Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Muendelee Kuwaheshimu Sana Watu wa Namna Hiyo’

‘Muendelee Kuwaheshimu Sana Watu wa Namna Hiyo’

TANGU mwaka wa 1992, Baraza Lenye Kuongoza limechagua wazee wenye uzoefu na wenye kukomaa kiroho ili wasaidie halmashauri mbalimbali za baraza hilo kufanya kazi. * (Soma maelezo ya chini.) Wasaidizi hao wenye kuwa kati ya “kondoo wengine,” wanasaidia sana ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza. (Yohana 10:16) Kila juma, wanahuzuria mukutano wa halmashauri zenye wanasaidia. Kazi yao ni kuleta habari zenye kuhitajiwa na kutoa mapendekezo. Kisha, ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wanakamata maamuzi ya mwisho, na kisha wasaidizi hao wanahakikisha kwamba mambo yenye iliamuliwa inatimizwa kabisa. Wasaidizi hao wako tayari kufanya kazi yoyote yenye wanapewa. Wanasafiri kwenye mikusanyiko ya pekee na ya kimataifa pamoja na ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza. Wanaweza pia kuombwa kuwa wajumbe wa makao yetu makubwa ili kutembelea Beteli mbalimbali.

Ndugu moja mwenye amekuwa musaidizi wa tangu mwaka wa 1992, anasema hivi: “Wakati ninatimiza muzuri mugawo wangu, hilo linasaidia ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza wakaze akili yao juu ya namna ya kutimiza madaraka yao.” Ndugu mwengine mwenye amekuwa musaidizi kwa miaka 20, anasema hivi: “Ni pendeleo kubwa sana lenye sikuwazia hata kidogo kwamba ningepata.”

Baraza Lenye Kuongoza limetolea wasaidizi hao madaraka mengi na linapendezwa na kazi ngumu yenye ndugu hao waaminifu wanafanya. Basi sisi wote ‘tuendelee kuwaheshimu sana watu wa namna hiyo.’—Wafilipi 2:29.

^ fu. 2 Ili kupata habari zaidi juu ya kazi za halmashauri sita za Baraza Lenye Kuongoza, soma ukurasa wa 131 katika kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala!