Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umushukuru Yehova kwa Ukarimu Wake

Umushukuru Yehova kwa Ukarimu Wake

YEHOVA ni Mungu mwenye kuonyesha ukarimu. (Yakobo 1:​17) Kila kitu chenye aliumba kinaonyesha kwamba yeye ni mukarimu. Alitia nyota nyingi sana katika anga, na aliumba miti na majani mazuri sana katika dunia.—Zaburi 65:12, 13; 147:7, 8; 148:3, 4.

Mwandikaji wa Zaburi ya 104 alimushukuru sana Yehova kwa sababu ya vitu vyote vyenye ameumba, ndiyo sababu aliandika wimbo ili kumusifu. Wakati unasoma zaburi hiyo, unamushukuru Yehova kama mwandikaji huyo? Alisema hivi: ‘Nitamuimbia Yehova katika maisha yangu yote; nitamupigia Mungu wangu muziki maadamu nipo [kadiri nitaendelea kuishi].’ (Zaburi 104:33) Unapenda kufanya hivyo pia?

MUFANO MUZURI ZAIDI WA UKARIMU

Yehova anapenda tuige ukarimu wake. Na anatutolea sababu nzuri za kuonyesha ukarimu. Alitumia roho yake ili kumuongoza mutume Paulo aandike hivi: ‘Uwapatie maagizo wale walio matajiri katika mufumo wa mambo wa sasa wasitake makubwa, na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika, bali katika Mungu, ambaye anatupatia sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie. [Uwaambie] wafanye mema, wakuwe matajiri katika matendo mazuri, wakuwe wakarimu, tayari kushiriki, wakijiwekea wenyewe kwa usalama hazina ya musingi muzuri kwa ajili ya wakati ujao, ili waushike imara uzima ulio wa kweli.’—1 Timotheo 6:17-19.

Katika barua yake ya pili kwa Wakorintho, mutume Paulo alieleza nia yenye tunapaswa kuwa nayo wakati tunatolea wengine. Alisema hivi: ‘Kila mumoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu anapenda mutoaji muchangamufu.’ (2 Wakorintho 9:7) Wakati tunaonyesha ukarimu, ni nani mwenye anapata faida? Mutume Paulo alisema kwamba tunasaidia wengine kwa kuwatolea mambo yenye wako nayo lazima, lakini pia tunajisaidia sisi wenyewe kwa sababu Yehova atatubariki.—2 Wakorintho 9:11-14.

Mutume Paulo alizungumuzia mufano muzuri zaidi wa ukarimu wa Mungu wakati alisema hivi: “Shukrani kwa ajili ya zawadi yake ya bure isiyoelezeka.” (2 Wakorintho 9:15) ‘Zawadi ya bure’ ya Yehova ni mambo yote mazuri yenye anatutolea kupitia Yesu Kristo. Hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kuonyesha kwamba zawadi hiyo ni ya maana sana.

Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani kwa ajili ya mambo yote yenye Yehova na Yesu wametufanyia na yenye watatufanyia? Njia moja ni kuwa wakarimu wakati tunatoa wakati, nguvu, na vitu vyetu vya kimwili kwa ajili ya ibada ya Yehova na kusaidia wengine wajifunze kumujua. Tunaweza kufanya hivyo iwe tuko na vitu vingi ao vidogo.—1 Mambo ya Nyakati 22:14; 29:3-5; Luka 21:1-4.

Telefone: 0998189791 ao 0815551000