Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ujitayarishe Tangu Leo Kuishi Katika Dunia Mupya

Ujitayarishe Tangu Leo Kuishi Katika Dunia Mupya

[Uwaambie] wafanye mema, . . . ili waushike imara uzima ulio wa kweli.”—1 TIMOTHEO 6:18, 19.

NYIMBO: 125, 40

1, 2. (a) Ni mambo gani unangojea kwa hamu katika Paradiso? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Katika dunia mupya, ni nini itatuletea furaha zaidi?

TUNANGOJEA kwa hamu “uzima wa milele.” Mutume Paulo alisema kwamba uzima huo ni “uzima ulio wa kweli.” (Soma 1 Timotheo 6:12, 19.) Kwa wengi kati yetu, hilo linatukumbusha tumaini la kuishi milele katika dunia Paradiso. Leo, hatuwezi kuelewa kabisa namna tutajisikia wakati kila asubuhi tutaamuka na afya njema, wenye furaha, na wenye kutosheka. (Isaya 35:5, 6) Fikiria furaha yenye tutapata wakati tutakuwa tunapitisha wakati pamoja na watu wa familia, marafiki, bila kusahau wale wenye watafufuliwa. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Utakuwa na wakati wa kujifunza ufundi mupya na utajua kufanya muzuri zaidi mambo yenye unafurahia. Kwa mufano, unaweza kujifunza mambo mengi juu ya sayansi. Ao unaweza kujifunza namna ya kutumia chombo fulani cha muziki ao kujijengea nyumba yako.

2 Tunangojea kwa hamu mambo hayo mazuri, lakini kumuabudu Yehova ndilo jambo lenye litatuletea furaha zaidi. Wazia maisha itakuwa namna gani wakati watu wote wataona jina la Yehova kuwa takatifu na kumukubali kuwa Mutawala wao. (Mathayo 6:9, 10) Tutafurahi sana kuona namna dunia inajaa wanadamu wakamilifu kama vile Mungu alipanga. Fikiria namna itakuwa mwepesi kwetu kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova kadiri tutafikia ukamilifu!—Zaburi 73:28; Yakobo 4:8.

3. Tunapaswa kujitayarisha kwa ajili ya nini tangu leo?

3 Tunatumaini kwamba Yehova atafanya mambo hayo ya ajabu, kwa sababu ‘kwa Mungu mambo yote inawezekana.’ (Mathayo 19:25, 26) Ikiwa tunapenda kuishi milele katika dunia mupya, huu ndio wakati wa ‘kushika imara’ uzima wa milele. Tunajua kwamba mwisho unakaribia sana; kwa hiyo, tunapaswa kuishi kwa njia yenye kuonyesha kwamba tunajua kuwa mwisho unaweza kufika wakati wowote. Tunapaswa kufanya yote yenye tunaweza leo ili kujitayarisha kwa ajili ya uzima katika dunia mupya. Tuzungumuzie basi namna ya kujitayarisha.

NAMNA YA KUJITAYARISHA

4. Namna gani tunaweza kujitayarisha tangu leo kwa ajili ya maisha katika dunia mupya? Toa mufano.

4 Namna gani tunaweza kujitayarisha tangu leo kwa ajili ya maisha katika dunia mupya? Ikiwa tunapanga kuenda kuishi katika inchi ingine, tunapaswa kufanya mambo fulani ili kujitayarisha. Kwa mufano, tunaweza kujifunza kwanza luga na desturi za watu wenye kuishi katika inchi hiyo. Tunaweza pia kuonja chakula fulani cha inchi hiyo. Vilevile, tunaweza kuanza kujitayarisha tangu leo kwa ajili ya maisha katika dunia mupya kwa kufanya yote yenye tunaweza ili kuishi kama vile tuko katika dunia mupya. Tuzungumuzie basi njia mbalimbali za kutusaidia kujitayarisha.

5, 6. Namna gani kuzoea kutii muongozo wenye tengenezo la Yehova linatutolea leo kunatutayarisha kuishi katika dunia mupya?

5 Katika ulimwengu huu, Shetani anapenda watu wafikiri kwamba wanaweza kufanya mambo yote yenye wanapenda. Watu wengi wanaona kwamba ni jambo la lazima wajiongoze wenyewe na kwamba haiko lazima wamutii Mungu. Hilo limekuwa na matokeo gani? Mateso na huzuni nyingi. (Yeremia 10:23) Lakini Yehova ni Mutawala mwenye upendo. Bila shaka, katika dunia mupya maisha itakuwa muzuri zaidi kwa sababu kila mutu atamutii Yehova.

6 Katika dunia mupya, tutafurahia kutii muongozo wenye tengenezo la Yehova litatutolea ili kufanya dunia ikuwe paradiso nzuri sana na kufundisha watu wenye watafufuliwa. Yehova atatupatia kazi nyingi za kufanya. Tutatenda namna gani ikiwa wale wenye kuongoza wanatuomba tufanye kazi fulani yenye hatupendi kabisa? Je, tutatii? Tutajikaza kutimiza kazi hiyo na kuifurahia? Ili kujitayarisha kuishi milele katika dunia mupya, tunapaswa kutii tangu leo muongozo wenye tengenezo la Yehova linatutolea.

7, 8. (a) Sababu gani tunapaswa kuunga mukono wale wenye kuongoza? (b) Wakristo fulani wameombwa kufanya mabadiliko gani? (c) Tunaweza kuwa hakika na jambo gani kuhusu maisha katika dunia mupya?

7 Ikiwa tunapenda kuwa tayari ili kuishi katika dunia mupya, tunapaswa kujifunza kutosheka na kutii muongozo wenye tengenezo la Yehova linatutolea, na kuwa na uhusiano muzuri pamoja na ndugu na dada. Tunapaswa pia kujizoeza kufurahia kazi na kuunga mukono wale wenye kuongoza. Kwa mufano, ikiwa tunapewa mugawo fulani, tunakuwa tayari kuukubali na tunajikaza kuutimiza kwa furaha na kutosheka. Ikiwa tunajizoeza leo kuunga mukono wale wenye kuongoza, tutakuwa tayari kufanya hivyo katika dunia mupya. (Soma Waebrania 13:17.) Wakati Waisraeli waliingia katika Inchi ya Ahadi, walipewa nafasi ya kuishi. (Hesabu 26:52-56; Yoshua 14:1, 2) Katika dunia mupya, hatujue nafasi ya kuishi yenye kila mumoja wetu atapewa. Lakini, ikiwa tumejizoeza kutii, tutafurahia kufanya mapenzi ya Yehova hata kama tutaishi wapi.

8 Itakuwa pendeleo kubwa sana kwetu kutumika katika dunia mupya ya Mungu yenye kutawaliwa na Ufalme wake. Kwa hiyo, tunafurahi kutii muongozo wenye tengenezo la Yehova linatutolea leo na kufanya yote yenye tunaombwa kufanya. Hata hivyo, wakati fulani, mugawo wetu unaweza kubadilika. Kwa mufano, katika inchi ya États-Unis, Wanabeteli fulani waliombwa kusimamisha kazi yao, na kutumwa katika kazi ya kuhubiri. Na kwa sababu ya uzee ao hali zingine, waangalizi fulani wenye kusafiri wameombwa kuwa mapainia wa pekee. Wanafurahia mugawo wao mupya, na Yehova anaendelea kuwabariki. Ikiwa tunaomba Yehova musaada, tunafanya yote tunaweza ili kumutumikia, na kujizoeza kukubali mugawo wowote wenye tunapewa, tutakuwa wenye furaha na Yehova atatubariki. (Soma Methali 10:22.) Utatenda namna gani katika dunia mupya, ikiwa unapenda kuishi nafasi fulani, lakini tengenezo la Yehova linakuomba uishi nafasi ingine? Wakati huo, jambo la lazima haitakuwa nafasi ya kuishi ao kazi yenye tutafanya. Tutakuwa wenye shukrani kwa sababu tunaishi katika dunia mupya.—Nehemia 8:10.

9, 10. (a) Sababu gani itatuomba kuonyesha uvumilivu katika dunia mupya? (b) Namna gani tunaweza kuonyesha uvumilivu leo?

9 Katika dunia mupya, pengine wakati fulani itatuomba kuwa wavumilivu. Kwa mufano, tunaweza kusikia watu fulani wanafurahi sana kwa sababu watu wa jamaa na marafiki wao wamefufuliwa. Hata hivyo, pengine itatuomba kungojea wakati fulani mbele wapendwa wetu wafufuliwe. Ikiwa jambo hilo linatokea, tutaonyesha uvumilivu na kufurahi pamoja na wengine? (Waroma 12:15) Ikiwa tangu leo tunajizoeza kungojea kwa uvumilivu Yehova atimize ahadi zake, hilo litatusaidia kuonyesha sifa hiyo wakati huo.Mhubiri 7:8.

10 Tunaweza pia kujitayarisha kuishi katika dunia mupya kwa kuonyesha uvumilivu wakati tunapokea mafasirio mapya juu ya kweli ya Biblia. Je, tunajifunza habari hiyo, na kuonyesha uvumilivu ikiwa hatuielewe kabisa? Tukifanya hivyo, tutakuwa tayari kuvumilia kila wakati Yehova atatutolea maagizo mapya katika dunia mupya.—Methali 4:18; Yohana 16:12.

11. Sababu gani tunapaswa kujizoeza kusamehe wengine leo, na hilo litatusaidia namna gani katika dunia mupya?

11 Kujizoeza kusamehe wengine ni njia ingine ya kujitayarisha kuishi katika dunia mupya. Katika Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu, itaomba wakati fulani upite ili tufikie ukamilifu. (Matendo 24:15) Je, tutaendelea kupendana na kusameheana? Ikiwa tunajizoeza kusamehe wengine na kuwa na urafiki pamoja nao leo, itakuwa mwepesi kufanya hivyo katika dunia mupya.—Soma Wakolosai 3:12-14.

Katika dunia mupya, tutahitaji kuonyesha sifa zenye Yehova anatufundisha leo

12. Sababu gani tunapaswa kujitayarisha leo kuishi katika dunia mupya?

12 Katika dunia mupya, inawezekana kila mara hatutapata kila kitu chenye tunapenda, ao itatuomba kungojea ili kukipata. Itaomba tukuwe wenye shukrani na wenye kutosheka katika hali yoyote. Kwa kweli, tutahitaji kuonyesha sifa zenye Yehova anatufundisha leo. Kwa hiyo, tukijizoeza kuonyesha sifa hizo leo, tutaonyesha kuwa tuko hakika kabisa kwamba dunia mupya haiko ya kuwazia tu, na kwamba tunajitayarisha kwa ajili ya uzima wa milele. (Waebrania 2:5; 11:1) Pia, tutaonyesha kwamba tunapenda kabisa kuishi katika dunia ambamo kila mutu atamutii Yehova.

KAZA AKILI YAKO JUU YA KAZI YA YEHOVA

Uhubiri habari njema kwa bidii

13. Katika dunia mupya, ni jambo gani lenye tutatia pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu?

13 Katika dunia mupya, tutakuwa na kila kitu chenye tunahitaji ili kufurahia maisha. Lakini jambo lenye litatuletea furaha kubwa kabisa ni urafiki wa sana pamoja na Yehova. (Mathayo 5:3) Yehova atatupatia kazi nyingi za kufanya, na tutafurahia kumutumikia. (Zaburi 37:4) Kwa hiyo, wakati tunamutia Yehova pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu leo, tunajitayarisha kuishi katika dunia mupya.—Soma Mathayo 6:19-21.

14. Vijana wanaweza kujiwekea miradi gani katika kazi ya Yehova?

14 Ni nini inaweza kutusaidia tufurahie zaidi kumutumikia Yehova? Njia moja ni kujiwekea miradi ya kiroho. Ikiwa wewe ni kijana, fikiria sana namna unaweza kutumia maisha yako ili kumutumikia Yehova. Kwa mufano, unaweza kutafuta katika vichapo vyetu habari zenye kuzungumuzia aina mbalimbali za utumishi wa wakati wote. Unaweza kuchagua aina moja ya utumishi huo na kuifanya ikuwe muradi wako. * (Ona maelezo ya chini.) Zungumuza na watumishi wa Yehova wenye wamefanya utumishi wa wakati wote kwa miaka mingi. Ikiwa unatumia maisha yako ili kumutumikia Yehova, utapata mazoezi mazuri. Mazoezi hayo itakusaidia umutumikie Yehova katika dunia mupya.

Ujiwekee miradi katika kazi ya Yehova

15. Taja miradi ingine yenye tunaweza kujiwekea katika kazi ya Yehova.

15 Kuna miradi mingi yenye tunaweza kujiwekea katika kazi ya Yehova. Kwa mufano, tunaweza kujifunza ufundi mupya wa kuhubiri. Ao tunaweza kujikaza kuelewa vizuri zaidi kanuni za Biblia na kujifunza namna ya kuzitumia katika maisha yetu. Tunaweza kujikaza kusoma muzuri zaidi mbele ya watu, kufundisha vizuri zaidi wakati tunatoa hotuba, na kutoa maelezo mazuri kwenye mikutano. Jambo la lazima ni hili: Wakati unajiwekea miradi katika kazi ya Yehova, hilo litakusaidia ukuwe na bidii zaidi na kujitayarisha kuishi katika dunia mupya.

NAMNA NZURI ZAIDI YA KUTUMIA MAISHA YETU LEO

Ukuwe mwenye shukrani kwa vitu vyote vyenye Yehova anakutolea

16 Je, kutumia wakati wetu ili kujitayarisha kwa ajili ya dunia mupya ya Mungu, kunamaanisha kwamba tunatumia vibaya maisha yetu? Hapana! Kumutumikia Yehova ndiyo njia nzuri zaidi ya kutumia maisha yetu. Hatufanye hivyo kwa sababu mutu fulani anatukaza, ao kwa sababu tunapenda tu kuokoka ziki kubwa. Ikiwa tuko na uhusiano muzuri pamoja na Yehova, maisha yetu inakuwa muzuri zaidi na tunakuwa wenye furaha zaidi. Hilo ndilo kusudi lake. Jambo la lazima zaidi katika maisha yetu ni kupendwa na Yehova na kuongozwa naye. (Soma Zaburi 63:1-3.) Kumuabudu Yehova kwa moyo wetu wote kunatuletea furaha. Wakristo fulani wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi wanaweza kuhakikisha kwamba hiyo ndiyo njia nzuri zaidi ya kutumia maisha yetu.—Zaburi 1:1-3; Isaya 58:13, 14.

Tafuta muongozo katika Biblia

17. Katika Paradiso, mambo yetu ya kipekee na ya kujifurahisha, itachukua nafasi gani katika maisha yetu?

17 Katika Paradiso, tutakuwa na wakati wa kufanya mambo yetu ya kipekee na ya kujifurahisha. Ni Yehova ndiye alituumba na tamaa hiyo, na ametuahidi kwamba ‘atatosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai.’ (Zaburi 145:16; Mhubiri 2:24) Tuko na lazima ya kujifurahisha na kupumuzika, lakini tunafurahia mambo hayo zaidi wakati tunatia urafiki wetu pamoja na Yehova pa nafasi ya kwanza. Itakuwa hivyo pia katika dunia mupya. Kwa hiyo, ni jambo la hekima ‘kutafuta kwanza Ufalme’ na kukazia akili yetu juu ya baraka zenye tunapata kwa kumutumikia Yehova.—Mathayo 6:33.

Wakati tuko na uhusiano muzuri pamoja na Yehova, hilo linafanya maisha yetu ikuwe muzuri zaidi na tunakuwa wenye furaha zaidi

18. Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunajitayarisha kuishi milele katika Paradiso?

18 Katika dunia mupya, maisha itakuwa muzuri zaidi kuliko namna tunawazia. Tuonyeshe basi kwamba tunatamani sana kuishi katika dunia mupya kwa kujitayarisha tangu leo kwa ajili ya “uzima ulio wa kweli.” Kwa hiyo, tukomalishe sifa zenye Yehova anatufundisha na tuhubiri habari njema kwa bidii. Tuendelee basi kutia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu, na hilo litatuletea furaha. Tuko hakika kabisa kwamba katika dunia mupya, Yehova atatimiza mambo yote yenye ameahidi. Kwa hiyo, tuishi kama vile tuko katika dunia mupya!

^ fu. 14 Ona kitabu Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2, ukurasa wa 311-318.