Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uzoeze Mutoto Wako Amutumikie Yehova

Uzoeze Mutoto Wako Amutumikie Yehova

‘Yule mutu wa Mungu wa kweli . . . na atufundishe yale tunayopaswa kumutendea huyo mutoto atakayezaliwa.’WAAMUZI 13:8.

NYIMBO: 88, 120

1. Manoa alifanya nini wakati alisikia kwamba atakuwa na mutoto?

MANOA na bibi yake hawakuwa tena na tumaini la kupata mutoto. Kisha, siku moja, malaika wa Yehova akamuambia bibi ya Manoa kwamba atazaa mutoto. Hiyo ilikuwa habari muzuri na yenye kushangaza sana! Wakati bibi yake alimuambia habari hiyo, Manoa alifurahi sana. Lakini Manoa alifikiria pia sana mambo yenye Yehova alipenda atimize kwa sababu angekuwa na mutoto. Namna gani Manoa na bibi yake wangezoeza mutoto wao ili amupende Yehova na kumutumikia, hata kama Waisraeli wengi sana walikuwa wanafanya mambo mabaya? Manoa alimuomba Yehova atume tena malaika wake. Alisema hivi: ‘Tafazali, yule mutu wa Mungu wa kweli ambaye ulimutuma na arudi kwetu tena, atufundishe yale tunayopaswa kumutendea huyo mutoto atakayezaliwa.’—Waamuzi 13:1-8.

2. Unapaswa kufundisha watoto wako mambo gani, na namna gani unaweza kufanya hivyo? (Soma pia kisanduku chenye kichwa “ Wanafunzi Wako wa Kwanza Kabisa.”)

2 Ikiwa uko na watoto, kwa kweli unaelewa namna Manoa alijisikia. Wewe pia uko na daraka la kusaidia watoto wako wamujue Yehova na kumupenda. (Methali 1:8) Wakati wa ibada ya familia, unaweza kuwasaidia waendelee kujifunza juu ya Yehova na juu ya Biblia. Ni kweli kwamba, unapaswa kufanya mengi zaidi kuliko tu kujifunza Biblia pamoja na watoto wako kila juma. (Soma Kumbukumbu la Torati 6:6-9.) Ni mambo mengine gani yenye itakusaidia uzoeze watoto wako wamupende Yehova na kumutumikia? Katika habari hii, tutazungumuzia mufano wa Yesu. Hata kama hakukuwa na watoto, unaweza kuiga namna alifundisha na kuzoeza wanafunzi wake. Yesu aliwapenda na alikuwa munyenyekevu. Alikuwa pia na utambuzi, ni kusema, alielewa kabisa namna walijisikia na alijua namna ya kuwasaidia. Acha sasa tuone namna tunaweza kuiga mufano wa Yesu.

UWAPENDE WATOTO WAKO

3Kila mara Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba anawapenda. (Soma Yohana 15:9.) Pia, alipitisha wakati mwingi pamoja nao. (Marko 6:31, 32; Yohana 2:2; 21:12, 13) Yesu hakuwa tu mwalimu wao, lakini alikuwa pia rafiki yao. Kwa hiyo, wanafunzi wake walikuwa hakika kwamba aliwapenda. Mufano wa Yesu unaweza kukufundisha nini?

4. Namna gani unaweza kuonyesha watoto wako kwamba unawapenda? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Uwaambie watoto wako kwamba unawapenda, na uwaonyeshe kwamba unawahangaikia sana. (Methali 4:3; Tito 2:4) Samuel, ndugu wa Australia, anasema hivi: “Wakati nilikuwa mutoto mudogo, Baba yangu alikuwa ananisomea kila mangaribi Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Alikuwa anajibu maulizo yangu, ananikumbatia, na kunibusu (kunipatia baiser) mbele niende kulala. Kisha, nilishangaa kujua kwamba wakati Baba yangu alikuwa mutoto, wazazi wake hawakuzoea kumubusu! Lakini, alijikaza sana kunionyesha kwamba ananipenda. Kwa hiyo, alikuwa rafiki yangu wa sana, na nilijisikia kuwa mwenye furaha na salama.” Uwasaidie watoto wako wajisikie pia hivyo kwa kuwaambia kila mara kwamba “unawapenda.” Uwakumbatie na kuwapatia baiser. Ujiwekee pia wakati wa kuzungumuza nao, kula nao, na kucheza nao.

5, 6. (a) Ili kuonyesha kwamba anapenda wanafunzi wake, Yesu alifanya nini? (b) Unapaswa kutumia njia gani ili kutolea watoto wako nizamu?

5 Yesu alisema hivi: ‘Wale wote ninaowapenda, mimi ninawakaripia na kuwatia nizamu.’ * (Soma maelezo ya chini.) (Ufunuo 3:19) Kwa mufano, wanafunzi wake walibishana mara nyingi ili kujua ni nani alikuwa mukubwa zaidi kati yao. Yesu hakuachilia jambo hilo. Lakini, aliendelea kuwashauria kwa uvumilivu. Hata hivyo, alionyesha kila mara sifa ya upole, na alitafuta nafasi na wakati wenye kufaa ili kuwashauria.—Marko 9:33-37.

Tafuta nafasi na wakati wenye kufaa ili kuwatia nizamu watoto wako, na ufanye hivyo kwa upole

6 Unatia watoto wako nizamu kwa sababu unawapenda. Wakati fulani inaomba tu kuwaelezea sababu gani jambo fulani ni la muzuri ao ni la mubaya. Lakini, utafanya nini ikiwa hawatii? (Methali 22:15) Uige mufano wa Yesu. Uendelee kuwatolea nizamu kwa kuwaongoza, kuwazoeza, na kuwashauria kwa uvumilivu. Uchague nafasi na wakati wenye kufaa ili kuwatolea nizamu, na ufanye hivyo kwa upole. Elaine, dada wa Afrika ya Kusini, anakumbuka namna wazazi wake walikuwa wanamutolea nizamu. Kila mara walimuambia mambo yenye walipenda afanye. Wakati walimuambia kwamba watamupatia malipizi kwa sababu ya kukosa kutii, walifanya hivyo. Lakini anasema hivi: “Hawakunipatia malipizi hata siku moja wakati walikuwa wenye kukasirika. Waliniambia kila mara sababu gani wananipatia malipizi.” Kwa hiyo, dada Elaine alikuwa hakika sikuzote kwamba wazazi wake walimupenda.

UKUWE MUNYENYEKEVU

7, 8. (a) Sala za Yesu ziliwafundisha nini wanafunzi wake? (b) Namna gani sala zako zinaweza kuwafundisha watoto wako wamutegemee Mungu?

7 Muda mufupi mbele akamatwe na kuuawa, Yesu alisali hivi kwa Baba yake: “Abba, Baba, mambo yote yanawezekana kwako; niondolee kikombe hiki. Lakini si lile ninalotaka, bali lile unalotaka.” * (Soma maelezo ya chini.) (Marko 14:36) Wazia namna wanafunzi wa Yesu walijisikia wakati walisikia, ao wakati walijifunza juu ya sala hiyo. Walitambua kwamba hata kama alikuwa mutu mukamilifu, alimuomba Baba yake musaada. Kwa hiyo, walielewa kwamba wao pia walipaswa kuwa wanyenyekevu na kumutegemea Yehova.

Wakati watoto wako wanakusikia unamuomba Yehova musaada, wao pia watajifunza kumutegemea

8 Sala zako zinaweza kufundisha watoto wako mambo mengi. Ni kweli kwamba hausali tu ili kufundisha watoto wako. Lakini wakati wanasikia namna unasali, wanaweza kujifunza kumutegemea Yehova. Katika sala zako, usimuombe tu Yehova asaidie watoto wako, lakini umuombe akusaidie wewe pia. Ana, dada mwenye kuishi Brazili, anasema hivi: “Wakati wa magumu, kama vile wakati wazazi wa wazazi wangu waligonjwa, baba na mama walimuomba Yehova awapatie nguvu ya kupambana na hali hiyo ngumu na awapatie hekima ili wachukue maamuzi mazuri. Hata wakati walipatwa na magumu makali, walimuambia Yehova magumu hayo. Kwa hiyo, nilijifunza kumutegemea Yehova.” Wakati watoto wako wanasikia namna unamuomba Yehova akusaidie uhubirie jirani yako ao akupatie nguvu ya kumuomba mukubwa wako wa kazi ruhusa ya kuhuzuria mukusanyiko fulani, wataelewa kwamba unamutegemea Yehova, nao pia watajifunza kufanya hivyo.

9. (a) Namna gani Yesu alifundisha wanafunzi wake ili wakuwe wanyenyekevu na wenye kufikiria wengine? (b) Ikiwa wewe ni munyenyekevu na mwenye kufikiria wengine, hilo litafundisha nini watoto wako?

9 Yesu aliwaambia wanafunzi wake wakuwe wanyenyekevu na wenye kufikiria wengine, na aliwaachia pia mufano. (Soma Luka 22:27.) Mitume wake walijionea namna alijitoa kabisa ili kumutumikia Yehova na kusaidia wengine, nao pia walijifunza kufanya hivyo. Wewe pia unaweza kufundisha watoto wako kupitia mufano wako. Debbie, dada mwenye kuwa na watoto wawili, anasema hivi: “Bwana yangu alipaswa kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada katika kutaniko kwa sababu yeye ni muzee. Hilo halikunihuzunisha hata kidogo. Nilijua kwamba, kila mara wakati familia yetu ilikuwa na lazima yake, angepitisha pia wakati pamoja na sisi.” (1 Timotheo 3: 4, 5) Mufano wa dada Debbie na bwana yake, Pranas, ulikuwa na matokeo gani juu ya familia yao? Ndugu Pranas anasema kwamba sikuzote watoto wake walikuwa tayari kujitoa ili kufanya kazi mbalimbali wakati wa mikusanyiko. Walikuwa wenye furaha, walipata marafiki wazuri, na walipenda kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada zao. Sasa wote katika familia hiyo wanamutumikia Yehova kwa wakati wote. Ikiwa uko munyenyekevu na unafikiria wengine, unafundisha watoto wako wakuwe tayari kusaidia wengine.

UKUWE NA UTAMBUZI

10. Namna gani Yesu alionyesha utambuzi wakati watu fulani wa Galilaya walimutafuta?

10 Yesu alikuwa mukamilifu; kwa hiyo, alikuwa na utambuzi wa hali ya juu. Hakukazia tu akili juu ya mambo yenye watu walifanya lakini pia alikazia akili juu ya mambo yenye iliwachochea watende hivyo. Alikuwa na uwezo wa kusoma katika mioyo yao. Kwa mufano, wakati fulani watu wa Galilaya walikuja kumutafuta. (Yohana 6:22-24) Alielewa kwamba sababu kubwa yenye iliwachochea wamutafute haikuwa kusikiliza mafundisho yake, lakini walipenda wapate chakula. (Yohana 2:25) Yesu alielewa kabisa namna watu hao walijisikia. Kisha aliwashauria kwa upole na kuwaambia kwamba walipaswa kubadilisha mawazo yao.—Soma Yohana 6:25-27.

Uwasaidie watoto wako wafurahie kazi ya kuhubiri (Picha hii inapatana na fungu la 11)

11. (a)Ni nini inaweza kukusaidia uelewe namna watoto wako wanaona kazi ya kuhubiri? (b) Unaweza kufanya nini ili kuwasaidia watoto wako wafurahie kazi ya kuhubiri?

11 Wewe pia unaweza kuwa na utambuzi hata kama hauna uwezo wa kusoma katika mioyo. Kwa mufano, unaweza kujikaza kuelewa namna watoto wako wanaona kazi ya kuhubiri. Unaweza kujiuliza hivi: ‘Watoto wangu wanangojea tu kwa hamu wakati tutasimamisha kazi ya kuhubiri ili kupumuzika na kula chakula ao kutumia kinywaji fulani?’ Ikiwa unatambua kwamba watoto wako hawafurahie kazi ya kuhubiri, ujikaze kuwasaidia wafurahie kabisa kazi hiyo. Uwaombe wafanye mambo fulani madogo-madogo katika mahubiri ili wajisikie kuwa wa lazima.

12. (a) Yesu aliwaonya wanafunzi wake juu ya mambo gani? (b) Sababu gani wanafunzi wa Yesu walikuwa na lazima kabisa ya onyo hilo?

12 Yesu alitumia utambuzi katika njia gani ingine? Alijua kwamba kosa moja linaweza kuongoza kwenye kosa lingine na hata kwenye zambi nzito, na alionya wanafunzi wake juu ya jambo hilo. Kwa mufano, wanafunzi walijua kwamba ni mubaya kufanya uasherati. Lakini Yesu aliwaonya juu ya mambo yenye ingeweza kuwachochea wafanye zambi hiyo. Alisema hivi: ‘Kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi [uzinifu] pamoja naye moyoni mwake. Ikiwa, sasa, hilo jicho lako la kuume linakufanya ukwazike, uliongoe ulitupilie mbali na wewe.’ (Mathayo 5:27-29) Wanafunzi wa Yesu waliishi kati ya Waroma wenye mwenendo mubaya. Watu hao walifurahia kuangalia michezo yenye kujaa mambo ya uasherati na maneno machafu. Kwa hiyo, Yesu alionya wanafunzi wake kwa upendo waepuke mambo yoyote yenye ingewachochea wafanye zambi.

13, 14. Namna gani unaweza kuwasaidia watoto wako waepuke mambo machafu ya kujifurahisha?

13 Ikiwa wewe ni muzazi, unaweza kutumia utambuzi ili kulinda watoto wako wasifanye mambo yenye kumuchukiza Yehova. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, leo hata watoto wadogo wako katika hatari ya kuangalia pornografia na mambo mengine ya uasherati. Kwa kweli, unapaswa kuambia watoto wako kwamba ni mubaya kuangalia mambo machafu. Lakini kuko mambo mengine yenye unapaswa kufanya ili kuwalinda. Ujiulize hivi: ‘Watoto wangu wanajua sababu gani ni mubaya sana kuangalia pornografia? Ni nini inaweza kuwachochea watafute kuangalia pornografia? Ninawasaidia wajisikie huru kuniambia mambo yao yote, ili wakuwe tayari kuniomba musaada hata wakati wanachochewa kuangalia pornografia?’ Hata ikiwa mutoto wako angali mudogo, unaweza kumuambia hivi: “Ikiwa siku moja unaona jambo fulani kwenye Internete lenye linaweza kukuchochea utafute kujua mambo mengi juu ya uasherati na unapenda kuangalia jambo hilo, tafazali uniambie. Usiogope ao usisikie haya kuniomba musaada. Niko tayari kukusaidia.”

14 Ili ukuwe mufano muzuri kwa watoto wako, uchague kwa uangalifu mambo ya kujifurahisha. Ndugu Pranas, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Unaweza kuwatolea watoto wako mashauri mengi juu ya mambo mbalimbali, lakini wataangalia mambo yenye unafanya na watakuiga.” Ikiwa kila mara unachagua kwa uangalifu muziki, vitabu, na filme zenye kuwa na mambo mazuri ya kujifurahisha, unaweza kuwasaidia watoto wako kufanya hivyo pia.—Waroma 2:21-24.

YEHOVA ATAWASAIDIA

15, 16. (a) Sababu gani munaweza kuwa hakika kwamba Yehova atawasaidia muzoeze watoto wenu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

15 Yehova alifanya nini wakati Manoa alimuomba amusaidie akuwe muzazi muzuri? ‘Mungu wa kweli alimusikiliza Manoa.’ (Waamuzi 13:9) Wazazi, Yehova atasikiliza pia sala zenu. Atawasaidia muzoeze watoto wenu. Atawasaidia pia muonyeshe upendo, mukuwe wanyenyekevu, na mukuwe na utambuzi.

16 Yehova atawasaidia muzoeze watoto wenu wakati wangali wadogo, vilevile atawasaidia muwazoeze wakati watakuwa vijana. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia namna mufano wa Yesu wa upendo, unyenyekevu, na utambuzi unaweza kuwasaidia muzoeze vijana wenu wamutumikie Yehova.

^ fu. 5 Biblia inafundisha kwamba nizamu inamaanisha kumuongoza mutoto, kumuzoeza, kumushauria, na hata kumupatia malipizi wakati fulani. Wazazi wanapaswa kutolea watoto wao nizamu kwa upole na wanapaswa kuepuka kabisa kufanya hivyo wakati wako wenye kukasirika.

^ fu. 7 Watoto wa wakati wa Yesu walizoea kuita baba yao Abba. Neno hilo lilionyesha upendo na heshima.—The International Standard Bible Encyclopedia.