Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ufikiri Sana Juu ya Upendo wa Yehova Wenye Hauna Mwisho

Ufikiri Sana Juu ya Upendo wa Yehova Wenye Hauna Mwisho

‘Nitatafakari [nitafikiri sana juu ya] utendaji wako wote.’ZABURI 77:12.

NYIMBO: 18, 61

1, 2. (a) Sababu gani uko hakika kwamba Yehova anawapenda watu wake? (b) Wakati Yehova aliumba wanadamu, aliwapatia uwezo gani?

NI NINI inakuhakikishia kwamba Yehova anawapenda watu wake? Mbele ya kujibu ulizo hilo, fikiria mifano hii: Kwa miaka mingi, ndugu na dada walimutia moyo dada Taylene. Walimuambia kwamba asitazamie kufanya zaidi ya uwezo wake. Dada Taylene anasema hivi: “Ikiwa Yehova hakuwa ananipenda, hangeendelea kunitolea mashauri.” Dada Brigitte alilea watoto wake wawili kisha bwana yake kufa. Anasema hivi: “Ni vigumu kulea watoto katika ulimwengu huu wa Shetani, zaidi sana kwa muzazi mwenye kuwa peke yake. Lakini niko hakika kwamba Yehova ananipenda kwa sababu ameniongoza wakati wa magumu, na hajaniacha hata kidogo nipate magumu yenye siwezi kuvumilia.” (1 Wakorintho 10:13) Dada Sandra iko na ugonjwa mubaya wenye hauwezi kupona. Kwenye mukusanyiko fulani, dada mumoja alionyesha kwamba anamuhangaikia kabisa. Bwana ya dada Sandra anasema hivi: “Hata kama hatukuwa tunamujua vizuri, namna alimuhangaikia Sandra ilitufurahisha sana. Upendo wenye ndugu na dada wanatuonyesha hata katika mambo madogo-madogo unanihakikishia kwamba Yehova anatupenda sana.”

2 Wakati Yehova aliumba wanadamu, aliwapatia uwezo wa kupenda na kujisikia kuwa wanapendwa. Hata hivyo, ni mwepesi kuvunjika moyo kwa sababu ya magonjwa, matatizo ya kukosa feza, ao kwa sababu hatupate matokeo mazuri katika mahubiri. Ikiwa tunaanza kufikiri kwamba Yehova hatupendi tena, tunapaswa kukumbuka kwamba sisi ni watu wa maana sana kwake na kwamba iko tayari kukamata mukono wetu wa kuume na kutusaidia. Ikiwa tuko waaminifu kwake, hawezi kutusahau hata kidogo.—Isaya 41:13; 49:15.

3. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe hakika kabisa kwamba upendo wenye Yehova anatuonyesha hauna mwisho?

3 Ndugu na dada wenye tumetoka kuzungumuzia walikuwa hakika kwamba Mungu aliwategemeza wakati wa magumu. Sisi pia tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova iko upande wetu. (Zaburi 118:6, 7) Katika habari hii, tutazungumuzia zawadi ine zenye kutuhakikishia kwamba Yehova anatupenda. Zawadi hizo ni (1) uumbaji, (2) Biblia, (3) sala, na (4) zabihu ya ukombozi. Kufikiri sana juu ya mambo mazuri yenye Yehova amefanya kunaweza kutusaidia tumushukuru sana kwa sababu ya upendo wake wenye hauna mwisho.—Soma Zaburi 77:11, 12.

UFIKIRI SANA JUU YA VITU VYENYE YEHOVA ALIUMBA

4. Vitu vyenye Yehova aliumba vinatufundisha nini?

4 Wakati tunaangalia vitu vyenye Yehova aliumba, tunaelewa kwamba anatupenda sana. (Waroma 1:20) Kwa mufano, Yehova aliumba dunia ili tuishi ndani yake na kufurahia mambo mengine. Ametupatia vitu vyote vyenye tuko navyo lazima ili tufurahie maisha. Tuko na lazima ya kula, lakini Yehova ametupatia chakula mbalimbali; na hilo linafanya tufurahie chakula! (Mhubiri 9:7) Dada Catherine anafurahia uumbaji wa Yehova, zaidi sana wakati wa kipindi cha kuota kwa majani katika inchi ya Kanada. Anasema hivi: “Inapendeza sana kuona namna vitu vinaanza kuishi tena, ni kusema, maua inaota, ndege wanarudia kutoka mahali kwenye walihamia, na hata ndege mudogo sana (colibri) anarudi bila kupotea na kufika mahali ninawekea ndege chakula inje ya dirisha la mafika yangu. Yehova anatupatia vitu hivyo vyenye kufurahisha kwa sababu anatupenda sana.” Baba yetu anapenda vitu vyenye aliumba, na anapenda sisi pia tuvifurahie.—Matendo 14:16, 17.

Wakati tunaangalia vitu vyenye Yehova aliumba, tunaelewa kwamba anatupenda sana

5. Upendo wa Yehova unaonekana namna gani katika njia wanadamu waliumbwa?

5 Wakati Yehova alituumba, alitupatia uwezo wa kufanya kazi za maana na kuzifurahia. (Mhubiri 2:24) Aliwapatia wanadamu kazi ya kuijaza dunia, kuilima, na kushugulikia samaki, ndege, na vitu vingine vyenye kuwa ndani. (Mwanzo 1:26-28) Pia, alitupatia sifa nzuri ili tuweze kumuiga!—Waefeso 5:1.

NENO LA MUNGU NI LA LAZIMA SANA

6. Sababu gani tunapaswa kupendezwa sana na Neno la Mungu?

6 Yehova ametupatia Biblia kwa sababu anatupenda sana. Biblia inatuambia mambo yenye tunapaswa kujua juu yake na namna anajisikia juu ya wanadamu. Kwa mufano, Biblia inatuonyesha namna Yehova alitenda wakati Waisraeli walimukosea kila mara. Zaburi 78:38 inasema hivi: ‘Alikuwa mwenye rehema; akawa akilifunika [akisamehe] kosa wala hakuwaharibu. Na mara nyingi akageuzia mbali hasira yake, naye akawa haiamushe gazabu yake yote.’ Kufikiri sana juu ya andiko hilo kunaweza kukusaidia kuona ni kwa kadiri gani Yehova anakupenda na kukuhangaikia. Tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova anatuhangaikia sana.—Soma 1 Petro 5:6, 7.

Biblia inatuambia mambo yenye tunapaswa kujua juu ya Mungu na namna anajisikia juu ya wanadamu

7. Sababu gani tunapaswa kuona Biblia kuwa ya lazima sana?

7 Tunapaswa kuona Biblia kuwa ya lazima sana. Sababu gani? Kwa sababu Yehova anazungumuza na sisi kupitia Neno lake. Wakati muzazi na mutoto wanazungumuza waziwazi, wanapendana na kutumainiana sana. Yehova ni Baba yetu mwenye upendo. Hata kama hatujamuonaka ao kusikia sauti yake, wakati tunasoma Biblia, ni kama vile tunazungumuza naye moja kwa moja. Tunapaswa kuendelea kumusikiliza! (Isaya 30:20, 21) Yehova anatuongoza na kutulinda. Wakati tunasoma Neno lake, tunafikia kumujua na kumutumainia.—Soma Zaburi 19:7-11; Methali 1:33.

Hata kama Yehu alipaswa kumushauria Yehoshafati, Yehova aliona “mambo mema” ndani ya mufalme huyo (Ona fungu la 8,9)

8, 9. Yehova anapenda tujue nini? Toa mufano moja wa Biblia.

8 Yehova anapenda tujue kwamba anatupenda na kwamba hakazie sana makosa yetu kwa sababu anatafuta mambo mazuri yenye kuwa ndani yetu. (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Acha sasa tuchunguze namna Yehova aliona mambo mazuri yenye ilikuwa ndani ya Mufalme Yehoshafati wa Yuda. Yehoshafati alifanya uamuzi mubaya kwa kujiunga na Mufalme Ahabu wa Israeli ili kupiganisha Wasiria huko Ramothi-gileadi. Hata kama manabii wa uongo 400 walimuambia Mufalme muovu Ahabu kwamba atapata ushindi, Mikaya, nabii wa kweli wa Yehova, aliambia Yehoshafati na Ahabu kwamba ikiwa wanapigana vita hiyo, watashindwa. Na maneno ya nabii Mikaya ilitimia kabisa. Ahabu alikufa kwenye vita, na Yehoshafati aliponea kwa bahati. Kisha vita hiyo, Yehova alitumia Yehu ili kumushauria Yehoshafati kwa sababu ya kosa lenye alifanya. Lakini, Yehu alimuambia pia hivi: “Kuna mambo mema ambayo yameonekana kwako.”—2 Mambo ya Nyakati 18:4, 5, 18-22, 33, 34; 19:1-3.

9 Miaka mingi mbele ya hapo, Yehoshafati alikuwa ameambia wakubwa, Walawi, na makuhani kwamba wazunguke katika miji yote ya Yuda ili kufundisha watu Sheria ya Yehova. Walipata matokeo mazuri sana, kwa sababu hata watu wa mataifa mengine walifikia kumujua Yehova. (2 Mambo ya Nyakati 17:3-10) Kwa hiyo, hata kama Yehoshafati alichukua uamuzi mubaya kisha, Yehova hakusahau mambo mazuri yenye alikuwa amefanya katika maisha yake hapo zamani. Mufano huo unatutia moyo sana kwa sababu wakati fulani sisi pia tunafanya makosa. Hata hivyo, ikiwa tunafanya nguvu yetu yote ili kumutumikia Yehova, ataendelea kutupenda na hatasahau mambo mazuri yenye tumefanya.

UFURAHIE PENDELEO LA KUSALI

10, 11. (a) Sababu gani sala ni zawadi ya pekee kutoka kwa Yehova? (b) Namna gani Mungu anajibu sala zetu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

10 Baba mwenye upendo anachukua wakati wa kusikiliza watoto wake wakati wanapenda kuzungumuza naye. Anapenda kujua watoto wake wanajisikia namna gani kwa sababu anawahangaikia sana. Yehova, Baba yetu mwenye upendo, anafanya hivyo. Anatusikiliza wakati tunasali kwake. Kwa hiyo, ni pendeleo kubwa sana kuzungumuza na Baba yetu!

Wakati tunasali kwa bidii, Yehova anatusikia na kutuelewa kuliko mutu mwengine yeyote

11 Tunaweza kusali kwa Yehova wakati wowote. Yeye ni Rafiki yetu, na kila mara iko tayari kutusikiliza wakati tunasali. Taylene mwenye tulizungumuzia mwanzoni, anasema hivi: “Unaweza kumuambia kila kitu ao jambo lolote.” Wakati tunamuambia Yehova mawazo yenye kuwa katika moyo wetu, anaweza kutujibu kupitia andiko fulani, habari fulani katika vichapo vyetu, ao kupitia kitia-moyo kutoka kwa ndugu ao dada yetu. Wakati tunasali kwa bidii, Yehova anatusikia na kutuelewa kuliko mutu mwengine yeyote. Wakati anajibu sala zetu, hilo linatuhakikishia kwamba upendo wake kwetu hauna mwisho.

12. Sababu gani tunapaswa kuchunguza sala zenye kupatikana katika Biblia? Toa mufano.

12 Tunaweza kujifunza mambo ya maana katika sala zenye kupatikana katika Biblia. Wakati fulani, ni vizuri kuchunguza sala fulani kati ya sala hizo wakati wa ibada ya familia. Sala zetu zitakuwa muzuri zaidi ikiwa tunafikiri sana juu ya sala za bidii zenye watumishi wa zamani wa Mungu walitoa. Kwa mufano, tunaweza kuchunguza sala yenye Yona alitoa kwa unyenyekevu wakati alikuwa katika tumbo la samaki mukubwa. (Yona 1:17–2:10) Tunaweza pia kuchunguza sala yenye Sulemani alitoa kutoka moyoni wakati wa kumutolea Yehova hekalu. (1 Wafalme 8:22-53) Na tunaweza kufikiri sana juu ya sala ya mufano ya Yesu. (Mathayo 6:9-13) Jambo la maana zaidi ni kufanya ‘maombi yetu yajulishwe Mungu’ kwa ukawaida. Kwa kufanya hivyo, ‘amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yetu na nguvu zetu za akili.’ Kwa hiyo, tutaendelea kupendezwa sana na upendo wa Yehova wenye hauna mwisho.—Wafilipi 4:6, 7.

UONYESHE KWAMBA UNAPENDEZWA NA ZABIHU YA UKOMBOZI

13. Zabihu ya ukombozi inatutolea nafasi gani?

13 Yehova alitupatia zawadi ya zabihu ya ukombozi ili “tupate uzima.” (1 Yohana 4:9) Kuhusu njia hiyo ya ajabu ya Mungu ya kuonyesha upendo, mutume Paulo aliandika hivi: ‘Kristo alikufa wakati uliowekwa kwa ajili ya watu wasiomuogopa Mungu. Kwa maana ni vigumu kwa yeyote kufa kwa ajili ya mutu mwadilifu; kwa kweli, labda, mutu anaweza kusubutu [kujaribu] kufa kwa ajili ya mutu mwema. Lakini Mungu anapendekeza upendo wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.’ (Waroma 5:6-8) Zabihu ya ukombozi ndiyo inaonyesha kwamba Mungu anatupenda sana, na inatolea wanadamu nafasi ya kuwa na urafiki wa sana pamoja naye.

14, 15. Zabihu ya ukombozi iko na faida gani kwa (a) Wakristo watiwa-mafuta? (b) wale wenye kuwa na tumaini la kuishi duniani?

14 Kikundi kidogo cha Wakristo wanajionea namna Yehova anawaonyesha upendo wenye hauna mwisho kwa njia ya pekee. (Yohana 1:12, 13; 3:5-7) Mungu amewatia mafuta kwa roho takatifu, na kwa hiyo wamefanywa kuwa watoto wake. (Waroma 8:15, 16) Kwa kuwa wamoja kati yao wangali duniani, sababu gani mutume Paulo alisema kwamba wanakaa “pamoja katika mahali pa kimbingu katika muungano na Kristo Yesu”? (Waefeso 2:6) Kwa sababu Yehova amewapatia tumaini la kuishi milele mbinguni.—Waefeso 1:13, 14; Wakolosai 1:5.

Zabihu ya ukombozi inaonyesha kwamba Yehova anapenda wanadamu wote

15 Wale wote wenye hawako Wakristo watiwa-mafuta wanaweza kuwa marafiki wa Mungu ikiwa wanaonyesha imani katika zabihu ya ukombozi. Wao pia wamepewa nafasi ya kufanywa kuwa watoto wa Mungu na kuishi milele katika paradiso duniani. Zabihu ya ukombozi inaonyesha kwamba Yehova anapenda wanadamu wote. (Yohana 3:16) Tunafurahi sana kwa sababu tunajua kwamba ikiwa tunaendelea kumutumikia Mungu kwa uaminifu, atatupatia uzima muzuri sana katika dunia mupya! Kwa hiyo, tuonyeshe kwamba tunapendezwa na zabihu ya ukombozi, ambayo inaonyesha kwa njia kubwa zaidi upendo wa Mungu wenye hauna mwisho.

UONYESHE KWAMBA UNAMUPENDA YEHOVA

16. Kisha kufikiri sana juu ya upendo wa Mungu, tutafanya nini?

16 Ni vigumu kuhesabu njia nyingi zenye Yehova anatumia ili kuonyesha kwamba anatupenda. Mufalme Daudi aliimba hivi: ‘Jinsi mawazo yako yalivyo yenye samani kwangu! Ee Mungu, jinsi jumla yake yote ilivyo kubwa! Kama ningejaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko hata chembe za muchanga.’ (Zaburi 139:17, 18) Kufikiri sana juu ya njia nyingi zenye Yehova anatumia ili kuonyesha kwamba anatupenda, kunatuchochea sisi pia tumupende na tumutumikie kwa nguvu zetu zote.

17, 18. Ni mambo gani fulani tunaweza kufanya ili kuonyesha kwamba tunamupenda Mungu?

17 Kuna mambo mengi yenye tunaweza kufanya ili kuonyesha kwamba tunamupenda Yehova. Kwa mufano, tunaweza kuhubiria wengine habari njema ya Ufalme kwa bidii. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Tunaweza pia kuonyesha kwamba tunamupenda Mungu kwa kuvumilia kwa uaminifu magumu yenye kutia imani yetu katika jaribu. (Soma Zaburi 84:11; Yakobo 1:2-5.) Hata kama tunapambana na majaribu makali, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova anaona mateso yetu na kwamba atatusaidia kwa sababu tuko watu wa maana kwake.—Zaburi 56:8.

18 Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea tufikiri sana juu ya vitu vya ajabu sana vyenye aliumba. Tunaonyesha kwamba tunamupenda Yehova na Neno lake kwa kujifunza vizuri Biblia. Tunasali kwa Yehova kwa ukawaida kwa sababu tunamupenda na tunapenda kutia nguvu urafiki wetu pamoja naye. Na wakati tunafikiri sana juu ya zabihu ya ukombozi, hilo linatuchochea tumupende zaidi. (1 Yohana 2:1, 2) Hiyo ni mambo fulani yenye tunaweza kufanya ili kuonyesha kwamba tunapendezwa na upendo wa Yehova wenye hauna mwisho.