Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tafsiri ya Biblia Yenye Kuwa Mwepesi Kueleweka

Tafsiri ya Biblia Yenye Kuwa Mwepesi Kueleweka

“Neno la Mungu liko hai.”—WAEBRANIA 4:12.

NYIMBO: 37, 116

1. (a) Mungu alimupatia Adamu kazi gani? (b) Tangu wakati huo, namna gani watu wa Mungu wametumikisha zawadi ya luga?

YEHOVA MUNGU aliwapatia wanadamu zawadi ya kutumia luga ili kuzungumuza. Katika shamba la Edeni, Mungu alimupatia Adamu kazi ya kuwapatia wanyama wote majina. Adamu alipatia kila munyama jina lenye kufaa. (Mwanzo 2:19, 20) Tangu wakati huo, watu wa Mungu wametumikisha zawadi ya luga ili kumusifu Yehova na kuzungumuza na wengine juu yake. Katika miaka ya hivi karibuni, watu wa Mungu wametumikisha zawadi ya luga katika kazi ya kutafsiri Biblia ili kusaidia watu wengi wajifunze kumujua Yehova.

2. (a) Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya, ilifuata kanuni gani katika kazi ya kutafsiri Biblia? (b) Tutajifunza nini katika habari hii?

2 Kuko tafsiri nyingi sana za Biblia, lakini tafsiri fulani ni za kweli kabisa kuliko zingine. Ili kutafsiri Biblia ya kweli kabisa, Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya iliamua kufuata kanuni tatu kubwa: (1) Kuheshimu jina la Mungu na kulirudisha katika Neno lake kila nafasi kwenye lilipatikana katika Maandishi ya zamani. (Soma Mathayo 6:9.) (2) Kutafsiri ujumbe wa Mungu neno kwa neno nafasi kwenye inawezekana. Na nafasi kwenye haiwezekane, kutafsiri kabisa maana ya ujumbe huo. (3) Kutumia maneno yenye kuwa mepesi kusoma na mepesi kueleweka. * (Soma maelezo ya chini.) (Soma Nehemia 8:8, 12.) Watafsiri wa Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya wamekuwa wakifuata kanuni hizo tatu katika luga zaidi ya 130. Katika habari hii, tutajifunza namna gani kanuni hizo zimetumikishwa katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya 2013 ya Kiingereza, na namna kanuni hizo zinafuatwa pia katika luga zingine.

TAFSIRI YENYE KUHESHIMU JINA LA MUNGU

3, 4. (a) Herufi ine za Kiebrania zenye kufanyiza jina la Mungu zinapatikana katika maandishi gani ya zamani? (b) Tafsiri nyingi za Biblia zimefanya nini na jina la Mungu?

3 Jina la Mungu linafanyizwa na herufi ine za Kiebrania zenye kuitwa Tetragramatoni. Tunaweza kupata herufi hizo katika maandishi mengi ya Kiebrania ya zamani, kama vile Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi. Tunaweza pia kupata herufi hizo katika kopi fulani za Septante ya Kigiriki. Kopi hizo zilifanywa kati ya mwaka wa 101 na wa 200 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu na kati ya mwaka wa 1 na wa 100 kisha kuzaliwa kwa Yesu. Watu wengi wanashangaa sana wakati wanaona jina la Mungu linapatikana sana katika maandishi ya zamani.

Watu wengi wanashangaa sana wakati wanaona jina la Mungu linapatikana sana katika maandishi ya zamani

4 Ni wazi kwamba jina la Mungu linapaswa kupatikana katika Biblia. Lakini tafsiri nyingi za Biblia hazitumie jina la Mungu. Kwa mufano, miaka mbili tu kisha kutolewa kwa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, tafsiri mupya ya American Standard Version ilitolewa pia. Tafsiri ya mwaka wa 1901 ilikuwa na jina la Mungu, lakini tafsiri ya 1952 haikuwa na jina hilo. Sababu gani? Kwa sababu watafsiri wa Biblia hiyo waliona kuwa “haifae kabisa” kutumia jina la Mungu. Tafsiri nyingi za Biblia za Kiingereza na za luga zingine zimefanya hivyo pia.

5. Sababu gani ni jambo la maana kutumia jina la Mungu katika Biblia?

5 Je, ni jambo la maana kutafuta kujua ikiwa watafsiri walitumia jina la Mungu ao hapana? Ndiyo! Yehova, Mwenye Aliandikisha Biblia, anapenda watu wajue jina lake. Mutafsiri muzuri anapaswa kujua mambo yenye mwandikaji anapenda, na hilo linapaswa kuongoza maamuzi yake katika kazi ya kutafsiri. Maandiko mengi inaonyesha kwamba jina la Mungu ni la maana na kwamba linapaswa kuheshimiwa. (Kutoka 3:15; Zaburi 83:18; 148:13; Isaya 42:8; 43:10; Yohana 17:6, 26; Matendo 15:14) Pia, Yehova alitumia roho yake ili kuongoza waandikaji wa Biblia watumie jina lake mara nyingi sana katika maandishi ya zamani. (Soma Ezekieli 38:23.) Kwa hiyo, wakati watafsiri wanaondoa jina la Mungu katika tafsiri yao, wanamukosea Mungu heshima.

6. Sababu gani jina la Mungu liliongezwa mara sita katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya 2013?

6 Leo, kuko mambo mengi yenye kuonyesha kwamba tunapaswa kutumia jina la Yehova. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya 2013 inatumia jina la Mungu mara 7216. Ni kusema, jina la Mungu linapatikana katika tafsiri hiyo mara sita zaidi kuliko katika tafsiri ya zamani kwa sababu jina hilo lilipatikana tena mara tano katika Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi vyenye vilipatikana hivi karibuni. * (Soma maelezo ya chini.) Jina hilo lilipatikana katika maandiko haya tano: 1 Samweli 2:25; 6:3; 10:26; 23:14, 16. Kuchunguza tena zaidi maandishi ya zamani ya Biblia yenye kutegemeka kulisaidia kupata andiko la sita; andiko hilo ni Waamuzi 19:18.

7, 8. Jina Yehova linamaanisha nini?

7 Wakristo wa kweli wanaona kuwa ni jambo la lazima kuelewa kabisa maana ya jina la Mungu. Jina lake linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” * (Soma maelezo ya chini.) Zamani, vichapo vyetu vilifasiria maana ya jina la Mungu kwa kutumia andiko la Kutoka 3:14. Andiko hilo linasema hivi: “Nitakuwa Kile Nitakachokuwa.” Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya 1984 ilieleza kwamba Yehova anajifanya kuwa chochote chenye anapenda kuwa ili atimize mambo yenye anapanga kufanya. * (Soma maelezo ya chini.) Lakini tafsiri ya 2013 inaeleza hivi: “Ni kweli kwamba jina la Yehova linaweza kuwa na maana hiyo; hata hivyo, halimaanishe tu kwamba anajifanya kuwa chochote chenye anapenda kuwa. Lakini, linamaanisha pia kwamba anaweza kutokeza jambo fulani kuelekea viumbe wake ili kutimiza kusudi lake.”

8 Yehova anafanya viumbe wake kuwa chochote anapenda. Kwa mufano, alimufanya Noa kuwa mujenzi wa safina, Bezaleli kuwa fundi mwenye uzoefu, Gideoni kuwa mupiganaji vita mukubwa, na mutume Paulo kuwa misionere. Watu wa Mungu wanaona kuwa jina la Mungu ni la maana sana, ndiyo sababu Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya ilitumia jina la Mungu katika tafsiri hiyo.

9. Sababu gani ni jambo la maana sana Tafsiri ya Ulimwengu Mpya itafsiriwe katika luga zingine?

9 Watafsiri wengi sana hawatumie jina la pekee la Mungu katika Biblia zao. Lakini wanatumia jina la cheo “Bwana” ao jina la mungu wa eneo lao. Ndiyo sababu ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza waliona kuwa ni jambo la maana sana watu wa luga zote wakuwe na tafsiri ya Biblia yenye kuheshimu jina la Mungu. (Soma Malaki 3:16.) Mupaka leo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inaendelea kuheshimu jina la Yehova katika luga zaidi ya 130.

TAFSIRI YENYE KUWA WAZI NA YA KWELI KABISA

10, 11. Ni magumu gani watafsiri wamepata wakati wa kutafsiri Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika luga zingine?

10 Watafsiri wamepata magumu fulani wakati wa kutafsiri Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kiingereza katika luga zingine. Kwa mufano, tafsiri ya Kiingereza ilitumia neno la Kiebrania “Sheoli” kwenye Mhubiri 9:10 na katika maandiko mengine. Neno hilo lilipatikana sana katika Biblia zingine za Kiingereza. Lakini, neno hilo halingeweza kutumiwa katika luga nyingi kwa sababu wasomaji wengi wa luga hizo hawajue neno la Kiebrania “Sheol.” Neno hilo halikupatikana katika kamusi zao, na hata wengine walifikiri kwamba Sheoli ilikuwa jina la nafasi fulani. Ndiyo sababu, watafsiri walipewa ruhusa ya kutafsiri neno la Kiebrania “Sheoli” na neno la Kigiriki “Hadesi” kuwa “Kaburi.” Hiyo ni tafsiri ya kweli na inaeleza mambo wazi.

11 Maneno ya Kiebrania na Kigiriki yenye kutafsiriwa “nafsi” ilikuwa vigumu kutafsiriwa katika luga fulani. Katika luga hizo, neno “nafsi” linamaanisha roho ao kitu fulani chenye kutoka katika mwili wa mutu wakati anakufa. Ili kuepuka makosa hayo, watafsiri walipewa ruhusa ya kutafsiri neno “nafsi” kulingana na habari yenye kuzungumuziwa. Maelezo ya maana mbalimbali ya neno “nafsi” inapatikana katika nyongeza ya Les Saintes Écritures—Traduction du monde nouveau—avec notes et références (rbi-8). Mafasirio ya maneno ya Kiebrania na Kigiriki inatiwa katika maelezo ya chini ya tafsiri ya sasa ili kusaidia watu wasome na kuelewa vizuri maandiko ya Biblia.

Wakati wa kazi hiyo, ndugu wa Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya walichunguza maulizo mengi sana ya watafsiri wa Biblia hiyo

12. Ni mabadiliko mengine gani yenye ilifanywa katika tafsiri ya 2013?

12 Maulizo ya watafsiri ilionyesha pia kwamba pengine kulikuwa mambo mengine yenye haikueleweka muzuri katika Biblia. Kwa hiyo, katika Mwezi wa 9, 2007, Baraza Lenye Kuongoza lilikubali Biblia ya Kiingereza irekebishwe ao irudiliwe tena. Wakati wa kazi hiyo, ndugu wa Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mpya walichunguza maulizo mengi sana ya watafsiri wa Biblia hiyo. Maneno ya Kiingereza yenye ilikuwa ya zamani iliondolewa na maneno ya sasa ilitumiwa bila kubadilisha maana ya ujumbe ili Biblia hiyo ikuwe mwepesi zaidi kusoma na kueleweka. Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya zenye zilikuwa zimefanywa hivi karibuni katika luga zingine zilisaidia pia kufanya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kiingereza ikuwe muzuri zaidi.—Methali 27:17.

SHUKRANI KUBWA SANA

13. Ndugu na dada wengi wamesema nini juu ya tafsiri ya 2013?

13 Ndugu na dada wengi walijisikia namna gani kisha kupokea Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa ya Kiingereza? Ndugu na dada wengi sana wametuma barua zao za shukrani kwenye makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova, Brooklyn, New York. Wengi kati yao walijisikia kama dada moja mwenye aliandika hivi: “Biblia ni kama sanduku lenye kujaa majiwe ya bei kali. Kusoma neno la Yehova waziwazi kwa kutumia tafsiri ya 2013 kunaweza kulinganishwa na kuchunguza kila jiwe, kufurahia sana umbo lake, namna linangaa, kufurahia sana rangi yake, na uzuri wake. Biblia hiyo imetumia maneno mepesi; hilo linanisaidia nimujue muzuri zaidi Yehova, mwenye kuwa kama baba mwenye ananikumbatia wakati ananisomea maneno mazuri sana.”

14, 15. Watu wanasema nini juu ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika luga zingine?

14 Watu wenye kuzungumuza luga zingine wameonyesha pia shukrani zao wakati walipata Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Mwanaume moja mwenye kuzeeka wa huko Sofia, Bulgaria, anasema hivi juu ya tafsiri ya Kibulgaria: “Nimesoma Biblia kwa miaka mingi, lakini sijasoma hata siku moja tafsiri yenye kuwa mwepesi kueleweka na yenye kugusa moyo wangu kama hii.” Vilevile, dada moja wa Albania aliandika hivi: “Ninaelewa muzuri sana Neno la Mungu katika Kialbania! Ni pendeleo kubwa sana kuona namna Yehova anazungumuza na sisi katika luga yetu!”

15 Katika inchi nyingi, haiko mwepesi kupata Biblia kwa sababu zinauzishwa kwa bei kali. Kupata Biblia ni baraka kubwa sana! Ndugu na dada wa Rwanda walisema kwamba “kwa muda murefu, wanafunzi wengi wa Biblia hawakufanya maendeleo kwa sababu hawakuwa na Biblia. Hawakuwa na uwezo wa kuuza Biblia za dini za eneo lao. Na mara nyingi hawakuelewa muzuri maana ya maandiko fulani, na hilo liliwazuia kufanya maendeleo.” Wakati Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ilitolewa katika Kinyarwanda, familia moja yenye kuwa na vijana ine iliandika hivi: “Tunamushukuru sana Yehova na mutumwa mwaminifu na mwenye busara kwa kututolea Biblia hii. Tuko masikini sana na hatukuwa na feza za kuuzia kila mutu Biblia katika familia yetu. Lakini sasa kila mutu amepata Biblia yake. Ili kuonyesha shukrani yetu kwa Yehova, tunasoma Biblia kila siku katika familia yetu.”

16, 17. (a) Yehova anapenda watu wake wafanye nini? (b) Tunapaswa kuendelea kufanya nini?

16 Wakati unaokuja, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa itatafsiriwa katika luga nyingi zaidi. Shetani anajaribu kuzuia kazi hiyo, lakini tunajua kwamba Yehova anapenda watu wake wote wasikilize waziwazi na kuelewa maneno yake wakati anazungumuza nao. (Soma Isaya 30:21.) Hivi karibuni, ‘dunia hakika itajawa na kumujua Yehova kama vile maji yanafunika bahari.’—Isaya 11:9.

17 Tuendelee basi kutumikisha kila zawadi yenye Yehova anatutolea, na kutumikisha pia tafsiri hiyo yenye kuheshimu jina lake. Umuruhusu azungumuze na wewe kila siku kupitia Neno lake. Anaweza kusikiliza sala zetu zote kwa uangalifu. Mazungumuzo hayo itatusaidia kumujua Yehova muzuri zaidi, na tutaendelea kumupenda sana.—Yohana 17:3.

“Ni pendeleo kubwa sana kuona namna Yehova anazungumuza na sisi katika luga yetu!”

^ fu. 2 Soma Nyongeza A1 katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya sasa ya Kiingereza; soma pia habari “Jinsi ya Kuchagua Tafsiri Nzuri ya Biblia,” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2008.

^ fu. 6 Vitabu vya kukunjwa vya Bahari ya Chumvi ni vya miaka 1000 mbele ya maandishi ya Kiebrania ya Wamasora.

^ fu. 7 Vitabu fulani vinatoa mafasirio hayo, lakini watu fulani wenye elimu ya Biblia hawakubali jambo hilo.

^ fu. 7 Soma Nyongeza 1A yenye kichwa “Le nom divin dans les Écritures hébraïques,” (Jina la Mungu katika Maandishi ya Kiebrania), katika Les Saintes Écritures—Traduction du monde nouveau—avec notes et références (rbi-8), ukurasa wa 1676