Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Utupatie Imani Zaidi’

‘Utupatie Imani Zaidi’

Unisaidie mahali ninahitaji imani!’—MARKO 9:24.

NYIMBO: 81, 135

1. Sababu gani imani ni ya maana sana? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

UMEKWISHA kujiuliza ikiwa Yehova atakuokoa wakati wa ziki kubwa? Mutume Paulo alisema kwamba sifa ya lazima sana yenye tunapaswa kuwa nayo ili tuokolewe ni imani. Alisema hivi: ‘Bila imani haiwezekane kamwe [hata kidogo] kumupendeza [Mungu] vema.’ (Waebrania 11:6) Tunaweza kuona kuwa maneno hayo haina maana fulani, lakini ukweli ni kwamba imani haiko mali ya watu wote. (2 Wathesalonike 3:2) Maandiko hayo mawili inatusaidia tuelewe kwamba kutia nguvu imani yetu ni jambo la maana sana.

2, 3. (a) Sababu gani imani yetu ni ya maana sana? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Mutume Petro alizungumuzia imani yenye ‘imejaribiwa.’ (Soma 1Petro 1:7.) Kwa sababu ziki kubwa inakaribia sana, tunapenda tukuwe ‘namna ya watu walio na imani ya kuihifazi hai nafsi [kulinda uzima] yetu.’ (Waebrania 10:39) Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza sana ili kutia nguvu imani yetu. Tunapenda kuwa kati ya wale wenye watapata baraka wakati wa kufunuliwa kwa Mufalme wetu, Yesu Kristo. Kwa hiyo, kama mwanaume mwenye alimuomba Yesu imani zaidi, sisi pia tunaweza kusema hivi: ‘Unisaidie mahali ninahitaji imani!’ (Marko 9:24) Ao, kama mitume, tunaweza kusema hivi: ‘Utupatie imani zaidi.’—Luka 17:5.

3 Katika habari hii, tutajibu maulizo haya: Namna gani tunaweza kukomalisha imani yetu? Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tuko na imani yenye nguvu? Na sababu gani tunaweza kuwa hakika kwamba Mungu atajibu sala yetu ya kuomba imani zaidi?

MUNGU ANAFURAHI WAKATI TUNAKOMALISHA IMANI YETU

4. Ni mifano ya watu gani yenye inaweza kutusaidia tutie nguvu imani yetu?

4 Kwa sababu imani ni ya maana sana, katika Biblia, Yehova ametutolea mifano mingi ya watu wenye walionyesha imani. Mifano hiyo ‘iliandikwa ili kutufundisha.’ (Waroma 15:4) Mufano wa Abrahamu, Sara, Isaka, Yakobo, Musa, Rahabu, Gideoni, Baraka, na wengine wengi inaweza kutusaidia tutie nguvu imani yetu. (Waebrania 11:32-35) Zaidi ya mifano ya watu wa zamani, tuko pia na mifano yenye kufurahisha ya ndugu na dada wenye wameonyesha imani. * (Soma maelezo ya chini.)

Tuko na mifano yenye kufurahisha ya ndugu na dada wenye wameonyesha imani

5. Namna gani nabii Eliya alionyesha kwamba alikuwa na imani yenye nguvu katika Yehova, na tunapaswa kujiuliza ulizo gani?

5 Tuzungumuzie mufano wa nabii Eliya. Wakati unafikiri sana juu ya mufano wake, utambue hali tano zenye alitumia ili kuonyesha imani yenye nguvu katika Yehova. (1) Wakati nabii Eliya alimuambia Mufalme Ahabu kwamba Yehova angeleta kipwa, alisema hivi kwa uhakika: “Kama anavyoishi Yehova Mungu wa Israeli, ambaye ninasimama mbele zake, miaka hii hakutakuwa na umande wala mvua.” (1 Wafalme 17:1) (2) Nabii Eliya aliamini kwamba wakati wa kipwa, Yehova angemupatia yeye na wengine mambo yenye walihitaji. (1 Wafalme 17:4, 5, 13, 14) (3) Nabii Eliya alikuwa pia hakika kwamba Yehova atamufufua mutoto wa mujane. (1 Wafalme 17:21) (4) Kwenye Mulima Karmeli, alikuwa hakika kwamba Yehova atatuma moto ili kuunguza zabihu yake. (1 Wafalme 18:24, 37) (5) Hata mbele mvua inyeshe, nabii Eliya alimuambia Ahabu kwa uhakika wote hivi: ‘Panda, ukule na kunywa, kwa maana kuna kishindo cha machafuko ya mvua kubwa [sauti ya mvua kubwa].’ (1 Wafalme 18:41) Kwa hiyo, kisha kuchunguza mifano hiyo, unaweza kujiuliza hivi: ‘Imani yangu iko yenye nguvu kama ile ya nabii Eliya?’

NI NINI ITATUSAIDIA TUKOMALISHE IMANI YETU?

6. Tunapaswa kumuomba Yehova nini ili tukomalishe imani yetu?

6 Hatuwezi kujitegemea sisi wenyewe ili kukomalisha imani yetu; kwa hiyo, tunapaswa kumuomba Mungu roho takatifu. Sababu gani? Kwa sababu imani ni sehemu ya tunda la roho takatifu. (Wagalatia 5:22) Tunatenda kwa hekima wakati tunatii shauri la Yesu la kumuomba Yehova roho takatifu zaidi. Yesu aliahidi kwamba Yehova ‘atawapatia roho takatifu wale wanaomuomba!’—Luka 11:13.

Tunatenda kwa hekima wakati tunatii shauri la Yesu la kumuomba Yehova roho takatifu zaidi

7. Tunapaswa kufanya nini ili imani yetu iendelee kuwa nguvu?

7 Kisha kuwa na imani yenye nguvu katika Mungu, tunapaswa kuendelea kuikomalisha. Tunaweza kulinganisha imani na moto. Wakati tunawasha moto, unaweza kuwaka mbio sana. Hata hivyo, ikiwa hatuongeze kuni, moto huo unaweza kufifia na kuzimika. Lakini ikiwa tunaongeza kuni kwa ukawaida, moto huo unaweza kuendelea kuwaka. Ni hivyo pia juu ya imani yetu. Ikiwa tunaendelea kusoma na kujifunza Neno la Mungu kila siku, tutapenda sana Biblia na upendo wetu kwa Yehova utaongezeka. Tukifanya hivyo, imani yetu itaendelea kuwa nguvu.

8. Ni nini itakusaidia ukomalishe imani yako na kuifanya iendelee kuwa nguvu?

8 Haupaswe kutosheka tu na mambo yenye ulijifunza mbele ya kubatizwa. (Waebrania 6:1, 2) Kwa mufano, kujifunza unabii mbalimbali wa Biblia wenye umekwisha kutimia kutakusaidia ukomalishe imani yako na kuifanya iendelee kuwa nguvu. Unaweza pia kutumia Neno la Mungu ili kuona ikiwa imani yako ni yenye nguvu kabisa.—Soma Yakobo 1:25; 2:24, 26.

9, 10. Namna gani imani yetu inatiwa nguvu kupitia (a) marafiki wazuri? (b) mikutano ya Kikristo? (c) kazi ya kuhubiri?

9 Mutume Paulo alisema kwamba Wakristo wanaweza kuwa ‘na ubadilishanaji wa kitia-moyo kati yao, kila mumoja kupitia imani ya mwengine.’ (Waroma 1:12) Hilo linamaanisha nini? Ikiwa tunapitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu, tunaweza kujengana imani. Zaidi sana ikiwa tunapitisha wakati pamoja na wale wenye imani yao ‘imejaribiwa.’ (Yakobo 1:3) Marafiki wabaya wanaharibu imani yetu, lakini marafiki wazuri wanatusaidia tuijenge. (1 Wakorintho 15:33) Ndiyo sababu tunatiwa moyo kuhuzuria mikutano kwa ukawaida. Kwenye mikutano, tunaweza kuendelea ‘kutiana moyo.’ (Soma Waebrania 10:24, 25.) Zaidi ya hilo, mashauri yenye tunapata kwenye mikutano inatia nguvu imani yetu. Biblia inasema kwamba ‘imani inafuata jambo lililosikiwa.’ (Waroma 10:17) Kwa hiyo, ujiulize hivi: ‘Je, ninahuzuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida?’

10 Pia, tunatia nguvu imani yetu wakati tunahubiria watu habari njema na kuwafundisha Biblia. Kama Wakristo wa kwanza-kwanza, tunajifunza kumutegemea Yehova na kuhubiri bila woga katika hali yoyote.—Matendo 4:17-20; 13:46.

11 Wakati tunaona namna Yehova anatusaidia na kujibu sala zetu, imani yetu inakomaa. Kalebu na Yoshua walijionea jambo hilo. Walionyesha imani katika Yehova wakati walipeleleza Inchi ya Ahadi. Kadiri wakati uliendelea kupita, imani yao ­iliendelea kuwa nguvu kila mara wakati waliona namna Yehova alikuwa anawasaidia. Ndiyo sababu Yoshua aliwaambia Waisraeli hivi kwa uhakika: “Halikukosa kutimia hata neno moja kati ya maneno yote mema ambayo Yehova Mungu wenu amewaambia ninyi.” Kisha alisema hivi: ‘[Kwa hiyo] mumuogope Yehova na kumutumikia kwa njia isiyo na kosa na katika kweli.’ Kisha aliongezea hivi: ‘Lakini mimi na nyumba yangu, tutamutumikia Yehova.’ (Yoshua 23:14; 24:14, 15) Wakati tunamutegemea Yehova na kuona namna anatusaidia katika maisha yetu, imani yetu inakuwa yenye nguvu zaidi.—Zaburi 34:8.

NAMNA TUNAWEZA KUONYESHA KWAMBA TUKO NA IMANI

12. Namna gani tunaonyesha kwamba tuko na imani yenye nguvu?

12 Namna gani tunaonyesha kwamba tuko na imani yenye nguvu? Mwanafunzi Yakobo alisema hivi: ‘Nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.’ (Yakobo 2:18) Matendo yetu inaonyesha ikiwa tuko na imani yenye nguvu. Namna gani?

Wale wenye kufanya yao yote katika kazi ya kuhubiri wanaonyesha kwamba wako na imani yenye nguvu

(Picha hizi zinapatana na fungu la 13)

13. Namna gani tunaonyesha kwamba tuko na imani kupitia kazi ya kuhubiri?

13 Njia nzuri zaidi ya kuonyesha kwamba tuko na imani, ni kazi ya kuhubiri. Sababu gani? Kwa sababu wakati tunahubiri, tunaonyesha kwamba tunaamini kuwa mwisho unakaribia na kwamba ‘hautachelewa!’ (Habakuki 2:3) Ili tujue ikiwa imani yetu ni yenye nguvu, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Ninaona kazi ya kuhubiri kuwa ya maana sana? Ninajikaza sana kuelezea wengine juu ya Mungu? Ninatafuta namna ya kumutumikia Yehova zaidi?’ (2 Wakorintho 13:5) Tuonyeshe basi kwamba tuko na imani yenye nguvu kwa kuendelea kufanya ‘tangazo la hazarani [mbele ya watu] kwa ajili ya wokovu,’ ni kusema kuhubiri habari njema.—Soma Waroma 10:10.

14, 15. (a) Namna gani tunaweza kuonyesha imani katika maisha yetu ya kila siku? (b) Toa mufano wenye kuonyesha imani yenye nguvu kupitia matendo.

14 Tunaonyesha pia kwamba tuko na imani katika Yehova wakati tunavumilia magumu yenye tunapambana nayo katika ulimwengu huu. Hata kama tuko masikini, wagonjwa, wenye huzuni, wenye kuvunjika moyo, ao tuko na magumu mengine, tunapaswa kuamini kwamba Yehova na Yesu ‘watatusaidia kwa wakati unaofaa.’ (Waebrania 4:16) Tunaonyesha kwamba tuko na imani katika Yehova wakati tunamuomba musaada. Yesu alisema kwamba tunaweza kumuomba Yehova atupatie ‘mukate kulingana na mahitaji yetu ya [kila] siku.’ (Luka 11:3) Biblia iko na habari zenye kuonyesha kwamba Yehova anaweza kutupatia mambo yote yenye tuko nayo lazima. Kwa mufano, wakati wa kipwa kali katika Israeli, Yehova alimupatia nabii Eliya chakula na maji. Biblia inasema kwamba ‘kunguru walikuwa wanamuletea mukate na nyama wakati wa asubuhi na mukate na nyama wakati wa jioni [mangaribi], naye akaendelea kunywa maji katika lile bonde la muto.’ (1 Wafalme 17:3-6) Sisi pia tunaamini kwamba Yehova anaweza kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima.

Tunaonyesha kwamba tuko na imani wakati tunavumilia magumu yenye tunapambana nayo katika ulimwengu huu

(Picha hizi zinapatana na fungu la 14))

15 Tuko hakika kwamba wakati tunatumikisha kanuni za Biblia, hilo litatusaidia kutimiza mahitaji ya familia yetu. Rebecca, dada mwenye kuolewa na mwenye kuishi Asia, anaeleza namna yeye na familia yake walitumikisha kanuni zenye kupatikana kwenye Mathayo 6:33 na Methali 10:4. Anasema kwamba bwana yake aliona kuwa kazi yake ilitia urafiki wao pamoja na Yehova katika hatari. Kwa hiyo, bwana yake aliacha kazi hiyo. Kwa sababu walikuwa na watoto ine wa kushugulikia, walianza kupiga chakula cha kuuzisha. Kwa sababu walitumika kwa bidii, hawakukosa feza za kuwasaidia kutimiza mahitaji ya familia yao. Dada Rebecca anasema hivi: “Tuliona kwamba Yehova hakutuacha hata kidogo. Hatukukosa chakula hata siku moja.” Umekwisha kujikuta katika hali kama hiyo yenye kutia nguvu imani yako?

Tuko hakika kwamba wakati tunatumikisha kanuni za Biblia, hilo litatusaidia kutimiza mahitaji ya familia yetu

16. Tutapata nini ikiwa tunamutumainia Mungu?

16 Tunapaswa kuwa hakika kwamba Yehova atatusaidia ikiwa tunafuata muongozo wake. Mutume Paulo alitaja maneno ya nabii Habakuki wakati alisema hivi: “Mwadilifu (mwenye haki) ataishi kwa sababu ya imani.” (Wagalatia 3:11; Habakuki 2:4) Ndiyo sababu tunapaswa kuwa na imani yenye nguvu katika Ule mwenye anaweza kutusaidia kabisa. Mutume Paulo anatukumbusha kwamba Mungu ‘anaweza, kulingana na nguvu zake zinazotenda ndani yetu, kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote tunaomba ao tunafikiri.’ (Waefeso 3:20) Watumishi wa Yehova wanajikaza kutimiza mapenzi ya Mungu, lakini wanajua pia kwamba wako na mipaka. Tuko wenye shukrani sana kwa sababu Mungu iko pamoja na sisi na anabariki nguvu zetu za kumutumikia.

MUNGU ANAJIBU SALA ZA KUOMBA IMANI

17. (a)Yesu alijibu mitume wake namna gani? (b) Sababu gani tunaweza kutumaini kwamba Yehova atajibu sala zetu za kuomba imani zaidi?

17 Mambo yenye tumezungumuzia inaweza kutusaidia tujisikie kama mitume wa Yesu wakati walimuambia hivi: ‘Utupatie imani zaidi.’ (Luka 17:5) Yesu aliwajibu kwa njia ya pekee kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, wakati walipata roho takatifu na kuwa uwezo wa kuelewa muzuri zaidi mapenzi ya Mungu juu ya wanadamu. Hilo liliwasaidia wakuwe na imani yenye nguvu. Matokeo ilikuwa nini? Ni wakati huo ndiyo walianza kazi kubwa zaidi ya kuhubiri. (Wakolosai 1:23) Tunaweza kutumaini kwamba Mungu atajibu sala zetu za kuomba imani zaidi? Yehova anatuahidi kwamba atajibu sala hizo ikiwa ‘tunaomba kulingana na mapenzi yake.’—1 Yohana 5: 14.

18. Namna gani Yehova anawabariki wale wenye kukomalisha imani yao?

18 Wakati tunamutegemea kabisa Yehova, hilo litamufurahisha. Atajibu sala yetu ya kumuomba imani zaidi, imani yetu itakuwa yenye nguvu, na tutakuwa wenye ‘kustahili Ufalme wa Mungu.’—2 Wathesalonike 1:3, 5.

^ fu. 4 Mifano fulani inapatikana katika habari zenye kichwa “Masimulizi Kuhusu Maisha ya Watu” katika Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 7, 1993 (Lillian Gobitas Klose); Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 2, 1994 (Feliks Borys); na Amuka! ya Mwezi wa 9, 2009 (Josephine Elias).