Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umutumikie Yehova Bila Kukengeushwa

Umutumikie Yehova Bila Kukengeushwa

‘Maria . . . aliendelea kusikiliza [mambo yenye Yesu alikuwa anasema].Martha . . . alikengeushwa na kazi nyingi.’ LUKA 10:39, 40.

NYIMBO: 94, 134

1, 2. Sababu gani Yesu alimupenda Martha, lakini Martha alifanya makosa gani yenye kuonyesha kwamba alikuwa hakamilike?

WAKATI unafikiria Martha, dada ya Lazaro, unamuona kuwa mutu wa namna gani? Biblia inaonyesha kwamba Martha alikuwa rafiki muzuri wa Yesu, na kwamba Yesu alikuwa anamupenda. Kwa kweli, Yesu alipenda pia wanawake wengine na kuwaonyesha heshima. Kwa mufano, Maria, mudogo yake na Martha, alikuwa pia rafiki wa sana wa Yesu. Pia, Yesu alimupenda Maria, mama yake. (Yohana 11:5; 19:25-27) Kwa hiyo, sababu gani Yesu alimupenda Martha?

2 Yesu alimupenda Martha kwa sababu alikuwa mwema na mukarimu, na mwenye kufanya kazi kwa bidii. Na sababu kubwa zaidi yenye ilimufanya Yesu amupende ni imani yake yenye nguvu. Martha aliamini mafundisho yote ya Yesu, na alikuwa hakika kwamba Yesu alikuwa Masiya mwenye aliahidiwa. (Yohana 11:21-27) Hata hivyo, Martha hakuwa mukamilifu. Kama wanadamu wengine wote, yeye pia alifanya makosa. Kwa mufano, siku moja, wakati Yesu alikuwa anawatembelea, Martha alimukasirikia Maria, na alimuomba Yesu amushaurie. Martha alisema hivi: ‘Bwana, haujali [hauhangaike] kwamba dada yangu ameniacha peke yangu kushugulikia mambo? Kwa hiyo, umuambie akuje anisaidie.’ (Soma Luka 10:38-42.) Sababu gani Martha alisema maneno hayo, na jibu la Yesu linaweza kutufundisha nini?

MARTHA ALIKENGEUSHWA

3, 4. Maria alifanya jambo gani lenye lilimupendeza Yesu, na hilo lilimufundisha Martha somo gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Yesu alishukuru kuona Martha na Maria wanamualika kwao, na alipenda kutumia nafasi hiyo ili kuwafundisha kweli ya maana sana. Bila kukawia Maria alikaa pembeni ya Yesu na akaendelea kusikiliza maneno yenye alikuwa anasema. Alipenda Mwalimu Mukubwa amufundishe mambo mengi zaidi. Martha pia angechagua kumusikiliza Yesu. Na Yesu angemupongeza ikiwa angeacha kwanza mambo yenye alikuwa anafanya na kusikiliza mafundisho yake.

4 Lakini Martha alikengeushwa. Alikuwa na kazi nyingi ya kufanya ili kumutayarishia Yesu chakula cha pekee na alijikaza sana ili tukio hilo likuwe lenye kupendeza. Wakati aliona kwamba Maria hakumusaidia, alikasirika na kumuambia Yesu amutume amusaidie. Yesu alijua kwamba Martha alikuwa anapenda kufanya mambo mengi. Kwa hiyo, alimuambia kwa upole hivi: “Martha, Martha, wewe unahangaika na kusumbuka juu ya mambo mengi.” Alisema pia kwamba chakula chenye hakitaomba mambo mengi kingetosha. Kisha Yesu alimupongeza Maria kwa sababu alimusikiliza kwa uangalifu. Alisema hivi: ‘Maria alichagua fungu njema, nalo halitaondolewa kwake.’ Ni kweli kwamba Maria alisahau chakula chenye alikula siku hiyo, lakini hangesahau hata kidogo mambo yenye Yesu alifundisha na namna alimupongeza. Kisha miaka zaidi ya 60, mutume Yohana aliandika hivi: ‘Yesu alimupenda Martha na dada yake.’ (Yohana 11:5) Maneno hayo inaonyesha kwamba Martha alikubali mashauri yenye Yesu alimutolea kwa upendo na alimutumikia Yehova kwa uaminifu katika maisha yake.

5. Sababu gani ni vigumu sana leo kukaza akili yetu juu ya mambo ya maana zaidi, na tutajibu maulizo gani?

5 Tofauti na zamani, leo kuna mambo mengi yenye inaweza kutukengeusha na kutuzuia kumutumikia Yehova. Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 9, 1958 katika Kiingereza, lilionya ndugu na dada kwamba wasiruhusu teknolojia iwakengeushe na kuwazuia kumutumikia Yehova. Hata wakati huo, inaonekana kwamba kila siku kulikuwa kitu fulani kipya. Vitu kama vile magazeti ya ulimwengu yenye kupendeza, radio, filme, na televizyo vilikuwa vimeenea sana. Gazeti hilo lilisema kwamba kadiri tunaendelea kukaribia mwisho wa ulimwengu huu muovu, “mambo ya kukengeusha itaongezeka.” Kuliko wakati mwingine wowote, leo kuna mambo mengi sana yenye inaweza kutukengeusha. Tunapaswa kufanya nini ili kumuiga Maria na kukaza akili yetu juu ya ibada ya Yehova?

USITUMIE ULIMWENGU SANA

6. Namna gani watu wa Yehova wametumia teknolojia?

6 Watu wa Yehova wametumia teknolojia ili kuhubiri habari njema. Kwa mufano, mbele na kisha vita ya kwanza ya ulimwengu, walionyesha watu “Foto-Drama ya Uumbaji.” Walihubiria watu wengi sana katika inchi nyingi kwa kutumia picha, na filme fupi zenye kuwa na picha za rangi na sauti. Mwisho wa filme “Foto-Drama ya Uumbaji” ulizungumuzia kipindi chenye amani wakati Yesu Kristo atatawala dunia. Kisha, watumishi wa Yehova walitumia radio ili kutangaza ujumbe wa Ufalme kwa watu wengi sana katika dunia yote. Leo, tunatumia ordinatere na Internete ili kuhubiria watu kila nafasi kwenye wanaishi, na hata wale wenye kupatikana katika maeneo ya mbali sana.

Usiruhusu mambo yenye haiko ya maana ikuzuie kumuabudu Yehova(picha hii inapatana na fungu la 7)

7. (a) Sababu gani ni mubaya kutumia ulimwengu sana? (b) Tunapaswa kufanya angalisho na mambo gani? (Soma maelezo ya chini.)

7 Biblia inatushauri kwamba tusitumie ulimwengu sana. Shauri hilo linahusu pia kuepuka kutumia wakati mwingi sana kwa ajili ya vitu vyenye ulimwengu huu unatutolea. (Soma 1 Wakorintho 7:29-31.) Mambo fulani yenye ulimwengu unatutolea haiko ya mubaya, lakini inaweza kuchukua wakati wetu wote. Kwa mufano, tunaweza kufurahia michezo fulani, kusoma vitabu, kuangalia televizyo, kutembelea nafasi zenye kupendeza, kuuza vitu, na kutafuta habari juu ya vyombo vya kielektroniki vya sasa ao vitu vingine vyenye kupendeza sana. Watu wengi wanapenda kutumiana ujumbe kwenye telefone ao kwenye Internete, kutafuta habari fulani, ao kutafuta habari za michezo. Lakini, watu fulani wanaweza kuwa watumwa wa mambo hayo. * (Soma maelezo ya chini.) (Mhubiri 3:1, 6) Ikiwa tunatumia wakati mwingi kwa ajili ya mambo yenye haiko ya maana, tunaweza kukosa wakati wa kutosha ili kufanya mambo ya maana zaidi, ni kusema, ibada yetu kwa Yehova.—Soma Waefeso 5:15-17.

8. Sababu gani tunapaswa kuepuka kupenda vitu vya ulimwengu?

8 Shetani anafanya yake yote ili kutuchochea tupende vitu vya ulimwengu na kutukengeusha ili tusiendelee kumutumikia Yehova. Shetani alitumia njia hiyo wakati wa mitume, na anaendelea kuitumia sana leo. (2 Timotheo 4:10) Kwa hiyo, tunapaswa kuendelea kujichunguza ili kujua mawazo yetu juu ya vitu vya ulimwengu na kufanya mabadiliko yenye kuhitajiwa. Biblia inatushauri tuepuke kupenda vitu vya ulimwengu. Lakini, tunapaswa kuendelea kutia nguvu upendo wetu kwa Yehova. Ikiwa tunafanya hivyo, tutakuwa tayari kumutii Yehova na tutabaki karibu naye.—1 Yohana 2:15-17.

UENDELEE KUKAZA AKILI JUU YA MAMBO YA MAANA ZAIDI

9. Yesu alishauria wanafunzi wake wakaze akili yao juu ya nini, na namna gani alituachia mufano?

9 Yesu alishauria kwa upole wanafunzi wake kwamba wasikengeushwe na mambo mengi, kama vile tu alimushauria Martha. Aliwatia moyo waendelee kukaza akili yao juu ya kumutumikia Yehova na juu ya Ufalme wake. (Soma Mathayo 6:22, 33.) Yesu mwenyewe alituachia mufano muzuri zaidi. Hakuwa na vitu vingi, na hakuwa na nyumba ao shamba.—Luka 9:58; 19:33-35.

10. Yesu alituachia mufano gani muzuri?

10 Yesu hakuruhusu hata jambo moja limukengeushe kufanya kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, muda mufupi kisha kuanza kazi yake ya kuhuburi, watu wengi katika muji wa Kapernaumu walipenda abaki nao muda murefu. Yesu alitenda namna gani? Aliendelea kukaza akili juu ya kazi yake ya kuhubiri. Alisema hivi: “Ni lazima nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.” (Luka 4:42-44) Yesu alifanya safari ndefu ili kuhubiri habari njema na kufundisha watu wengi zaidi. Alikuwa mukamilifu, lakini alikuwa anachoka na alikuwa na lazima ya kupumuzika kwa sababu alikuwa anatumika sana.—Luka 8:23; Yohana 4:6.

Yesu alitufundisha kwamba ikiwa tunakaza akili yetu juu ya kupata vituvingi, hilo linaweza kutuzuia tuendelee kumutumikia Mungu

11. Yesu alifanya nini wakati mwanaume moja alimuelezea magumu yake? Yesu alifundisha wanafunzi wake somo gani?

11 Kisha, wakati Yesu alikuwa anafundisha wanafunzi wake jambo fulani la maana sana, mutu moja alimukatiza kwa kusema hivi: ‘Mwalimu, umuambie ndugu yangu tugawane uriti.’ Yesu hakumusaidia mwanaume huyo kumaliza magumu yake. Hakuacha mwanaume huyo amukengeushe kufundisha wanafunzi wake. Lakini, alitumia nafasi hiyo ili kufundisha wanafunzi wake kwamba ikiwa wanakaza akili yao juu ya kupata vitu vingi, hilo lingewazuia kuendelea kumutumikia Mungu.—Luka 12:13-15.

12, 13. (a) Katika muji wa Yerusalemu, Yesu alifanya mambo gani yenye ilishangaza Wagiriki fulani? (b) Yesu alitenda namna gani wakati Filipo alimuambia kwamba Wagiriki fulani walipenda kumuona?

12 Katika siku zake za mwisho-mwisho hapa duniani, Yesu alikuwa na mambo mengi sana ya kufanya. (Mathayo 26:38; Yohana 12:27) Alijua kwamba atateseka sana na kufa. Alijua pia kwamba alikuwa na kazi nyingi za kufanya mbele akufe. Kwa mufano, Siku ya Yenga tarehe 9 mwezi wa Nisani, aliingia katika muji wa Yerusalemu akiwa mwenye kukaa juu ya punda. Watu wengi sana walimukaribisha kama Mufalme. (Luka 19:38) Siku yenye ilifuata, bidii ya Yesu ilimuchochea aingie katika hekalu na kufukuza wafanya-biashara wenye pupa wenye walikuwa wanaiba watu kwa kuwauzisha vitu kwa bei kali.—Luka 19:45, 46.

13 Wagiriki fulani wenye walikuja Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka, waliona mambo yenye Yesu alifanya na walishangaa sana. Kwa hiyo, walimuuliza mutume Filipo ikiwa wangeweza kumuona Yesu ili wazungumuze naye. Lakini Yesu hakuwa na lazima ya watu wa kumutegemeza ao wa kumupigania juu ya maadui wake. Alijua mambo yenye ilikuwa ya maana zaidi. Aliendelea kukaza akili yake juu ya mambo yenye Yehova alipenda afanye, ni kusema, kutoa uzima wake kuwa zabihu ya ukombozi. Kwa hiyo, aliwakumbusha wanafunzi wake kwamba alikuwa karibu kufa na kwamba wale wote wenye kumufuata wanapaswa kuwa tayari pia kutoa uzima wao. Alisema hivi: ‘Ule anaipenda sana nafsi [uzima] yake anaiangamiza, lakini ule anaichukia nafsi yake katika ulimwengu huu atailinda kwa ajili ya uzima wa milele.’ Lakini Yesu aliahidi pia kwamba ‘Baba atawaheshimu’ wafuasi wake na kuwapatia uzima wa milele. Inawezekana Filipo aliwaambia Wagiriki hao ujumbe huo wenye kutia moyo.—Yohana 12:20-26.

14. Hata kama Yesu alitia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza katika maisha yake, ni mambo mengine gani alifanya?

14 Wakati alikuwa duniani, kazi yake kubwa ilikuwa kuhubiri habari njema. Hata kama alikaza akili yake juu ya kazi ya kuhubiri, alikuwa na wakati wa kufanya mambo mengine. Kwa mufano, alienda kwenye karamu fulani ya ndoa. Kwenye karamu hiyo, aligeuza maji kuwa divai nzuri. (Yohana 2:2, 6-10) Pia, marafiki wake na wale wenye walipendezwa na habari njema walimualika nyumbani kwao ili kula chakula. (Luka 5:29; Yohana 12:2) Jambo la maana zaidi ni kwamba, kila mara Yesu alijipangia wakati wa kusali, kutafakari, na kupumuzika.—Mathayo 14:23; Marko 1:35; 631, 32.

“TUONDOE KILA UZITO”

15. Mutume Paulo alisema kwamba Wakristo wanapaswa kufanya nini, na namna gani alituachia mufano muzuri?

15 Mutume Paulo alisema kwamba Wakristo ni kama wakimbiaji katika shindano ndefu la mbio. Ili wamalize mbio hiyo, wanapaswa kuondoa kila kitu chenye kinaweza kuwasimamisha ao kuwazuia kukimbia. (Soma Waebrania 12:1.) Mutume Paulo mwenyewe alituachia mufano muzuri. Angekuwa tajiri na mwalimu wa dini ya Kiyahudi mwenye kujulikana sana, lakini alikataa mambo hayo ili kukaza akili yake juu ya “mambo yaliyo ya maana zaidi.” Alihubiri kwa bidii na alisafiri katika maeneo mengi kama vile, Siria, Asia Ndogo, Makedonia, na Yudea. Mutume Paulo alingojea kwa hamu kupata zawadi yake ya kuenda mbinguni. Alisema hivi: ‘Ninasahau mambo ya nyuma na kujinyoosha kuenda mbele kuelekea mambo yaliyo mbele, ninafuatilia kuelekea ule muradi kwa ajili ya tuzo [zawadi].’ (Wafilipi 1:10; 3:8, 13, 14) Mutume Paulo hakuoa, na hilo lilimusaidia aendelee kujitoa “bila kukengeushwa fikira.”—1 Wakorintho 7:32-35.

Mutume Paulo alikataa mambo ya ulimwengu huu ili kukaza akili yake juu ya “mambo yaliyo ya maana zaidi”

16, 17. Iwe tumeoa ao kuolewa ao hapana, namna gani tunaweza kufuata mufano wa mutume Paulo? Namna gani ndugu Mark na dada Claire walifanya hivyo?

16 Kama mutume Paulo, leo watumishi fulani wa Yehova wanaamua kubakia bila kuoa ao kuolewa ili waweze kufanya mengi katika kazi ya Yehova. (Mathayo 19:11, 12) Kwa kawaida, watu wenye hawajaoa ao kuolewa hawana madaraka mengi ya familia kama wale wenye kuoa ao kuolewa. Lakini, iwe tumeoa ao kuolewa ao hapana, sisi wote tunapaswa ‘kuondoa kila uzito’ wenye unaweza kutukengeusha na kutufanya tusiendelee kumutumikia Yehova. Ili tukuwe na mengi ya kufanya katika kazi ya Yehova, tunapaswa kubadilisha tabia zetu ili tutumie wakati wetu kwa hekima.

17 Kwa mufano, ndugu Mark na dada Claire, wenye walikomalia huko Pays de Galles, walianza kazi ya upainia wakati walimaliza masomo. Kisha kuoana, waliendelea kufanya kazi ya upainia. Lakini walipenda kufanya mengi zaidi. Ndugu Mark anasema hivi: “Tulifanya maisha yetu ikuwe mwepesi zaidi kwa kuuzisha nyumba yetu yenye ilikuwa na vyumba tatu vya kulalia, na kwa kuacha kazi yetu ya muda ili tuanze kazi ya ujenzi ya ulimwenguni pote.” Katika miaka 20 yenye imepita, wamesafiri katika sehemu nyingi za Afrika ili kujenga Majumba ya Ufalme. Wakati fulani walikuwa na feza kidogo, lakini sikuzote Yehova aliwahangaikia. Dada Claire anasema hivi: “Tunapata furaha kubwa sana kwa kufanya kazi ya Yehova kila siku. Tumepata marafiki wengi sana, na hatukose kitu. Hatuwezi kulinganisha hata kidogo furaha yenye tunapata kwa kumutumikia Yehova kwa wakati wote, na vitu vidogo vyenye tumeacha.” Watumishi wengi wa wakati wote wanasema maneno kama hayo. *—Soma maelezo ya chini.

18. Ni maulizo gani yenye unaweza kujiuliza?

18 Unawaza kama unaweza kupata furaha zaidi katika kazi ya Yehova? Kuna mambo fulani yenye kukukengeusha ili usikaze akili yako juu ya mambo ya maana zaidi? Ikiwa ni hivyo, unapaswa kufanya nini? Pengine unaweza kusoma na kujifunza Biblia muzuri zaidi. Habari yenye kufuata itaeleza namna unaweza kufanya hivyo.

^ fu. 17 Soma pia masimulizi kuhusu maisha ya Hadyn na Melody Sanderson katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 3, 2006, yenye kichwa “Kujua Yaliyo Sawa na Kuyatenda.” Biashara yao ilikuwa inaendelea muzuri katika inchi ya Australia, lakini waliacha biashara yao na kuanza utumishi wa wakati wote. Soma habari hiyo ili kujua walifanya nini wakati feza zao ziliisha wakati walikuwa wamisionere katika India.