Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Muhubiri 5:8 inazungumuzia watawala wanadamu tu, ao inamuhusu pia Yehova?

Ile andiko inasema hivi: “Kama unaona maskini wanakandamizwa kwa njia yoyote na haki inavunjwa na uadilifu havifuatwe katika wilaya yako, jambo hilo lisikushangaze. Kwa maana ofisa mukubwa iko anaangaliwa na ule mwenye kuwa juu zaidi kuliko yeye, na kuko wengine wenye wako tena juu yao.”​—Muh. 5:8.

Kwa maoni ya wanadamu, ile andiko inaweza kuonekana kama inahusu tu wanadamu wenye kuwa na mamlaka. Lakini, kama tunaifikiria zaidi, tutaona kama inazungumuzia jambo fulani juu ya Yehova. Na ile jambo inaweza kutufariji na kutupatia tumaini.

Muhubiri 5:8 inazungumuzia mutawala mwenye iko anatesa maskini na kuwatendea bila haki. Anapaswa kukumbuka kama kuko mutawala mwingine mwenye iko na mamlaka zaidi kuliko yeye, mwenye iko anaona mambo yote yenye iko anafanya. Na kunaweza kuwa watawala wengine wenye wako na mamlaka zaidi kuliko wale watawala wawili. Inahuzunisha kuona kama mu serikali za wanadamu, wale watawala wote, wanaweza kutendea wengine bila haki. Na ile inaweza kufanya wale wenye wako chini ya mamlaka yao wateseke.

Lakini tunajua kama Yehova iko anaona mambo yenye ‘maofisa wakubwa’ wa serikali za wanadamu wako wanafanya. Kwa hiyo, hata wakati wanatutendea bila haki na tunawaza kama hakuna tena tumaini, hatuache ile ituvunje moyo. Kuliko kufanya vile, tunasali kwa Yehova na kumuomba atusaidie. (Zb. 55:22; Flp. 4:6, 7) Tunajua kama “macho ya Yehova yanaenda huku na huku katika dunia yote ili kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.”​—2 Ny. 16:9.

Kwa kifupi, Muhubiri 5:8 inatukumbusha kama mu serikali za wanadamu, kunakuwaka mutu mwenye iko na mamlaka zaidi ya wengine. Na jambo la maana zaidi, ile andiko inatukumbusha kama Yehova njo iko na mamlaka ya juu zaidi. Na sasa iko anatawala mbinguni kupitia Mwana wake Yesu Kristo, Mufalme wa Ufalme wake. Yehova, Mungu Mweza-Yote, iko anaona mambo yote yenye iko inafanyika, na haiko sawa vile watawala wanadamu, yeye ni mwenye haki kabisa na Yesu Kristo Mwana wake ni mwenye haki pia.