Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ufanye Angalisho na Marafiki Wabaya Katika Siku Hizi za Mwisho

Ufanye Angalisho na Marafiki Wabaya Katika Siku Hizi za Mwisho

Mashirika [marafiki] mabaya inaharibu tabia nzuri.’ —1 WAKORINTHO 15:33.

NYIMBO: 73, 119

1. Tunaishi katika kipindi gani?

TUNAISHI katika ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’ Tangu mwaka wa 1914, wakati “siku za mwisho” zilianza, hali ya ulimwengu imekuwa mubaya zaidi kuliko wakati mwengine wowote. (2 Timotheo 3:1-5) Tunaweza kuwa hakika kwamba hali ya ulimwengu itaendelea kuwa mubaya zaidi, kwa sababu unabii wa Biblia unasema kwamba ‘watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.’—2 Timotheo 3:13.

2. Watu wengi wanafurahia mambo gani ya kujifurahisha? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Leo, watu wanaangalia ao kufanya mambo ya uasherati na ya jeuri, ao ya uchawi ili kujifurahisha. Kwa mufano, mara nyingi Internete, vipindi vya televizyo, filme, vitabu, na magazeti ya ulimwengu, vinaonyesha mambo ya jeuri na ya uasherati kuwa haina ubaya wowote. Na mwenendo wenye watu walikuwa wanaona kuwa mubaya zamani umekubaliwa sasa, na unaruhusiwa na sheria katika maeneo fulani. Lakini hilo halimaanishe kwamba Yehova naye anakubali mwenendo huo.—Soma Waroma 1:28-32.

3. Watu wengi wanaona namna gani wale wenye wanaishi kupatana na kanuni za Mungu?

3 Wakati wa mitume pia, watu waliangalia mambo ya uasherati na ya jeuri ili kujifurahisha. Lakini, wafuasi wa Yesu hawakuangalia mambo hayo kwa sababu waliishi kupatana na kanuni za Mungu. Jambo hilo “lilishangaza” watu wenye waliwazunguka. Matokeo ilikuwa nini? Watu walichekelea Wakristo na kuwatesa. (1 Petro 4:4) Leo pia, watu wengi wanazarau wale wenye wanaishi kupatana na kanuni za Mungu. Kwa kweli, Biblia inatuonya kwamba wale wenye kuiga mufano wa Kristo Yesu “watateswa pia.”—2 Timotheo 3:12.

MARAFIKI WABAYA WANAHARIBU TABIA NZURI

4. Sababu gani hatupaswe kupenda ulimwengu huu?

4 Ikiwa tunapenda kufanya mapenzi ya Mungu, hatutapenda ‘ulimwengu ao vitu vilivyo katika ulimwengu.’ (Soma 1 Yohana 2:15, 16.) Shetani, ‘mungu wa mufumo huu wa mambo,’ anatawala ulimwengu huu. Anatumia dini ya uongo, mashirika ya biashara, na vyombo vya kutangaza habari kama vile radio, televizyo, na Internete ili kudanganya watu. (2 Wakorintho 4:4; 1 Yohana 5:19) Hatupendi ulimwengu huu utuchochee, ndiyo sababu, tunapaswa kuepuka marafiki wabaya, ni kusema, watu ao mambo yenye inaweza kutuchochea kufanya mambo mabaya. Biblia inasema waziwazi hivi: ‘Musipotoshwe [musidanganywe]. Mashirika mabaya inaharibu tabia nzuri.’—1 Wakorintho 15:33.

5, 6. Tunapaswa kuepuka kufanya urafiki na nani, na sababu gani?

5 Ili tuendelee kuwa na uhusiano muzuri pamoja na Yehova, tunapaswa kuepuka kufanya urafiki pamoja na mutu yeyote mwenye anazoea kufanya matendo mabaya. Hilo linahusu pia watu wenye kusema kwamba wanamuabudu Yehova lakini wanamukosea kwa kupenda. Ikiwa watu kama hao wanafanya zambi nzito na wanakosa kutubu, tunavunja urafiki pamoja nao.—Waroma 16:17, 18.

6 Kwa kawaida, watu wanapenda kufurahisha marafiki wao na wanapenda kukubaliwa nao. Kwa hiyo, ikiwa tunafanya urafiki pamoja na watu wenye hawamutii Mungu, tunaweza kuiga tabia zao. Kwa mufano, ikiwa tunafanya urafiki wa sana pamoja na watu wenye kufanya mambo ya uasherati, tunaweza kuwaiga pia. Ndugu na dada zetu fulani wameangukia katika mutego huo. Na wale wenye walikosa kutubu walitengwa na kutaniko. (1 Wakorintho 5:11-13) Ikiwa hawatubu, hali yao inaweza kufanana na ile yenye mutume Petro anazungumuzia.—Soma 2 Petro 2:20-22.

7. Tunapaswa kufanya urafiki wa sana pamoja na watu gani?

7 Hata kama tunapenda kutendea watu wote kwa wema, hatupaswe hata kidogo kufanya urafiki wa sana pamoja na wale wenye hawamutii Mungu. Ni mubaya ikiwa Shahidi wa Yehova anachumbiana na mutu mwenye haiko mutumishi wa Yehova mwenye kubatizwa. Ni vizuri zaidi kukubaliwa na Mungu kuliko kukubaliwa na watu wenye hawamupendi. Tunapaswa tu kufanya urafiki wa sana na watu wenye kufanya mapenzi ya Mungu. Yesu alisema hivi: “Yeyote yule anayefanya mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu na dada yangu na mama yangu.”—Marko 3:35.

Ni vizuri zaidi kukubaliwa na Yehova kuliko kukubaliwa na watu wenye hawamupendi

8. Marafiki wabaya walikuwa na matokeo gani juu ya Waisraeli wa zamani?

8 Marafiki wabaya wanatuingiza katika hatari. Kwa mufano, tufikirie jambo lenye liliwapata Waisraeli. Mbele waingie katika Inchi ya Ahadi, Yehova aliwaonya juu ya watu wenye walikuwa wanaishi katika inchi hiyo. Aliwaambia hivi: ‘Musiinamie miungu yao wala kuchochewa kuitumikia, wala musifanyize chochote kilicho kama kazi zao, bali lazima mutawaangusha nawe lazima uzivunje nguzo zao takatifu. Nanyi mutamutumikia Yehova Mungu wenu.’ (Kutoka 23:24, 25) Lakini Waisraeli wengi hawakutii maagizo ya Mungu; kwa hiyo, hawakuendelea kuwa waaminifu kwake. (Zaburi 106:35-39) Matokeo ilikuwa nini? Kisha muda fulani, Yehova aliwakataa na akachagua kutaniko la Kikristo kuwa watu wake.—Mathayo 23:38; Matendo 2:1-4.

UKUWE MWANGALIFU JUU YA MAMBO YENYE UNASOMA NA KUANGALIA

9. Sababu gani vyombo vya kutangaza habari vya ulimwengu huu vinaweza kutuingiza katika hatari?

9 Vyombo vingi vya kutangaza habari vya ulimwengu huu, kama vile programu za televizyo, Internete, na vitabu, vinaweza kuharibu urafiki wetu pamoja na Yehova. Kusudi la vyombo hivyo haiko kusaidia Wakristo wakuwe na imani katika Yehova na katika ahadi zake. Lakini, vinachochea watu wamutumainie Shetani na ulimwengu wake muovu. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu sana ili tusiangalie, kusoma, ao kusikiliza mambo yenye inaweza kutuchochea tukuwe na “tamaa za kilimwengu.”—Tito 2:12.

10. Vyombo vya kutangaza habari vya ulimwengu huu vitapatwa na nini?

10 Hivi karibuni, ulimwengu wa Shetani na vyombo vyake vya kutangaza habari vyenye kuleta hatari vitaharibiwa. Biblia inasema hivi: “Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:17) Muandikaji mumoja wa zaburi aliandika hivi: “Watenda-maovu watakatiliwa mbali.” Kisha aliongeza hivi: ‘Bali wale wanaomutumainia Yehova ndio watakaomiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.’ Kwa muda gani? “Waadilifu [wenye haki] wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”—Zaburi 37:9, 11, 29.

11. Namna gani Mungu anatusaidia tubaki waaminifu kwake?

11 Tofauti na ulimwengu wa shetani, tengenezo la Yehova linatusaidia kuishi kwa njia yenye itatusaidia kupata uzima wa milele. Yesu alisali kwa Yehova hivi: ‘Uzima wa milele ndio huu, [wafikie kukujua] wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na yule uliyemutuma, Yesu Kristo.’ (Yohana 17:3) Yehova anatumia tengenezo lake ili kututolea mambo yote yenye tunahitaji ili tufikie kumujua. Kwa mufano, magazeti, broshua, vitabu, video, na adresi yetu ya Internete, vinatusaidia tumutumikie Mungu. Tengenezo lake linafanya pia mipango ili ndugu na dada katika dunia yote wakusanyike kwa ukawaida katika makutaniko zaidi ya 110000. Mafundisho ya Biblia yenye tunapata kwenye mikutano hiyo na mikusanyiko mikubwa-mikubwa inatia nguvu imani yetu katika Yehova na katika ahadi zake.—Waebrania 10:24, 25.

KUOA AO KUOLEWA “KATIKA BWANA TU”

12. Eleza maana ya amri ya Biblia ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu.”

12 Wakristo wenye wanapenda kuoa ao kuolewa, wanapaswa kuwa waangalifu sana kuhusu mutu mwenye wanachagua kuchumbia. Neno la Mungu linatuonya hivi: ‘Musifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria? Ao nuru ina ushirika gani na giza?’ (2 Wakorintho 6:14) Biblia inawaomba watumishi wa Mungu waoe ao kuolewa “katika Bwana tu,” ni kusema, kuoa ao kuolewa tu na mutu mwenye amekwisha kujitoa kwa Mungu na kubatizwa, na mwenye anaishi kupatana na kanuni za Yehova. (1 Wakorintho 7:39) Wakati unaoa ao kuolewa na mutu kama huyo, ni kusema, mutu mwenye kumupenda Yehova, unapata mutu mwenye atakusaidia uendelee kuwa mwaminifu kwa Mungu.

Wakati unaoa ao kuolewa na mutu mwenye anamupenda Yehova, unapata mutu mwenye atakusaidia uendelee kuwa mwaminifu kwa Mungu

13. Mungu aliwapatia Waisraeli amri gani juu ya ndoa?

13 Yehova anajua mambo yenye inafaa kabisa kwetu, na amri yake ya kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu” haiko ya sasa. Kwa mufano, fikiria mambo yenye Yehova aliwaambia Waisraeli juu ya watu wenye hawakuwa watumishi wake. Kupitia Musa, aliwatolea amri hii: ‘Nawe usifanye mapatano yoyote ya ndoa pamoja nao. Binti zako usiwape wana wake, wala binti zake usiwachukue kwa ajili ya wana wako. Kwa maana watawageuza wana wako waache kunifuata, nao watatumikia miungu mingine; na hasira ya Yehova itawaka kwelikweli juu yenu, naye hakika atakuangamiza haraka.’—Kumbukumbu la Torati 7:3, 4.

14, 15. Sulemani alipatwa na jambo gani kwa sababu ya kuzarau amri ya Yehova juu ya ndoa?

14 Kisha kuwa mufalme wa Israeli, Sulemani alisali ili Yehova amupatie hekima, na Yehova alijibu sala yake. Kwa hiyo, Sulemani akakuwa mufalme mwenye kujulikana sana wa taifa lenye kuendelea. Kwa kweli, malkia wa Sheba alishangazwa sana na hekima ya Sulemani na alimuambia hivi: “Umezidi katika hekima na mafanikio, mambo yale niliyoyasikia.” (1 Wafalme 10:7) Lakini, mufano wa Sulemani unatufundisha jambo lenye linaweza kutufikia ikiwa tunazarau amri ya Mungu ya kuoa ao kuolewa tu na mutu mwenye anamutumikia.—Mhubiri 4:13.

15 Hata kama Yehova alikuwa amemubariki, Sulemani hakutii amri ya Mungu yenye ilikuwa wazi. Sulemani ‘akawapenda wanawake wengi wageni’ wenye hawakuwa wanamutumikia Yehova, na alifikia kuwa na bibi 700 na masuria 300. Matokeo ilikuwa nini? Wakati Sulemani alikuwa muzee, bibi zake ‘waligeuza moyo wake ukaifuata miungu mingine, . . . na Sulemani akaanza kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.’ (1 Wafalme 11:1-6) Bibi hao walimuchochea, na hakuendelea tena kuwa muaminifu kwa Yehova. Kwa sababu jambo hilo lilimufikia Sulemani, linaweza pia kumufikia kila Mukristo kati yetu. Ndiyo sababu hatufikirie hata kidogo kuoa ao kuolewa na mutu mwenye hamupendi Yehova!

16. Ni shauri gani Biblia inatolea mutu mwenye kuoa ao kuolewa na mutu mwenye haiko Shahidi wa Yehova?

16 Tuseme nini juu ya mutu mwenye anakuwa Shahidi wa Yehova kisha kuoa ao kuolewa na mutu mwenye haiko Shahidi? Biblia inasema hivi: ‘Ninyi wake [bibi], mujitiishe kwa waume [bwana] zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu kwa lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa wake zao.’ (1 Petro 3:1) Kwa kweli, maneno hayo inahusu pia bwana mwenye iko na bibi mwenye haiko Shahidi wa Yehova. Shauri hilo la Biblia liko wazi: Ukuwe bwana ao bibi muzuri, na utumikishe kanuni za Mungu katika ndoa yako. Kwa hiyo, wakati bibi ao bwana yako ataona kwamba umebadilika, anaweza pia kuwa na tamaa ya kumutumikia Yehova. Ndugu na dada wengi wenye kuoa ao kuolewa wamejionea jambo hilo.

UFANYE URAFIKI NA WATU WENYE KUMUPENDA YEHOVA

17, 18. Ni nini ilimusaidia Noa aokoke Garika, na ni nini iliwasaidia Wakristo wa wakati wa mitume waokoke uharibifu wa muji wa Yerusalemu?

17 Marafiki wabaya wanaweza kukuchochea ukose kumutii Yehova, lakini marafiki wazuri wanaweza kukusaidia uendelee kuwa mwaminifu kwake. Noa alituachia mufano muzuri. Aliishi wakati “ubaya wa mwanadamu ulikuwa mwingi duniani” na ‘kila mwelekeo wa fikira za moyo wake ulikuwa mubaya tu wakati wote.’ (Mwanzo 6:5) Kwa sababu watu walikuwa wabaya sana, Yehova aliamua kuharibu ulimwengu huo muovu. Lakini Noa alikuwa tofauti na watu hao. Biblia inamuita ‘mutu mwadilifu’ na mwenye “alitembea pamoja na Mungu wa kweli.”—Mwanzo 6:7-9.

18 Noa hakufanya urafiki na watu wenye hawakuwa wanamupenda Yehova. Yeye na familia yake walitumika sana ili kujenga safina, na alikuwa pia ‘muhubiri wa uadilifu.’ (2 Petro 2:5) Noa, bibi yake, watoto wake watatu, na bibi za watoto wake walikuwa na uhusiano muzuri kati yao. Waliendelea kufanya kwa bidii kazi yenye kumupendeza Mungu, na matokeo ni kwamba, waliokoka Garika. Sisi wote leo tuko wazao wao, kwa hiyo, tunapaswa kuwa wenye shukrani kwa sababu Noa na familia yake walimutii Yehova na waliepuka kuwa na marafiki wabaya. Vilevile, Wakristo wa wakati wa mitume hawakufanya urafiki na watu wenye hawakuwa wanamupenda Yehova. Walimutii Yehova na kuokolewa wakati muji wa Yerusalemu uliharibiwa katika mwaka wa 70.—Luka 21:20-22.

Kufanya urafiki na wale wanamupenda Yehova kunaweza kutusaidia tufikirie namna maisha itakuwa katika dunia mupya

(Ona fungu la 19)

19. Ni nini itatusaidia kubaki waaminifu kwa Yehova?

19 Sisi pia tunaiga mufano wa Noa, familia yake, na Wakristo wa wakati wa mitume, kwa kuepuka kufanya urafiki na mutu yeyote mwenye hamupendi Yehova. Tunaweza kuchagua marafiki wetu kati ya mamilioni ya ndugu na dada zetu waaminifu. Watatusaidia ‘kusimama imara katika imani,’ katika nyakati hizi ngumu sana. (1 Wakorintho 16:13; Methali 13:20) Wazia namna itapendeza sana kuokoka mwisho wa ulimwengu huu muovu na kuishi katika dunia mupya ya Yehova! Ni jambo la lazima sana kuepuka marafiki wabaya sasa!