Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Mutu Asiye na Uzoefu Anaamini Kila Neno’

‘Mutu Asiye na Uzoefu Anaamini Kila Neno’

“Mujinga ni mutu mwenye hasomake gazeti la habari; na mujinga sana ni ule mwenye anaamini mambo yenye anasoma kwa sababu tu inapatikana katika gazeti la habari.”

—August von Schlözer, mwanahistoria na mwandikaji wa Alemanye (1735-1809).

KUMEPITA miaka 200, watu hawakuwa wanaamini kila jambo lenye liliandikwa katika magazeti ya habari. Leo, sisi pia hatuwezi kuamini kila jambo lenye tunasoma ao kuona kwenye Internete. Kuna habari nyingi sana kwenye Internete, na teknolojia ya sasa inatusaidia kupata habari hizo. Habari nyingi ni za kweli, za maana, na hazina hatari, lakini nyingi sana ni za uongo, hazina maana, na ni zenye hatari. Ndiyo sababu tunapaswa kuchagua kwa uangalifu habari zenye tunasoma. Wakati watu fulani wanaanza kutumia Internete, wanaweza kufikiri kwamba habari fulani ni za kweli kwa sababu tu zinapatikana kwenye Internete ao kwa sababu tu marafiki wao ndio waliwatumia habari hizo. Wanaweza kuamini habari fulani hata kama ni ya uongo kabisa. Biblia inatuonya hivi: ‘Mutu asiye na uzoefu anaamini kila neno, lakini mutu mwerevu anazifikiria hatua zake.’—Methali 14:15.Tunapaswa kuwa werevu, kuliko kuwa watu wenye kukosa uzoefu, ao wenye kuamini bila kufikiri kila jambo lenye wanasikia. Uwerevu utatusaidia kuwa waangalifu na kuamini tu mambo yenye tunajua kwamba ni ya kweli. Hata kama habari fulani ya uongo yenye tumesoma kwenye Internete inaweza kuwa inajulikana sana, hatutadanganywa na kuamini habari hiyo. Ni nini inaweza kukusaidia ukuwe mwerevu? Kwanza, ujiulize hivi: ‘Habari hii inatoka kwenye adresi ya Internete yenye kujulikana na sheria na yenye kutegemeka? Ao inatoka kwenye adresi ya Internete kwenye kila mutu anaweza kuandika mawazo yake ao nafasi ingine yenye haijulikane? Je, adresi ingine yenye kutegemeka imekwisha kuonyesha kwamba habari hiyo ni ya uongo?’ * (Soma maelezo ya chini.) Kisha utumie akili nzuri. (Methali 7:7) Ikiwa habari fulani inaonekana kuwa haiko ya kweli ao haiwezekane kabisa, pengine inaweza kuwa hivyo. Pia, ikiwa unasoma habari zenye kushushia wengine heshima, ufikirie ni nani mwenye atafurahi ikiwa habari hiyo inaenea sana na sababu gani anapenda habari hiyo ienee.

UNAZOEA KUTUMIA WENGINE HABARI ZENYE UNAPATA?

Watu fulani wanaweza kutumia marafiki wao wote habari zenye wamepata bila hata kuchunguza ikiwa habari hizo ni za kweli ao bila hata kufikiria mambo yenye inaweza kutokea kisha wao kutuma habari hizo. Pengine ni kwa sababu kila mara wanapenda wajulikane na watu na wakuwe wa kwanza kueneza habari fulani. (2 Samweli 13:28-33) Lakini mutu mwerevu anafikiria mambo mabaya yenye inaweza kutokea. Kwa mufano, habari hizo zinaweza kuharibu sifa ya mutu ao ya shirika fulani.

Mutu mwenye anatuma habari fulani anaweza kukosa kuichunguza kwa sababu kufanya hivyo kunaomba wakati na bidii. Anafikiri tu kwamba wale wenye watapata habari hiyo ndio wataichunguza. Lakini wakati wao ni wa maana pia. (Waefeso 5:15, 16) Kwa hiyo, kuliko kutumia wengine habari zenye hatujue ikiwa ni za kweli, tunapaswa kufikiri hivi: “Ikiwa niko na mashaka juu ya habari hizi, ninapaswa kuzivuta!”

Ujiulize hivi: ‘Ninazoea kutumia wengine habari zenye ninapata? Je, wakati fulani ilikuwa lazima niombe marafiki wangu musamaha kwa sababu niliwatumia habari zenye hazifae ao za uongo? Je, mutu fulani amekwisha kuniambia niache kumutumia habari zenye ninapata?’ Kumbuka kwamba, ikiwa marafiki wako wana adresi ya Internete, wanaweza pia kuitumia, na kwa hiyo hawatahitaji musaada wako ili kutafuta mambo yenye kuwapendeza. Hawapendi kupata habari nyingi zenye kuwa na video, picha, ao habari zenye kuchekesha. Pia, haiko muzuri kutumia wengine rekodi ao maandishi ya hotuba zenye kutegemea Biblia. * (Soma maelezo ya chini.) Na ukumbuke kwamba mutu atapata faida kubwa ikiwa anajitafutia habari katika vichapo vyetu, anajisomea maandiko katika Biblia, ao anatayarisha majibu yake kwa ajili ya mikutano.

Nimutumie mutu mwengine habari hii?

Utafanya nini ikiwa unaona kwenye Internete habari fulani ya uongo juu ya tengenezo la Yehova? Usisome hata kidogo habari hiyo! Usiamini habari hiyo. Kuwatumia wengine habari hiyo na kuwaomba watoe maoni yao ni kukosa hekima, kwa sababu hilo litafanya habari hiyo ienee sana. Ikiwa jambo fulani lenye umeona kwenye Internete linakuogopesha, umuombe Yehova hekima na uzungumuze na ndugu wenye kukomaa kiroho. (Yakobo 1:5, 6; Yuda 22, 23) Hatupaswe kushangaa wakati watu wanasema uongo juu yetu. Watu walisema uongo juu ya Yesu, na aliambia wanafunzi wake kwamba maadui wao watawatesa na ‘kusema kwa uongo kila namna ya jambo mbaya juu yao.’ (Mathayo 5:11; 11:19; Yohana 10:19-21) Kwa hiyo, ikiwa unatumia hekima na kufikiri kwa uangalifu, unaweza kutambua ikiwa mutu fulani anasema uongo na ikiwa anajaribu kudanganya wengine.—Methali 2:10-16.

UHESHIMU WENGINE

Pia, tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu kuelezea wengine habari zenye kuhusu ndugu na dada zetu ao mambo yenye tumesikia. Hata kama habari fulani ni ya kweli, wakati fulani tutaonyesha hekima na upendo kwa kuepuka kueneza habari hiyo. (Mathayo 7:12) Kwa mufano, ni kukosa upendo kutumia watu habari za kushushia wengine heshima. (2 Thesalonike 3:11; 1 Timotheo 5:13) Pia, habari fulani zinapaswa kuchungwa kuwa siri. Watu wenyewe wanaweza kupenda kufunua habari hizo kisha wakati fulani ao kwa njia fulani ya pekee. Tunapaswa kuheshimu haki yao ya kuamua wakati na namna ya kufunua habari hizo. Kwa kweli, ikiwa tunafunua habari hizo mbele ya wakati, hilo linaweza kuwa na matokeo mabaya.

Leo, habari zinaweza kuenea mbio sana, iwe ni za kweli ao za uongo, za maana ao hapana, zenye kuwa na hatari ao hapana. Hata kama unatumia mutu habari fulani, mutu huyo anaweza kuitumia wengine katika dunia yote kwa muda mufupi tu. Kwa hiyo, tuepuke kutumia bila kukawia marafiki wetu wote habari zenye tumepata. Hata kama upendo ‘unaamini mambo yote’ na hauna mashaka, tunapaswa kuepuka kuwa wajinga na kuamini habari yoyote ya mupya na yenye kufurahisha. (1 Wakorintho 13:7) Pia, hatupendi kuamini hata kidogo mambo ya uongo ao habari zenye kuchukiza kuhusu tengenezo la Yehova na kuhusu ndugu na dada zetu, wenye tunapenda. Ukumbuke kwamba wale wenye kuanzisha habari hizo za uongo na kuzieneza wanamupendeza Shetani Ibilisi, ‘baba ya uongo.’ (Yohana 8:44) Kwa hiyo, tukuwe werevu na kila mara tufikirie kwa uangalifu namna tunatumia habari nyingi sana zenye kupatikana leo. Biblia inasema kwamba ‘wasio na uzoefu hakika watariti upumbavu, lakini werevu watavaa ujuzi kama vazi [nguo] la kichwani.’—Methali 14:18.

^ fu. 4 Mara kwa mara, habari fulani inaweza kutokea tena, hata kama zamani ilijulikana kuwa ni ya uongo. Inaweza kubadilishwa kidogo tu ili ionekane kuwa ya kweli.

^ fu. 8 Soma “Kisanduku cha Maulizo” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 4, 2010.