Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ukombozi Wenu Unakaribia”!

“Ukombozi Wenu Unakaribia”!

‘Musimame wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.’LUKA 21:28.

NYIMBO: 133, 43

1. Ni mambo gani ilitokea katika mwaka wa 66? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

FIKIRIA kwamba wewe ni Mukristo mwenye kuishi katika muji wa Yerusalemu katika mwaka wa 66. Mambo mengi inafanyika katika muji huo. Mukubwa mumoja Muroma mwenye kuitwa Florus ameiba talanta 17 katika hazina ya hekalu. Wayahudi wanakasirika mara moja. Wanaua askari wengi wa Roma na wanatangaza kwamba hawapendi tena kutawaliwa na Roma. Lakini Roma inatenda bila kukawia. Kwa kipindi cha miezi tatu, askari 30000 wenye kuongozwa na Cestius Gallus wanazunguka muji wa Yerusalemu. Wayahudi waasi wanakimbilia katika hekalu, lakini askari wa Roma wanafika kwenye ukuta wa inje wa hekalu na wanatafuta kuingia kwa nguvu. Watu wote katika muji wanaanza kuogopa sana. Ungejisikia namna gani kwa kuona mambo hayo yote?

2. Wakristo walipaswa kufanya nini wakati waliona askari wa Roma wanazunguka muji wao, na jambo hilo liliwezekana namna gani?

2 Miaka mingi mbele ya hapo, Yesu aliwaonya wanafunzi wake juu ya tukio hilo na kuwatolea maagizo haya: ‘Mutakapoona Yerusalemu limezingirwa [limezungukwa] na majeshi yaliyopiga kambi, ndipo mujue kwamba kufanywa ukiwa [kuharibiwa] kwake kumekaribia. Ndipo wale walio katika Yudea waanze kukimbilia milimani, na wale walio katikati yake na waondoke, nao wale walio katika sehemu za mashambani wasiingie ndani.’ (Luka 21:20, 21) Kwa sababu askari walikuwa wamezunguka muji wa Yerusalemu, namna gani wanafunzi wangeweza kutii maagizo ya Yesu ya kutoka katika muji? Jambo fulani lenye kushangaza lilitokea. Askari wa Roma waliondoka mara moja katika Yerusalemu! Kama vile Yesu alisema, shambulizi hilo ‘lilifupishwa.’ (Mathayo 24:22) Kisha askari kuondoka katika muji, hilo lilitolea Wakristo waaminifu nafasi ya kutii maagizo ya Yesu kwa kukimbilia kwenye milima bila kukawia. * (Ona maelezo ya chini.) Kisha, katika mwaka wa 70, Roma ilituma askari wengine katika Yerusalemu. Wakati huo, askari wa Roma waliharibu muji wa Yerusalemu. Lakini watu wote wenye walitii maagizo ya Yesu waliokolewa.

3. Ni matukio gani yenye kufanana na ile ya zamani Wakristo watapambana nayo hivi karibuni, na tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Sisi pia tunapaswa kutumia mashauri na maagizo hayo ya Yesu leo. Hivi karibuni, tutakuwa katika hali kama hiyo. Yesu alitumia matukio ya siku za mitume ili kueleza mambo yenye itatokea wakati ‘ziki kubwa’ itaanza kwa njia ya kushitukia. (Mathayo 24:3, 21, 29) Kama vile kulikuwa Wakristo waaminifu wenye waliokoka wakati muji wa Yerusalemu uliharibiwa, kutakuwa pia ‘umati mukubwa [mukutano mukubwa]’ wenye utaokoka musiba wenye utatokea katika dunia yote. (Soma Ufunuo 7:9, 13, 14.) Ni jambo la lazima sana tuelewe mambo yenye Biblia inatuambia juu ya matukio hayo ya wakati unaokuja. Sababu gani? Kwa sababu uzima wetu unategemea matukio hayo. Acha basi tuzungumuzie namna matukio hayo inahusu kila mumoja wetu.

ZIKI KUBWA INAANZA

4. Ziki kubwa itaanza namna gani?

4 Ziki kubwa itaanza namna gani? Itaanza na kuharibiwa kwa dini zote za uongo. Katika Biblia, dini za uongo zinaitwa ‘Babiloni Mukubwa, mama wa makahaba.’ (Ufunuo 17:5-7) Sababu gani zinaitwa kahaba? Kwa sababu viongozi wa dini hizo wamekosa kuwa waaminifu kwa Mungu. Kuliko kutegemeza Yesu na Ufalme wake, wameunga mukono serikali za wanadamu na kutia pembeni mafundisho ya Biblia ili waweze kuchochea sana viongozi wa politike na watu wengi zaidi. Ibada yao ni tofauti na ibada safi yenye Wakristo watiwa-mafuta wanamutolea Mungu. (2 Wakorintho 11:2; Yakobo 1:27; Ufunuo 14:4) Lakini, ni nani ataharibu Babiloni Mukubwa? Yehova atachochea “zile pembe kumi” za ule ‘munyama-mwitu mwenye rangi nyekundu’ ili “kutekeleza wazo lake.” ‘Munyama-mwitu mwenye rangi nyekundu’ anafananisha Umoja wa Mataifa, na “zile pembe kumi” zinafananisha mamlaka zote za politike zenye kumuunga mukono.—Soma Ufunuo 17:3, 16-18.

5, 6. Sababu gani tunasema kwamba watu wote wenye kuwa katika dini za uongo hawatauawa wakati Babiloni Mukubwa ataharibiwa?

5 Je, watu wote wenye kuwa katika dini za uongo watauawa wakati Babiloni Mukubwa ataharibiwa? Hapana. Kupitia roho yake, Yehova alimuongoza nabii Zekaria aandike mambo yenye itatokea wakati huo. Wakati huo, mutu fulani mwenye alikuwa katika dini ya uongo hapo zamani atasema hivi: “‘Mimi si nabii. Mimi ni mutu anayelima udongo, kwa sababu mutu fulani alinichukua tangu ujana wangu.’ Na mutu atamuambia, ‘Haya majeraha [vidonda] mwilini mwako kati ya mikono yako ni nini?’ Naye atajibu, ‘Ni yale niliyotiwa nyumbani mwa wale wanaonipenda sana.’” (Zekaria 13:4-6) Kwa hiyo, hata viongozi wa dini watasema kwamba hawana dini fulani na kwamba hawako hata kidogo katika dini hizo za uongo.

6 Watu wa Mungu watapatwa na nini wakati huo? Yesu alisema hivi: “Kwa kweli, kama siku hizo hazingefupishwa, hakuna chochote chenye mwili ambacho kingeokolewa; lakini kwa sababu ya wale waliochaguliwa siku hizo zitafupishwa.” (Mathayo 24:22) Wakati wa mitume, ziki ‘ilifupishwa’ katika muji wa Yerusalemu. Hilo lilisaidia “wale waliochaguliwa,” ni kusema, Wakristo watiwa-mafuta wakimbie. Vilevile, sehemu ya kwanza ya ziki kubwa ‘itafupishwa’ kwa sababu ya “wale waliochaguliwa.” Mungu hataacha mamlaka za siasa, ni kusema, “zile pembe kumi,” ziharibu watumishi wake. Lakini, kutakuwa kipindi kifupi cha amani kisha tu shambulizi la kwanza kumalizika.

WAKATI WA MAGUMU NA HUKUMU

7 Ni nini itatokea kisha kuharibiwa kwa dini ya uongo? Itakuwa wakati wa kuonyesha kabisa mambo yenye kuwa katika moyo wetu. Wakati huo, watu wengi watajaribu kutafuta ulinzi na musaada katika matengenezo ya wanadamu, ni kusema, “miamba ya milima.” (Ufunuo 6:15-17) Lakini, watumishi wa Yehova watategemea ulinzi kutoka kwake. Wakati shambulizi ‘lilifupishwa’ katika siku za mitume, haikuwa ndio wakati kwa Wayahudi wote kugeuka palepale na kuwa Wakristo. Lakini, ilikuwa wakati kwa wale wenye tayari walikuwa Wakristo kutoka katika muji wa Yerusalemu kama vile Yesu aliwaagiza. Vilevile wakati unaokuja, ni kusema, wakati shambulizi juu ya Babiloni Mukubwa ‘litafupishwa,’ tusitazamie kwamba watu wengi watageuka palepale na kuwa Wakristo wa kweli. Lakini, wakati huo utawatolea waabudu wote wa kweli nafasi ya kuonyesha kabisa kwamba wanamupenda Yehova na kwamba wanaunga mukono Wakristo watiwa-mafuta.—Mathayo 25:34-40.

Itakuwa nafasi ya kuonyesha kabisa kwamba tunamupenda Yehova na kwamba tunaunga mukono Wakristo watiwa-mafuta

7, 8. Watumishi wa Mungu watakuwa na nafasi gani kisha dini za uongo kuharibiwa, na namna gani wataonekana kuwa tofauti na watu wengine wakati huo?

8 Hatujue kabisa mambo yenye itatokea katika kipindi hicho kigumu. Hata hivyo, tunatazamia kwamba maisha haitakuwa mwepesi wakati huo na kwamba itatuomba kuacha mambo fulani. Wakati wa mitume, Wakristo walipaswa kuacha nyumba zao na kuvumilia magumu mengi ili waokolewe. (Marko 13:15-18) Kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Niko tayari kuacha vitu vya kimwili? Niko tayari kufanya kila jambo lenye linaombwa ili niendelee kuwa mwaminifu kwa Yehova?’ Fikiri kidogo! Hata kutokee nini wakati huo, sisi tutaendelea tu kumuabudu Mungu wetu kama vile nabii Danieli alifanya.—Danieli 6:10, 11.

“Ule mwisho” utakuwa umefika!

9, 10. (a) Watumishi wa Mungu watatangaza ujumbe gani wakati wa ziki kubwa? (b) Maadui wa watumishi wa Mungu watafanya nini?

9 Wakati wa ziki kubwa, haitakuwa wakati wa kuhubiri “habari njema ya Ufalme.” Wakati wa kuhubiri ujumbe huo utakuwa umeisha. “Ule mwisho” utakuwa umefika! (Mathayo 24:14) Watumishi wa Mungu watatangaza kwa bidii ujumbe muzito wa hukumu yenye itawafikia watu wote. Pengine ujumbe huo utaonyesha kwamba ulimwengu muovu wa Shetani unataka kuharibiwa kabisa. Biblia inafananisha ujumbe huo na mvua ya majiwe. Inasema hivi: ‘Na mvua kubwa ya majiwe iliyo na kila jiwe lenye uzito wa karibu talanta moja ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu, na wale wanadamu wakamukufuru [wakamutukana] Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya majiwe, kwa sababu pigo lake lilikuwa kubwa isivyo kawaida.’—Ufunuo 16:21.

10 Maadui wetu watasikia ujumbe huo muzito. Kupitia roho yake, Yehova alimuongoza nabii Ezekieli aeleze namna muungano ao vikundi vya mataifa, vyenye kuitwa katika Biblia,Gogu wa Magogu vitatenda. Alisema hivi: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Na itatukia katika siku hiyo kwamba mambo yataingia moyoni mwako, na wewe hakika utapanga hila yenye mazara [kuumiza]. Na wewe utasema: ‘Nitapanda juu ya inchi iliyo wazi ya mashambani. Nitawaingilia wale wasio na usumbufu, wanaokaa kwa usalama, wote wanaokaa bila ukuta, nao hawana hata mapingo na milango. Ili kuteka nyara kubwa na kupora kwa wingi, ili kuugeuzia mukono wako kuelekea mahali palipoharibiwa panapoikaliwa tena na juu ya kikundi cha watu waliokusanywa pamoja kutoka katika mataifa, wanaokusanya utajiri na mali, wale wanaokaa katikati ya dunia.’” (Ezekieli 38:10-12) Watumishi wa Mungu watakuwa tofauti kabisa na watu wengine; watakuwa kama vile wanaishi “katikati ya dunia.” Mataifa itakuwa tayari kuwashambulia. Itakuwa na hamu ya kushambulia watiwa-mafuta wa Yehova na wale wenye kuwaunga mukono.

11. (a) Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu namna matukio itafuatana wakati wa ziki kubwa? (b) Watu watakuwa katika hali gani wakati wataona alama?

11 Kisha kutatokea nini? Biblia haituambie waziwazi namna matukio hayo itafuatana, lakini inawezekana matukio fulani itatokea kwa wakati mumoja. Katika unabii wake juu ya mwisho wa ulimwengu huu muovu, Yesu alisema hivi: ‘Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota, na juu ya dunia maumivu makali ya mataifa, bila kujua njia ya kutokea kwa sababu ya kunguruma kwa bahari na musukosuko wake. Huku watu wakizimia kwa woga na tarajio la mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa. Na ndipo watamuona Mwana wa binadamu anakuja katika wingu akiwa na nguvu na utukufu mwingi.’ (Luka 21:25-27; soma Marko 13:24-26.) Je, utimizo wa unabii huo unaonyesha pia kwamba kutakuwa ishara ao alama zenye kuogopesha na matukio fulani katika anga? Tunapaswa kungojea ili tuone. Hata hivyo, tunajua kwamba wakati maadui wa Mungu wataona alama hizo, wataogopa sana na kutetemeka.

Hatutaogopa kwa sababu tunajua kwamba tutaokoka! (Ona fungu la 12, 13)

12, 13. (a) Ni nini itatokea wakati Yesu atakuja “na nguvu na utukufu mwingi”? (b) Watumishi wa Mungu watafanya nini wakati huo?

12 Ni nini itatokea wakati Yesu atakuja “na nguvu na utukufu mwingi”? Atawapatia zawadi wale wenye walibaki waaminifu na kuharibu wale wenye walikosa kuwa waaminifu. (Mathayo 24:46, 47, 50, 51; 25:19, 28-30) Ili kufasiria zaidi jambo hilo, Yesu alitumia mufano. Alisema hivi: ‘Wakati Mwana wa binadamu atafika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo ataketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mumoja kutoka kwa mwenzake, kama vile muchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi. Naye atawaweka kondoo kwenye mukono wake wa kuume, lakini mbuzi kwenye mukono wake wa kushoto.’ (Mathayo 25:31-33) Kondoo na mbuzi watapatwa na nini? Watahukumiwa. Mbuzi, ao wale wenye walikosa kuwa waaminifu, “watakatiliwa mbali milele [wataharibiwa milele].” Lakini kondoo, ao wale wenye walibaki waaminifu, watapata uzima wa milele.—Mathayo 25:46.

13 Wale wenye kufananishwa na mbuzi watafanya nini wakati watatambua kwamba wataharibiwa? ‘Watajipiga-piga wenyewe kwa kuomboleza [kulia sana].’ (Mathayo 24:30) Lakini, Wakristo watiwa-mafuta na wale wenye kuwaunga mukono watafanya nini? Watafanya kulingana na maneno haya ya Yesu: ‘Mambo haya yanapoanza kutukia, musimame wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.’—Luka 21:28.

WANAANGAA KATIKA UFALME

14, 15. Ni kazi gani ya kukusanya itafanyika kisha shambulizi la Gogu wa Magogu kuanza, na litafanyika namna gani?

14 Ni nini itatokea wakati Gogu wa Magogu ataanza kushambulia watumishi wa Mungu? Biblia inasema kwamba Mwana wa binadamu ‘atawatuma malaika zake pamoja na muvumo mukubwa wa tarumbeta, nao watawakusanya pamoja watu wake waliochaguliwa kutoka kwenye zile pepo ine, kutoka mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho wake mwingine.’ (Marko 13:27; Mathayo 24:31) Kazi hiyo ya kukusanya haizungumuzie wakati Wakristo watiwa-mafuta wanachaguliwa kwa mara ya kwanza. Tena, haizungumuzie wakati Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali duniani watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho. (Mathayo 13:37, 38) Wakristo hao watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho muda mufupi tu mbele ya ziki kubwa kuanza. (Ufunuo 7:1-4) Kwa hiyo, kazi hiyo ya kukusanya itafanywa wakati gani? Itafanywa wakati Wakristo watiwa-mafuta wenye wangali hapa duniani watapata zawadi yao ya kuenda mbinguni. (1 Wathesalonike 4:15-17; Ufunuo 14:1) Kazi hiyo ya kukusanya itafanywa wakati fulani kisha tu Gogu wa Magogu kuanza shambulizi lake. (Ezekieli 38:11) Kisha, kama vile Yesu alisema, ‘waadilifu wataangaa kwa uangavu kama jua katika Ufalme wa Baba yao.’Mathayo 13:43. * (Ona maelezo ya chini.)

15 Je, hilo linamaanisha kwamba Wakristo watiwa-mafuta “watanyakuliwa”? Watu wengi wenye kujiita kuwa Wakristo wanaamini kwamba Wakristo watachukuliwa kuenda mbinguni wakiwa na mwili wa wanadamu. Pia, wanafikiri kwamba wakati Yesu atarudia kutawala dunia, watamuona na macho ya kimwili. Lakini, Biblia inasema waziwazi kwamba wakati Yesu atarudia, watu hawatamuona na macho ya kimwili. Inasema hivi: ‘Ishara ya Mwana wa binadamu itaonekana mbinguni’ na, Yesu atakuja “juu ya mawingu ya mbinguni.” (Mathayo 24:30) Biblia inasema pia kwamba ‘nyama na damu haviwezi kuuriti Ufalme wa Mungu.’ Kwa hiyo, wale wenye wataenda mbinguni watakuwa kwanza na lazima ya ‘kubadilishwa, kwa muda mufupi, kufumba na kufumbua jicho, wakati wa tarumbeta ya mwisho.’ * (Ona maelezo ya chini.) (Soma 1 Wakorintho 15:50-53.) Hatutumie neno “kunyakuliwa” ili kuzungumuzia tukio hilo kwa sababu neno hilo linapatana na mafundisho ya uongo ya dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. Lakini, Wakristo watiwa-mafuta waaminifu wenye wangali duniani watakusanywa pamoja mara moja.

16, 17. Ni jambo gani linapaswa kufanyika mbele ya ndoa ya Mwana-Kondoo?

16 Kisha Wakristo watiwa-mafuta wote 144000 kufika mbinguni, matayarisho ya mwisho kuhusu ndoa ya Mwana-Kondoo itaanza. (Ufunuo 19:9) Lakini jambo fulani linapaswa kutokea kwanza mbele ndoa hiyo yenye kufurahisha ifanyike. Usisahau kwamba Gogu atashambulia watumishi wa Mungu wakati mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta watakuwa wangali hapa duniani. (Ezekieli 38:16) Watumishi wa Mungu watafanya nini wakati huo? Watatii maagizo haya: ‘Hamutahitaji kupigana [vita hii]. Musimame mahali penu, musimame tuli, muone wokovu wa Yehova kwa ajili yenu. . . . Musiogope wala musikuwe na hofu.’ (2 Mambo ya Nyakati 20:17) Wakati fulani kisha tu shambulizi la Gogu kuanza, Wakristo watiwa-mafuta wote wenye watakuwa wangali duniani watachukuliwa na kuenda mbinguni. Andiko la Ufunuo 17:14 linatuambia jambo lenye litafanyika wakati Gogu atashambulia watumishi wa Mungu. Maadui wa watumishi wa Mungu ‘watapigana na Mwana-Kondoo, lakini, kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mufalme wa wafalme, Mwana-Kondoo atawashinda [atapata ushindi juu yao]. Pia, wale walioitwa na waliochaguliwa na walio waaminifu pamoja naye watawashinda.’ Kwa hiyo, Yesu pamoja na wafalme watiwa-mafuta 144000 huko mbinguni, watakomboa watumishi wa Mungu wenye kuwa duniani.

17 Ukombozi huo utafanyika kupitia vita ya Har-Magedoni, yenye itatukuza jina takatifu la Yehova. (Ufunuo 16:16) Wale wote watahukumiwa kuwa mbuzi, ao wenye kukosa uaminifu, wataharibiwa. Mambo mabaya haitakuwa tena duniani, na ‘umati mukubwa’ utaokoka vita ya Har-Magedoni. Mwishowe, tukio lenye kufurahisha sana, ni kusema, ndoa ya Mwana-Kondoo yenye kuzungumuziwa katika kitabu cha Ufunuo itafanyika! (Ufunuo 21:1-4) * (Ona maelezo ya chini.) Wale wote wenye wataokoka hapa duniani, Mungu atawakubali, atawaonyesha upendo na ukarimu. Tunangojea wakati huo kwa hamu sana. Kwa kweli, karamu ya ndoa hiyo itakuwa nzuri sana!—Soma 2 Petro 3:13.

18. Kwa sababu tunangojea hivi karibuni mambo yenye kufurahisha yenye ilitabiriwa, kila mumoja wetu anapaswa kufanya nini?

18 Kwa sababu mambo hayo yenye kufurahisha itafanyika hivi karibuni, kila mumoja wetu anapaswa kuendelea kufanya nini? Yehova alimuongoza mutume Petro aandike hivi: ‘Kwa kuwa hivyo vitu vyote vitayeyushwa jinsi hiyo, ninyi munapaswa kuwa watu wa namna gani katika matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu, mukingojea na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova . . . Kwa hiyo, wapendwa, kwa kuwa munangojea mambo hayo, mufanye yote munayoweza ili mwishowe yeye awapate ninyi mukiwa bila doa na bila dosari na mukiwa katika amani.’ (2 Petro 3:11, 12, 14) Kwa hiyo, tuazimie kumutolea Yehova ibada safi, ni kusema, ibada yenye haina mafundisho ya dini za uongo, na tuunge mukono Mufalme wa Amani, Yesu Kristo.

^ fu. 2 Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 4, 2012, ukurasa wa 25-26.

^ fu. 14 Ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2013, ukurasa wa 13-14.

^ fu. 15 Wakristo watiwa-mafuta wenye watakuwa wangali duniani wakati huo hawataenda mbinguni na miili yao ya nyama na damu. (1 Wakorintho 15:48, 49) Inawezekana Mungu atafanya miili yao isionekane kama vile alifanya kuhusu mwili wa Yesu.

^ fu. 17 Zaburi ya 45 inatoa pia maelezo fulani kuhusu namna matukio hayo itafuatana. Kwanza Mufalme atapigana vita, na kisha anafanya ndoa.