Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Saidia Kufanya Paradiso ya Kiroho Ikuwe Muzuri Zaidi

Saidia Kufanya Paradiso ya Kiroho Ikuwe Muzuri Zaidi

“Nitapatukuza mahali pangu pa miguu.”ISAYA 60:13.

NYIMBO: 102, 75

1, 2. Maneno “kiti cha miguu yangu” inaweza kumaanisha nini katika Maandiko ya Kiebrania?

YEHOVA MUNGU alisema hivi: “Mbingu ni kiti changu cha ufalme, na dunia ni kiti cha miguu yangu.” (Isaya 66:1) Pia, Mungu alikuwa anazungumuzia “kiti cha miguu” yake wakati alisema hivi: “Nitapatukuza mahali pangu pa miguu.” (Isaya 60:13) Namna gani anatukuza mahali pa miguu yake, ao kupafanya pakuwe nafasi muzuri sana? Na hilo linamaanisha nini kwa wale wenye kuishi kwenye kiti cha miguu yake, ni kusema, duniani?

2 Katika Maandiko ya Kiebrania, maneno “kiti cha miguu yangu” inatumiwa pia ili kuzungumuzia hekalu lenye lilikuwa katika Israeli ya zamani. (1 Mambo ya Nyakati 28:2; Zaburi 132:7) Kwa sababu hekalu ilikuwa nafasi ya kufanyia ibada ya kweli, Yehova aliliona kuwa lenye kupendeza sana. Na hekalu hilo lilitumiwa ili kumutukuza Yehova duniani.

3. Ibada ya kweli inafanyika wapi leo, na mupango huo ulianza wakati gani?

3 Ibada ya kweli inafanyika wapi leo? Haifanyike katika hekalu fulani kama katika Israeli zamani. Lakini inafanyika katika hekalu la kiroho, na hekalu hilo linamutukuza Yehova kuliko nyumba ingine yoyote. Hekalu la kiroho ni nini? Ni mupango wenye Mungu amefanya ili kuwawezesha wanadamu wakuwe marafiki wake na wamuabudu. Zabihu ya Yesu ya ukombozi ndiyo inafanya mupango huo uwezekane. Mupango huo ulianza mwaka wa 29, wakati Yesu alibatizwa na kutiwa mafuta ili akuwe Kuhani Mukubwa katika hekalu la kiroho la Yehova.—Waebrania 9:11, 12.

Watumishi wa Yehova wanapaswa kumusifu leo, hapa duniani

4, 5. (a) Kulingana na Zaburi 99, watumishi wa kweli wa Yehova wanapaswa kufanya nini? (b) Tunapaswa kujiuliza ulizo gani?

4 Tunamushukuru sana Mungu kwa sababu alifanya mupango kwa ajili ya ibada ya kweli. Tunaonyesha kwamba tunapendezwa na mupango huo wakati tunajulisha wengine jina la Yehova na zawadi nzuri sana ya zabihu ya ukombozi yenye alitoa. Tunafurahi sana kwa sababu kuna Wakristo wa kweli zaidi ya milioni 8 wenye kumusifu Yehova kila siku! Watu wenye kuwa katika dini za uongo wanajidanganya kwa kufikiri kwamba watamusifu Mungu huko mbinguni kisha wao kufa. Lakini sisi watumishi wa Yehova tunajua kwamba ni jambo la lazima sana kumusifu Yehova leo, hapa duniani.

5 Wakati tunamusifu Yehova, tunaiga watumishi wake waaminifu wenye kuzungumuziwa kwenye Zaburi 99:1-3, 5. (Soma.) Zamani, wanaume waaminifu kama vile Musa, Haruni, na Samweli walitegemeza kwa moyo wote mupango wa Mungu kwa ajili ya ibada ya kweli. (Zaburi 99:6, 7) Mbele wakuwe makuhani pamoja na Yesu mbinguni, Wakristo watiwa-mafuta wenye kuwa duniani wanamutumikia Yehova kwa uaminifu katika sehemu ya hekalu la kiroho yenye kuwa duniani. Mamilioni ya “kondoo wengine” wanawasaidia kwa uaminifu. (Yohana 10:16) Wakristo hao wote wanamuabudu Yehova katika umoja. Hata hivyo, kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Ninategemeza kwa moyo wote mupango wa Yehova kwa ajili ya ibada ya kweli?’

WALE WENYE KUTUMIKIA KWENYE HEKALU LA KIROHO LA MUNGU

6, 7. Ni magumu gani yenye ilitokea katika kutaniko la Kikristo la kwanza-kwanza, na ni jambo gani lenye lilitokea katika mwaka wa 1919?

6 Karibu miaka 100 kisha kutaniko la Kikristo kuanza, uasi-imani wenye ulitabiriwa ulikuwa umeenea. (Matendo 20:28-30; 2 Wathesalonike 2:3, 4) Kisha wakati huo, ilikuwa vigumu sana kutambua waabudu wa kweli wa Mungu. Kisha miaka mingi, Yehova alitumia Yesu ili kutambulisha wale wenye walikuwa wanamutumikia kabisa Mungu kwenye hekalu Lake la kiroho.

7 Katika mwaka wa 1919, watu wenye Mungu alikubali na wenye walikuwa wanatumikia kwenye hekalu lake la kiroho walitambuliwa waziwazi. Walikuwa wamefanya mabadiliko ili Yehova akubali kabisa ibada yao. (Isaya 4:2, 3; Malaki 3:1-4) Kwa hiyo, maono yenye mutume Paulo aliona kumepita miaka mingi sana ilianza kutimia.

8, 9. “Paradiso” yenye mutume Paulo aliona ni nini?

8 Mambo yenye mutume Paulo aliona katika maono inazungumuziwa kwenye 2 Wakorintho 12:1-4. (Soma.) Katika maono hayo, Yehova alimuonyesha mutume Paulo jambo fulani lenye lingetokea wakati unaokuja. “Paradiso” yenye mutume Paulo aliona ni nini? Kwanza, inaweza kumaanisha Paradiso yenye itakuwa duniani hivi karibuni. (Luka 23:43) Pili, inaweza kumaanisha paradiso ya kiroho kamilifu katika dunia mupya. Na tatu, inaweza kumaanisha hali nzuri sana katika “paradiso ya Mungu” huko mbinguni.—Ufunuo 2:7.

9 Hata hivyo, sababu gani mutume Paulo alisema kwamba ‘alisikia maneno yasiyoweza kutamukwa ambayo si halali [hairuhusiwe] mutu kuyasema’? Kwa sababu wakati ulikuwa haujafika ili afasirie kila jambo lenye aliona katika maono hayo ya ajabu. Lakini, leo Yehova ameturuhusu tuwaelezee wengine baraka zenye watu wake watafurahia hivi karibuni!

10. Sababu gani paradiso ya kiroho ni tofauti na hekalu la kiroho?

10 Kila mara tunazungumuzia paradiso ya kiroho, lakini, paradiso hiyo ni nini? Ni hali ya amani ya pekee yenye Mungu anawapatia watumishi wake. Kwa hiyo, paradiso ya kiroho ni tofauti na hekalu la kiroho. Hekalu la kiroho ni mupango wenye Mungu amefanya kwa ajili ya ibada ya kweli. Paradiso ya kiroho inaonyesha waziwazi wale wenye Mungu amekubali na wenye kumutolea ibada kwenye hekalu lake la kiroho.—Malaki 3:18.

11. Tuko na pendeleo gani leo?

11 Ni jambo lenye kufurahisha kujua kwamba, tangu mwaka wa 1919, Yehova amepatia wanadamu wenye hawakamilike pendeleo la kuanzisha, kutia nguvu, na kupanua paradiso ya kiroho. Je, unasaidia kufanya kazi hiyo yenye kupendeza sana? Unafurahia pendeleo lako la kutumika pamoja na Yehova ili kumuletea utukufu hapa duniani?

YEHOVA ANAENDELEA KUFANYA TENGENEZO LAKE LIKUWE MUZURI ZAIDI

12. Tunajua namna gani kwamba andiko la Isaya 60:17 limetimia? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

12 Nabii Isaya alitabiri kwamba mabadiliko mengi ya ajabu ingefanywa katika sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Mungu. (Soma Isaya 60:17.) Wakristo vijana ao wale wenye wamebatizwa hivi karibuni wamesikia ao kusoma tu habari juu ya mabadiliko hayo. Lakini kuna ndugu na dada wengi wenye wamejionea mabadiliko hayo ya ajabu sana! Wakristo hao waaminifu wamesadiki kabisa kwamba Mungu anatumia Mufalme wetu, Yesu Kristo, ili kuongoza tengenezo Lake! Wakati Wakristo hao wapendwa wanatuelezea mambo hayo yenye wamejionea katika tengenezo la Yehova, tunamutegemea kabisa Yehova, na imani yetu inakuwa nguvu.

Paradiso ya kiroho inaonyesha hali ya pekee yenye amani ambayo Wakristo wa kweli wako nayo leo

13. Kulingana na Zaburi 48:12-14, tunapaswa kufanya nini?

13 Wakristo wote wa kweli wanapaswa kuelezea watu wengine juu ya tengenezo la Yehova. Ni jambo lenye kushangaza kuona kwamba, hata kama tuko katika ulimwengu muovu wa Shetani, tunaishi kwa amani na umoja pamoja na ndugu na dada zetu katika dunia yote! Tunapaswa kuelezea kwa furaha ‘vizazi vya wakati unaokuja’ kuhusu tengenezo la Yehova na paradiso ya kiroho!—Soma Zaburi 48:12-14.

14, 15. Ni mabadiliko gani yenye ilifanywa kisha mwaka wa 1970, na tengenezo limepata faida gani?

14 Katika makutaniko yetu, ndugu na dada wengi wenye kuzeeka wamejionea mabadiliko mengi yenye imefanywa katika sehemu yenye kuonekana ya tengenezo la Yehova ili ikuwe muzuri zaidi. Wanakumbuka wakati kutaniko liliongozwa na mutumishi wa kutaniko kuliko kuongozwa na baraza la wazee, wakati biro ya tawi iliongozwa na mutumishi kuliko kuongozwa na Halmashauri ya Tawi, ao wakati Watch Tower Society iliongozwa na musimamizi kuliko kuongozwa na Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova. Hata kama ndugu hao walikuwa na wasaidizi waaminifu, ni mutu moja tu ndiye alikuwa na daraka la kuchukua maamuzi katika kutaniko, kwenye biro ya tawi, na kwenye makao yetu makubwa. Kisha mwaka wa 1970, mabadiliko ilifanywa ili baraza la wazee likuwe na daraka la kuchukua maamuzi katika kutaniko kuliko kuchukuliwa na muzee moja.

15 Sababu gani mabadiliko hayo ilileta faida katika tengenezo? Kwa sababu ilitegemea uelewaji muzuri wa Maandiko. Kuliko muzee mumoja achukue maamuzi yote, tengenezo linafaidika na sifa za wazee wote, ni kusema, “zawadi katika wanadamu,” zenye Yehova anatutolea.—Waefeso 4:8; Methali 24:6.

Yehova anatolea watu wenye kuwa katika dunia yote muongozo wenye wanahitaji katika maisha yao (Ona fungu la 16, 17)

16, 17. Ni mabadiliko gani ya hivi karibuni yenye umefurahia, na sababu gani?

16 Fikiria mabadiliko fulani yenye ilifanywa hivi karibuni kuhusu vichapo vyetu. Katika mahubiri, tunafurahi kutolea watu vichapo vyenye vitawasaidia na kuwavutia. Fikiria pia namna tunatumia teknolojia ya sasa katika kazi yetu ya kuhubiri habari njema. Kwa mufano, watu wengi zaidi wanaweza kutumia adresi yetu ya Internete jw.org ili kupata musaada wa kiroho. Mabadiliko hayo yote inaonyesha kwamba Yehova anahangaikia sana watu na anawapenda kabisa.

Tuko wenye shukrani kwa sababu tunapata mazoezi kwenye masomo yetu mbalimbali ya Biblia

17 Tunapendezwa pia na mabadiliko yenye imefanywa juu ya mikutano yetu ili tupate wakati wa kufanya ibada ya familia ao funzo la pekee. Tena tunafurahia mabadiliko yenye imefanywa juu ya programu za mikusanyiko yetu. Programu hizo zinaendelea kuwa muzuri zaidi kila mwaka! Tuko pia wenye shukrani kwa sababu tunapata mazoezi kwenye masomo yetu mbalimbali ya Biblia. Mabadiliko hayo yote, inaonyesha kabisa kwamba Yehova anaongoza tengenezo lake na kwamba anaendelea kufanya paradiso ya kiroho ikuwe muzuri zaidi!

NAMNA TUNASAIDIA PARADISO YA KIROHO IKUWE MUZURI ZAIDI

18, 19. Namna gani tunaweza kusaidia ili paradiso ya kiroho ikuwe muzuri zaidi?

18 Yehova ametupatia pendeleo la kusaidia paradiso yetu ya kiroho ikuwe muzuri zaidi. Lakini, tunafanya hivyo namna gani? Kwa kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii na kufanya wanafunzi wengi zaidi. Wakati tunasaidia mutu fulani akuwe mutumishi wa Mungu, tunasaidia kupanua paradiso yetu ya kiroho.—Isaya 26:15; 54:2.

19 Pia, tunasaidia paradiso yetu ya kiroho ikuwe muzuri zaidi wakati tunajikaza kuwa na sifa nzuri za Kikristo. Sifa hizo zinafanya paradiso ya kiroho iwavutie zaidi watu wengine. Kwa kawaida, watu hawavutiwe tu na mambo mengi yenye tunajua katika Biblia, lakini mwenendo wetu safi na wa kupenda amani ndiyo inawachochea watu waingie katika tengenezo na kumupenda Yehova na Yesu.

Unaweza kusaidia ili paradiso ya kiroho ipanuke (Ona fungu la 18, 19)

20. Kulingana na andiko la Methali 14:35, tunapaswa kufanya nini?

20 Yehova na Yesu wanafurahi sana wakati wanaona namna paradiso yetu ya kiroho inapendeza sana leo. Furaha yenye tunapata leo kwa kufanya paradiso yetu ya kiroho ikuwe muzuri zaidi ni kuonja tu furaha yenye tutapata wakati tutasaidia kufanya dunia yetu ikuwe paradiso. Tunapaswa kukumbuka kila mara andiko la Methali 14:35, lenye kusema hivi: ‘Furaha ya mufalme iko katika mutumishi anayetenda kwa ufahamu.’ Acha basi tukuwe na hekima wakati tunaendelea kutumika sana ili kufanya paradiso yetu ya kiroho ikuwe muzuri zaidi!