Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MASIMULIZI KUHUSU MAISHA YA WATU

Nimekuwa na Amani Pamoja na Mungu na Pamoja na Mama Yangu

Nimekuwa na Amani Pamoja na Mungu na Pamoja na Mama Yangu

MAMA yangu aliniuliza hivi: “Sababu gani unakataa kuabudu wazazi wako wa zamani? Haujue kwamba ikiwa unaishi leo ni kwa sababu walituzaa? Sababu gani haupendi kuwaonyesha shukrani? Namna gani unaweza kukataa desturi zenye wazazi wetu na sisi tumefuata kwa miaka mingi? Kukataa kuheshimu wazazi wetu wa zamani, kunaonyesha kwamba ibada yetu ni ya upumbavu.” Kisha kusema maneno hayo, Mama yangu alianza kulia.

Miezi kidogo mbele ya hapo, Mashahidi wa Yehova walikuwa wamemuomba mama yangu ajifunze Biblia pamoja nao. Hakupenda kujifunza, lakini ili kuwaonyesha heshima aliwaambia waanze kujifunza na mimi. Kwa kawaida mama yangu hakuwa ananikasirikia kwa sababu nilikuwa ninamutii sikuzote; lakini sasa alikuwa amenikasirikia. Mara hiyo nilikataa kumutii kwa sababu nilipenda kumufurahisha Yehova. Haikuwa mwepesi kufanya hivyo, lakini Yehova alinipatia nguvu.

NINAJIFUNZA JUU YA YEHOVA

Kama watu wengi katika Japani, familia yangu ilikuwa katika dini ya Wabuda. Lakini, kisha kujifunza pamoja na Mashahidi wa Yehova kwa miezi mbili, niliamini kabisa kwamba Biblia inafundisha kweli. Wakati nilijifunza kwamba niko na Baba wa mbinguni, nilipenda kumujua vizuri kabisa. Mwanzoni, mimi na Mama yangu tulifurahia kuzungumuzia mambo yenye nilikuwa ninajifunza. Kila Siku ya Yenga nilianza kuhuzuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme. Wakati niliendelea kujifunza mambo mengi, nilimuambia Mama yangu kwamba sitashiriki tena katika ibada ya dini ya Wabuda. Alibadilisha mawazo yake palepale. Alisema hivi: “Ni jambo la haya katika familia kuwa na mutu mwenye haonyeshe upendo kwa wazazi wetu wa zamani.” Aliniambia niache kujifunza Biblia na kuenda kwenye mikutano. Sikufikiria hata kidogo kwamba mama yangu angeniambia hivyo! Alibadilika kabisa.

Baba pia alimuunga Mama yangu mukono. Nilijifunza katika andiko la Waefeso sura ya 6 kwamba Yehova anapenda niwatii wazazi wangu. Nilipenda amani ikuwe tena katika familia yetu, na nilifikiri kwamba ikiwa ninawatii, mwishowe wao pia watanielewa. Wakati huo, nilipaswa kujitayarisha kwa ajili ya mashindano kwenye masomo, kwa hiyo nilikubali kuacha kukusanyika na kujifunza Biblia kwa muda wa miezi tatu. Lakini, nilimuahidi Yehova kwamba nitaanza tena kukusanyika kisha miezi hiyo tatu.

Nilichukua maamuzi mabaya. Sababu gani? Kwanza, nilifikiri kwamba kisha miezi hiyo tatu nitaendelea kuwa na hamu kubwa ya kumutumikia Yehova. Lakini, bila kukawia urafiki wangu pamoja na Yehova ulikuwa zaifu. Pili, Mama na Baba yangu waliendelea sana kunikaza niache kumutumikia Yehova.

NINAPINGWA NA KUPATA MUSAADA

Kwenye Jumba la Ufalme, nilizungumuza na Mashahidi wengi wenye walipingwa pia katika familia zao. Walinihakikishia kwamba Yehova atanipatia nguvu. (Mathayo 10:34-37) Waliniambia kwamba ikiwa ninaendelea kuwa mwaminifu kwa Yehova, watu wa familia yangu wanaweza kujifunza pia juu ya Yehova. Nilipenda kumutegemea Yehova, kwa hiyo, nilianza kusali sana.

Familia yangu ilitumia njia mbalimbali ili kunipinga. Mama aliniomba niache kujifunza na alijikaza kunionyesha sababu gani nisiendelee kujifunza. Mara nyingi nilikuwa ninabakia kimya. Mara nyingi, wakati nilijaribu kusema jambo fulani, tulibishana sana kwa sababu kila mutu alipenda aonyeshe kwamba dini yake ndiyo ya kweli. Sasa ninaelewa kwamba ikiwa niliheshimu kabisa mambo yenye mama alikuwa anaamini na namna alikuwa anajisikia, mambo haingeendelea kuharibika. Wazazi wangu walinipatia kazi nyingi za kufanya ili nibakie katika nyumba. Wakati fulani walifunga mulango ili nisiingie katika nyumba, ao walikataa kunipatia chakula.

Mama aliomba watu wengine wamusaidie kunisadikisha nimuache Yehova. Aliambia mwalimu wangu, lakini mwalimu huyo alishindwa kunisadikisha. Mama yangu alinipeleka kwa mukubwa wake wa kazi ili anisadikishe kwamba dini zingine zote hazina maana. Aliita pia watu wa jamaa yetu kwenye telefone na kulia wakati aliwaomba wamusaidie. Jambo hilo lilinikasirisha sana. Lakini kwenye mikutano, wazee wa kutaniko walinikumbusha kwamba wakati Mama yangu alikuwa anaelezea watu wengine juu ya hali yetu, kwa kweli alikuwa anawahubiria.

Wazazi wangu walipenda nisome masomo ya juu ili nipate kazi ya muzuri. Kwa sababu sisi wote tulikuwa wenye kukasirika, ilikuwa vigumu kuzungumuzia jambo hilo kwa utulivu. Kwa hiyo, niliwaandikia barua nyingi ili kuwaelezea miradi yangu. Baba alikasirika sana na alisema hivi: “Ikiwa unawaza kama unaweza kupata kazi, uipate kesho, ao uondoke katika nyumba yangu.” Nilisali kwa Yehova na kumuomba musaada. Siku yenye ilifuata, wakati nilikuwa katika mahubiri, dada wawili walinipatia kazi. Kila mumoja wao aliniomba nifundishe watoto wake. Baba hakufurahi, kwa hiyo aliacha kuzungumuza na mimi na alianza kunizarau. Mama yangu alisema kwamba ingekuwa muzuri zaidi nikuwe mutu mwenye kufanya mambo mabaya kuliko kuwa Shahidi wa Yehova.

Yehova alinisaidia kubadilisha mawazo yangu na kujua mambo ya kufanya

Wakati fulani sikuwa hakika ikiwa Yehova alipenda niendelee kukataa kutii wazazi wangu. Kwa hiyo, nilisali kwa Yehova na nilifikiri sana juu ya mambo yenye Biblia inasema juu ya upendo wake. Kufanya hivyo kulinisaidia niendelee kuwa na maoni mazuri na kuelewa kwamba wazazi wangu walinipinga kwa sababu walinihangaikia. Yehova alinisaidia kubadilisha mawazo yangu na kujua mambo ya kufanya. Pia, kadiri niliendelea kuhubiri, nilianza kufurahia zaidi kazi hiyo. Kwa kweli, nilipenda kuwa painia.

NINAKUWA PAINIA

Wakati dada fulani walisikia kwamba ninapenda kuwa painia, waliniambia kwamba ninapaswa kungojea kwanza wazazi wangu watulie. Nilimuomba Yehova anipatie hekima, nilitafuta habari katika vichapo vyetu, nilifikiria sababu zenye zilinichochea nikuwe painia, na nilizungumuza na ndugu na dada wenye uzoefu. Kisha, niliamua kwamba ninapenda kumufurahisha Yehova. Nilielewa pia kwamba hata kama ninangojea wakati fulani upite mbele nikuwe painia, wazazi wangu wataendelea tu kunipinga.

Nilianza kazi ya upainia wakati nilikuwa katika mwaka wangu wa mwisho wa masomo ya segondere. Kisha kuwa painia kwa muda fulani, nilipenda kuhamia mahali penye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Lakini Mama na Baba yangu hawakupenda nihame. Kwa hiyo, nilingojea kwanza nikuwe na miaka 20. Kisha, niliomba biro ya tawi inipatie eneo lenye kuwa karibu na watu wa jamaa yangu kusini mwa inchi ya Japani ili Mama yangu asikuwe na wasiwasi sana.

Wakati nilikuwa katika mugawo wangu, nilifurahi kuona namna wanafunzi wangu wengi wa Biblia wanabatizwa. Kwa sababu nilipenda kupanua utumishi wangu, nilianza kujifunza luga ya Kiingereza. Kisha kuona bidii ya mapainia wa pekee wawili katika kutaniko letu na namna walisaidia ndugu na dada, niliamua pia kuwa painia wa pekee. Wakati huo, Mama yangu aligonjwa sana mara mbili, na nilirudia nyumbani mara mbili ili kumusaidia. Jambo hilo lilimushangaza sana, na alianza kunitendea kwa upole.

YEHOVA AMENIBARIKI SANA

Kisha miaka saba, Atsushi, moja kati ya mapainia wa pekee wawili wenye nimezungumuzia, alinitumia barua. Alipenda anioe na alipenda kujua mawazo yangu juu yake. Sikufikiria hata kidogo kwamba ninaweza kumupenda Atsushi, na kwamba yeye pia angeweza kunipenda. Kisha mwezi moja, nilimujibu kwamba ninapenda kumujua zaidi. Tuliona kuwa tulikuwa na miradi ileile. Tulipenda kuendelea kufanya utumishi wa wakati wote na tulikuwa tayari kukubali kila mugawo wenye tungepewa. Mwishowe tulioana. Nilifurahi sana kwa sababu Mama, Baba, na watu wengine wa jamaa yetu walikuja kwenye ndoa yetu.

Nepali

Kisha muda mufupi, wakati tulikuwa mapainia wa kawaida, Atsushi aliwekwa kuwa mwangalizi wa badala ao mwangalizi musaidizi. Baadaye, tukakuwa mapainia wa pekee na kisha tukaanza kufanya kazi ya muzunguko. Wakati tulimaliza kutembelea kwa mara ya kwanza makutaniko yote ya muzunguko wetu, biro ya tawi ilituita kwenye telefone. Tuliulizwa ikiwa tuko tayari kuhamia katika inchi ya Nepali na kuendelea kutembelea makutaniko katika inchi hiyo.

Kutumikia katika inchi mbalimbali kumenifundisha mambo mengi juu ya Yehova

Nilijiuliza ikiwa wazazi wangu watajisikia namna gani wakati nitahamia katika inchi hiyo ya mbali. Wakati niliwaambia kwenye telefone, Baba yangu alijibu hivi: “Utahamia katika eneo nzuri sana.” Juma moja tu mbele ya hapo, rafiki moja ya baba yangu alimupatia kitabu kimoja chenye kuzungumuzia inchi ya Nepali, na Baba yangu alikuwa anafikiri kwamba hiyo ingekuwa nafasi nzuri ya kutembelea.

Tulifurahia sana kuwa pamoja na watu wa Nepali wenye kuwa tayari kufanya urafiki. Kisha, makutaniko ya Bangladesh iliongezwa kwenye muzunguko wetu. Inchi hiyo iko karibu na Nepali, lakini watu wa inchi hiyo wako tofauti sana na Wanepali. Tuliona mambo yenye kuwa tofauti katika mahubiri. Kisha miaka tano, tulitumwa tena katika inchi ya Japani, sasa tunafurahia kazi ya kutembelea makutaniko katika inchi hiyo.

Nilijifunza mambo mengi juu ya Yehova wakati nilikuwa ninatumikia katika inchi ya Japani, Nepali, na Bangladesh. Watu wa inchi hizo wako na desturi, tabia, na namna ya kuishi yenye kuwa tofauti. Na katika kila inchi, kila mutu iko tofauti kabisa na mwengine. Nimeona namna Yehova anahangaikia watu, anawakubali, anawasaidia na kuwabariki.

Niko na mambo mengi yenye kunichochea nimushukuru Yehova. Amenisaidia nimujue na kufanya kazi yake, na amenipatia mwanaume muzuri Mukristo. Mungu amenisaidia kuchukua maamuzi mazuri, na leo niko na uhusiano muzuri pamoja naye na pamoja na familia yangu. Ninamushukuru Yehova kwa sababu mimi na Mama yangu tumekuwa tena marafiki wazuri. Niko mwenye shukrani sana kwa sababu nimekuwa na amani pamoja na Mungu na pamoja na mama yangu.

Tunapata furaha nyingi katika kazi ya kutembelea makutaniko