Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Unamupenda Jirani Yako Kama Wewe Mwenyewe’?

‘Unamupenda Jirani Yako Kama Wewe Mwenyewe’?

‘Umupende jirani yako kama wewe mwenyewe.’MATHAYO 22:39.

NYIMBO: 73, 36

1, 2. Namna gani Maandiko inaonyesha kwamba upendo ni wa maana sana?

SIFA kubwa zaidi ya Mungu ni upendo. (1 Yohana 4:16) Yesu Kristo, kiumbe wake wa kwanza, aliishi pamoja na Baba yake huko mbinguni kwa mamiliare ya miaka, na alielewa muzuri kwamba Yehova ni Mungu mwenye upendo. (Wakolosai 1:15) Yesu ameonyesha upendo kama huo katika maisha yake yote, ni kusema, wakati alikuwa mbinguni na wakati alikuwa duniani. Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kwamba sikuzote Yehova na Yesu wanatawala kwa njia yenye upendo.

2 Wakati mutu moja alimuuliza Yesu ni amri gani yenye kuwa kubwa zaidi, Yesu alimujibu hivi: “‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’ Hii ndiyo amri iliyo kubwa na ya kwanza. Ya pili, kama hiyo, ni hii: ‘Umupende jirani yako kama wewe mwenyewe.’”—Mathayo 22:37-39.

3. “Jirani” yetu ni nani?

3 Ni jambo la lazima tuonyeshe upendo katika uhusiano wetu wote pamoja na wengine. Yesu alisema kwamba tunapaswa kumupenda Yehova na kupenda jirani yetu. Lakini, “jirani” yetu ni nani? Ikiwa umeoa ao kuolewa, jirani yako wa karibu zaidi ni bwana ao bibi yako. Pia, ndugu na dada zetu katika kutaniko, na watu wenye tunakutana nao katika mahubiri ni majirani wetu. Katika habari hii, tutajifunza namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunapenda majirani wetu.

UMUPENDE BIBI AO BWANA YAKO

4. Ni nini inaweza kufanya ndoa ikuwe yenye furaha, hata kama bibi na bwana hawakamilike?

4 Yehova aliumba Adamu na Eva na kuwaunganisha ili waishi pamoja. Hiyo ilikuwa ndoa ya kwanza. Mungu alipenda wakuwe na ndoa yenye furaha, wazae watoto na kuijaza dunia. (Mwanzo 1:27, 28) Lakini, kisha kumukosea Yehova, ndoa yao iliharibika, na wakatuachia sisi wote zambi na kifo. (Waroma 5:12) Hata hivyo, inawezekana leo kuwa na ndoa yenye furaha. Yehova, mwenye alianzisha ndoa, ametolea bibi na bwana mashauri mazuri sana kupitia Biblia.—Soma 2 Timotheo 3:16, 17.

Yehova anaomba bwana atumie muzuri ukichwa wake

5. Sababu gani upendo ni wa maana sana katika ndoa?

5 Biblia inaonyesha kwamba ili tukuwe na uhusiano muzuri pamoja na wengine, ni jambo la lazima tukuwe wenye kuchangamuka na kuonyesha upendo wenye huruma. Jambo hilo ni la maana sana katika ndoa. Mutume Paulo alifasiria upendo wa kweli wakati aliandika hivi: ‘Upendo ni wenye uvumilivu na wenye fazili. Upendo hauna wivu. Haujigambe [haujivimbishe kwa kiburi], haujivune, haujiendeshe bila adabu, hautafute faida zake wenyewe, hauchokozeke. Hauweke hesabu ya ubaya. Haushangilie juu ya ukosefu wa uadilifu, bali unashangilia pamoja na kweli. Unahimili mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote, unavumilia mambo yote. Upendo haushindwe kamwe [hata kidogo].’ (1 Wakorintho 13:4-8) Ikiwa tunafikiri sana juu ya maneno hayo ya mutume Paulo na kuitumikisha, tunaweza kuwa na ndoa yenye furaha.

Biblia inatuonyesha namna ya kuwa na ndoa yenye furaha (Picha hii inapatana na fungu la 6, 7)

6, 7. (a)Biblia inasema nini juu ya ukichwa? (b) Bwana Mukristo anapaswa kumutendea bibi yake namna gani?

6 Yehova aliamua ni nani anapaswa kuwa kichwa cha familia. Mutume Paulo alisema hivi: ‘Ninataka mujue kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo; nacho kichwa cha mwanamuke ni mwanaume; nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.’ (1 Wakorintho 11:3) Lakini Yehova anaomba bwana atumie muzuri ukichwa wake, ni kusema, asikuwe mugumu ao mukali. Yehova anatumia muzuri Ukichwa wake na anahangaikia wengine. Kwa hiyo, Yesu anaheshimu namna Mungu anatumia mamlaka yake kwa upendo. Alisema hivi: ‘Ninamupenda Baba.’ (Yohana 14:31) Yesu hangesema maneno hayo ikiwa Yehova alikuwa anamutendea kwa ukali.

7 Bwana ni kichwa cha bibi yake; lakini Biblia inamuomba amuheshimu. (1 Petro 3:7) Namna gani bwana anaweza kufanya hivyo? Anaweza kufikiria mambo yenye bibi yake iko nayo lazima, na kuheshimu mambo yenye anapenda. Biblia inasema hivi: ‘Waume [bwana], muendelee kuwapenda wake [bibi] zenu, kama vile Kristo pia alipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake.’ (Waefeso 5:25) Ndiyo, Yesu alifikia hata kutoa uzima wake kwa ajili ya wafuasi wake. Ikiwa bwana anamuiga Yesu kwa kutumia ukichwa wake muzuri, bibi yake atakuwa tayari kumupenda, kumuheshimu, na kuheshimu maamuzi yake.—Soma Tito 2:3-5.

UWAPENDE NDUGU NA DADA ZAKO

8. Namna gani tunapaswa kuwatendea ndugu na dada zetu?

8 Leo, mamilioni ya watu katika dunia yote wanamuabudu Yehova. Ni ndugu na dada zetu. Tunapaswa kuwatendea namna gani? Biblia inasema hivi: “Tuwatendee wote mema, na hasa [zaidi] wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Wagalatia 6:10; soma Waroma 12:10.) Mutume Petro aliandika kwamba ikiwa tunakuwa “watiifu kwa ile kweli,” hilo litafanya tukuwe na “upendo wa kindugu” wa kweli. Aliwaambia pia Wakristo wenzake hivi: ‘Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mukubwa ninyi kwa ninyi.’—1 Petro 1:22; 4:8.

9, 10. Sababu gani watumishi wa Mungu wako na umoja?

9 Tengenezo letu la duniani pote ni la pekee. Sababu gani? Kwa sababu tunawapenda sana ndugu na dada zetu, na upendo huo ni wa kweli. Na jambo la maana zaidi ni kwamba, kwa sababu tunamupenda Yehova na tunatii amri zake, anatutegemeza kupitia nguvu yake kubwa zaidi, ni kusema, roho yake takatifu. Roho ya Mungu inatusaidia tukuwe na umoja wa kweli pamoja na ndugu na dada zetu katika dunia yote.—Soma 1 Yohana 4:20, 21.

10 Mutume Paulo alikazia kwamba ni jambo la lazima kupenda ndugu na dada zetu. Aliandika hivi: ‘Mujivike upendo mwororo wenye huruma, fazili, unyenyekevu wa akili, upole, na ustahimilivu. Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa hiari [kwa kupenda] ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine. Kama vile Yehova aliwasamehe ninyi kwa hiari, nanyi mufanye vivyo hivyo pia. Lakini, zaidi ya mambo haya yote, mujivike upendo, kwa maana huo ni kifungo kikamilifu cha muungano.’ (Wakolosai 3:12-14) Tuko wenye shukrani sana kwa sababu hata kama tumetoka nafasi mbalimbali, tuko na “kifungo kikamilifu cha muungano,” ni kusema, upendo!

Upendo na umoja vinaonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ni wafuasi wa kweli wa Kristo, ni kusema, watu wenye Mungu anatumia ili kuhubiri habari njema ya Ufalme katika dunia yote

11. Ni nini inaonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ndio wafuasi wa kweli wa Kristo?

11 Upendo na umoja wa kweli wenye kuwa kati ya watumishi wa Yehova unaonyesha waziwazi kwamba wako katika dini ya kweli. Yesu alisema hivi: ‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukiwa na upendo kati yenu wenyewe.’ (Yohana 13:34, 35) Mutume Yohana aliandika pia hivi: ‘Watoto wa Mungu na watoto wa Ibilisi ni wazi kwa jambo hili: Kila mutu ambaye haendelee kufanya uadilifu hatokane na Mungu, wala yeye ambaye hamupende ndugu yake. Kwa maana huu ndio ujumbe ambao mumesikia tangu mwanzo, kwamba tunapaswa kupendana.’ (1 Yohana 3:10, 11) Upendo na umoja vinaonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ni wafuasi wa kweli wa Kristo, ni kusema, watu wenye Mungu anatumia ili kuhubiri habari njema ya Ufalme katika dunia yote.—Mathayo 24:14.

KAZI YA KUKUSANYA MUKUTANO MUKUBWA

12, 13. Watu wa mukutano mukubwa wanafanya nini leo, na watajionea mambo gani hivi karibuni?

12 Wengi kati ya watumishi wa Yehova leo ni wa ‘umati [mukutano] mukubwa’ wenye kutoka katika sehemu mbalimbali za dunia, na wanategemeza Ufalme. Biblia inasema kwamba ‘hawa ndio wale wanaotoka katika ile ziki kubwa, nao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo,’ ni kusema, wameonyesha imani katika zabihu ya Yesu ya ukombozi. Watu wa mukutano mukubwa wanamupenda Yehova na Mwana wake, na wanamuabudu Yehova ‘muchana na usiku.’—Ufunuo 7:9, 14, 15.

13 Hivi karibuni, Mungu ataharibu ulimwengu huu muovu wakati wa ‘ziki kubwa.’ (Mathayo 24:21; soma Yeremia 25:32, 33.) Lakini, Yehova atawalinda na kuwaongoza watumishi wake ili waingie katika dunia yake mupya kwa sababu anawapenda. Kama vile aliahidi katika Neno lake kumepita miaka 2 000 hivi, ‘atafuta [atapanguza] kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwa tena.’ Unangojea kwa hamu kuishi katika Paradiso wakati mambo mabaya, mateso, na kifo haitakuwa tena?—Ufunuo 21:4.

14. Leo, watu wa mukutano mukubwa wamefikia hesabu gani?

14 Wakati siku za mwisho zilianza katika mwaka wa 1914, hesabu ya watumishi wa Mungu ilikuwa kidogo. Ndugu na dada hao watiwa-mafuta walipambana na magumu mengi, lakini roho takatifu ya Mungu na upendo wao kwa majirani wao viliwachochea kuhubiri habari njema kwa bidii. Wamepata matokeo gani? Leo, kazi ya kukusanya mukutano mukubwa wa watu wenye kuwa na tumaini la kuishi milele duniani inafanywa. Kuko Mashahidi wa Yehova 8 000 000 hivi katika makutaniko zaidi ya 115 400 katika dunia yote, na hesabu yao inaendelea kuongezeka. Kwa mufano, watu zaidi ya 275 500 walibatizwa na kuwa Mashahidi katika mwaka wa utumishi wa 2014. Ni kusema, watu karibu 5 300 wanabatizwa kila juma.

15 Inashangaza sana kuona kwamba watu wengi sana wamesikia habari njema ya Ufalme. Leo, vichapo vyetu vinapatikana katika luga zaidi ya 700. Munara wa Mulinzi ndilo gazeti lenye kugawanywa sana katika dunia yote. Magazeti zaidi ya 52 000 000 inachapishwa kila mwezi, na gazeti hilo linatolewa katika luga 247. Pia, kitabu chenye tunatumia ili kufundisha watu Biblia, ni kusema, Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kimetafsiriwa katika luga zaidi ya 250. Kufikia leo, vitabu 200 000 000 vimechapishwa.

16. Sababu gani tengenezo la Yehova linaendelea kupanuka?

16 Tengenezo letu linaendelea kupanuka kwa sababu tunamuamini Mungu na tunaamini pia kwamba Neno lake Biblia, liliongozwa na roho yake takatifu. (1 Wathesalonike 2:13) Yehova anaendelea kutubariki hata kama Shetani anatuchukia na kutupinga.—2 Wakorintho 4:4.

UENDELEE KUWAPENDA WENGINE

17, 18. Yehova anatuomba tuwatendee namna gani watu wenye hawamuabudu?

17 Watu wanatenda kwa njia mbalimbali wakati tunawahubiria. Watu fulani wanatusikiliza, na wengine wanakataa kusikiliza ujumbe wetu. Yehova anatuomba tuwatendee namna gani watu wenye hawamuabudu? Iwe wanasikiliza ujumbe wetu ao hapana, tunafuata shauri hili la Biblia: ‘Maneno yenu na yakuwe yenye neema sikuzote, yenye kukolezwa chumvi, ili mujue jinsi [namna] munapaswa kumujibu kila mutu.’ (Wakolosai 4:6) Wakati tunatetea mambo yenye tunaamini, tunapaswa kila mara kufanya hivyo “kwa tabia-pole na heshima kubwa” kwa sababu tunapenda majirani wetu.—1 Petro 3:15.

18 Hata wakati watu wanakasirika na kukataa ujumbe wetu, tunaonyesha kwamba tunawapenda na kwamba tunaiga mufano wa Yesu. Wakati Yesu ‘alitukanwa, hakujibu kwa matukano. Alipokuwa akiteseka, hakutoa vitisho [hakuogopesha].’ Lakini, Yesu alimutegemea Yehova. (1 Petro 2:23) Kwa hiyo, kila mara, tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kutii shauri hili: ‘Musilipe ubaya kwa ubaya ao matukano kwa matukano. [Lakini], mutoe baraka.’—1 Petro 3:8, 9.

Tunapaswa kuwapenda maadui wetu hata kama wanatutendea namna gani

19. Namna gani tunapaswa kuwatendea maadui wetu?

19 Unyenyekevu unatusaidia kutii kanuni ya maana sana yenye Yesu alitutolea. Alisema hivi: “Mulisikia kwamba ilisemwa: ‘Umupende jirani yako na kumuchukia adui yako.’ Hata hivyo, mimi ninawaambia ninyi: Muendelee kuwapenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi, ili mupate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni, kwa kuwa yeye analichomoza jua lake juu ya watu waovu na wema na ananyesha mvua juu ya watu waadilifu na wasio waadilifu.” (Mathayo 5:43-45) Kwa sababu sisi ni watumishi wa Mungu, tunapaswa kuwapenda maadui wetu hata kama wanatutendea namna gani.

20. Tunajua namna gani kwamba watu katika dunia yote watapenda Mungu na majirani wao? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

20 Wakati wote, tunapaswa kuonyesha kwamba tunapenda Yehova na majirani wetu. Hata kama watu wanatupinga sisi na ujumbe wetu, tunawasaidia wakati wako na lazima ya musaada. Mutume Paulo aliandika hivi: “Musikuwe na deni la hata jambo moja la mutu yeyote, isipokuwa kupendana; kwa maana yeye anayemupenda mwanadamu mwenzake ameitimiza sheria. Kwa maana sheria zinazosema, ‘Usifanye uzinzi, usiue, usiibe, usitamani,’ na amri nyingine yoyote iliyoko, zimejumlishwa katika neno hili, yaani: ‘Umupende jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Upendo haumufanyie uovu jirani ya mutu; kwa hiyo upendo ndio utimizo wa sheria.” (Waroma 13:8-10) Watu wa ulimwengu huu ni wenye migawanyiko, wenye jeuri, na wenye kutawaliwa na Shetani; lakini, watumishi wa Mungu wanaonyesha majirani wao upendo wa kweli. (1 Yohana 5:19) Upendo utajaa katika dunia yote kisha Yehova kuharibu ulimwengu huu muovu, Shetani, na mashetani wake. Itakuwa baraka kubwa sana wakati watu wote katika dunia watamupenda Yehova na majirani wao!