Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uendelee Kutafakari Juu ya Mambo ya Kiroho

Uendelee Kutafakari Juu ya Mambo ya Kiroho

‘Utafakari mambo haya; uzame katika hayo, ili maendeleo yako ikuwe wazi kwa watu wote’—1TIMOTHEO 4:15.

NYIMBO: 57, 52

1, 2. Ni nini inafanya wanadamu wakuwe tofauti na wanyama?

UBONGO wa mwanadamu ni wa pekee sana. Kwa mufano, wanadamu wako na uwezo wa kujifunza luga. Na luga inatusaidia tusome, tuandike, tuseme, na tuelewe mambo yenye tunasikia. Inatusaidia pia tusali na kumuimbia Yehova sifa. Mambo hayo yote inatufanya tukuwe tofauti na wanyama. Wanasayansi hawaelewe kabisa namna ubongo wetu unafikia kufanya mambo hayo yote yenye kushangaza.

2 Uwezo wa kutumia luga ni zawadi yenye Yehova alitupatia. (Zaburi 139:14; Ufunuo 4:11) Ametupatia pia zawadi ingine yenye kutufanya tukuwe tofauti na wanyama. Wanadamu waliumbwa ‘kwa mufano wa Mungu.’ Tuko na uhuru wa kuchagua, ni kusema, uhuru wa kuchukua maamuzi yetu sisi wenyewe. Na tunaweza kuamua kutumia luga ili kumusifu Yehova na kumutumikia.—Mwanzo 1:27.

3 Yehova ametupatia Biblia ili kutusaidia tujue namna ya kumutumikia na kumusifu. Biblia yote nzima ao sehemu inapatikana katika luga zaidi ya 2 800. Ikiwa tunatafakari juu ya mambo yenye Biblia inasema, tunaweza kuanza kuona mambo namna Mungu anaiona. (Zaburi 40:5; 92:5; 139:17) Kufanya hivyo kutatusaidia tukuwe na hekima na kutatuongoza kwenye uzima wa milele.—Soma 2 Timotheo 3:14-17.

4 Kutafakari kunamaanisha kukaza akili juu ya jambo fulani na kufikiri sana na kwa uangalifu juu ya jambo hilo. (Zaburi 77:12; Methali 24:1, 2) Tunapata faida kubwa sana wakati tunatafakari juu ya mambo yenye tunajifunza juu ya Yehova na Yesu. (Yohana 17:3) Katika habari hii tutajibu maulizo haya: Namna gani tunaweza kusoma kwa njia yenye kutusaidia kutafakari? Tunaweza kutafakari juu ya mambo gani? Na ni nini inaweza kutusaidia tutafakari kwa ukawaida na tufurahie kufanya hivyo?

UHAKIKISHE KWAMBA FUNZO LAKO LINAKULETEA FAIDA

5 Je, umekwisha kutambua kwamba kuna mambo fulani yenye tunafanya bila hata kuifikiria, kama vile, kupumua, kutembea, ao kutembeza kinga? Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, wakati fulani unaweza kusoma bila hata kufikiri. Pengine, wakati unasoma unaweza kuanza kufikiria mambo mengine. Unaweza kufanya nini ili kuepuka jambo hilo? Ni jambo la lazima ukaze akili yako juu ya mambo yenye unasoma na kufikiri sana juu ya maana ya mambo hayo. Kisha, wakati unamaliza kusoma fungu ao kichwa kidogo cha habari fulani katika kichapo, unaweza kupumuzika na kutafakari juu ya mambo yenye umesoma. Ufikiri juu ya mambo yenye umejifunza, na uhakikishe kabisa kwamba umeelewa mambo hayo.

Kusoma Biblia kwa sauti kutakusaidia ukaze zaidi akili yako juu ya mambo yenye unasoma na kutakusaidia uikumbuke

5, 6. Ni nini inaweza kukusaidia ukumbuke mambo yenye unasoma na kuielewa muzuri zaidi?

6 Wanasayansi wamevumbua kwamba ni vyepesi kukumbuka jambo fulani ikiwa tunalisoma kwa sauti ao kwa kutamuka maneno. Muumbaji wetu anajua jambo hilo, ndiyo sababu alimuambia Yoshua kwamba asome kitabu cha Sheria “kwa sauti ya chini,” ni kusema, kujisomea kwa utulivu. (Soma Yoshua 1:8.) Kusoma Biblia kwa sauti kutakusaidia pia ukaze zaidi akili yako juu ya mambo yenye unasoma na kutakusaidia uikumbuke.

7.Ni wakati gani wenye kufaa zaidi ili kutafakari juu ya mambo yenye tunasoma katika Biblia? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

7 Tunapaswa kujikaza sana ili kutafakari na kukaza akili yetu juu ya mambo yenye tunasoma. Ndiyo sababu ni muzuri zaidi kutafakari wakati hauchoke na wakati uko nafasi kwenye kuwa kimya, ni kusema, kwenye hakuna mambo mengi yenye inaweza kukukengeusha. Daudi alikuwa anatafakari usiku wakati alikuwa kwenye kitanda chake. (Zaburi 63:6) Yesu alikuwa mukamilifu, lakini alienda nafasi zenye kuwa kimya ili kutafakari na kusali.—Luka 6:12.

MAMBO MAZURI YENYE TUNAWEZA KUTAFAKARI

8 Zaidi ya mambo yenye unasoma katika Biblia, kuna mambo mengine yenye unaweza kutafakari. Kwa mufano, wakati unaona kitu fulani kati ya vitu vyenye kupendeza sana vyenye Yehova aliumba, unaweza kusimama kidogo na kujiuliza hivi: ‘Kitu hiki kinanifundisha nini juu ya Yehova?’ Kutafakari juu ya mambo kama hayo kutakuchochea kabisa umushukuru Yehova katika sala. Na wakati utakuwa pamoja na wengine, utafurahia kuwaelezea namna unajisikia juu ya mambo hayo. (Zaburi 104:24; Matendo 14:17) Wakati tunatafakari, tunasali, na kuzungumuza na wengine juu ya Yehova, anasikiliza na anafurahi. Biblia inatuhakikishia kwamba ‘kitabu cha kumbukumbu kinaanza kuandikwa mbele zake kwa ajili ya wale wenye kumuogopa Yehova na kwa ajili ya wale [wenye kutafakari juu ya] jina lake.’—Malaki 3:16.

Unatafakari juu ya namna ya kusaidia wanafunzi wako wa Biblia? (Picha hizi zinapatana na fungu la 9)

9. (a) Mutume Paulo alimuambia Timotheo atafakari juu ya mambo gani? (b) Unaweza kutafakari juu ya mambo gani wakati unajitayarisha kwa ajili ya mahubiri?

9 Mutume Paulo alimuambia Timotheo atafakari juu ya matokeo ya maneno, mwenendo, na mafundisho yake juu ya wengine. (Soma 1 Timotheo 4:12-16.) Wewe pia unaweza kutafakari juu ya mambo hayo. Kwa mufano, wakati unajitayarisha ili kuongoza funzo la Biblia, unapaswa kuwa na wakati wa kutafakari. Ufikirie mwanafunzi wako, na ujikaze kutafuta ulizo ao mufano fulani wenye utatumia ili kumusaidia afanye maendeleo. Wakati unajitayarisha hivyo ili kuongoza mafunzo ya Biblia, hilo litakusaidia kutia nguvu imani yako, kuwa mwalimu muzuri zaidi, na kufundisha wengine kwa furaha. Pia utapata faida ikiwa unatafakari mbele ya kuenda katika kazi ya kuhubiri. (Soma Ezra 7: 10.) Pengine unaweza kusoma sura fulani katika kitabu cha Matendo ya mitume ili ikusaidie ukuwe na bidii zaidi katika kazi ya kuhubiri. Unaweza pia kutafakari juu ya andiko fulani la Biblia lenye umepanga kutumia na kutafakari juu ya vichapo vyenye umepanga kuwatolea watu katika mahubiri siku hiyo. (2 Timotheo 1:6) Ufikirie watu wa eneo lako na mambo yenye utasema ili wapendezwe na habari njema. Wakati unafanya hivyo, utakuwa na uwezo wa kutumia Biblia muzuri zaidi ili kuwahubiria wengine.—1 Wakorintho 2:4.

Uruhusu mambo yenye unasoma iguse moyo wako, na umushukuru Yehova juu ya mambo mazuri yenye umejifunza

10. Tunaweza kutafakari juu ya mambo gani mengine mazuri?

10 Tunaweza kutafakari juu ya mambo mengine gani? Ikiwa unaandika mambo fulani wakati wa hotuba ya watu wote, ao kwenye mikusanyiko, uchukue wakati wa kurudilia mambo hayo. Wakati unafanya hivyo, ujiulize hivi: ‘Nimejifunza nini katika Neno la Mungu na katika tengenezo lake?’ Unaweza pia kutafakari juu ya habari zenye kutolewa kila mwezi katika gazeti Munara wa Mulinzi na Amuka! na katika vichapo vyenye vimetolewa hivi karibuni kwenye mikusanyiko. Wakati unasoma katika Kitabu cha Mwaka habari fulani yenye kupendeza, tua kidogo ili ufikiri juu ya habari hiyo, na uiache iguse moyo wako. Wakati unasoma vichapo vyetu, unaweza kufurahia kutia kistari mambo makubwa ao kuandika mambo fulani pembeni katika kitabu chako. Mambo hayo inaweza kukusaidia wakati unajitayarisha ili kurudilia watu, wakati unatembelea ndugu na dada ili kuwatia moyo kiroho, na wakati unatayarisha hotuba. Jambo la maana zaidi ni kwamba, wakati unapumuzika kidogo ili kutafakari juu ya mambo yenye umesoma, unaruhusu mambo hayo iguse moyo wako na unapata nafasi ya kusali ili kumushukuru Yehova kwa ajili ya mambo mazuri yenye umejifunza.

UTAFAKARI KILA SIKU JUU YA NENO LA MUNGU

11. Tunapaswa kutafakari juu ya kitabu gani cha maana sana, na kufanya hivyo kunaweza kutusaidia namna gani? (Soma pia maelezo ya chini.)

11 Kwa kweli, kuliko vitabu vingine vyote, tunapaswa kutafakari juu ya Biblia kwa sababu ni kitabu cha maana sana. Lakini, utafanya nini ikiwa siku moja unakatazwa kuwa na Biblia? * (Soma maelezo ya chini.) Hakuna mutu mwenye anaweza kukuzuia kutafakari juu ya mambo yenye tayari umechunga katika akili yako, kama vile maandiko ao nyimbo fulani za Ufalme zenye unapenda sana. (Matendo 16:25) Pia, roho ya Mungu itakusaidia ukumbuke mambo yenye umekwisha kujifunza yenye inaweza kukusaidia uendelee kuwa mwaminifu.—Yohana 14:26.

12. Ni njia moja gani yenye unaweza kutumia ili kupanga programu yako ya kusoma Biblia kila siku?

12 Ni njia moja gani yenye unaweza kutumia ili kupanga programu yako ya kusoma Biblia kila siku? Pengine siku fulani katika juma, unaweza kusoma na kutafakari juu ya Usomaji wa Biblia wa kila juma kwa ajili ya Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Siku zingine unaweza kusoma vitabu vya Injili kama vile Mathayo, Marko, Luka, na Yohana na kutafakari juu ya mambo yenye Yesu alisema na kufanya. (Waroma 10:17; Waebrania 12:2; 1 Petro 2:21) Pia tuko na kichapo chenye kueleza mambo yenye Yesu alifanya katika maisha yake. Kichapo hicho kinaweza kukusaidia kabisa upate faida wakati unasoma vitabu vya Injili.—Yohana 14:6.

SABABU GANI KUTAFAKARI NI JAMBO LA MAANA SANA?

13Kutafakari juu ya Yehova na Yesu kunaweza kusaidia Mukristo akomae kiroho na kufanya imani yake iendelee kuwa nguvu. (Waebrania 5:14; 6:1) Mukristo mwenye hatumie wakati wa kutosha ili kufikiri juu ya Yehova, anaweza kupoteza polepole urafiki wake pamoja naye ao hata kufikia kuacha kumutumikia. (Waebrania 2:1; 3:12) Yesu alisema kwamba ikiwa hatusikilize, ao kukubali, Neno la Mungu ‘kwa moyo muzuri na mwema,’ ‘hatutalihifazi [kulichunga].’ Lakini tunaweza kwa vyepesi “kuchukuliwa na mahangaiko na utajiri na raha za maisha haya.”—Luka 8:14, 15.

13, 14. Sababu gani ni lazima tuendelee kutafakari juu ya Yehova na Yesu, na kufanya hivyo kutatuchochea tufanye nini?

14 Kwa hiyo, tuendelee kutafakari juu ya Biblia na tufikie kumujua Yehova muzuri zaidi. Kufanya hivyo kutatuchochea tuige kabisa sifa zake. (2 Wakorintho 3:18) Tunaweza kuendelea kujifunza mengi juu ya Baba yetu wa mbinguni na kumuiga milele. Hilo ni pendeleo kubwa sana!—Mhubiri 3:11.

Kutafakari juu ya Yehova na Yesu kunakusaidia umutumikie Yehova kwa bidii

15, 16. (a) Kutafakari juu ya Yehova na Yesu kumekuletea faida gani? (b) Sababu gani wakati fulani inaweza kuwa vigumu kutafakari, lakini sababu gani tunapaswa kuendelea kujikaza kufanya hivyo?

15 Kutafakari juu ya Yehova na Yesu kunaweza kukusaidia umutumikie Yehova kwa bidii. Bidii yako itatia moyo ndugu na dada zako na watu wenye unakutana nao katika mahubiri. Na wakati unatafakari juu ya mambo yenye Yehova alifanya kwa ajili yako kwa kutoa Yesu kuwa zabihu ya ukombozi, utaendelea kuona urafiki wako wa sana pamoja na Mungu kuwa wa lazima. (Waroma 3:24; Yakobo 4:8) Mark, ndugu wa Afrika Kusini mwenye alifungwa miaka tatu kwa ajili ya imani yake, alisema hivi: “Tunaweza kulinganisha kutafakari na matembezi yenye kufurahisha sana. Wakati tunaendelea kutafakari juu ya mambo ya kiroho, tutavumbua mambo mapya juu ya Yehova, Mungu wetu. Wakati fulani ninajisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo ao kuhangaika juu ya wakati unaokuja; kwa hiyo, ninakamata Biblia na kutafakari juu ya Andiko moja. Kisha ninajisikia kuwa nimetulia kabisa.”

16 Maisha katika ulimwengu huu inajaa sana mambo ya kukengeusha, na hilo linafanya ikuwe vigumu kuwa na wakati wa kutafakari juu ya Biblia. Patrick, ndugu mwenye kuishi katika Afrika, alisema hivi: “Akili yangu iko kama kisanduku cha kupokea barua chenye kuwa na habari mbalimbali zenye ninapenda na zenye sipendi, na zenye zinapaswa kupangwa kila siku. Wakati ninafikiria mambo yenye kuwa katika akili yangu, ninatambua kila mara mawazo yenye kuhuzunisha, na ninapaswa kumuelezea Yehova mawazo hayo katika sala ili niweze kuwa na akili safi mbele ya kutafakari. Hata kama kufanya hivyo kunaweza kuchukua muda fulani mbele nianze kutafakari juu ya mambo ya kiroho, ninajisikia kuwa karibu na Yehova. Kufanya hivyo kunafungua akili yangu ili nielewe muzuri zaidi kweli za Biblia.” (Zaburi 94:19) Kwa kweli, tunapata faida kubwa wakati tunatafakari kila siku juu ya Biblia.—Matendo 17:11.

UNAPATA WAKATI NAMNA GANI?

17. Unapata namna gani wakati wa kutafakari?

17 Watu fulani wanaamuka asubuhi sana ili kusoma, kutafakari, na kusali. Wengine wanafanya hivyo wakati wanapumuzika ili kula chakula cha muchana. Pengine wewe unaona kuwa ni muzuri zaidi kusoma Biblia mangaribi ao mbele ya kulala. Wengine wanafurahia kusoma Biblia asubuhi na mangaribi mbele ya kulala. (Yoshua 1:8) Jambo la maana ni kutumia vizuri zaidi wakati wetu, ni kusema, kutumia wakati wenye tunapitisha katika mambo yenye haiko ya maana sana, na kuutumia ili kutafakari kila siku juu ya Neno la Mungu.—Waefeso 5:15, 16.

18. Biblia inaahidi nini wale wenye kutafakari juu ya Neno la Mungu na wenye kutumikisha mambo yenye wamejifunza?

18 Biblia inatuahidi kwamba Yehova atabariki wale wenye kutafakari juu ya Neno lake na wenye kujikaza kutumia katika maisha yao mambo yenye wamejifunza. (Soma Zaburi 1:1-3.) Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!” (Luka 11:28) Lakini jambo la maana zaidi ni kwamba, kutafakari kila siku juu ya Neno la Yehova kutatusaidia kutenda kwa njia yenye kumuletea utukufu. Wakati tunafanya hivyo, Yehova atatubariki kwa kutupatia furaha leo na uzima wa milele katika dunia mupya.—Yakobo 1:25; Ufunuo 1:3.

^ fu. 11 Soma habari yenye kichwa “Pigano Letu la Kubaki Wenye Nguvu Kiroho,” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 12, 2006.