Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MASIMULIZI KUHUSU MAISHA YA WATU

“Na Vile Visiwa Vingi Vishangilie”

“Na Vile Visiwa Vingi Vishangilie”

Nitaendelea kukumbuka siku hiyo katika Brooklyn. Mimi na ndugu wengine kutoka sehemu mbalimbali za dunia tulikuwa tunangojea katika chumba cha kufanyia mikutano cha Baraza Lenye Kuongoza. Tulikuwa tunangojea ndugu wa Halmashauri ya Uandikaji. Tulikuwa katika chumba hicho ili kuzungumuzia namna ya kumaliza matatizo fulani yenye watafsiri wanapata katika kazi yao, na tulikuwa na wasiwasi. Ilikuwa tarehe 22 Mwezi wa 5, 2000. Lakini, sababu gani mukutano huo ulikuwa wa maana sana? Mbele niwaelezee, acha kwanza niwaambie mambo fulani juu ya maisha yangu.

Nilibatizwa katika Queensland, nilikuwa painia katika Tasmania, na nilikuwa misionere katika Tuvalu, Samoa, na Fiji

NILIZALIWA mwaka wa 1955 katika jimbo la Queensland, Australia. Kisha muda mufupi, mama yangu, Estelle, alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Kisha mwaka moja, alibatizwa, na baba yangu, Ron, alikubali kweli kisha miaka 13. Nilibatizwa katika mwaka wa 1968, katika eneo la mashamba la Queensland.

Tangu wakati nilikuwa kijana mudogo, nilipendezwa na vitabu na mambo ya luga. Kila mara wakati mimi na wazazi wangu tulisafiri kwa motokari, nilikuwa ninakaa kwenye kiti cha nyuma na kusoma kitabu fulani. Wazazi wangu walikasirika kwa sababu sikukuwa ninaangalia mazingira. Lakini kupenda kusoma kulinisaidia sana wakati nilikuwa kwenye masomo. Wakati nilikuwa kwenye masomo ya segondere katika muji wa Glenorchy, katika kisiwa cha Tasmania, nilipata zawadi nyingi.

Wakati huo, nilipaswa kuchukua uamuzi wa maana. Je, ningekubali nafasi yenye nilipewa ili kusoma bure masomo ya juu (université)? Hata kama nilipenda vitabu na kujifunza, ninamushukuru mama yangu kwa sababu alinifundisha kumupenda Yehova zaidi kuliko mutu ao kitu kingine chochote. (1 Wakorintho 3:18, 19) Wazazi wangu waliniruhusu nianze kazi ya upainia kisha tu kumaliza masomo ya segondere. Nilianza kazi ya upainia katika Mwezi wa 1, 1971, wakati nilikuwa na miaka 15.

Miaka munane yenye ilifuata, nilipata pendeleo la kuwa painia katika kisiwa cha Tasmania. Na huko, nilioa Jenny Alcock, binti mwenye sura nzuri. Tulikuwa mapainia wa pekee kwa miaka ine katika miji ya mbali ya Smithton na Queenstown.

KAZI YA UMISIONERE KATIKA VISIWA VYA PASIFIKI

Katika mwaka wa 1978, mimi na bibi yangu tulisafiri kwenda Port Moresby, huko Papouasie-Nouvelle-Guinée, ili kuhuzuria mukusanyiko fulani wa kimataifa. Ninakumbuka zaidi sana hotuba yenye misionere mumoja alitoa katika luga ya Hiri Motu. Hata kama sikuelewa mambo yenye alikuwa anasema, nilianza pia kufikiria kuwa misionere, kujifunza luga ingine, na kuwa na uwezo wa kutia moyo ndugu na dada kwa kutoa hotuba katika luga yao. Kisha, nilifikia kutambua namna ninaweza kutumia katika kazi ya Yehova uwezo wangu wa kupenda luga.

Wakati tulirudia nyumbani, tulishangaa sana kuona tunaombwa kuwa wamisionere. Tulifika katika kisiwa cha Funafuti, huko Tuvalu, Mwezi wa 1, 1979. Katika kisiwa cha Tuvalu chote, kulikuwa wahubiri 3 tu wenye kubatizwa.

Mimi na Jenny katika Tuvalu

Haikuwa mwepesi kwetu kujifunza Kituvalu. “Agano Jipya” ndiyo kitabu kimoja tu chenye kilipatikana katika luga hiyo. Kwa sababu hakukuwa hata kamusi moja ao masomo ya kujifunza luga, tuliamua kujikaza kujifunza maneno mapya 10 ao 20 kila siku. Lakini, kisha muda mufupi tulitambua kwamba hatukuwa tunaelewa vizuri maana ya maneno mengi yenye tulikuwa tunajifunza. Kuliko kuambia watu kwamba kuabudu mashetani ni mubaya, tulikuwa tunawaambia wasitumie vyombo vya kupima kilo na wasitumie fimbo kwa ajili ya kutembea! Lakini tulipaswa kuendelea kujifunza luga hiyo kwa sababu tulikuwa tumeanzisha mafunzo mengi ya Biblia. Kisha miaka mingi, mumoja kati ya wanafunzi wetu wa kwanza-kwanza wa Biblia alituambia hivi: “Tunafurahi sana kwa sababu sasa munaweza kuzungumuza muzuri luga yetu. Mwanzoni, hatukuelewa mambo yenye mulikuwa munataka kutuambia!”

Lakini, kulikuwa jambo fulani lenye lilitusaidia kujifunza haraka luga hiyo. Kwa sababu hakukuwa nyumba za kulipia, tulipaswa kuishi pamoja na familia za Mashahidi wa Yehova katika kijiji kimoja kikubwa. Tulipaswa kuzungumuza Kituvalu kila nafasi na hata nyumbani. Kisha kuacha kuzungumuza Kiingereza kwa miaka fulani, tulitambua kwamba Kituvalu imekuwa luga yetu kubwa.

Muda mufupi tu kisha sisi kufika, watu wengi walianza kufurahia kweli. Lakini tungetumia nini ili kujifunza na watu hao? Hatukuwa hata na kichapo kimoja katika luga yao. Namna gani wangeweza kufanya funzo la pekee? Wakati wangeanza kuja kwenye mikutano, wangeimba nyimbo gani, namna gani wangeweza kutoa hotuba, na namna gani wangetayarisha mikutano? Namna gani wangefikia kubatizwa? Watu hao wanyenyekevu walihitaji kupata vichapo katika luga yao ili wajifunze juu ya Yehova! (1 Wakorintho 14:9) Tulijiuliza hivi: ‘Je, itawezekana kabisa siku moja kupata vichapo katika Kituvalu, yenye kuzungumuziwa tu na watu 15000 hivi?’ Yehova alijibu maulizo hayo kupitia mambo mawili: (1) Anapenda watu wa “visiwa vilivyo mbali” wajifunze juu yake, na (2) anapenda watu wenye ulimwengu unaona kuwa ni “wanyenyekevu na wa hali ya chini” wapate kimbilio katika jina lake.—Yeremia 31:10; Sefania 3:12.

KAZI YA KUTAFSIRI ILI KUFUNDISHA KWELI

Katika mwaka wa 1980, biro ya tawi ilitupatia mugawo wa kutafsiri vichapo katika Kituvalu. Tulianza kazi hiyo hata kama tulijisikia kuwa hatujue muzuri luga hiyo. (1 Wakorintho 1:28, 29) Mwanzoni, tuliuza mashini ya zamani kutoka kwa serikali ili tuchapishe sisi wenyewe vichapo kwa ajili ya mikutano yetu. Kisha, tulitafsiri hata kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele katika Kituvalu na tulikichapisha kwa kutumia mashini ndogo. Ningali ninakumbuka namna harufu ya wino ilikuwa kali, na pia namna joto kali ilifanya ikuwe vigumu kuchapisha vichapo hivyo vyote kwa mikono. Wakati huo hatukuwa na umeme (courant)!

Haikuwa mwepesi kutafsiri katika Kituvalu kwa sababu hakukuwa kamusi ao vitabu vingine vya Kituvalu vya kutusaidia. Lakini, wakati fulani tulipata musaada katika njia zingine. Asubuhi moja nilitembelea bila kujua nyumba ya mutu mumoja mwenye alikuwa anapinga sana kweli. Mwanaume huyo mwenye kuzeeka alikuwa mwalimu, alinikumbusha kwamba hatupaswe tena kumutembelea. Kisha alisema hivi: “Ninapenda tu kukuambia jambo moja. Katika vichapo vyenu, munazoea kutumia njia ya kuandika yenye haionyeshe kitu ao mutu mwenye kutenda jambo fulani. Njia hiyo ya kuandika haitumiwe sana katika Kituvalu.” Kisha kuchunguza jambo hilo pamoja na wengine, tukaona kwamba mwanaume huyo alisema kweli. Kwa hiyo, tulifanya mabadiliko ili kutafsiri muzuri zaidi. Nilishangaa kuona kwamba Yehova alitutolea musaada kupitia mwanaume huyo mwenye alikuwa anasoma vichapo vyetu hata kama alikuwa anapinga kweli!

Habari ya Ufalme Na. 30 katika Kituvalu

Kichapo cha kwanza cha Kituvalu chenye tulitolea watu ilikuwa mwaliko wa Ukumbusho. Kisha tukapokea trakte Habari ya Ufalme Na. 30, yenye ilitolewa wakati moja na trakte ya Kiingereza. Tulifurahi sana kuona kwamba tulikuwa sasa na uwezo wa kutolea watu vichapo ao kitu fulani cha kusoma katika luga yao! Kisha muda mufupi, tulipata pia broshua na hata vitabu fulani katika Kituvalu. Katika mwaka wa 1983, Beteli ya Australia ilianza kuchapisha gazeti Munara wa Mulinzi katika Kituvalu. Gazeti hilo lilikuwa na kurasa 24 na lilikuwa linatokea kisha kila miezi tatu. Je, watu wa Tuvalu walifurahia vitabu na magazeti hayo? Ndiyo, kwa sababu walikuwa wanapenda kusoma. Kila mara tulitangaza kutolewa kwa kichapo kipya, radio ya guvernema ilitangaza habari hiyo, na wakati fulani hiyo ndiyo ilikuwa habari yenye ilizungumuziwa zaidi siku hiyo! *—Ona maelezo ya chini.

Namna gani kazi ya kutafsiri ilifanywa? Kwanza, tuliandika habari zote kwa mukono. Kisha, tuliandika mara nyingi mambo yenye tumetafsiri mupaka ilikuwa tayari kutumwa kwenye Beteli ya Australia. Kwenye Beteli hiyo, dada wawili waliandika maandishi hayo ya Kituvalu kwenye ordinatere, hata kama hawakuwa wanaelewa luga hiyo. Lakini, kuandika kwenye ordinatere maandishi hayo mara mbili na kuilinganisha kuliwasaidia waepuke makosa. Kisha, kwenye Beteli hiyo maandishi ilipangwa, ni kusema, ilitiwa pamoja na picha. Kisha walitutumia maandishi hayo kwa njia ya avion. Tuliichunguza na kuituma tena kwenye Beteli ili ichapishwe.

Kazi ya kutafsiri imekwisha kuendelea sana! Leo, ndugu na dada wenye kutafsiri wanaandika habari moja kwa moja kwenye ordinatere na kuichunguza muzuri. Kwa kawaida, mutu mwengine mwenye kuwa pamoja na watafsiri ndiye anafanya kazi ya kuchanga picha na maandishi katika vichapo. Kisha, watafsiri wanatumia Internete ili kutuma maandishi hayo kwenye Beteli zenye kuchapisha. Hakuna tena lazima ya kubeba katika dakika za mwisho-mwisho kwenye biro ya posta maandishi yenye kutafsiriwa ili kuituma.

TUNAPEWA MIGAWO INGINE

Kadiri miaka iliendelea kupita, mimi na Jenny tulipewa migawo tofauti katika maeneo mbalimbali ya Pasifiki. Katika mwaka wa 1985, tuliombwa kutoka Tuvalu na kuenda kutumikia kwenye Beteli ya Samoa. Kwenye Beteli hiyo, tulisaidia kutafsiri katika Kisamoa, Kitonga, na Kitokelau; tulisaidia pia kutafsiri katika Kituvalu. * (Ona maelezo ya chini.) Kisha, katika mwaka wa 1996, tulitumwa kutumikia kwenye Beteli ya Fiji; huko tulisaidia kutafsiri vichapo katika luga ya Kifiji, Kiribati, Kinauru, na Kituvalu.

Tulitumia vichapo katika Kituvalu ili kusaidia watu wengine

Sikuzote ninashangaa kuona namna watafsiri wanapenda kazi yao hata kama haiko mwepesi na ni yenye kuchokesha sana. Kama Yehova, ndugu na dada hao waaminifu wanapenda kabisa watu wasikie habari njema katika luga yao. (Ufunuo 14:6) Kwa mufano, wakati mipango ilichukuliwa ili kutafsiri gazeti Munara wa Mulinzi katika luga ya Kitonga, nilifanya mukutano pamoja na wazee wote katika Tonga na nikauliza ni nani angepewa mazoezi ili kuwa mutafsiri. Muzee mumoja kati yao, mwenye alikuwa fundi wa motere (mécanicien), alisema kwamba siku yenye kufuata ataacha kazi yake na kuanza mara moja kazi ya kutafsiri. Imani yake yenye kuwa nguvu ilinitia moyo, kwa sababu alikuwa na familia na hakujua namna anaweza kupata feza za kutosha ili kutimiza mahitaji ya familia yake. Lakini Yehova alimuhangaikia yeye na familia yake, na alifanya kazi ya kutafsiri kwa miaka mingi.

Kama watafsiri, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanahangaikia sana kutafsiri vichapo katika luga zote, hata katika luga zenye kuzungumuziwa na watu wadogo. Kwa mufano, ulizo lilitokezwa ili kujua ikiwa ni lazima kabisa kutafsiri vichapo katika Kituvalu. Nilitiwa moyo sana wakati nilisoma jibu hili kutoka kwa Baraza Lenye Kuongoza: “Hatuone sababu yoyote ya kuacha kutafsiri vichapo katika Kituvalu. Hata kama watu wenye kuzungumuza Kituvalu ni wadogo kwa kuwalinganisha na watu wenye kuzungumuza luga zingine, watu wangali na lazima ya kupata habari njema katika luga yao.”

Ninabatiza mutu katika maji

Katika mwaka wa 2003, mimi na Jenny tulitoka kwenye Idara ya Kutafsiri ya Fiji na kutumwa kwenye Idara ya Utumishi wa Kutafsiri ya Patterson, New York. Ilikuwa kama vile ndoto imekuwa kweli! Tulianza kutumika na kikundi chenye kusaidia kazi ya kutafsiri vichapo vyetu katika luga nyingi zaidi. Miaka mbili yenye tulifanya katika Idara ya Utumishi wa Kutafsiri, tulipewa mugawo wa kusaidia kuzoeza watafsiri katika inchi mbalimbali.

MAAMUZI YA MAANA SANA

Acha sasa nirudilie habari juu ya mukutano wa maana wenye nilitaja kwenye mwanzo wa habari hii. Katika mwaka wa 2000, Baraza Lenye Kuongoza liliona kwamba ilikuwa lazima kusaidia watafsiri katika dunia yote ili wafanye muzuri kazi yao. Watafsiri wengi walikuwa hawajapata mazoezi yoyote juu ya kazi ya kutafsiri. Kisha kumaliza mukutano pamoja na Halmashauri ya Uandikaji, Baraza Lenye Kuongoza liliamua kwamba watafsiri katika dunia yote wanapaswa kupewa mazoezi. Watafsiri walipaswa kufundishwa namna ya kuelewa Kiingereza, namna ya kumaliza matatizo yenye wanapata katika kazi yao, na namna ya kutumika katika umoja.

Mazoezi hayo imekuwa na matokeo gani? Kazi ya kutafsiri inafanywa sasa muzuri zaidi. Pia, vichapo vyetu vinatafsiriwa katika luga nyingi zaidi kuliko zamani. Katika mwaka wa 1979, wakati tulipewa mugawo wa kuwa wamisionere, gazeti Munara wa Mulinzi lilikuwa linatafsiriwa katika luga 82 tu. Hata hivyo, katika luga nyingi Munara wa Mulinzi ulikuwa unapatikana miezi kidogo kisha gazeti la Kiingereza kutolewa. Lakini sasa gazeti Munara wa Mulinzi linatafsiriwa katika luga zaidi ya 240, na katika luga nyingi kati ya hizo, gazeti hilo linatokea wakati mumoja na la Kiingereza. Leo, watu wanaweza kusoma vichapo vyenye kuwafundisha kweli ya Biblia katika luga zaidi ya 700. Miaka fulani yenye imepita, ilionekana kuwa jambo hilo haliwezekane.

Katika mwaka wa 2004, Baraza Lenye Kuongoza liliamua kwamba ilikuwa jambo la maana sana kutafsiri Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika luga nyingi zaidi na bila kukawia. Kwa hiyo, watu wengi zaidi wanaweza kusoma sasa Biblia hiyo katika luga zao. Ni kweli kabisa kwa sababu katika mwaka wa 2014, Biblia nzima ao sehemu ilipatikana katika luga 128, kati ya luga hizo kuna luga zenye kuzungumuziwa katika maeneo ya Kusini mwa Pasifiki.

Wakati Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika Kituvalu

Jambo moja lenye siwezi kusahau hata kidogo ni lile niliona katika mwaka wa 2011 kwenye mukusanyiko moja huko Tuvalu. Kwa miezi mingi, kulikuwa kipwa kali katika inchi yote. Ndugu na dada walifikiri kwamba mukusanyiko hautafanywa. Lakini jambo lenye kufurahisha ni kwamba, mangaribi ya siku yenye tulifika, mvua kubwa ilinyesha. Kwa hiyo, tulipata nafasi ya kufanya mukusanyiko wetu! Niliona kuwa ni pendeleo kubwa kutangaza kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kituvalu! Hata kama ndugu na dada wenye kuzungumuza luga hiyo ni wadogo, wao pia walipata zawadi hiyo nzuri sana kutoka kwa Yehova. Kisha, mwisho wa mukusanyiko huo, mvua kubwa ilinyesha tena. Kwa hiyo, kila mutu alipata maji mengi ya kiroho na pia maji mengi ya mvua!

Ninauliza wazazi wangu, Ron na Estelle maulizo kwenye mukusanyiko moja katika Townsville, Australia, mwaka wa 2014

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, Jenny, bibi yangu mupendwa, hakukuwa pamoja na mimi. Alikuwa amekufa katika mwaka wa 2009, kisha kugonjwa kansere kwa muda wa miaka kumi. Tuliishi pamoja naye kwa miaka 35. Wakati atafufuliwa, atafurahi kusikia kwamba Biblia ilitolewa katika Kituvalu.

Yehova amenibariki kwa kunitolea bibi mwingine muzuri, Loraini Sikivou. Loraini na Jenny walitumika pamoja kwenye Beteli ya Fiji, na Loraini pia alikuwa mutafsiri. Kwa hiyo, niko tena na bibi mwenye anamutumikia Yehova kwa uaminifu pamoja na mimi, na mwenye kupenda mambo ya luga kama mimi!

Mimi na Loraini tunahubiri katika Fiji

Kwa miaka mingi, nimeona namna Yehova, Baba yetu mwenye upendo, anahangaikia mahitaji ya watu wa luga zote, hata kama luga yao inazungumuziwa na watu wadogo tu. (Zaburi 49:1-3) Nimeona namna watu wanafurahi sana wakati wanapata vichapo vyetu kwa mara ya kwanza katika luga yao ao wakati wanamuimbia Yehova katika luga ya moyo wao. Wakati kama huo, ninatambua kwamba Yehova anatupenda sana. (Matendo 2:8, 11) Ningali ninakumbuka maneno ya Saulo Teasi, ndugu mumoja mwenye kuzeeka wa Tuvalu. Kisha kuimba nyimbo za Ufalme kwa mara ya kwanza katika luga yake, alisema hivi: “Ninafikiri kwamba unapaswa kuambia Baraza Lenye Kuongoza kwamba nyimbo hizi ni nzuri sana katika Kituvalu kuliko katika Kiingereza.”

Katika Mwezi wa 9, 2005, nilishangaa kupewa pendeleo la kuwa mumoja wa ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova. Hata kama siko tena mutafsiri, ninamushukuru Yehova kwa sababu ananipatia nafasi ya kuendelea kutegemeza kazi ya kutafsiri yenye inafanywa katika dunia yote. Ninafurahi kuona kwamba Yehova anahangaikia mahitaji ya watumishi wake wote, hata ya wale wenye kupatikana kwenye visiwa vya mbali sana katikati ya Bahari kubwa ya Pasifiki! Kwa kweli, kama vile muandikaji mumoja wa zaburi alisema, ‘Yehova amekuwa mufalme! Dunia na ishangilie. Na vile visiwa vingi vishangilie.’—Zaburi 97:1.

^ fu. 18 Ili kupata habari zaidi juu ya namna watu waliona vichapo vyetu, soma Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 12, 2000, ukurasa wa 32; Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 1, 1988, ukurasa wa 22; na Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 12, 2000, ukurasa wa 9.

^ fu. 22 Ili kupata habari zaidi juu ya kazi ya kutafsiri katika kisiwa cha Samoa, soma Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2009, ukurasa wa 120-121, 123-124.