Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 36

Uko Tayari Kuwa Muvuvi wa Watu?

Uko Tayari Kuwa Muvuvi wa Watu?

“Acha kuogopa. Kuanzia sasa utakuwa unavua watu wakiwa wazima.”​—LU. 5:10.

WIMBO 73 Tupe Ujasiri

KIFUPI CHA HABARI *

1. Yesu aliambia nini wanaume ine wenye walikuwa wavuvi wa samaki, na walifanya nini?

PETRO, Andrea, Yakobo, na Yohana wenye walifikia kuwa wanafunzi wa Yesu walikuwa wanafanya kazi ya kuvua samaki ili kupata feza. Wazia namna walishangaa wakati Yesu aliwaambia hivi: “Munifuate, na mimi nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.” * Walifanya nini wakati walisikia vile? Biblia inasema hivi: “Mara moja wakaacha nyavu zao na kumufuata.” (Mt. 4:18-22) Uamuzi wenye walikamata ungebadilisha kabisa maisha yao. Kuliko kuvua samaki wangeanza ‘kuvua watu wakiwa wazima.’ (Lu. 5:10) Leo pia, Yesu anaita watu wenye kuwa na mioyo mizuri na wenye kupenda kweli ili wafanye ile kazi. (Mt. 28:19, 20) Ulishakubali mualiko wa Yesu wa kukuwa muvuvi wa watu?

2. Juu ya nini tunapaswa kufikiri sana mbele ya kukamata uamuzi wa kukuwa wavuvi wa watu, na nini njo itatusaidia tukamate ule uamuzi?

Pengine umejifunza Biblia kwa wakati fulani, na umefanya mabadiliko mu maisha yako. Na sasa unapenda kuwa muhubiri wa habari njema. Kama uko unasita kukuwa muhubiri, usivunjike moyo. Pengine uko unasita juu unaelewa kama ule ni uamuzi wa maana sana. Ni kweli kuwa Biblia inasema kama Petro na wenzake waliacha nyavu zao “mara moja.” Lakini, ile haimaanishe kama Petro na ndugu yake waliamua bila kufikiri. Kulikuwa kumepita zaidi ya miezi sita tangu wakati walimujua Yesu na kuamini kama alikuwa Masiya. (Yoh. 1:35-42) Pengine wewe pia ulishajifunza mambo mingi juu ya Yehova na Yesu, na unapenda kufanya maendeleo ya kiroho. Lakini mbele ya kukamata uamuzi wa kukuwa muhubiri, unapaswa kufikiri sana. Nini njo ilisaidia Petro, Andrea, na wengine wakamate uamuzi wa kukuwa wavuvi wa watu?

3. Ni nini itakusaidia ukubali kuwa muhubiri?

3 Wanafunzi wa kwanza wa Yesu walipenda sana kazi yao ya kuvua samaki. Walijua kuifanya muzuri, walikuwa hodari, na walijikaza kutumika hata wakati ilikuwa nguvu kufanya vile. Bila shaka, ile mambo iliwasaidia wapate matokeo ya muzuri wakati walifikia kuwa wahubiri. Kufuata mufano wa wanafunzi wa Yesu kutakusaidia ufikie kuwa muhubiri muzuri. Hii habari itakusaidia ujue namna unaweza kufanya vile.

UPENDE SANA KAZI YA KUHUBIRI

Petro na wenzake walifikia kuwa wavuvi wa watu. Ile kazi ya maana iko inaendelea mupaka leo (Ona fungu la 4-5)

4. Juu ya nini Petro alifanya kazi ya kuvua samaki?

Petro alifanya kazi ya kuvua samaki juu apate feza za kutegemeza familia yake. Lakini zaidi ya ile, alifanya ile kazi juu aliipenda. (Yoh. 21:3, 9-15) Alifikia pia kupenda kazi ya kuhubiri. Na kwa musaada wa Yehova, alifikia kuwa muhubiri muzuri.​—Mdo. 2:14, 41.

5. Kulingana na Luka 5:8-11, juu ya nini Petro aliogopa, na ni nini inaweza kutusaidia tusiogope kuwa wavuvi wa watu?

5 Sababu kubwa yenye inatuchochea tufanye kazi ya kuhubiri ni hii: tunamupenda Yehova. Kumupenda Yehova kunaweza kutusaidia tuhubiri hata kama pengine tunaona kuwa hatutaweza kufanya vile. Wakati Yesu alimuita Petro ili akuwe muvuvi wa watu alimuambia hivi: “Acha kuogopa.” (Soma Luka 5:8-11.) Maneno ya Yesu haimaanishe kama Petro aliogopa mambo yenye ingemupata kama anakuwa mwanafunzi wa Yesu. Lakini Petro aliogopa juu alijiona kuwa hafae kutumika pamoja na Yesu. Alijisikia vile juu aliona namna Yesu aliwasaidia wavue samaki wengi kwa njia ya muujiza. Kama Petro, wewe pia unaweza kuogopa. Wakati unafikiria mambo yenye mwanafunzi wa Yesu anapaswa kufanya, unaweza kuwaza kama hautaweza. Kama ni vile, ujikaze umupende sana Yehova, Yesu, na watu wengine. Ile itakusaidia usiogope kuwa muvuvi wa watu.​—Mt. 22:37, 39; Yoh. 14:15.

6. Ni sababu gani zingine zenye zinatuchochea kuhubiri?

6 Kuko sababu zingine zenye zinatuchochea tuhubiri. Tunapenda kutii amri hii ya Yesu: “Muende, na mufanye wanafunzi.” (Mt. 28:19, 20) Pia, tunahubiri juu watu wako kama kondoo wenye “wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku” na wako na lazima kabisa ya kujifunza kweli kuhusu Ufalme wa Mungu. (Mt. 9:36) Yehova anapenda watu wa namna zote wapate ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli, ili waokolewe.​—1 Ti. 2:4.

7. Kulingana na Waroma 10:13-15, juu ya nini kazi ya kuhubiri ni ya maana?

7 Kama tunafikiria namna kazi ya kuhubiri inaweza kusaidia watu waokolewe, tutapenda kuhubiri. Muvuvi wa samaki anakulaka ao kuuzisha samaki wenye anavua. Lakini sisi ‘tunavua’ watu, ni kusema, tunawahubiria ili waokolewe.​—Soma Waroma 10:13-15; 1 Ti. 4:16.

UJUE MUZURI NAMNA YA KUHUBIRI

8-9. Muvuvi anapaswa kujua nini, na juu ya nini?

8 Wakati wa Yesu, muvuvi Muisraeli alipaswa kujua ni samaki wa aina gani njo iko anaenda kutafuta. (Law. 11:9-12) Alipaswa pia kujua ni wapi atapata ile aina ya samaki. Mara mingi samaki wanakuwaka fasi kwenye maji iko namna wanapenda, na kwenye kuko chakula mingi. Muvuvi anapaswa pia kufikiria ni wakati gani ataenda kuvua samaki. Misionere mumoja mwenye anaishi mu kisiwa fulani cha Pasifiki, alijifunza kama kuko wakati wenye kufaa wa kuenda kuvua samaki. Wakati ndugu mumoja wa mu ile eneo alimuambia waende wavue samaki, ule misionere alisema hivi: “Tukutane kesho saa tatu ya asubui.” Lakini ule ndugu alimujibia hivi: “Hapana ile saa. Hatuendake saa yenye tunapenda. Tunaendaka saa yenye tunajua kama tunaweza kukamata samaki.”

9 Njo vile wanafunzi wa Yesu wenye walifikia kuwa wavuvi wa watu walikuwa wanafanya. Walikuwa wanaenda kutafuta watu fasi kwenye wangewapata. Kwa mufano, wafuasi wa Yesu walikuwa wanahubiri ku hekalu na mu masinagogi, nyumba kwa nyumba na mu masoko. (Mdo. 5:42; 17:17; 18:4) Sisi pia tunapaswa kupatanisha programu yetu ya kuhubiri na watu wa eneo letu. Tunapaswa kuwatafuta saa yenye tunaweza kuwapata, na fasi kwenye tunaweza kuwapata.​—1 Ko. 9:19-23.

WAVUVI WENYE UFUNDI . . . 1. wanaendaka kutumika saa yenye inawezekana wapate samaki, na fasi kwenye inawezekana waipate (Ona fungu la 8-9)

10. Tengenezo la Yehova linatutolea vyombo gani?

10 Muvuvi anapaswa kuwa na vyombo vyenye kufaa na anapaswa kujua namna ya kuvitumikisha. Sisi pia tunapaswa kuwa na vyombo vyenye kufaa kwa ajili ya kazi ya kuhubiri na tunapaswa kujua namna ya kuvitumikisha. Yesu alipatia wanafunzi wake maagizo juu ya namna ya kuhubiri habari njema. Aliwaambia vitu vyenye walipaswa kubeba, wangehubiria wapi, na mambo yenye walipaswa kusema. (Mt. 10:5-7; Lu. 10:1-11) Leo, tengenezo la Yehova linatutolea vyombo vya kufundishia vyenye vinatusaidia tupate matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri. * Na tunapata mazoezi yenye inatusaidia kujua namna ya kutumia vile vyombo. Ile mazoezi inatusaidia tusikuwe na woga, na tukuwe na ufundi wenye unatusaidia tupate matokeo ya muzuri mu kazi yetu.​—2 Ti. 2:15.

WAVUVI WENYE UFUNDI . . . 2. wanakuwaka na vyombo vyenye kufaa na wanajua kuvitumia muzuri (Ona fungu la 10)

UKUWE HODARI

11. Juu ya nini wavuvi wa watu wanapaswa kuwa hodari?

11 Wavuvi wa samaki wanapaswa kuwa hodari. Juu ya nini? Juu wakati fulani mu bahari, hali ya hewa inabadilikaka bila kutazamia. Tena mara mingi wanatumikaka usiku, na upepo mukali unaweza kutokea kwa kushitukia. Wavuvi wa watu wanapaswa pia kuwa hodari. Wakati unaanza kuhubiri na kuambia wengine kama umekuwa Shahidi wa Yehova, unaweza kupata matatizo yenye iko kama “upepo mukali.” Kwa mufano, watu wa familia wanaweza kukupinga, marafiki wanaweza kukuzarau, na watu wanaweza kukataa kusikiliza ujumbe wenye unawahubiria. Lakini ile haitushangaze. Juu wakati Yesu alituma wanafunzi wake waende kuhubiri, aliwaambia mbele ya wakati kama watu watawapinga.​—Mt. 10:16.

12. Kulingana na Yoshua 1:7-9, tunaweza kufanya nini ili tukuwe hodari?

12 Unaweza kufanya nini juu ukuwe hodari? Kwanza, ukuwe hakika kama Yesu anaendelea kuongoza kazi ya kuhubiri. (Yoh. 16:33; Ufu. 14:14-16) Kisha, ukuwe na imani kama Yehova atakutimizia mahitaji yako. Kama imani yako inaongezeka, utakuwa pia hodari zaidi. (Mt. 6:32-34) Petro na wenzake walionyesha kama wako na imani yenye nguvu wakati waliacha kazi yao ya kuvua samaki na kumufuata Yesu. Wewe pia ulionyesha kama uko na imani yenye nguvu wakati uliambia marafiki na watu wa familia yako kama umeanza kujifunza Biblia na kukusanyika pamoja na Mashahidi wa Yehova. Bila shaka, umefanya mabadiliko makubwa juu mwenendo na maisha yako vipatane na kanuni za Mungu za haki. Ile pia inaonyesha kama uko na imani na uhodari. Wakati unaendelea kuwa hodari unaweza kuwa hakika kama “Yehova Mungu wako iko pamoja na wewe kila mahali kwenye unaenda.”​—Soma Yoshua 1:7-9.

WAVUVI WENYE UFUNDI . . . 3. wanakuwaka hodari na wanajikazaka kutumika hata wakati hali inabadilika (Ona fungu la 11-12)

13. Namna gani kusali na kufikiri sana kunaweza kukusaidia ukuwe hodari?

13 Unaweza kufanya nini ingine ili ukuwe hodari? Umuombe Yehova akusaidie ukuwe hodari na usiogope. (Mdo. 4:29, 31) Yehova atajibia sala zako na hatakuacha hata kidogo. Ataendelea kukutegemeza. Pia unaweza kufikiri sana juu ya namna Yehova aliokoa watu wake wakati wa zamani. Fikiria pia namna amekusaidia ushinde magumu fulani na ufanye mabadiliko mu maisha yako. Sawa vile alisaidia watu wake ili wavuke Bahari Nyekundu, bila shaka anaweza kukusaidia wewe pia ukuwe mwanafunzi wa Kristo. (Kut. 14:13) Ukuwe na imani sawa ya muandikaji wa zaburi mwenye alisema hivi: “Yehova iko upande wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunifanya nini?”​—Zb. 118:6.

14. Mambo yenye ilifikia Masae na Tomoyo inakufundisha nini?

14 Jambo lingine lenye linaweza kukusaidia ukuwe hodari ni kufikiria namna Yehova alisaidia watu wenye walikuwa na haya, ili wakuwe hodari. Fikiria mufano wa dada mwenye kuitwa Masae, alikuwa na haya na aliwaza kama hatawezaka kuhubiria wengine. Aliona kama kuzungumuza na watu wenye hajue, ni sawa vile kupanda mulima murefu sana, na aliona kama hataweza kufanya vile. Kwa hiyo alijikaza kumupenda Mungu sana na kupenda watu wengine. Alifikiri juu ya wakati wenye tunaishi na aliona kama kunabakia wakati kidogo kwa ajili ya kazi ya kuhubiri. Pia alimuomba Yehova amusaidie ili apende sana kazi ya kuhubiri. Ile ilimusaidia aache kuogopa na alifikia hata kuwa painia wa kawaida. Yehova anaweza pia kusaidia wahubiri wapya ili wao pia ‘wakuwe hodari.’ Fikiria mufano wa dada mwingine mwenye kuitwa Tomoyo. Wakati alianza kuhubiri nyumba kwa nyumba, mutu wa kwanza mwenye alijaribu kuzungumuza naye alimuambia hivi kwa ukali: “Sipendi kuzungumuza na Mashahidi wa Yehova!” Na akafunga mulango. Tomoyo hakuogopa lakini aliambia muhubiri mwenzake hivi: “Ulisikia? Nilikuwa sijasema hata kitu lakini alijua kama niko Shahidi wa Yehova. Nafurahi sana!” Leo, Tomoyo iko painia wa kawaida.

UJIKAZE KUHUBIRI HATA WAKATI NI NGUVU KUFANYA VILE

15. Namna gani tunaweza kufuata mufano wa muvuvi muzuri, na juu ya nini tunapaswa kufanya vile?

15 Muvuvi muzuri anajikazaka sana ili kufanya kazi yake. Kwa mufano, anaamukaka asubui sana, anavumiliaka mupaka amalize kazi, na anaendeleaka kutumika hata wakati hali ya hewa haiko muzuri. Sisi pia tunapaswa kujikaza sana mu kazi yetu ya kuhubiri. Kama tunafanya vile, tutaendelea kuhubiri na kuvumilia mupaka mwisho.​—Mt. 10:22.

16. Nini njo inaweza kutusaidia tufanye mambo yenye tunaona kama haiko mwepesi?

16 Mara mingi tunapendaka kufanya mambo ya mwepesi. Lakini, wakati fulani mambo ya maana haikuwake mwepesi. Njo maana tunapaswa kujikaza kuonyesha sifa ya kujizuia ili tuweze kufanya ile mambo. Kwa hiyo, tuko na lazima ya musaada ili tujizoeze kufanya mambo yenye tunaona kuwa haiko mwepesi. Yehova anatutolea ule musaada kupitia roho yake takatifu.​—Gal. 5:22, 23.

17. Kulingana na 1 Wakorinto 9:25-27, mutume Paulo alipaswa kufanya nini ili aendelee kufanya mambo yenye kuwa sawa?

17 Mutume Paulo alikuwa anajikaza kufanya mambo yenye kuwa sawa. Lakini ile haikukuwa mwepesi. Njo maana alisema kama alikuwa “anapiga-piga” mwili wake ili aweze kufanya vile. (Soma 1 Wakorinto 9:25-27.) Alishauria wengine wajikaze sana ili wafanye mambo yote kwa “adabu na kwa utaratibu.” (1 Ko. 14:40) Sisi pia tunapaswa kujikaza sana ili kuendelea kumuabudu Yehova. Ile inatia ndani kuendelea kujikaza kuhubiri na kufundisha habari njema.​—Mdo. 2:46.

UKUWE MUHUBIRI BILA KUKAWIA

18. Tunapaswa kufanya nini ili Yehova aone kama tunafanya muzuri kazi ya kuhubiri?

18 Muvuvi anaonaka kuwa anafanya kazi yake muzuri, kama anakamata samaki wengi. Lakini kazi yetu ya kuhubiri haiko vile. Haiko hesabu ya watu wenye tunasaidia wakuwe Mashahidi njo inaonyesha kama tuko wahubiri wazuri ao hapana. (Lu. 8:11-15) Kama tu tunaendelea kuhubiri na kufundisha, tukuwe hakika kama Yehova anaona kuwa tunafanya kazi yetu muzuri. Juu ya nini? Juu wakati tunafanya vile tunaonyesha kama tunamutii yeye na Mwana wake.​—Mk. 13:10; Mdo. 5:28, 29.

19-20. Juu ya nini huu njo wakati ya kujikaza kuhubiri haraka sana?

19 Mu inchi fulani, watu wanaruhusiwa kuvua samaki mu miezi fulani tu. Wakati ile miezi inakaribia kuisha, muvuvi anaonaka kama ni jambo la lazima atumike haraka sana. Sisi pia tunaona kama ni jambo la lazima tuhubiri haraka sana, juu mwisho wa ulimwengu unakaribia sana. Tunabakia na wakati kidogo sana wa kuhubiria watu habari njema yenye inaweza kuwasaidia waokolewe. Usingoje mupaka mambo yote ikuwe muzuri mu maisha yako njo uanze kazi ya kuhubiri.​—Muh. 11:4.

20 Huu njo wakati wa kujikaza kupenda kazi ya kuhubiri, kuelewa muzuri mafundisho ya Biblia, kukuwa hodari, na kujikaza sana kuhubiri hata wakati ni nguvu kufanya vile. Ujiunge na watu zaidi ya milioni munane wenye kufanya kazi ya kuvua watu. Kama unafanya vile utapata furaha yenye Yehova anapatia watumishi wake. (Ne. 8:10) Ujikaze basi kuhubiri kwa nguvu yako yote na uendelee kufanya vile mupaka wakati ile kazi itafikia mwisho. Habari yenye kufuata itazungumuzia mambo tatu yenye itatuchochea tuendelee kuhubiri habari njema ya Ufalme.

WIMBO 66 Tangaza Habari Njema

^ fu. 5 Yesu aliita wanaume fulani wenye walikuwa wanafanya kazi ya kuvua samaki ili wakuwe wanafunzi wake. Wale wanaume walikuwa wanyenyekevu na walikuwa na bidii mu kazi yao. Leo pia, Yesu iko anaita watu wenye wako na zile sifa ili wakuwe wavuvi wa watu. Mu hii habari tutazungumuzia mambo yenye wanafunzi wa Biblia wenye wako wanaogopa kuwa wavuvi wa watu wanapaswa kufanya.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Maneno “wavuvi wa watu” inazungumuzia wale wote wenye wako wanahubiri na kufundisha watu wengine, ili kusaidia wale watu wafikie kuwa wanafunzi wa Kristo.

^ fu. 10 Ona habari yenye kichwa “Tufundishe Kweli” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 10, 2018, uku. 11-16.