Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 38

Tenda kwa Hekima Wakati Kungali Amani

Tenda kwa Hekima Wakati Kungali Amani

“Inchi haikukuwa na usumbufu na hapakukuwa vita juu yake katika miaka hiyo, kwa maana Yehova alimupatia pumuziko.”​—2 NY. 14:6.

WIMBO 60 Ni Uzima Kwao

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni wakati gani inaweza kuwa nguvu kumutumikia Yehova?

UNAWAZA ni wakati gani njo inaweza kuwa nguvu kumutumikia Yehova? Ni wakati uko na matatizo ao wakati hauna matatizo? Wakati tunapambana na magumu, ni mwepesi kumutumainia Yehova. Lakini, tunafanyaka namna gani wakati hatuna magumu? Inawezekana tumusahau Mungu? Yehova aliambiaka Waisraeli kama wangeweza kumusahau.​—Kum. 6:10-12.

Mufalme Asa alijikaza sana ili kumaliza ibada ya uongo (Ona fungu la 2) *

2. Mufalme Asa alituachia mufano gani?

2 Mufalme Asa alituachia mufano muzuri sana. Alitenda kwa hekima kwa kumutumainia Yehova kabisa. Alimutumikia Yehova wakati alikuwa na magumu na pia wakati hakukuwa na magumu. “Moyo wa Asa ulikuwa kamili kumuelekea Yehova,” tangu zamani mu maisha yake. (1 Fa. 15:14) Asa alionyesha kama alipenda sana kumutumikia Yehova kwa kumaliza kabisa ibada ya uongo katika Yuda. Biblia inasema kama “aliondoa mazabahu za kigeni na mahali pa juu, akavunja-vunja nguzo takatifu, na kukata miti mitakatifu.” (2 Ny. 14:3, 5) Hata aliondoa Maaka, tate yake, kwenye cheo cha malkia mama ya mufalme, juu Maaka alikuwa anachochea watu waabudu sanamu.​—1 Fa. 15:11-13.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Zaidi ya kumaliza ibada ya uongo, kuko jambo lingine lenye Asa alifanya, alisaidia watu wa Yuda waanze tena kumutumikia Yehova. Yehova alimubariki Asa na Waisraeli kwa kuwasaidia waishi kwa amani. * Mu kipindi cha miaka kumi wakati wa utawala wa Asa, “inchi haikukuwa na usumbufu.” (2 Ny. 14:1, 4, 6) Mu hii habari, tutazungumuzia namna Asa alitenda mu kile kipindi cha amani. Kisha tutazungumuzia namna Wakristo wa karne ya kwanza pia walitenda kwa hekima wakati walikuwa na amani. Ku mwisho tutajibia hii ulizo: Kama mu inchi yenu Mashahidi wa Yehova wako wanamutumikia Yehova kwa uhuru, unaweza kutenda namna gani huu wakati wa amani?

MAMBO YENYE ASA ALIFANYA WAKATI KULIKUWA AMANI

4. Kulingana na 2 Mambo ya Nyakati 14:2, 6, 7, Asa alifanya nini wakati kulikuwa amani?

4 Soma 2 Mambo ya Nyakati 14:2, 6, 7. Asa aliambia watu kama ni Yehova njo alikuwa ‘amewapatia pumuziko kuzunguka pande zote.’ Asa hakuona kama ule wakati wa amani ulikuwa wakati wa kufurahia maisha. Lakini, alitumia ile wakati ili kujenga miji, kuta, minara, na milango mikubwa. Aliambia watu wa Yuda hivi: “Inchi ingali katika mikono yetu.” Asa alipenda kusema nini? Alipenda kusema kama watu wangeweza kutembea katika inchi kwa uhuru na kama hakuna maadui wenye wangewazuia kujenga. Kwa hiyo, aliambia watu watumie muzuri ule wakati wa amani.

5. Juu ya nini Asa alifanya jeshi lake likuwe na nguvu?

5 Pia, Asa alitumia ule wakati wa amani ili kufanya jeshi lake likuwe na nguvu. (2 Ny. 14:8) Ile ilionyesha kama Asa hakukuwa anamutumainia Yehova? Hapana. Lakini, Asa alijua kama kwa sababu alikuwa mufalme, alipaswa kusaidia watu wajitayarishe kwa ajili ya vita yenye ingeweza kutokea. Asa alijua kama ile wakati wa amani haingeendelea milele, na ni vile mambo ilifanyika.

MAMBO YENYE WAKRISTO WA KARNE YA KWANZA WALIFANYA WAKATI KULIKUWA AMANI

6. Wakristo wa karne ya kwanza walifanya nini wakati kulikuwa amani?

6 Hata kama Wakristo wa karne ya kwanza waliteswa mara mingi, wakati fulani walikuwa pia na amani. Walifanya nini mu ule wakati wa amani? Walihubiri habari njema bila kuacha. Habari yenye kuwa mu kitabu cha Matendo inasema kama ‘walitembea katika woga wa Yehova.’ Waliendelea kuhubiri habari njema na ile ilifanya ‘waendelee kuongezeka.’ Bila shaka, Yehova aliwabariki kwa sababu waliendelea kuhubiri kwa bidii wakati kulikuwa amani.​—Mdo. 9:26-31.

7-8. Paulo na wengine walijikaza kufanya nini? Fasiria.

7 Wakristo wa karne ya kwanza walijikaza kuhubiri kila mara wakati iliwezekana kufanya vile. Kwa mufano, wakati mutume Paulo alikuwa Efeso, aliona kama angeweza kuhubiria watu wengi, kwa hiyo alibakia kule ili kuhubiri.​—1 Ko. 16:8, 9.

8 Mu mwaka wa 49, Paulo na wengine walipata nafasi ya kuhubiria watu wengi wakati mitume na wazee walimaliza tatizo lenye lilihusu kutahiriwa. (Mdo. 15:23-29) Kisha Paulo na wengine kujulisha makutaniko uamuzi wenye mitume na wazee walikamata, wote walijikaza sana ili kutangaza “habari njema ya Neno la Yehova.” (Mdo. 15:30-35) Walipata matokeo gani? Biblia inasema kama ‘makutaniko yaliendelea kuwa nguvu katika imani na hesabu ya waamini iliendelea kuongezeka siku kwa siku.’​—Mdo. 16:4, 5.

MAMBO YA KUFANYA WAKATI KUKO AMANI

9. Hali iko namna gani mu inchi za mingi leo, na tunaweza kujiuliza ulizo gani?

9 Leo, mu inchi za mingi, Mashahidi wa Yehova wako na uhuru wa kuhubiri. Mambo iko vile kwenye unaishi? Kama ni vile, ujiulize hivi, ‘Niko nafanya nini mu hii wakati wa uhuru?’ Mu hizi siku za mwisho, watu wa Yehova wako wanahubiri sana kuliko wakati mwingine wowote. Ile ni jambo yenye kufurahisha sana. (Mk. 13:10) Kwa kweli, tuko na mambo mingi ya kufanya mu kazi ya Yehova.

Wakristo wengi wamepata baraka kwa sababu walijitoa ili kuenda kuhubiri mu inchi ingine ao ili kuhubiria watu wenye kuzungumuza luga ingine (Ona fungu la 10-12) *

10. Kulingana na 2 Timoteo 4:2, tunapaswa kufanya nini?

10 Unapaswa kufanya nini mu hii wakati wenye kuko amani? (Soma 2 Timoteo 4:2.) Chunguza hali ya familia yako ili uone kama wewe ao mutu mwingine mu familia yako anaweza kujitoa sana mu kazi ya kuhubiri ao hata kukuwa painia. Hii haiko wakati wa kupenda kuwa tajiri, juu wakati wa taabu kubwa utajiri hautatusaidia.​—Mez. 11:4; Mt. 6:31-33; 1 Yo. 2:15-17.

11. Wakristo fulani wamefanya nini ili waweze kuhubiria watu wengi habari njema?

11 Wahubiri wengi wamejifunza luga ingine ili waweze kuhubiria watu wenye kuzungumuza ile luga. Tengenezo la Yehova linatutolea habari mu luga mbalimbali, na ile, inasaidia sana. Kwa mufano, mu 2010, vichapo vyetu vilikuwa mu luga 500 hivi. Lakini leo, vinapatikana mu luga zaidi ya 1 000!

12. Watu wanajisikiaka namna gani wakati wanasikia habari njema mu luga yao? Leta mufano.

12 Watu wanajisikiaka namna gani wakati wanasikia habari njema mu luga yao? Fikiria mufano wa dada mumoja mwenye alihuzuria mukusanyiko wa eneo mu Inchi ya Amerika. Mukusanyiko ulifanyika mu Kinyarwanda, luga yenye kuzungumuziwa mu inchi ya Rwanda, Congo (Kinshasa), na Uganda. Kisha mukusanyiko, ule dada alisema hivi: “Nimefanya miaka 17 mu inchi ya Amerika, tangu nifike hapa, hii njo mara ya kwanza yenye ninaelewa muzuri mafundisho yenye kutolewa ku mukusanyiko.” Kwa kweli, ule dada aliguswa moyo wakati alisikiliza mukusanyiko mu luga yake. Kama hali yako inaruhusu, unaweza kujifunza luga ingine ili kusaidia watu fulani mu eneo lenu? Pengine ile inaweza kusaidia watu wa mu eneo lenu wenye wanafurahiaka kuzungumuza mu ile luga. Kama unajikaza kufanya vile, utapata baraka mingi.

13. Ndugu zetu wa Urusi walifanya nini wakati walikuwa na amani?

13 Mu inchi fulani, ndugu zetu hawana uhuru wa kuhubiri juu wenye mamlaka wamekataza kazi yetu ya kuhubiri. Kwa mufano, fikiria ndugu zetu mu inchi ya Urusi. Waliteswa kwa miaka mingi, lakini mu Mwezi wa 3, 1991, wenye mamlaka walifikia kukubali kazi yetu. Ile wakati kulikuwa wahubiri 16 000 hivi mu inchi ya Urusi. Kisha miaka makumi mbili, hesabu ya wahubiri iliongezeka na kufikia 160 000! Ile inaonyesha kama ndugu zetu walitenda kwa hekima wakati walikuwa na uhuru wa kuhubiri. Ule wakati wa amani haukuendelea. Lakini hata kama hali ilibadilika, hawakupunguza bidii yao. Wanaendelea kumutumikia Yehova kulingana na uwezo wao.

WAKATI WA AMANI HAUTAENDELEA MILELE

Kisha mufalme Asa kusali sana, Yehova alisaidia watu wa Yuda washinde maadui wao wenye walikuwa wengi sana (Ona fungu la 14-15)

14-15. Namna gani Yehova alimusaidia Asa?

14 Mu siku za Asa, amani haikuendelea milele. Jeshi kubwa la Waetiopia, lenye lilikuwa na maaskari zaidi ya milioni moja, lilikuja kushambulia Yuda. Zera, mukubwa wa jeshi hilo, alikuwa hakika kama yeye na maaskari wake watashinda Yuda. Lakini, Asa alimutumainia tu Yehova, hakutumainia hesabu ya maaskari wake. Alisali hivi: “Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea wewe, na katika jina lako tumekuja kupigana na watu hawa wengi.”​—2 Ny. 14:11.

15 Hata kama maaskari Waetiopia walikuwa wengi sana kuliko maaskari wa Yuda, Asa alijua kama Yehova iko na nguvu na kama angeweza kuokoa watu wake. Na kwa kweli, Yehova aliokoa watu wake. Walishinda kabisa jeshi la Waetiopia.​—2 Ny. 14:8-13.

16. Ni nini inatusaidia kujua kama wakati wa amani hautaendelea milele?

16 Hatujue mambo yenye itapata kila mumoja wetu wakati wenye kuja, lakini tunajua kama wakati wa amani hautaendelea milele. Kumbuka kuwa, Yesu alisema kama mu siku za mwisho, wanafunzi wake ‘watachukiwa na mataifa yote.’ (Mt. 24:9) Mutume Paulo pia, alisema kama “wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.” (2 Ti. 3:12) Shetani iko na “kasirani kali,” na kuwaza kama tunaweza kuepuka ile kasirani yake ni kujidanganya kabisa.​—Ufu. 12:12.

17. Pengine imani yetu itajaribiwa namna gani?

17 Hivi karibuni, imani yetu itajaribiwa. “Kutakuwa taabu kubwa yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa.” (Mt. 24:21) Mu ile wakati, pengine watu wa familia yetu watatupinga, na pengine wenye mamlaka watakataza kazi yetu. (Mt. 10:35, 36) Utamutumainia Yehova na kuwa hakika kama atakusaidia na kukulinda kama vile Asa alifanya?

18. Kulingana na Waebrania 10:38, 39, tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kumutumikia Yehova wakati amani itaisha?

18 Yehova iko anatutayarisha kwa ajili ya mambo yenye itatokea wakati wenye kuja. Iko anaongoza “mutumwa mwaminifu na mwenye busara” ili atutolee “chakula . . . kwa wakati wenye kufaa.” (Mt. 24:45) Ile chakula ya kiroho inatusaidia tuendelee kumutumikia Yehova, lakini sisi pia tunapaswa kujikaza sana ili kuwa na imani ya nguvu.​—Soma Waebrania 10:38, 39.

19-20. Kulingana na 1 Mambo ya Nyakati 28:9, tunapaswa kujiuliza maulizo gani, na juu ya nini?

19 Tunapaswa ‘kumutafuta Yehova’ kama vile Mufalme Asa alifanya. (2 Ny. 14:4; 15:1, 2) Jambo la kwanza lenye tunafanya ili kuonyesha kama tunamutafuta Yehova ni kujifunza juu yake na kubatizwa. Kisha tunafanya yote yenye tunaweza ili tukomalishe upendo wetu kwa Yehova. Ili kujua kama uko unafanya vile, unaweza kujiuliza hivi: ‘Ninahuzuriaka mikutano kwa ukawaida?’ Wakati tunahuzuria mikutano, tunapata nguvu ya kuendelea kumutumikia Yehova, na ndugu na dada zetu wanatutia moyo. (Mt. 11:28) Tunaweza pia kujiuliza hivi: ‘Ninajifunzaka Biblia kwa ukawaida?’ Kama uko mu familia, munafanyaka ibada ya familia kila juma? Ao kama unaishi peke yako, unafanyaka funzo la kipekee kila juma? Unafanyaka yako yote ili kuhubiri na kufundisha?

20 Juu ya nini tunapaswa kujiuliza ile maulizo? Biblia inasema kama Yehova anachunguza mawazo yetu na mambo yenye kuwa mu mioyo yetu. Njo maana sisi pia tunapaswa kujichunguza. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9.) Kama tunaona kuwa tunapaswa kubadilisha miradi na mawazo yetu, tunapaswa kumuomba Yehova atusaidie tufanye vile. Huu njo wakati wa kujitayarisha ili kupambana na majaribu yenye tutapata wakati wenye kuja. Uendelee basi kutenda kwa hekima wakati kungali amani!

WIMBO 62 Wimbo Mpya

^ fu. 5 Mu inchi yenu, Mashahidi wa Yehova wako huru kumutumikia Yehova? Kama ni vile, uko unatenda namna gani hivi kungali amani? Mu hii habari, tutazungumuzia mufano wa Mufalme Asa na mufano wa Wakristo wa karne ya kwanza. Walitenda kwa hekima wakati kulikuwa kungali amani.

^ fu. 3 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Neno “amani” haimaanishe tu kipindi chenye hakuna vita. Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa amani linamaanisha pia afya ya muzuri, usalama, ao hali ya muzuri ya maisha.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Mufalme Asa alimuondoa tate yake kwenye cheo cha malkia mama ya mufalme, juu tate yake alikuwa anachochea watu waabudu sanamu. Watu wenye walimuunga Asa mukono walifuata mufano wake na waliharibu sanamu zenye watu walikuwa wanaabudu.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana wenye bidii wanafanya maisha yao ikuwe mwepesi ili waweze kusaidia mahali kwenye kuwa lazima ya wahubiri.