Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Atakutegemeza

Yehova Atakutegemeza

‘Yehova atamutegemeza katika kitanda chake cha ugonjwa.’—ZABURI 41:3.

NYIMBO: 23, 138

1, 2. Mungu alifanya nini zamani, na watu fulani wanaweza kujiuliza ulizo gani wakati wanagonjwa?

IKIWA umekwisha kugonjwa sana wakati fulani, pengine ulijiuliza hivi: ‘Nitapona kabisa?’ Ao pengine mutu wa familia ao rafiki yako ni mugonjwa na unajiuliza ikiwa atapona. Ni jambo la kawaida kupenda wewe na watu wenye unapenda wakuwe na afya nzuri. Tunasoma katika Biblia habari za watu fulani wenye waligonjwa na walipenda kujua ikiwa watapona. Kwa mufano, Mufalme Ahazia, mwana wa Ahabu na Yezebeli, alijiuliza ikiwa vidonda vyake vitapona. Na kisha, Mufalme Ben-hadadi wa Siria alikuwa mugonjwa na aliuliza ikiwa atapona.—2 Wafalme 1:2; 8:7, 8.

2 Biblia inasema pia kwamba zamani, wakati fulani Yehova aliponyesha watu kwa njia ya muujiza na alitumia hata manabii wake ili kufufua watu fulani wenye walikuwa wamekufa. (1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:17-20, 32-35) Leo, wagonjwa fulani wanaweza kujiuliza ikiwa Mungu atafanya jambo fulani ili kuwaponyesha.

3-5. Yehova na Yesu wanaweza kufanya nini, na tutachunguza maulizo gani?

3 Yehova iko na uwezo juu ya afya ya watu. Alipiga watu fulani kwa ugonjwa. Kwa mufano, wakati wa Abrahamu alimupiga Farao kwa ugonjwa, na kisha Miriamu dada ya Musa. (Mwanzo 12:17; Hesabu 12:9, 10; 2 Samweli 24:15) Wakati Waisraeli walikosa uaminifu kwake, aliwapatia malipizi kwa ‘ugonjwa ao pigo.’ (Kumbukumbu la Torati 28:58-61) Nyakati nyingine, Yehova alilinda watu wake wasipatwe na magonjwa. (Kutoka 23:25; Kumbukumbu la Torati 7:15) Aliponyesha pia watu fulani. Kwa mufano, wakati Ayubu alikuwa mugonjwa na alipenda akufe, Yehova alimuponyesha.—Ayubu 2:7; 3:11-13; 42:10, 16.

4 Tuko hakika kwamba Yehova iko na uwezo wa kuponyesha wagonjwa. Yesu pia anaweza kuponyesha wagonjwa. Wakati alikuwa duniani, aliponyesha watu wenye walikuwa na ugonjwa kama vile, ukoma ao kifafa. Aliponyesha vipofu na watu wenye kupooza. (Soma Mathayo 4:23, 24; Yohana 9:1-7) Miujiza hiyo inatusaidia tungojee kwa hamu mambo mazuri sana yenye Yesu atafanya katika dunia mupya. Wakati huo, “hakuna mukaaji atakayesema: ‘Mimi ni mugonjwa.’”—Isaya 33:24.

5 Lakini, ikiwa tunagonjwa sana, tunaweza kufikiri kwamba Yehova ao Yesu atatuponyesha kwa njia ya muujiza leo? Na tunapaswa kufikiria mambo gani wakati tunachagua matunzo?

UMUTEGEMEE YEHOVA WAKATI UNAGONJWA

6. Biblia inasema nini juu ya miujiza yenye Wakristo walifanya wakati wa mitume?

6 Wakati wa mitume, Yehova alitia Wakristo mafuta kupitia roho yake takatifu na alipatia wamoja kati yao uwezo wa kufanya miujiza. (Matendo 3:2-7; 9:36-42) Kwa mufano, walikuwa na uwezo wa kuponyesha watu na kusema luga mbalimbali. (1 Wakorintho 12:4-11) Lakini, kama vile tu Biblia ilisema, miujiza hiyo ilifikia mwisho. (1 Wakorintho 13:8) Kwa hiyo, leo hatupaswe kufikiri kwamba Mungu atafanya muujiza ili kutuponyesha sisi na watu wenye tunapenda.

Yehova anajua muzuri kabisa mateso yenye watumishi wake wanapambana nayo, na hasahau uaminifu wao

7. Namna gani Zaburi 41:3 inaweza kututia moyo?

7 Lakini ikiwa uko mugonjwa, Yehova atakufariji na kukutegemeza, kama vile aliwafanyia watumishi wake wa zamani. Mufalme Daudi aliandika hivi: ‘Mwenye furaha ni mutu yeyote anayetenda kwa kumufikiria mutu wa hali ya chini; katika siku ya musiba Yehova atamuokoa. Yehova mwenyewe atamulinda na kumuhifazi [kumuchunga] hai.’ (Zaburi 41:1, 2) Kwa kweli, Daudi hakumaanisha kwamba mutu muzuri mwenye alikuwa anaishi wakati ule na mwenye alimufikiria mutu wa hali chini hangekufa hata kidogo. Kwa hiyo, namna gani Yehova angesaidia mutu huyo muzuri? Daudi alisema hivi: ‘Yehova mwenyewe atamutegemeza katika kitanda cha ugonjwa; kitanda chake chote hakika utakibadilisha wakati wa ugonjwa wake.’ (Zaburi 41:3) Yehova anajua muzuri kabisa mateso yenye watumishi wake wanapambana nayo, na hawasahau. Anaweza kuwapatia nguvu na hekima. Pia, wakati Yehova aliumba mwanadamu, alimupatia mwili wenye kuwa na uwezo wa kujiponyesha.

8. Kulingana na Zaburi 41:4, Daudi alimuomba Yehova nini wakati alikuwa mugonjwa sana?

8 Katika Zaburi ya 41, Daudi anazungumuzia pia wakati aligonjwa sana na alijisikia kuwa muzaifu na mwenye kuhangaika. Pengine wakati huo, Absalomu, mutoto wake, alikuwa anajaribu kuwa mufalme pa nafasi yake. Daudi alikuwa mugonjwa sana na hangeweza kumuzuia Absalomu. Alijua vizuri kwamba familia yake ilipatwa na magumu hayo kwa sababu ya zambi yake na Bath-sheba. (2 Samweli 12:7-14) Kwa hiyo, alifanya nini? Alisali hivi: ‘Ee Yehova, nionyeshe kibali. Uiponyeshe nafsi yangu [uniponyeshe], kwa maana nimekutendea zambi.’ (Zaburi 41:4) Daudi alijua kwamba Yehova alikuwa amesamehe zambi yake; kwa hiyo, wakati alikuwa mugonjwa, alimutegemea. Lakini, Daudi alikuwa anafikiri kwamba Yehova atamuponyesha kwa njia ya muujiza?

9. (a) Yehova alimufanyia Mufalme Hezekia jambo gani? (b) Daudi alitumaini kwamba Yehova atamufanyia nini?

9 Ni kweli kwamba wakati fulani Mungu aliona kuwa ni muzuri aponyeshe watu fulani. Kwa mufano, wakati Mufalme Hezekia alikuwa mugonjwa sana na kuwa karibu kufa, Yehova alimuponyesha. Kisha hapo, Hezekia aliishi tena miaka 15. (2 Wafalme 20:1-6) Lakini Daudi hakufikiri kwamba ataponyeshwa kwa njia ya muujiza. Hata hivyo, alikuwa anafikiri kwamba Mungu angemusaidia kama vile anasaidia kila mutu mwenye kuhangaikia mutu wa hali ya chini. Daudi alikuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova, ndiyo sababu wakati alikuwa mugonjwa, alimuomba Yehova amufariji na kumuhangaikia. Aliomba pia apone na ajisikie muzuri. Sisi pia tunaweza kumuomba Yehova atutendee hivyo.—Zaburi 103:3.

10. Trofimo na Epafrodito walipatwa na nini, na jambo hilo linatufundisha nini?

10 Wakati wa mitume, mutume Paulo na wengine waliponyesha wagonjwa kwa njia ya miujiza, lakini haiko Wakristo wote ndio waliponyeshwa kwa njia hiyo. (Soma Matendo 14:8-10.) Mutume Paulo alimuponyesha baba ya Publio mwenye alikuwa na homa na ugonjwa fulani wa kuambukiza. Mutume Paulo ‘alisali, akaweka mikono yake juu yake akamuponyesha.’ (Matendo 28:8) Lakini Paulo hakuponyesha watu wote wenye alikuwa anajua. Trofimo, moja kati ya marafiki wa Paulo, alisafiri pamoja naye katika safari yake ya umisionere. (Matendo 20:3-5, 22; 21:29) Wakati Trofimo aligonjwa, mutume Paulo hakumuponyesha. Kwa hiyo, Trofimo hakuendelea kusafiri pamoja na mutume Paulo, lakini alibakia Mileto ili apate matunzo. (2 Timotheo 4:20) Epafrodito, rafiki mwengine wa mutume Paulo, aligonjwa sana na kuwa karibu kufa. Lakini Biblia haiseme kwamba mutume Paulo alimuponyesha.—Wafilipi 2:25-27, 30.

UTAKUBALI MASHAURI YA NANI?

11, 12. Tunajua mambo gani juu ya Luka, na inawezekana alimusaidia mutume Paulo namna gani?

11 Luka alikuwa muganga, na alisafiri pamoja na mutume Paulo. (Matendo 16:10-12; 20:5, 6; Wakolosai 4:14) Pengine alisaidia mutume Paulo na wengine wakati waligonjwa katika safari zao za umisionere. (Wagalatia 4:13) Kama vile tu Yesu alisema, “wale wanaougua [wanaogonjwa]” ndio wako na lazima ya muganga.—Luka 5:31.

Tunapaswa kuwa waangalifu wakati mutu fulani anatupatia mashauri juu ya mambo ya matunzo

12 Luka hakukuwa tu mutu mwenye alipenda tu kutolea wengine mashauri juu ya mambo ya matunzo. Alizoezwa katika mambo ya kiganga. Biblia haiseme wakati ao nafasi kwenye Luka alipata mazoezi hayo. Lakini inasema kwamba mutume Paulo aliwatumia Wakristo Wakolosai salamu za Luka. Kwa hiyo, inawezekana Luka alijifunza mambo ya kiganga kwenye masomo fulani katika Laodikia, muji wenye ulikuwa karibu na Kolosai. Pia, wakati Luka aliandika Injili yake na kitabu cha Matendo ya Mitume, alitumia maneno fulani ya pekee yenye kutumiwa katika mambo ya matunzo. Kwa sababu alikuwa muganga, aliandika habari zenye kuzungumuzia namna Yesu aliponyesha watu.

13. Tunapaswa kukumbuka nini mbele ya kutoa ao kukubali mashauri fulani juu ya mambo ya matunzo?

13 Leo, hakuna ndugu ao dada mwenye anaweza kufanya miujiza na kutuponyesha. Lakini, kwa sababu wanapenda kutusaidia, wamoja kati yao wanaweza kututolea mashauri hata wakati hatuna lazima ya mashauri hayo. Ni kweli kwamba mashauri fulani haina ubaya wowote. Kwa mufano, mutume Paulo alimushauria Timotheo atumie divai kidogo. Timotheo alikuwa na magonjwa ya tumbo, pengine kwa sababu alikunywa maji yenye haikuwa safi. * (Soma maelezo ya chini.) (Soma 1 Timotheo 5:23.) Lakini tunapaswa kuwa waangalifu. Ndugu ao dada fulani anaweza kutusadikisha kwamba tutumie dawa ao majani fulani, ao tukule ao tusikule chakula fulani. Anaweza kutuambia kwamba mutu fulani katika familia yao alikuwa na magonjwa kama yetu, na kwamba mambo hayo ilimusaidia. Lakini, hilo halimaanishe kwamba mambo hayo itatusaidia sisi pia. Tunapaswa kukumbuka kwamba hata kama watu wengi wanatumia dawa ao aina fulani ya matunzo, pengine inaweza kuleta tu matokeo mabaya.—Soma Methali 27:12.

UTUMIE AKILI NZURI

14, 15. (a) Tunapaswa kuepuka watu wa namna gani? (b) Methali 14:15 inaweza kutufundisha nini?

14 Sisi wote tunapenda kuwa na afya njema ili tuendelee kumutumikia Yehova kwa bidii. Lakini, hatuwezi kuepuka magonjwa yote kwa sababu hatukamilike. Wakati tunagonjwa, kunaweza kuwa aina mbalimbali ya matunzo, lakini tuko na haki ya kuamua matunzo yenye tutakubali. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu na mashirika fulani ya mambo ya matunzo wanasema kwamba wamepata dawa fulani yenye itatunza magonjwa yetu yote. Wanasema hivyo kwa sababu tu wanapenda kupata feza nyingi. Wanaweza kusema kwamba dawa hiyo imekwisha kuponyesha watu wengi. Na ikiwa tunagonjwa, tunaweza kuwa tayari kutumia dawa yoyote yenye inaweza kutusaidia tupone na tuendelee kuishi. Lakini tunapaswa kukumbuka shauri hili la Neno la Mungu: ‘Mutu asiye na uzoefu anaamini kila neno, lakini mutu mwerevu anazifikiria hatua zake.’—Methali 14:15.

Tunapaswa kutumia akili nzuri na kuwa waangalifu juu ya mashauri yenye tunakubali

15 Ikiwa tuko werevu, ao wenye hekima, tutakuwa waangalifu juu ya mashauri yenye tunakubali, zaidi sana ikiwa mutu mwenye kututolea mashauri hayo hana uzoefu wowote. Tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Mutu huyu anasema kwamba dawa, majani, ao chakula fulani kiliponyesha watu, lakini, niko hakika kwamba walipona kabisa? Hata kama dawa hiyo imeponyesha wengine, ni nini inaonyesha kwamba itaniponyesha pia? Ninapaswa kutafuta habari zaidi na kuzungumuza na watu fulani wenye kuwa na uzoefu wa kutunza magonjwa yangu?’—Kumbukumbu la Torati 17:6.

16. Tunapaswa kufikiria nini wakati tunachukua maamuzi juu ya mambo ya matunzo?

16 Wakati tunaamua vipimo vya afya vyenye tutafanya ao matunzo yenye tutakubali, tunapaswa kuwa na “utimamu wa akili,” ao kutumia akili nzuri. (Tito 2:12) Ni jambo la maana sana kufanya hivyo ikiwa vipimo ao matunzo fulani inaonekana kuwa haiko ya kawaida. Je, muganga mwenye tunatembelea anaweza kutufasiria zaidi namna kipimo ao matunzo fulani inafanyika? Tunaelewa muzuri kabisa mafasirio yake? Waganga wengi wanakubali kwamba kipimo ao matunzo hayo inaweza kuponyesha watu? (Methali 22:29) Pengine mutu fulani anatuambia kwamba dawa mupya imevumbuliwa katika eneo fulani, na kwamba waganga wengi hawajapata habari juu ya dawa hiyo. Lakini, kuko jambo fulani lenye kuhakikisha kwamba dawa hiyo imepatikana? Watu fulani wanaweza hata kutushauria tutumie dawa zenye kutengenezwa na vitu vyenye havijulikane muzuri ao yenye kuponyesha kwa njia yenye haieleweke wazi. Hilo linaweza kutuletea hatari kubwa sana. Kumbuka kwamba Mungu anatuonya tuepuke kutumia nguvu zenye haziko za kawaida, ni kusema, nguvu za uchawi.—Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Isaya 1:13.

“AFYA NJEMA KWENU!”

17. Tunatamani jambo gani la kawaida?

17 Baraza lenye kuongoza la wakati wa mitume lilitumia ndugu na dada katika makutaniko barua ili kuwajulisha mambo fulani yenye walipaswa kuepuka. Baraza hilo lilimalizia barua hiyo kwa kuandika hivi: ‘Mukijiepusha kwa uangalifu na mambo haya, mutafanikiwa. Afya njema kwenu!’ (Matendo 15:29) Hata kama maneno ya mwisho-mwisho ya barua hiyo ilimaanisha pia kuagana na ndugu na dada, inatukumbusha kwamba ni jambo la kawaida kupenda kuwa na afya njema.

Tunapenda kuwa na afya njema, lakini tunapaswa kukaza akili yetu juu ya kazi ya Yehova(Picha hizi zinapatana na fungu la 17)

18, 19. Tunangojea nini kwa hamu katika dunia mupya?

18 Hatuwezi kuepuka magonjwa yote kwa sababu hatukamilike. Na wakati tunagonjwa, hatufikiri kwamba Yehova atatuponyesha kwa njia ya muujiza. Lakini tunaweza kungojea kwa hamu wakati unaokuja, wakati Mungu atatuponyesha kabisa-kabisa. Kwenye Ufunuo 22:1, 2, mutume Yohana alizungumuzia “maji ya uzima” na “miti ya uzima” yenye itaponyesha kila mutu. Mambo hayo haimaanishe dawa fulani ya majani yenye tunaweza kutumia leo ao katika dunia mupya ili ituponyeshe. Lakini, inamaanisha mipango yote yenye Yehova na Yesu watafanya ili tuishi milele.—Isaya 35:5, 6.

19 Tunangojea kwa hamu wakati huo. Lakini kwa sasa, tuko hakika kwamba Yehova anapenda kila mumoja wetu na kwamba anaelewa namna tunajisikia wakati tunagonjwa. Kama vile Daudi, tuko hakika kwamba ikiwa tunagonjwa, Yehova hatatuacha. Sikuzote, ataendelea kuhangaikia wale wote wenye kuwa waaminifu kwake.—Zaburi 41:12.

^ fu. 13 kitabu The Origins and Ancient History of Wine kinasema kwamba wanasayansi wamevumbua kwamba mikrobe ya homa ya matumbo (typhoïde) na mikrobe mingine mingi yenye kuwa hatari inakufa haraka wakati inatiwa katika divai.