Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utumie Muzuri Uwezo wa Ulimi Wako

Utumie Muzuri Uwezo wa Ulimi Wako

Maneno ya kinywa changu. . . na yakuwe yenye kupendeza mbele zako, Ee Yehova.’—ZABURI 19:14.

NYIMBO: 82, 77

1, 2. Sababu gani Biblia inalinganisha uwezo wetu wa kusema na moto?

KATIKA mwaka wa 1871, pori ya Wisconsin, États-Unis, ilianza kuwaka moto. Moto huo ulienea mbio sana na kulunguza kabisa miti mingi sana. Watu zaidi ya 1200 walikufa. Kwa kweli, huo ndio moto wenye uliua watu wengi sana katika inchi hiyo. Pengine treni zenye zilikuwa zinapita katika pori hiyo zilitokeza sehemu ndogo-ndogo sana za moto na sehemu hizo ziliwasha moto huo mukubwa sana. Tukio hilo linatukumbusha andiko moja la Biblia lenye kusema hivi: ‘Mutazame! Ni moto mudogo tu unaohitajika ili kuuwasha mwitu [pori] mukubwa!’ (Yakobo 3:5) Sababu gani mwandikaji wa Biblia Yakobo alisema maneno hayo?

2 Anasema hivi: “Ulimi [pia] ni moto.” (Yakobo 3:6) “Ulimi” unamaanisha uwezo wetu wa kusema. Na kama moto, mambo yenye tunasema inaweza kuleta matokeo mabaya sana. Maneno yetu inaweza kuwachochea sana wengine. Biblia inasema pia kwamba maneno yetu inaweza kuletea wengine kifo ao uzima. (Methali 18:21) Lakini, hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kuacha kusema kwa sababu tunaweza kusema jambo fulani la mubaya? Hapana. Hatuwezi kuacha kutumia moto kwa sababu tu unaweza kutulunguza. Lakini, tunapaswa kuutumia kwa uangalifu. Kwa mufano, tunaweza kutumia moto ili kupika chakula, kuota, na kupata mwangaza. Vilevile, tukitumia maneno yetu kwa uangalifu, tunaweza kutumia uwezo wetu wa kusema ili kumuletea Yehova heshima na kuletea wengine faida.—Zaburi 19:14.

3. Ni mambo gani tatu yenye itatusaidia tutie wengine moyo wakati tunasema?

3 Yehova alitupatia uwezo wa kuambia wengine mawazo yetu na namna tunajisikia; tunafanya hivyo kwa kusema ao kwa kutumia luga ya ishara. Kwa hiyo, namna gani tunaweza kutumia zawadi hiyo nzuri zaidi ili kutia wengine moyo? (Soma Yakobo 3:9, 10.) Tunapaswa kujua wakati wa kusema, mambo ya kusema, na namna ya kusema.

NI WAKATI GANI TUNAPASWA KUSEMA?

4. Ni wakati gani tunapaswa kubakia kimya?

4 Wakati fulani ni muzuri kubakia kimya. Biblia inasema kwamba kuna “wakati wa kukaa [kubakia] kimya.” (Mhubiri 3:7) Kwa mufano, wakati wengine wanasema, tunabakia kimya ili kuonyesha kwamba tunawaheshimia. (Ayubu 6:24) Pia, tunaepuka kusema mambo fulani ya siri na yenye watu wengine hawapaswe kujua. (Methali 20:19) Na wakati mutu fulani anatukasirisha, ni jambo la hekima ikiwa tunajikaza kunyamaza.—Zaburi 4:4.

5. Namna gani tunaweza kumuonyesha Yehova kwamba tuko wenye shukrani kwa sababu ya uwezo wa kusema wenye ametupatia?

5 Lakini, wakati fulani ni muzuri kusema. (Mhubiri 3:7) Kuna wakati wa kumusifu Yehova, kutia wengine moyo, kusema namna tunajisikia, na kuambia wengine mambo yenye tuko nayo lazima. (Zaburi 51:15) Ikiwa tunafanya hivyo, tunaonyesha kwamba tuko wenye shukrani kwa Yehova kwa sababu ametupatia zawadi hiyo. Ni kweli kwamba, wakati rafiki yetu anatupatia zawadi nzuri sana, tunajikaza kuitumia kwa njia ya muzuri zaidi.

6. Sababu gani ni jambo la maana tuchague wakati wenye kufaa ili kusema?

6 Sababu gani ni jambo la maana tuchague wakati wenye kufaa ili kusema? Andiko la Methali 25:11 linasema hivi: ‘Neno linalosemwa wakati unaofaa ni kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye chombo cha feza kilichopambwa.’ Matunda ya mutofaa (pommes) ya zahabu ni yenye kupendeza sana, lakini inaweza kupendeza zaidi wakati inatiwa kwenye chombo cha feza. Vilevile, tunaweza kuwa na jambo fulani nzuri la kumuambia mutu fulani. Lakini, ikiwa tunachagua wakati wenye kufaa ili kusema, tunaweza kumusaidia zaidi. Namna gani tunaweza kufanya hivyo?

7, 8. Namna gani ndugu na dada zetu wa Japani waliiga mufano wa Yesu?

7 Ikiwa hatuchague wakati wenye kufaa, watu wanaweza kukosa kuelewa mambo yenye tunasema ao kuikubali. (Soma Methali 15:23.) Kwa mufano, katika Mwezi wa 3, 2011, tetemeko la inchi na tsunami viliharibu miji yenye kupatikana mashariki katika inchi ya Japani. Watu zaidi ya 15000 walikufa. Mashahidi wengi wa Yehova walipoteza watu wa familia na marafiki; lakini, walikuwa tayari kutumia Biblia ili kusaidia watu wengi wenye walipatwa pia na mugumu hayo. Lakini, Mashahidi wa Yehova walijua kwamba wengi kati ya watu hao wako katika dini ya Wabuda na hawajue mambo mengi juu ya Biblia. Kwa hiyo, kuliko kuzungumuza nao wakati huo juu ya ufufuo, ndugu na dada waliwatia moyo na kuwaelezea sababu gani watu wazuri wanapatwa na mambo mabaya kama hayo.

8 Ndugu na dada hao walimuiga Yesu. Alijua wakati wa kunyamaza na wakati wa kusema. (Yohana 18:33-37; 19:8-11) Pia, alingojea wakati wenye kufaa ili kufundisha wanafunzi wake mambo fulani. (Yohana 16:12) Ndugu na dada wa inchi ya Japani walingojea wakati wenye kufaa ili kuzungumuza na watu juu ya ufufuo. Miaka mbili na nusu kisha tsunami, walitolea watu trakte yenye kichwa Watu Waliokufa, Wanaweza Kweli Kuishi Tena? Watu wengi walikubali trakte hiyo na habari yenye walisoma katika trakte hiyo iliwafariji. Sisi pia, tunapaswa kufikiria desturi na mambo yenye watu wa eneo letu wanaamini ili tuweze kujua wakati wenye kufaa ili kuzungumuza nao.

Tunapaswa kuonyesha uvumilivu na kutafuta wakati wengine wako tayari kutusikiliza

9. Ni katika hali gani zingine tunapaswa kungojea wakati wenye kufaa ili kusema?

9 Ni katika hali gani zingine tunapaswa kungojea wakati wenye kufaa ili kusema? Pengine mutu fulani anatuambia jambo fulani lenye kutukwaza. Kuliko kumujibu mara moja ao kusema jambo fulani bila kufikiri, ni jambo la hekima kubakia kimya na kujiuliza hivi: ‘Alipanga kuniambia mambo hayo mabaya? Je, ninapaswa kabisa kuzungumuza naye juu ya jambo hilo?’ Inaweza kuwa muzuri kunyamaza. Lakini, ikiwa tunaona kwamba ni muzuri kuzungumuza naye, tunapaswa kungojea tutulie kwanza. (Soma Methali 15:28.) Ao pengine tunapenda kuwatia moyo watu wa jamaa yetu wenye hawako Mashahidi wajifunze kumujua Yehova. Tunapaswa kuonyesha uvumilivu, kufikiria kwa uangalifu mambo yenye tutawaambia, na kutafuta wakati wenye watakuwa tayari kutusikiliza.

TUNAPASWA KUSEMA NINI?

10. (a) Sababu gani tunapaswa kuchagua kwa uangalifu maneno yetu? (b) Tunapaswa kuepuka maneno gani?

10 Maneno yetu inaweza kuumiza wengine ao kuwatia moyo. (Soma Methali 12:18.) Katika ulimwengu huu wa Shetani, watu wengi wanatumia “maneno makali” yenye kuwa kama “mishale” ao “upanga,” kwa sababu wanataka kuumiza wengine na kuwakasirisha. (Zaburi 64:3) Wengi wanajifunza maneno hayo katika filme na vipindi vya televizyo vyenye wanaangalia. Lakini Wakristo wanapaswa kuepuka kusema maneno makali na yenye kukosa upole, hata kama wanapenda tu kuchekesha wengine. Ni muzuri kuchekesha wengine, kwa sababu hilo linaweza kuwafanya wafurahie sana mambo yenye tunasema. Lakini tunapaswa kuepuka kabisa kutumia maneno makali ya kuchambua, ni kusema, maneno ya matusi ao ya kushushia wengine heshima, ili kuchekesha tu wengine. Biblia inashauria Wakristo waepuke kutumia “matukano.” Inasema tena hivi: ‘Neno lililooza na lisitoke kinywani mwenu, bali neno lolote ambalo ni njema kwa ajili ya kujenga kulingana na uhitaji, ili liwape wasikiaji lile linalofaa.’—Waefeso 4:29, 31.

11. Ni nini inaweza kutusaidia tuchague maneno yenye kufaa?

11 Yesu alifundisha kwamba “kinywa kinasema kutokana na mambo yaliyojaa katika moyo.” (Mathayo 12:34) Hilo linamaanisha kwamba mambo yenye tunasema inaweza kuonyesha kabisa namna tunajisikia. Kwa hiyo, ikiwa tunapenda wengine na kuwahangaikia kabisa, tutachagua maneno yenye kufaa wakati tunazungumuza nao. Mambo yenye tutawaambia itakuwa mazuri na yenye kutia moyo.

12. Ni jambo gani lingine lenye litatusaidia tuchague maneno yenye kufaa?

12 Inaomba kujikaza sana ili kupata maneno yenye kufaa. Mufalme Sulemani alikuwa na hekima, lakini “alitafakari [alifikiri sana] na kutafuta kwa bidii,” ili aandike maneno yenye kufaa na yenye kupendeza. (Mhubiri 12:9, 10) Ni nini inaweza kutusaidia tujue mambo ya kusema? Biblia na vichapo vyetu vinaweza kutusaidia tujue njia ya muzuri ya kuzungumuza na wengine. Tunaweza kujifunza maana ya maneno yenye hatuelewe. Tunaweza pia kujifunza mufano wa Yesu ili tujue kusema kwa njia yenye itasaidia wengine. Alijua kabisa mambo ya kusema kwa sababu Yehova alimufundisha namna ya kujibu kwa maneno yenye kufaa mutu mwenye kuchoka. (Isaya 50:4) Ni jambo la maana pia kufikiria matokeo ya maneno yetu juu ya wengine. (Yakobo 1:19) Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Ikiwa ninatumia maneno haya, mutu ataelewa kabisa mambo yenye ninapenda kumuambia? Atajisikia namna gani?’

13. Sababu gani tunapaswa kusema kwa njia yenye kueleweka muzuri?

13 Zamani, Waisraeli walitumia sauti za tarumbeta ili kutoa ujumbe fulani. Sauti moja ilijulisha watu kwamba wanapaswa kukusanyika pamoja. Sauti ingine yenye kuwa tofauti ilijulisha maaskari kwamba wanapaswa kujitayarisha ili kupigana vita. Ufikirie jambo lenye lingewapata maaskari ikiwa sauti ya tarumbeta haikueleweka muzuri! Biblia inalinganisha sauti ya tarumbeta yenye kueleweka muzuri na maneno yenye kuwa mepesi kueleweka. Ikiwa hatufasirie muzuri mambo fulani, watu wanaweza kuvurugika ao kuamini mambo yenye haiko ya kweli. Tunapenda watu waelewe muzuri mambo yenye tunasema, lakini tunapaswa kuwa waangalifu ili tusitumie maneno yenye kukosa adabu ao yenye kushushia wengine heshima.—Soma 1 Wakorintho 14:8, 9.

14. Ni mufano gani wenye kuonyesha kwamba Yesu alisema kwa njia yenye kuwa mwepesi kueleweka?

14 Kitabu cha Mathayo sura ya 5 mupaka 7 kinaonyesha namna Yesu alichagua maneno yenye kuwa mepesi kueleweka. Huo ni mufano muzuri sana wa kuiga. Katika hotuba yenye alitoa, hakujaribu kushangaza watu kwa kutumia maneno yenye kuwa magumu kueleweka ao yenye haifae. Pia, hakutumia maneno yenye ingewaumiza wengine. Yesu alitumia maneno mepesi kueleweka ili kufundisha watu mambo mazito na ya maana sana. Kwa mufano, alipenda kuhakikishia wanafunzi wake kwamba hawakupaswa kuhangaika kwa ajili ya chakula cha kila siku. Kwa hiyo, aliwaambia kwamba Yehova anakulisha ndege sikuzote. Kisha, aliwauliza hivi: “Je, ninyi si bora kuliko wao?” (Mathayo 6:26) Kupitia maneno hayo mepesi, Yesu aliwasaidia wajifunze somo la maana na watiwe moyo.

NAMNA GANI TUNAPASWA KUSEMA NA WENGINE?

15. Sababu gani tunapaswa kusema kwa upole?

15 Namna tunaongea na wengine inaweza kuwa ya maana sana sawasawa na mambo yenye tunasema. Watu walifurahia kumusikiliza Yesu kwa sababu alisema kwa njia “yenye kuvutia sana [yenye kupendeza sana],” ao kwa upole. (Luka 4:22) Wakati tunasema kwa upole, watu wanaweza kufurahia zaidi kutusikiliza na kukubali mambo yenye tunasema. (Methali 25:15) Ikiwa tunawaheshimu wengine na kuhangaikia namna wanajisikia, hilo litatusaidia kuzungumuza nao kwa upole. Yesu alifanya hivyo. Kwa mufano, wakati aliona kikundi cha watu wanajikaza sana kumusikiliza, alifurahi sana kupitisha nao wakati na kuwafundisha. (Marko 6:34) Hata wakati watu walimutukana, Yesu hakuwarudishia matukano.—1 Petro 2:23.

16, 17. (a) Namna gani tunaweza kumuiga Yesu wakati tunazungumuza na watu wa familia na marafiki wetu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Mama moja alipata faida gani kwa kujibu kwa upole?

16 Hata kama tunapenda watu wa familia na marafiki wetu, tunaweza kusema nao kwa kutumia maneno yenye haifae kwa sababu tunawajua muzuri sana. Tunaweza kufikiri kwamba haiko jambo la lazima kutumia maneno yetu kwa uangalifu wakati tunazungumuza nao. Lakini, Yesu hakutumia hata kidogo maneno yenye haifae wakati alizungumuza na marafiki wake. Wakati wamoja kati yao walikuwa wanabishana ili kujua ni nani mwenye alikuwa mukubwa zaidi kati yao, aliwashauria kwa upole na alitumia mufano wa mutoto mudogo ili kuwasaidia wabadilishe mawazo yao. (Marko 9:33-37) Wazee wanaweza kuiga mufano wa Yesu kwa kutolea wengine mashauri kwa upole.—Wagalatia 6:1.

17 Hata ikiwa mutu anatuambia jambo fulani lenye kutukasirisha, tutatenda kwa hekima ikiwa tunazungumuza naye kwa upole. (Methali 15:1) Kwa mufano, mama moja alikuwa na kijana mwanaume mwenye alionekana kuwa anamutumikia Yehova lakini aliendelea kuwa na mwenendo mubaya. Dada moja katika kutaniko alimusikilia mama huyo huruma na alimuambia hivi: “Inahuzunisha sana kuona namna umeshindwa kumulea mutoto wako.” Mama huyo alinyamaza kwanza, kisha alimujibu dada huyo hivi: “Ni kweli kwamba leo mambo haiendeke muzuri, lakini ninaendelea kumuzoeza. Uniulize kisha Har-magedoni ili kujua ikiwa nimeshindwa kumulea ao hapana.” Kwa sababu mama huyo alibakia kwanza kimya na kisha alimujibu dada huyo kwa upole, wote wawili waliendelea kuwa marafiki. Pia, kijana huyo alisikia namna mama yake anamujibu dada huyo, na alitambua kwamba mama yake anaendelea kutumaini kwamba anaweza kubadilika. Kwa hiyo, aliachana na marafiki wabaya, alibatizwa, na kisha alitumikia kwenye Beteli. Iwe tunazungumuza na ndugu na dada zetu, watu wa familia yetu, ao watu wenye hatujuane nao, maneno yetu inapaswa kuwa “yenye neema sikuzote, yenye kukolezwa chumvi.”—Wakolosai 4:6.

18. Namna gani tunaweza kufuata mufano wa Yesu katika namna yetu ya kusema?

18 Uwezo wa kuambia wengine mawazo yetu na namna tunajisikia ni zawadi nzuri kabisa yenye Yehova ametupatia. Ikiwa tunafuata mufano wa Yesu, tutachagua wakati wenye kufaa wa kusema, tutakuwa waangalifu juu ya mambo yenye tunasema, na sikuzote tutajikaza kusema kwa upole. Kwa hiyo, tuendelee kutumia maneno yetu ili kutia wengine moyo na kumufurahisha Yehova.