yenye kushangaza. Aliponyesha watu wenye ukoma, na pia watu wenye walikuwa na ulemavu wa aina mbalimbali. Biblia inasema hivi: ‘Umati [watu wengi] wakashangaa walipoona mabubu wakisema na viwete [vilema] wakitembea na vipofu wakiona, nao wakamutukuza Mungu wa Israeli.’ (Mt. 15:31) Leo, waganga wanatumia viungo vya mwili vya watu wengine ili kutunza wagonjwa fulani. Lakini Yesu hakuhitaji viungo fulani ili kuponyesha watu. Alikuwa anaponyesha watu palepale, na wakati fulani aliponyesha watu wenye walikuwa mbali naye. (Yoh. 4:46-54) Miujiza hiyo yenye kushangaza inatufundisha nini? Inatufundisha kwamba Yesu mwenye amefanywa kuwa Mufalme huko mbinguni, iko na nguvu na anatamani kuponyesha watu milele. Kuelewa namna Yesu alitendea watu kunatuhakikishia kwamba, katika dunia mupya, unabii huu wa Biblia utatimia: ‘Atamusikitikia mutu wa hali ya chini na masikini.’ (Zab. 72:13) Wakati huo, Yesu ataponyesha watu wote wenye kuteseka, kwa sababu anapenda kufanya hivyo.

‘SIMAMA! UCHUKUE KITANDA CHAKO NA UTEMBEE’

7, 8. Eleza mambo yenye ilifanyika mbele Yesu akutane na mwanaume mumoja mugonjwa kwenye kisima cha Bethzatha.

7 Miezi fulani imepita tangu Yesu amuponyeshe mwanaume mumoja mwenye ukoma huko Galilaya. Anasafiri sasa kutoka Galilaya kuenda Yudea ili kuhubiri na kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu. Watu wengi sana wanaguswa moyo na ujumbe wake na namna yake ya kufundisha. Bila shaka anapenda kuhubiria masikini habari njema, kutangaza uhuru kwa wale wenye kuchukuliwa mateka [wafungwa], na kufunga majeraha (vidonda) ya watu wenye kuvunjika moyo.—Isa. 61:1, 2; Lu. 4:18-21.

8 Sasa mwezi wa Nisani umefika. Ili kuonyesha kwamba anatii amri ya Baba yake, Yesu anasafiri kuenda Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka. Muji huo ni wenye kuchangamuka kwa sababu watu wengi wanaendelea kufika kwa ajili ya sikukuu hiyo takatifu. Kaskazini mwa hekalu kulikuwa kisima chenye kuitwa Bethzatha; kwenye kisima hicho, Yesu anakutana na mwanaume mumoja mugonjwa.

9, 10. (a) Sababu gani wagonjwa na vilema walikuwa wanaenda kwenye kisima cha Bethzatha? (b) Yesu alifanya nini kwenye kisima hicho, na jambo hilo linatufundisha nini? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

9 Wagonjwa wengi sana na vilema walikuwa wanakutana kwenye kisima cha Bethzatha. Sababu gani? Kwa sababu walifikiri kwamba, ikiwa mugonjwa angeingia katika kisima hicho wakati maji inachangamuka ao kucheza-cheza, angepona kwa njia ya muujiza. Waza ni katika hali gani watu walikuwa kwenye kisima hicho. Watu hao walikuwa na huzuni, wasiwasi, na bila tumaini. Lakini, ni nini ilimuchochea Yesu, mutu mwenye hakukuwa na ugonjwa wala ulemavu wowote, aende kwenye kisima hicho? Huruma ilimuchochea Yesu amukaribie mwanaume mumoja mwenye alikuwa mugonjwa kwa miaka mingi, mbele hata Yesu akuje hapa duniani.—Soma Yohana 5:5-9.

10 Unaweza kuona katika akili yako namna mwanaume huyo mugonjwa anaangalia kwa huzuni wakati Yesu anamuuliza ikiwa anapenda kupona? Mwanaume huyo alijibu mara moja. Mwanaume huyo alipenda apone, lakini hakujua angepona namna gani, kwa sababu hakuwa na mutu wa kumusaidia aingie katika kisima. Kisha, Yesu akamuomba afanye jambo lenye haliwezekane, ni kusema, achukue kitanda chake na atembee. Kwa hiyo, mwanaume huyo akachukua kitanda chake na akaanza kutembea. Muujiza huo unaonyesha mambo makubwa yenye Yesu atafanya katika dunia mupya! Unaonyesha pia kwamba Yesu anapenda sana watu. Alitafuta watu wenye walikuwa na lazima ya musaada. Mufano wa Yesu unapaswa kutuchochea tuendelee kutafuta katika eneo letu watu wenye wanahangaishwa na mambo yote mabaya yenye inafanyika katika ulimwengu huu wa Shetani.

‘NI NANI AMEGUSA MAVAZI YANGU YA INJE?’

11. Namna gani andiko la Marko 5:25-34 linakazia upendo wa Yesu kwa wagonjwa?

11 Soma Marko 5:25-34. Kwa muda wa miaka 12, mwanamuke huyo aliishi na ugonjwa wenye ulimufanya asikie haya. Ugonjwa wake uligusa maisha yake yote, na pia ibada yake kwa Yehova. Hata kama “alikuwa ameumizwa sana na matabibu [waganga] wengi na alikuwa ametumia mali zake zote,” hali yake iliendelea kuwa mubaya zaidi. Lakini siku moja, mwanamuke huyo alifanya mupango mwengine wenye ungemusaidia apone. Alijikaza sana ili amukaribie Yesu. Alipita katikati ya kikundi cha watu wengi na kugusa vazi la inje la Yesu. (Law. 15:19, 25) Yesu alitambua kwamba nguvu fulani ilikuwa imemutoka; kwa hiyo akauliza: Ni nani amenigusa? Mwanamuke huyo ‘akaogopa na kutetemeka,’ na ‘akaanguka chini mbele yake, akamuambia kweli yote.’ Wakati alitambua kwamba Yehova, Baba yake, alikuwa amemuponyesha mwanamuke huyo, Yesu alimuambia kwa upole hivi: ‘Binti yangu, imani yako imekuponya. Enda kwa amani, na ukuwe na afya njema kutokana na ugonjwa wako wenye kuhuzunisha.’

Miujiza ya Yesu ilionyesha kwamba anatuhangaikia kabisa sisi na magumu yetu (Ona fungu la 11, 12)

12. (a) Kulingana na mambo yenye tumejifunza, umevumbua sifa gani ya Yesu? (b) Yesu alituachia mufano gani?

12 Yesu ni mwema kabisa! Tunaelewa kwamba anahangaikia kabisa wale wote wanateseka kwa sababu ya magonjwa. Shetani anapenda tusadiki kwamba hakuna mutu mwenye anaweza kutupenda, na kwamba sisi ni watu bure. Lakini, kupitia miujiza yake, Yesu alionyesha wazi kwamba anatuhangaikia kabisa sisi na magumu yetu. Kwa kweli, yeye ni Mufalme na Kuhani Mukubwa mwenye huruma! (Ebr. 4:15) Inaweza kuwa vigumu kwetu kujitia pa nafasi ya watu wenye kuwa na ugonjwa wa siku nyingi, zaidi sana ikiwa sisi wenyewe hatujapata ugonjwa kama huo. Tunaelewa kwamba Yesu alijitia pa nafasi ya wagonjwa, hata kama yeye mwenyewe hajapata ugonjwa hata kidogo. Acha basi mufano wa Yesu utuchochee kufanya nguvu yetu yote ili tujitie pa nafasi ya wagonjwa.—1 Pet. 3:8.

“YESU AKATOKWA NA MACHOZI”

13. Ufufuo wa Lazaro unaonyesha sifa gani ya Yesu?

13 Mateso ya wengine ilimuhuzunisha sana Yesu. Wakati aliona watu wanalia kwenye kifo cha rafiki yake Lazaro, Yesu “akaugua [akaumia]” na “kutaabika [kusumbuka].” Alijisikia hivyo hata kama alijua kwamba alikuwa karibu kumufufua Lazaro. (Soma Yohana 11:33-36.) Yesu hakusikia haya kulia mbele ya watu. Watu wenye walikuwa hapo, waliona namna Yesu alikuwa anapenda Lazaro na familia yake. Yesu alionyesha upendo mukubwa wakati alitumia nguvu zenye Mungu alimupatia ili kufufua rafiki yake.—Yoh. 11:43, 44.

14, 15. (a) Ni nini inaonyesha kwamba Yehova anatamani sana kumaliza magumu ya wanadamu? (b) Maneno “makaburi ya ukumbusho” inatufundisha nini?

14 Biblia inasema kwamba Yesu ni ‘mwakilisho [mufano] sawasawa wa utu [wa Muumbaji] wenyewe.’ (Ebr. 1:3) Kwa hiyo, miujiza ya Yesu ilionyesha kwamba yeye na Baba yake wanatamani sana kumaliza magonjwa, maumivu, na kifo. Yehova na Yesu wanatamani kufufua watu wengi zaidi kuliko wale wenye walifufuliwa na wenye kuzungumuziwa katika Biblia. Yesu alisema hivi: ‘Saa inakuja ambayo wale wote walio ndani ya makaburi ya ukumbusho . . . watatoka.’—Yoh. 5:28, 29.

15 Yesu alitumia maneno “makaburi ya ukumbusho,” kwa sababu maneno hayo yanaonyesha kwamba Mungu iko na uwezo wa kukumbuka mambo yote. Mungu Mweza-Yote, mwenye aliumba ulimwengu wote muzima, anaweza kukumbuka hata mambo madogo-madogo juu ya wapendwa wetu wenye walikufa, kama vile sura na tabia zao mbalimbali. (Isa. 40:26) Haimaanishe tu kwamba anaweza kukumbuka, lakini pia yeye na Mwana wake wanapenda kufanya hivyo. Ufufuo wa Lazaro na ule wa watu wengine wenye kuzungumuziwa katika Biblia, unaonyesha ufufuo wenye utafanyika duniani pote katika dunia mupya.

MIUJIZA YA YESU INATUFUNDISHA NINI?

16. Watumishi wa Yehova wenye watabaki waaminifu watapewa pendeleo gani?

16 Ikiwa tunaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu, tutajionea muujiza mukubwa wenye haujatokea hata siku moja, ni kusema, kuokoka ziki kubwa. Kisha tu vita ya Har-Magedoni, tutaona miujiza mingi sana. Wakati huo, watu wote watakuwa na afya nzuri sana. (Isa. 33:24; 35:5, 6; Ufu. 21:4) Waza kwamba unaona namna watu wanatupa lineti zao, fimbo za kuwasaidia kutembea, mikongojo (béquilles), vyombo vya kusaidia watu kusikia, na vitu vingine kama hivyo. Watu hao watapewa kazi ya kufanya. Ndiyo sababu Yehova atawapatia afya nzuri. Watatumika kwa bidii ili kufanya dunia hii, zawadi kutoka kwa Mungu, ikuwe paradiso.—Zab. 115:16.

17, 18. (a) Sababu gani Yesu alifanya miujiza? (b) Sababu gani unapaswa kujikaza sana ili uingie katika dunia mupya ya Mungu?

17 Leo, watumishi wa Mungu wa ‘mukutano mukubwa’ wanatiwa moyo wakati wanasoma habari juu ya miujiza yenye Yesu alifanya ili kuponyesha wagonjwa. (Ufu. 7:9) Miujiza hiyo inatia nguvu tumaini letu nzuri sana la kuponywa kabisa-kabisa wakati unaokuja. Hilo linaonyesha kwamba Mwana muzaliwa wa kwanza wa Mungu anapenda sana watu. (Yoh. 10:11; 15:12, 13) Upendo mukubwa wa Yesu unaonyesha kwamba Yehova anahangaikia kila mutumishi wake.—Yoh. 5:19.

18 Leo, watu wanagonjwa, wanateseka sana, na wanakufa. (Rom. 8:22) Tunahitaji kabisa dunia mupya ya Mungu; katika dunia hiyo, Yehova atatimiza ahadi yake, ni kusema, kuwapatia watu afya nzuri. Malaki 4:2 inatuhakikishia kwamba watu wenye wataponyeshwa ‘watakanyanga udongo kama ndama [vitoto vya ngombe] waliononeshwa;’ tutafurahi sana kwa sababu tutakuwa tumepona na kuwekwa huru kutoka katika hali ya kutokamilika. Kwa hiyo, tujikaze sana ili tustahili kuingia katika dunia mupya. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tuko wenye shukrani kwa Mungu na kwamba tunaamini kabisa ahadi zake. Tunatiwa moyo sana kujua kwamba miujiza yenye Yesu alifanya wakati alikuwa duniani inaonyesha mambo mengi mazuri yenye atafanyia wanadamu katika Utawala wake wa Miaka Elfu!