Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kumukaribia Mungu Kumekuwa Kwema Kwangu

Kumukaribia Mungu Kumekuwa Kwema Kwangu

WAKATI nilikuwa na miaka 9, sikuendelea tena kurefuka. Leo niko na miaka 43, lakini niko na urefu wa metre 1 tu. Wakati wazazi wangu walitambua kwamba singerefuka tena, walinitia moyo nitumike sana ili nisiendelee kufikiria sana urefu wangu. Kwa hiyo, ili nikuwe na kazi nyingi ya kufanya, nilikuwa ninatandika matunda ya kuuzisha mbele ya nyumba yetu na niliendelea kusafisha muzuri nafasi hiyo. Kufanya hivyo kulichochea watu wengi wakuje kuuza matunda.

Kwa kweli, kuwa na kazi nyingi ya kufanya hakukubadilisha kitu. Nilibakia tu mufupi sana, na nilishindwa hata kufanya mambo ya kawaida katika maisha, kama vile kufika kwenye urefu wa nafasi ya kulipia feza mahali pa kuuzia vitu. Ilionekana kuwa vitu vyote vilifanywa kwa ajili ya watu wenye walikuwa warefu kuliko mimi. Nilikuwa na huzuni kwa sababu sikurefuka, lakini mambo ilibadilika wakati nilikuwa na miaka 14.

Siku moja, wanawake wawili wenye walikuwa Mashahidi wa Yehova waliuza matunda na waliniomba nianze kujifunza Biblia. Kisha muda mufupi, nilitambua kwamba kufikia kumujua Yehova na mambo yenye anapanga kufanyia wanadamu ndilo jambo la maana zaidi kuliko urefu wangu. Kujua mambo hayo kulinisaidia sana. Nilipenda sana andiko la Zaburi 73:28. Sehemu ya kwanza ya andiko hilo inasema hivi: ‘Kumukaribia Mungu ni kwema kwangu.’

Mara moja familia yetu ikatoka Côte d’Ivoire na kuhamia Burkina Faso, na maisha yangu ikabadilika sana. Katika Côte d’Ivoire, watu walizoea kuniona nafasi nilikuwa ninauzishia matunda. Lakini katika Burkina Faso, nilikuwa mugeni, na watu waliniona kuwa tofauti kabisa na wengine. Watu walikuwa wananiangalia sana, kwa hiyo, nilibakia katika nyumba kwa majuma mengi. Kisha nikakumbuka namna kumukaribia Yehova kumekuwa kwema kwangu. Niliandikia biro ya tawi ya Mashahidi wa Yehova, na walituma mutu mwenye kufaa kabisa. Dada Nani, mwenye alikuwa misionere, alitumia pikipiki ili kuja kunitembelea.

Barabara zenye vumbi za nafasi kwenye tulikuwa tunaishi zilikuwa kila mara zenye kutereza, na wakati wa mvua zilikuwa na matope mengi. Dada Nani alianguka mara nyingi na pikipiki yake wakati alikuwa anakuja kujifunza na mimi, lakini hakuacha kuja kunifundisha. Siku moja, aliniomba tuende pamoja naye kwenye mikutano. Nilijua kwamba nilipaswa kuacha nyumba yangu na kuvumilia namna watu wataniangalia sana. Zaidi ya hilo, kunibeba kwenye pikipiki yake kungeongeza kilo na kufanya ikuwe tena vigumu zaidi kuitembeza. Hata hivyo, nilikubali kwenda pamoja naye, na niliendelea kukumbuka sehemu ya pili ya andiko lenye ninapenda sana. Sehemu hiyo inasema hivi: “Nimeweka kimbilio langu katika Bwana Mwenye Enzi Kuu [Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi] Yehova.”

Wakati fulani, mimi na dada Nani tulianguka katika matope, lakini kwa sababu tulipenda mikutano, hilo halikutuhangaisha hata kidogo. Mahali tulikuwa tunaishi watu walikuwa wananiangalia sana, lakini katika Jumba la Ufalme nilikaribishwa kwa upendo na sura za kicheko! Kisha miezi 9, nikabatizwa.

Sehemu ya tatu ya andiko hilo lenye ninapenda sana inasema hivi: “Ili kutangaza kazi zako zote.” Nilijua kwamba ingekuwa vigumu sana kwangu kuhubiri. Ninaendelea kukumbuka wakati nilienda katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba kwa mara ya kwanza. Watu wakubwa na watoto waliniangalia sana, walinifuata, na kuchekelea namna yangu ya kutembea. Jambo hilo lilinivunja moyo sana, lakini nilivumilia kwa sababu nilijua kwamba mimi na watu hao wote tulikuwa kabisa na lazima ya Paradiso.

Niliuza kinga ya kuendesha na mikono ili inisaidie katika kazi yangu ya kuhubiri. Mutu mwenye nilihubiri naye alikuwa ananisukuma wakati wa kupanda milima na kisha alipanda kwenye kinga wakati tulifika nafasi ya kuteremuka. Hata kama mwanzoni ilikuwa vigumu kwangu kuhubiri, kisha muda mufupi nilianza kufurahia sana kazi hiyo. Kwa hiyo, katika mwaka wa 1998 nikakuwa painia wa kawaida.

Nilijifunza Biblia na watu wengi, na ine kati yao walibatizwa. Zaidi ya hilo, mumoja kati ya dada zangu alikubali pia kweli! Mara nyingi, wakati ninasikia maendeleo yenye wengine wamefanya, hilo linanitia moyo sana. Siku moja, wakati nilikuwa ninagonjwa malaria, nilipokea barua kutoka Côte d’Ivoire. Nilikuwa nimeanza kujifunza Biblia pamoja na mwanafunzi fulani wa Burkina Faso mwenye alikuwa kwenye masomo ya juu, na nilikuwa nimemuachia ndugu mumoja funzo hilo. Kisha mwanafunzi huyo alihamia katika Côte d’Ivoire. Nilifurahi sana kusikia kwamba amekuwa muhubiri mwenye hajabatizwa!

Ninafanya nini ili kujitegemeza? Shirika moja lenye kusaidia walemavu lilinisaidia kujifunza kazi ya kushona manguo. Mwalimu wangu moja alitambua namna nilikuwa ninatumika na akasema hivi: “Tutakufundisha namna ya kutengeneza sabuni.” Walinifundisha kazi hiyo. Leo ninatengeneza sabuni za kusafisha manguo na vitu vyenye kuwa katika nyumba. Watu wengi wanafurahia sana sabuni zangu na wanaambia wengine waziuze. Ninapelekea watu sabuni hizo nyumbani kwao kwa kutumia pikipiki yangu.

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba katika mwaka wa 2004, niliacha kazi ya upania kwa sababu ya maumivu makali ya mugongo. Lakini ninaendelea kuhubiri kwa ukawaida.

Watu wanasema kwamba ninajulikana kuwa mutu mwenye sura ya kicheko. Niko mwenye furaha sana kwa sababu kumukaribia Yehova kumekuwa kwema kwangu.—Imeelezwa na Sarah Maiga.