Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 37

“Usiache Mukono Wako Upumuzike”

“Usiache Mukono Wako Upumuzike”

“Panda mbegu zako asubui na usiache mukono wako upumuzike mupaka mangaribi.”​—MUH. 11:6.

WIMBO 68 Kupanda Mbegu ya Ufalme

KIFUPI CHA HABARI *

1-2. Muhubiri 11:6 inapatana namna gani na kazi yetu ya kuhubiri?

MU INCHI fulani, watu wanafurahia sana kusikiliza habari njema, lakini mu inchi zingine watu wengi hawafurahie mafundisho ya Biblia ao mazungumuzo yenye inahusu Mungu. Watu wa mu eneo lenu wako namna gani? Ikuwe wanafurahia kusikiliza habari njema ao hapana, Yehova anapenda tuendelee kuhubiri mupaka wakati ile kazi itafikia mwisho!

2 Yehova alishaamua wakati wenye tutaacha kuhubiri. Saa ile wakati itafika, “mwisho utakuja.” (Mt. 24:14, 36) Mbele ile wakati ifike, tunapaswa kutii maneno yenye kuwa mu Muhubiri 11:6, yenye kusema: “Usiache mukono wako upumuzike.” * Mu fungu lenye kufuata tutaona namna tunaweza kufanya vile.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Mu habari yenye ilitangulia tulizungumuzia mambo ine yenye inaweza kutusaidia tukuwe “wavuvi wa watu,” wenye kupata matokeo ya muzuri. (Mt. 4:19) Mu hii habari tutazungumuzia mambo tatu yenye inaweza kutusaidia tuendelee kujikaza kuhubiri hata ikuwe tunapambana na magumu ya namna gani. Tutaona juu ya nini ni jambo la maana (1) tuendelee kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, (2) tukuwe wavumilivu, na (3) tuendelee kuwa na imani yenye nguvu.

ENDELEA KUTIA KAZI YA KUHUBIRI PA NAFASI YA KWANZA

4. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kutia pa nafasi ya kwanza kazi yenye Yehova ametupatia?

4 Yesu alisema mbele ya wakati mambo yenye ingeonyesha kama tunaishi mu siku za mwisho. Ile mambo ingeweza kufanya wanafunzi wake wasitie kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza. Njo maana aliwaambia ‘waendelee kukesha.’ (Mt. 24:42) Mu siku za Noa kulikuwa mambo mingi yenye ilifanya watu wasisikilize ujumbe wenye aliwatangazia. Ile mambo inaweza kutukengeusha pia leo. (Mt. 24:37-39; 2 Pe. 2:5) Kwa hiyo, tunapaswa kuendelea kutia pa nafasi ya kwanza kazi yenye Yehova ametupatia.

5. Kulingana na Matendo 1:6-8, kazi ya kuhubiri ingefanywa mupaka wapi?

5 Tunapaswa kuendelea kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza leo. Yesu alisema kama wanafunzi wake wangeendelea kuhubiri kisha yeye kufa na kama wangehubiri sana kuliko yeye. (Yoh. 14:12) Kisha Yesu kufa, wanafunzi wake fulani walirudilia kazi ya kuvua samaki. Na kisha kufufuliwa kwake, Yesu aliwasaidia wakamate samaki wengi kwa njia ya muujiza. Kisha alikazia kama kazi ya kuhubiri njo kazi ya maana sana kuliko kazi zingine zote. (Yoh. 21:15-17) Na mbele tu Yesu apande mbinguni, aliambia wanafunzi wake kama kazi ya kuhubiri yenye alikuwa ameanzisha haingeishia tu Israeli lakini ingeendelea mupaka sehemu za mbali za dunia. (Soma Matendo 1:6-8.) Miaka mingi kisha pale, Yesu alionyesha mutume Yohana mambo yenye ingetokea “katika siku ya Bwana.” * Kati ya ile mambo, Yohana aliona jambo fulani lenye kushangaza sana: “Habari njema ya milele” ilikuwa inahubiriwa kwa “kila taifa na kabila na luga na watu,” na malaika njo alikuwa anaongoza ile kazi. (Ufu. 1:10; 14:6) Ni wazi kama Yehova anapenda tufanye kazi ya kuhubiri mupaka wakati ile kazi itafikia mwisho.

6. Nini njo inaweza kutusaidia tutie kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza?

6 Tunaweza kuendelea kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza kama tunafikiri sana juu ya mambo yenye Yehova iko anafanya ili kutusaidia. Kwa mufano, anatutolea chakula mingi ya kiroho kupitia vichapo vyenye kuchapishwa na vya kielektronike, kupitia habari za kusikiliza tu na video, na kupitia JW Télédiffusion. Waza kidogo: Ku site yetu ya Enternete, unaweza kupata habari mbalimbali mu luga zaidi ya 1 000! (Mt. 24:45-47) Mu dunia, watu hawana umoja kwa sababu ya mambo ya politike na ya dini, na kwa sababu wamoja ni maskini na wengine ni matajiri. Lakini watu zaidi ya milioni munane mu dunia yote wako wanamutumikia Mungu kwa umoja. Kwa mufano, Siku ya Tano tarehe 19 Mwezi wa 4, 2019, Mashahidi wa Yehova mu dunia yote walifuata video ya andiko la siku. Ile inaonyesha kweli kama wako na umoja. Mangaribi ya ile siku, watu 20 919 041 walikutana pamoja ili kufanya Ukumbusho wa kifo cha Yesu. Wakati tunafikiria pendeleo lenye tuko nalo la kujionea mambo ya ajabu yenye Yehova iko anatimiza na la kuwa kati ya watu wake wenye umoja, ile inatuchochea tuendelee kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza.

Yesu hakuacha hata jambo moja limufanye aache kuhubiri (Ona fungu la 7)

7. Namna gani mufano wa Yesu unatusaidia tuendelee kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza?

7 Jambo lingine lenye linaweza kutusaidia tuendelee kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza ni kufuata mufano wa Yesu. Hakuacha hata jambo moja limukengeushe na limufanye aache kuhubiri. (Yoh. 18:37) Hakushawishiwa wakati Shetani alimuambia kama atamupatia “falme zote za ulimwengu na utukufu wa falme hizo”; ao wakati watu walijaribu kumufanya akuwe mufalme. (Mt. 4:8, 9; Yoh. 6:15) Hakukengeushwa na tamaa ya vitu vya kimwili; wala hakuogopa wakati watu walimupinga kwa ukali. (Lu. 9:58; Yoh. 8:59) Mutume Paulo alishauria Wakristo waendelee kufuata mufano wa Yesu ‘ili wasichoke na kuacha’ kumutumikia Yehova. Kukumbuka ile shauri, kunaweza kutusaidia tuendelee kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza hata wakati imani yetu inajaribiwa.​—Ebr. 12:3.

UKUWE MUVUMILIVU

8. Uvumilivu ni nini, na juu ya nini ni sifa ya lazima sana leo?

8 Uvumilivu ni uwezo wa kungojea kwa utulivu mupaka hali fulani ibadilike. Tuko na lazima ya uvumilivu mu hali mbalimbali. Ile sifa inaweza kutusaidia wakati tuko tunapambana na magumu na tunapenda imalizike ao wakati tuko tunangojea jambo fulani la muzuri lifanyike. Nabii Habakuki alipenda sana jeuri iishe katika Yuda na alikuwa anangojea jambo hilo. (Hab. 1:2) Wanafunzi wa Yesu walitumaini kama Ufalme “ungeonekana mara moja” na kuwakomboa kutoka katika utawala wa Roma. (Lu. 19:11) Sisi pia tunangojea sana Ufalme wa Mungu utoshe mambo yote ya mubaya na ulete ulimwengu mupya wenye haki. (2 Pe. 3:13) Lakini, tunapaswa kuvumilia na kungojea mupaka wakati wenye Yehova ameweka. Tuone basi namna Yehova anatufundisha uvumilivu katika njia mbalimbali.

9. Ni mifano gani yenye inaonyesha kama Yehova ni muvumilivu?

9 Yehova anatuwekea mufano muzuri wa namna ya kuonyesha uvumilivu. Wakati aliambia Noa ajenge safina na ahubiri, alimuachia wakati wenye alikuwa nao lazima ili kufanya ile mambo yote. (2 Pe. 2:5; 1 Pe. 3:20) Pia, Yehova alisikiliza kwa uvumilivu wakati Abrahamu alimuuliza maulizo mingi juu ya uamuzi wake wa kuharibu miji ya Sodoma na Gomora, yenye ilikuwa na watu wabaya sana. (Mwa. 18:20-33) Tena, kwa miaka mingi, Yehova alivumilia sana taifa la Israeli lenye lilikosa uaminifu. (Ne. 9:30, 31) Leo pia, tunaona namna Yehova anaonyesha uvumilivu kwa sababu anaacha wakati ili wale wenye anapenda wakuwe marafiki wake “wafikie kutubu.” (2 Pe. 3:9; Yoh. 6:44; 1 Ti. 2:3, 4) Mufano wa Yehova unatuchochea tuendelee kuvumilia wakati tuko tunahubiri na kufundisha. Pia, anatufundisha sifa ya uvumilivu kupitia mufano fulani wenye aliandikisha katika Neno lake.

Kama mulimaji, tunapaswa kutumika kwa bidii na kuwa wavumilivu (Ona fungu la 10-11)

10. Mufano wa mulimaji wenye unazungumuziwa mu Yakobo 5:7, 8 unaweza kutufundisha nini?

10 Soma Yakobo 5:7, 8. Mufano wa mulimaji unatufundisha namna ya kuwa wavumilivu. Kusema kweli, mimea fulani inakomalaka mbio. Lakini mimea mingi, zaidi sana mimea yenye inatoshaka matunda, haikomalake mbio. Katika Israeli, kipindi cha kulima kilikuwa kinakamata miezi sita. Mulimaji alikuwa anapanda mbegu kisha mvua ya kwanza-kwanza, ni kusema katikati ya Mwezi wa 10 na alikuwa anavuna kisha mvua ya mwisho-mwisho, ni kusema katikati ya Mwezi wa 4. (Mk. 4:28) Sisi pia tunapaswa kujikaza kuwa wavumilivu kama mulimaji. Lakini wakati fulani haiko mwepesi.

11. Uvumilivu unaweza kutusaidia namna gani mu mahubiri?

11 Kwa sababu hatukamilike, tunapendaka tuone matokeo ya kazi yetu palepale. Lakini ili mulimaji apate matokeo ya muzuri, hapaswe kufunga mikono, anapaswa kulima, kupanda mimea, kupalilia, na kumwangia mimea maji. Ni vile pia kuhusu kazi yetu ya kuhubiri, tunapaswa kutumika sana kama tunapenda tupate matokeo ya muzuri. Kwa mufano, inaomba wakati ili tusaidie wanafunzi wetu wa Biblia waachane na tabia ya ubaguzi na wajifunze kupenda wengine. Uvumilivu utatusaidia tusivunjike moyo wakati watu wanakataa kutusikiliza. Hata wakati watu wanakubali kutusikiliza, tunapaswa tu kuendelea kuonyesha sifa ya uvumilivu, kwa sababu hatuwezi kukaza wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo. Wakati fulani, hata wanafunzi wa Yesu hawakuelewa haraka mambo yenye Yesu alikuwa anawafundisha. (Yoh. 14:9) Kwa hiyo, tunapaswa kukumbuka kama kazi yetu ni kupanda na kumwangia maji, lakini Mungu njo anakomalishaka.​—1 Ko. 3:6.

12. Namna gani tunaweza kuonyesha sifa ya uvumilivu wakati tunahubiria watu wa familia yetu wenye hawako Mashahidi?

12 Inaweza kuwa nguvu kuonyesha uvumilivu wakati tunahubiria watu wa familia yetu wenye hawako Mashahidi. Lakini kanuni yenye kuwa mu andiko la Muhubiri 3:1, 7 inaweza kutusaidia. Inasema kama kuko “wakati wa kunyamaza na wakati wa kusema.” Hata kama hatuseme kitu, mwenendo wetu muzuri unaweza kufanya watu wa familia yetu wafurahie kujifunza Biblia. Lakini tunapaswa kuendelea kuwa tayari kuwahubiria wakati nafasi inajitokeza. (1 Pe. 3:1, 2) Tuendelee basi kuhubiri kwa bidii, lakini tusisahau kama tunapaswa kuendelea kuvumilia watu wote, hata watu wa familia yetu.

13-14. Leta mifano ya watumishi fulani wa Yehova wenye walionyesha uvumilivu.

13 Mifano ya watumishi wa Yehova waaminifu wa zamani na wa leo inaweza kutusaidia tukuwe wavumilivu. Habakuki alipenda sana uovu uishe, lakini alionyesha kama iko muvumilivu wakati alisema hivi: “Nitaendelea kusimama mahali pangu pa kufanyia ulinzi.” (Hab. 2:1) Mutume Paulo pia alionyesha kama alikuwa muvumilivu kwa kuendelea “kutoa ushahidi kamili juu ya habari njema” hata kama alipenda “kumaliza” utumishi wake.​—Mdo. 20:24.

14 Fikiria mufano wa bibi na bwana fulani wenye walisoma Masomo ya Gileadi. Walitumwa mu inchi kwenye hakuna Mashahidi wengi na kwenye watu wengi hawako Wakristo. Watu kidogo tu njo walifurahia kujifunza Biblia. Lakini ndugu na dada wengine wenye walisomaka nao Masomo ya Gileadi, wenye walikuwa wanatumikia mu inchi zingine, walikuwa wanawaambia habari za muzuri juu ya kazi ya kuhubiri. Walikuwa wanawaambia kama walikuwa wanaongoza mafunzo mingi ya Biblia na ile mafunzo ilikuwa inafanya maendeleo. Wale bibi na bwana waliendelea kuhubiri hata kama watu wengi hawakukuwa wanasikiliza. Kisha kuhubiri kwa miaka munane mu ile eneo, walifurahi sana wakati mwanafunzi wao mumoja wa Biblia alifikia kubatizwa. Ile mifano ya watumishi wa Yehova wa zamani na wa leo inatufundisha nini? Hawakupunguza bidii yao ao kuacha mikono yao ipumuzike, na Yehova aliwabariki kwa sababu walionyesha uvumilivu. Tuendelee basi kuwa “waigaji wa wale wenye kupitia imani na uvumilivu wanariti ahadi.”​—Ebr. 6:10-12.

UENDELEE KUWA NA IMANI YA NGUVU

15. Namna gani imani inatusaidia tujikaze kuendelea kuhubiri?

15 Tunaamini mambo yenye tunahubiri, njo maana tunapendaka sana kuielezea watu wengi kadiri inawezekana. Tuko hakika kama ahadi zenye kuwa mu Biblia zitatimia. (Zb. 119:42; Isa. 40:8) Tunajionea namna unabii wa Biblia uko unatimia leo. Pia, tunajionea namna mashauri ya Biblia inasaidia watu kubadilika. Ile inafanya tukuwe hakika kabisa kama watu wote wako na lazima ya kusikia habari njema ya Ufalme.

16. Kulingana na Zaburi 46:1-3, namna gani kumuamini Yehova na Yesu kunatusaidia tujikaze kuendelea kuhubiri?

16 Tunamuamini pia Yehova, mwenye habari yenye tunahubiri inatoka kwake, na tunamuamini Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu. (Yoh. 14:1) Hata tupate magumu ya namna gani, Yehova ataendelea kuwa kimbilio letu na nguvu yetu. (Soma Zaburi 46:1-3.) Zaidi ya ile, tuko hakika kama Yesu iko anatumia nguvu na mamlaka yenye Yehova amemupatia ili kuongoza kazi ya kuhubiri.​—Mt. 28:18-20.

17. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuhubiri? Leta mufano.

17 Kama tuko na imani, tutakuwa hakika kama Yehova atatubariki kwa sababu ya bidii yetu, na wakati fulani anafanya vile mu njia yenye hatukuwazia. (Muh. 11:6) Kwa mufano, kila siku watu wengi wanaonaka vichapo vyenye tunatia ku prezantware ao ku meza ya vichapo. Ile njia ya kuhubiri inakuwaka na matokeo ya muzuri? Ndiyo kabisa! Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 11, 2014 ilizungumuzia mwanafunzi mumoja mwenye alipenda kuandika habari fulani juu ya Mashahidi wa Yehova. Hakujua kwenye Jumba la Ufalme lilikuwa, lakini ku masomo yao aliona wahubiri wenye walikuwa pembeni ya meza ya vichapo na walimusaidia kupata habari yenye alikuwa anatafuta. Kisha alifikia kubatizwa, na leo iko painia wa kawaida. Mifano ya vile inatusaidia tuendelee kuhubiri juu inaonyesha kama kungali watu wenye wako na lazima ya kusikia habari njema ya Ufalme.

USIACHE MUKONO WAKO UPUMUZIKE

18. Juu ya nini tuko hakika kama kazi ya kuhubiri itamalizika mu wakati wenye Yehova aliweka?

18 Tuko hakika kama kazi ya kuhubiri itamalizika mu wakati wenye Yehova aliweka. Mambo yenye ilifanyika wakati wa Noa inatusaidia kuelewa kama Yehova anaheshimiaka wakati wenye alipanga kufanya mambo fulani. Miaka 120 hivi mbele garika ifike, Yehova alikuwa amepanga wakati wenye ingeanza. Miaka fulani kisha pale, Yehova alipatia Noa kazi ya kujenga safina. Noa aliendelea kufanya ile kazi kwa bidii hata kama ilikamata miaka 40 ao 50 hivi mbele garika ifike. Alihubiri hata kama watu hawakumusikiliza. Na aliendelea kufanya vile mupaka siku yenye Yehova alimuambia kama ni wakati sasa wa kuingiza wanyama mu safina. Kisha kwa wakati wenye kufaa, ‘Yehova alifunga mulango.’​—Mwa. 6:3; 7:1, 2, 16.

19. Tutaona mambo gani kama hatuache mukono wetu upumuzike?

19 Hivi karibuni, Yehova atatusaidia kuelewa kama wakati wa kuacha kuhubiri umefika. Kisha ataharibu ulimwengu wa Shetani na kuleta ulimwengu mupya wenye haki. Mbele ile wakati ifike, tuendelee basi kufuata mufano wa Noa, Habakuki, na mufano wa watumishi wengine wa Yehova wenye hawakuacha mukono wao upumuzike. Tuendelee basi kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, kuwa wavumilivu, kumuamini kabisa Yehova, na kuwa hakika kama ahadi zake zitatimia.

WIMBO 75 “Mimi Hapa! Nitume Mimi”

^ fu. 5 Habari yenye kutangulia ilitia moyo wanafunzi wa Biblia wenye wako wanafanya maendeleo wakubali kuwa wavuvi wa watu. Mu hii habari tutazungumuzia mambo tatu yenye inaweza kusaidia wahubiri wote, ikuwe wako wa mupya ao walishakawia, ili waendelee kujikaza kuhubiri mupaka wakati Yehova atasema tuache sasa kuhubiri.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Mu hii habari maneno “usiache mukono wako upumuzike” inamaanisha kama tunapaswa kujikaza kuendelea kuhubiri habari njema mupaka wakati Yehova atasema tuache sasa.

^ fu. 5 “Siku ya Bwana” ilianza wakati Yesu aliwekwa kuwa Mufalme mu mwaka wa 1914 na itaendelea mupaka mwisho wa Utawala Wake wa Miaka Elfu Moja.