Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Njia Gani Zenye Kuonyesha Kwamba Yehova Anatupenda?

Ni Njia Gani Zenye Kuonyesha Kwamba Yehova Anatupenda?

Muone namna ya upendo ambao Baba ametupa sisi!’—1 YOHANA 3:1.

NYIMBO: 91, 13

1. Mutume Yohana anatutia moyo tufikiri juu ya nini, na sababu gani?

MUTUME Yohana anatutia moyo tufikiri sana juu ya upendo mukubwa wenye Yehova anatuonyesha. Andiko la 1 Yohana 3:1 linasema hivi: ‘Muone namna ya upendo ambao Baba ametupa sisi!’ Wakati tunafikiri sana juu ya namna Yehova anatupenda na njia zenye anatumia ili kutuonyesha upendo, tunamukaribia na kumupenda zaidi.

2. Sababu gani watu fulani wanashindwa kuelewa kwamba Mungu anawapenda?

2 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu fulani hawaelewe namna gani Mungu anaweza kuwapenda. Wanawaza kama Mungu hahangaikie watu. Pengine wanaamini kwamba Mungu anapatia tu watu sheria na kupatia malipizi wale wenye hawamutii. Kwa sababu ya mafundisho ya uongo, watu fulani wanafikia kuwaza kama Mungu ni mukali sana na kwamba haiwezekane kumupenda. Wengine wanafikiri kwamba Mungu anapenda watu wote hata kama wanafanya mambo mazuri ao mabaya. Lakini kujifunza Biblia kumekusaidia ufikie kujua ukweli juu ya Yehova. Unajua kwamba upendo ndiyo sifa yake kubwa sana na kwamba alitoa Mwana wake kuwa zabihu ya ukombozi kwa ajili yako. (Yohana 3:16; 1 Yohana 4:8) Lakini, unaweza kushindwa kuelewa kwamba Yehova anakupenda sana kwa sababu ya magumu yenye umepata katika maisha yako.

3. Ni nini inaweza kutusaidia tuelewe kwamba Yehova anatupenda?

3 Ili tuelewe kwamba Yehova anatupenda, ni lazima tujue kwanza kwamba ni yeye alituumba. Alitupatia uzima. (Soma Zaburi 100:3-5.) Ndiyo sababu Biblia inamuita mwanadamu wa kwanza “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Pia, Yesu alitufundisha tumuite Yehova “Baba yetu uliye mbinguni.” (Mathayo 6:9) Kwa hiyo, Yehova ni Baba yetu, na anatupenda kama vile baba muzuri anawapenda watoto wake.

4. (a) Yehova ni Baba wa namna gani? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii na ile yenye kufuata?

4 Watu fulani wanashindwa kuelewa kwamba baba yao anawapenda. Pengine ni kwa sababu wanakumbuka mambo mabaya yenye baba yao aliwatendea wakati walikuwa wangali watoto. Yehova hawezi hata kidogo kutendea watoto wake hivyo. Yeye ndiye Baba muzuri zaidi. (Zaburi 27:10) Anatupenda sana na anatuhangaikia katika njia mbalimbali. Wakati tunaendelea kuelewa namna Yehova anatupenda, hilo linatufanya tumupende zaidi. (Yakobo 4:8) Katika habari hii, tutazungumuzia njia ine zenye Yehova anatumia ili kutuonyesha upendo. Na katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia njia ine zenye tunaweza kutumia ili kuonyesha kwamba tunamupenda Yehova.

YEHOVA NI MWENYE UPENDO NA MUKARIMU

5. Mungu amewapatia watu wote nini?

5 Wakati mutume Paulo alikuwa katika muji wa Athene, Ugiriki, aliona sanamu nyingi na alitambua kwamba watu waliamini kama miungu yao ndiyo iliwapatia uzima. Kwa hiyo, aliwahubiria juu ya ‘Mungu aliyefanya ulimwengu na vitu vyote vilivyo ndani.’ Aliwaambia kwamba Mungu ‘anawapatia watu wote uhai [uzima] na pumuzi na vitu vyote’ na kwamba “kupitia kwake tuna uhai na tunaenda na kuwako.” (Matendo 17:24, 25, 28) Yehova anatupatia kila kitu chenye tuko nacho lazima ili tuishi na tufurahie maisha. Tufikirie vitu fulani vyenye Yehova ametupatia vyenye kuonyesha kwamba anatupenda.

6. Yehova ametupatia nafasi ya kuishi yenye kuwa namna gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

6 Kwa mufano, Yehova ametutayarishia nafasi nzuri ya kuishi. (Zaburi 115:15, 16) Kati ya sayari (planètes) zote zenye aliumba, dunia ni tofauti kabisa na sayari zingine zote. Wanasayansi wamesafiri katika anga na wamevumbua sayari nyingi, lakini hawajapata sayari yenye kuwa na kila kitu chenye wanadamu wako nacho lazima ili kuishi. Yehova anatupatia kila kitu chenye tuko nacho lazima ili tuendelee kuishi, lakini pia aliumba dunia ili ikuwe nafasi yenye kufaa, yenye kupendeza, na yenye kuwa salama ili tufurahie maisha. (Isaya 45:18) Wakati tunafikiri juu ya nafasi ya kuishi yenye Yehova, Baba yetu wa mbinguni, ametupatia, tunaelewa kabisa kwamba anatupenda sana.—Soma Ayubu 38:4, 7; Zaburi 8:3-5.

7. Wakati Yehova alituumba, alitupatia uwezo gani wenye kuonyesha kwamba anatupenda?

7 Wakati Yehova alituumba, alitupatia uwezo wa kumuiga. Hiyo ni njia ingine yenye kuonyesha kwamba anatupenda. (Mwanzo 1:27) Ni kusema, tunaweza kujionea namna Yehova anatupenda na kisha sisi pia tunaonyesha kwamba tunamupenda. Anajua kwamba kufanya hivyo kunatuletea furaha ya kweli. Kwa kweli, watoto wanafurahi sana wakati wanaona kwamba wazazi wao wanawapenda. Pia, ukumbuke kwamba, Yesu alitufundisha kama tutakuwa na furaha ikiwa tunamukaribia Yehova, Baba yetu. (Mathayo 5:3) Anatupatia ‘vitu vyote ili tuvifurahie.’ Ndiyo, Yehova ni mukarimu na anatupenda sana.—1 Timotheo 6:17; Zaburi 145:16.

YEHOVA ANATUFUNDISHA KWELI

8. Sababu gani tunapenda Yehova atufundishe?

8 Baba wanapenda watoto wao na hawawezi kupenda wadanganywe. Lakini, leo wazazi wengi hawatii kanuni za Biblia juu ya mema na mabaya. Kwa hiyo, hawawezi kuongoza vizuri watoto wao, na mara nyingi hilo linafanya familia ikuwe na huzuni na ikose furaha. (Methali 14:12) Lakini, Yehova anawapatia watoto wake muongozo muzuri zaidi kwa sababu yeye ni “Mungu wa ukweli.” (Zaburi 31:5) Anafurahi kutufundisha kweli juu yake. Anatufundisha pia namna ya kumuabudu na anatuonyesha njia nzuri zaidi ya kutumia maisha yetu. (Soma Zaburi 43:3.) Kwa hiyo, mambo yenye Yehova ametufundisha, inaonyesha namna gani kwamba anatupenda sana?

Baba Wakristo wanamuiga Yehova kwa kufundisha watoto wao kweli na kuwasaidia wakuwe na urafiki muzuri pamoja na Baba yao wa mbinguni (Ona fungu la 8-10)

9, 10. (a) Sababu gani Yehova anatufundisha mambo mengi juu yake? (b) Anatufundisha nini juu ya mipango yake kwa ajili yetu?

9 Kwanza kabisa, Yehova anatuelezea mambo mengi juu yake. Anapenda tufikie kumujua. (Yakobo 4:8) Ndiyo sababu anatuambia jina lake. Biblia inataja jina lake mara nyingi kuliko jina lingine lolote. Pia, Yehova anatuambia yeye ni Mutu wa namna gani. Wakati tunaangalia vitu vyenye aliumba, tunaelewa kwamba ni mwenye nguvu na mwenye hekima. (Waroma 1:20) Na wakati tunasoma Biblia, tunaelewa kwamba yeye ni mwenye haki na anatupenda sana. Wakati tunafikia kujua sifa nzuri za Yehova, tunajisikia kuwa karibu naye.

Wakati tunafikia kujua sifa nzuri za Yehova, tunajisikia kuwa karibu naye

10 Yehova anatufundisha pia mipango yake. Anatuambia kwamba tuko katika familia yake. Anatuelezea pia mambo yenye anapenda tufanye ili tutumike katika umoja na amani pamoja na kila mutu katika familia yake. Biblia inaonyesha wazi kwamba wakati Yehova alituumba, hakutupatia haki ya kujiamulia sisi wenyewe mema na mabaya. (Yeremia 10:23) Yehova anajua kabisa mambo yenye tuko nayo lazima. Anajua pia kwamba tutakuwa na maisha yenye amani na yenye furaha ikiwa tu tunakubali atutawale na kumutii. Yehova ametufundisha mambo hayo yote ya maana kwa sababu anatupenda.

11. Baba yetu mwenye upendo ametufundisha nini juu ya wakati unaokuja?

11 Baba mwenye upendo anafikiri sana juu ya wakati unaokuja wa watoto wake. Anapenda wakuwe na maisha yenye furaha. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, leo watu wanahangaika juu ya wakati wao unaokuja, na wengi wanatumia sana maisha yao ili kutafuta vitu vyenye haviwezi kukawia. (Zaburi 90:10) Tunamushukuru sana Baba yetu, Yehova, kwa sababu ametufundisha namna ya kuwa na maisha yenye furaha leo, na ametuahidi wakati unaokuja muzuri zaidi!

YEHOVA ANAONGOZA WATOTO WAKE NA KUWAPATIA NIZAMU

12. Yehova alitolea Kaini na Baruku mashauri gani?

12 Wakati Yehova aliona kwamba Kaini anataka kufanya zambi, alijaribu kumusaidia kwa kumuuliza hivi: ‘Kwa nini umewaka hasira na kwa nini uso wako umekunjama? Ukigeuka utende mema, je, hautainuliwa?’ (Mwanzo 4:6, 7) Kaini alikataa shauri la Yehova, na akapatwa na matokeo mabaya. (Mwanzo 4:11-13) Wakati mwingine, Yehova alitambua kwamba Baruku alikuwa amechoka na kuvunjika moyo kwa sababu alikuwa na mawazo mabaya. Kwa hiyo, Yehova alimuambia Baruku kwamba mawazo yake ilikuwa mubaya na kwamba anapaswa kuibadilisha. Baruku alitii shauri la Yehova, na hilo lilifanya aokoe uzima wake.—Yeremia 45:2-5.

13. Mambo yenye watumishi waaminifu wa Yehova walijifunza wakati wa magumu, iliwasaidia namna gani?

13 Yehova anatuongoza na kutupatia nizamu kwa sababu anatupenda. Anatupatia mashauri wakati tuko nayo lazima, lakini anatuzoeza pia. (Waebrania 12:6) Katika Biblia, tunasoma habari za watumishi waaminifu wenye Yehova alizoeza ili wakuwe watu wazuri. Kwa mufano, Yosefu, Musa, na Daudi walipatwa na magumu makali sana. Wakati wa magumu hayo, Yehova alikuwa pamoja nao. Na mambo yenye walijifunza wakati wa magumu hayo, iliwasaidia wakati Yehova aliwapatia madaraka makubwa zaidi. Wakati tunasoma katika Biblia namna Yehova alitegemeza na kuzoeza watu wake, tunaelewa kwamba anatupenda kabisa.—Soma Methali 3:11, 12.

14. Wakati tunafanya makosa, namna gani Yehova anaonyesha kwamba anatupenda?

14 Hata wakati tunafanya makosa, Yehova anaendelea kutuonyesha kwamba anatupenda. Ikiwa tunakubali nizamu yake na kutubu, anatusamehe “kwa njia kubwa.” (Isaya 55:7) Hilo linamaanisha nini? Maneno ya Daudi inatuonyesha kwamba Yehova ni Baba mwenye kusamehe na mwenye rehema. Daudi aliandika hivi: ‘Yeye anasamehe makosa yako yote, na anaponyesha magonjwa yako yote; anaokoa uhai [uzima] wako kutoka katika shimo, anakuvika taji la fazili zenye upendo na rehema. Kama vile mashariki iko mbali sana na mangaribi, ndivyo ameweka makosa yetu mbali sana na sisi.’ (Zaburi 103:3, 4, 12) Yehova anatupatia nizamu na kutuongoza katika njia mbalimbali. Unafanya mabadiliko bila kukawia? Usisahau kwamba Yehova anatupatia nizamu kwa sababu anatupenda.—Zaburi 30:5.

YEHOVA ANATULINDA

15. Yehova anatumia njia ingine gani ili kuonyesha kwamba anatupenda?

15 Baba mwenye upendo analinda familia yake ili isipatwe na hatari. Yehova, Baba yetu, anafanya hivyo. Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi juu ya Yehova: ‘Analinda [uzima wa] washikamanifu wake; anawakomboa kutoka katika mukono wa waovu.’ (Zaburi 97:10) Fikiria jambo hili: Unafanya haraka ili kulinda macho yako kwa sababu ni ya maana sana; vilevile, Yehova anafanya haraka ili kulinda watumishi wake kwa sababu anawaona kuwa wa maana sana.—Soma Zekaria 2:8.

Yehova anafanya haraka ili kulinda watumishi wake kwa sababu anawaona kuwa wa maana sana

16, 17. Namna gani Yehova amelinda watumishi wake wa zamani na wa leo?

16 Malaika ni njia ingine yenye Yehova ametumia ili kulinda watumishi wake wa zamani na wa leo. (Zaburi 91:11) Ili kuokoa watumishi wa Mungu, katika usiku moja, malaika moja tu aliua askari Waasiria 185000. (2 Wafalme 19:35) Wakati wa mitume, malaika waliokoa Petro na wengine kutoka katika gereza. (Matendo 5:18-20; 12:6-11) Hivi karibuni, kulikuwa vita kali katika inchi moja ya Afrika. Inchi hiyo iliharibika sana kwa sababu ya mapigano, wizi, kulala wanawake kinguvu, na mauaji. Hakuna ndugu ao dada mwenye alikufa, lakini wengi kati yao walipoteza vitu vyote. Lakini wote walijionea upendo wa Yehova na walitambua kwamba alikuwa anawahangaikia. Hata kama walipatwa na mambo hayo yote, waliendelea kuwa na furaha. Wakati mujumbe wa makao yetu makubwa aliwatembelea na kuwauliza juu ya hali yao, walimuambia hivi: “Mambo yote ni sawa, tunamushukuru Yehova!”

17 Lakini, watumishi fulani wa Yehova, kama vile mwanafunzi Stefano na wengine, wamekufa kwa sababu walibaki waaminifu. Yehova hazuie sikuzote watumishi wake kupatwa na kifo. Lakini analinda watumishi wake wote kwa kuwaonya juu ya njia mbalimbali zenye Shetani anatumia ili kuwadanganya. (Waefeso 6:10-12) Tunapata maonyo hayo katika Biblia na katika vichapo vyenye tengenezo la Yehova linatutolea. Kwa mufano, tunajifunza juu ya hatari ya Internete, hatari ya kupenda feza, na hatari ya kuangalia filme, ao michezo, ao kusoma vitabu vyenye kuonyesha mambo ya uasherati na jeuri. Kwa kweli, Yehova anatupenda na anapenda kutulinda.

PENDELEO KUBWA SANA

18. Unajisikia namna gani wakati unafikiria namna Yehova anakupenda?

18 Wakati Musa alifikiria miaka yote yenye alimutumikia Yehova, alikuwa hakika kwamba Yehova alimupenda. Musa alisema hivi: ‘Utushibishe asubuhi kwa fazili zako zenye upendo, ili tupate kupiga vigelegele kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote.’ (Zaburi 90:14) Tumebarikiwa kwa sababu tunaelewa kwamba Yehova anatupenda na tunajionea upendo huo. Ni pendeleo kubwa sana kupendwa na Yehova! Tunajisikia kama mutume Yohana, mwenye aliandika hivi: ‘Muone namna ya upendo ambao Baba ametupa sisi!’—1 Yohana 3:1.