Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunapaswa Kusali Juu ya Mambo Gani?

Tunapaswa Kusali Juu ya Mambo Gani?

SALA ya Baba Yetu njo sala yenye Wakristo wamerudilia-rudilia sana kuliko sala ingine yoyote. Hata vile, wengi wanarudiliaka-rudiliaka maneno ya ile sala bila kuelewa maana yake. Watu wengi wanairudiliaka-rudiliaka kila siku. Lakini Yesu hakupendaka ile sala ikuwe inarudiliwa-rudiliwa vile. Juu ya nini tunasema vile?

Mbele tu Yesu afundishe ile sala, alisemaka hivi: “Wakati munasali, musiseme mambo yaleyale tena na tena.” (Matayo 6:7) Sasa, juu ya nini Yesu alifundishaka watu ile sala? Alipenda watu waiweke mu akili na wakuwe wanairudilia-rudilia? Hapana. Yesu alipenda njo kutufundisha mambo yenye tunapaswa kusema na ya kutia pa nafasi ya kwanza wakati tuko tunasali. Tuchunguze muzuri maneno ya ile sala. Inapatikana mu Matayo 6:9-​13.

“Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.”

Kwa kusema vile, Yesu alikumbusha wanafunzi wake kama sala zote zinapaswa kumuendea Baba yake, Yehova. Lakini unajua juu ya nini jina ya Mungu ni ya maana na juu ya nini inapaswa kutakaswa, ao kufanywa kuwa takatifu?

Tangu wanadamu waanze kuishi ku dunia, Mungu amesemewa mambo mingi ya uongo, yenye imechafua jina yake. Shetani, adui ya Mungu, alimuita Yehova kuwa Mutawala muongo, mwenye anatawala tu kwa faida yake, na alisema kama Yehova hana haki ya kutawala viumbe vyake. (Mwanzo 3:1-6) Watu wengi wameunga mukono mawazo ya Shetani, na wanafundisha kama Mungu hana upendo, hana huruma, na anapendaka kulipiza kisasi. Na hata wengine wanasema kama haiko Mungu njo aliumbaka vitu vyote. Tena, wamefikia hata kushambulia jina yake. Wameondoa jina Yehova mu tafsiri fulani za Biblia na wanakataza watu kuitaya.

Biblia inaonyesha kama Mungu atamaliza ile mambo yote ya ukosefu wa haki. (Ezekieli 39:7) Wakati atafanya vile, atakupatia mambo yote yenye uko nayo lazima na atamaliza magumu yako yote. Atafanya vile namna gani? Maneno yenye kufuata mu sala ya Yesu inajibia ile ulizo.

“Ufalme wako ukuje.”

Leo, viongozi wa dini wako na mawazo yenye kupingana juu ya Ufalme wa Mungu. Lakini, wale wenye walikuwa wanamusikiliza Yesu wakati alikuwa anafundisha namna ya kusali, walijua kama manabii walikuwa wamesema kama kutatokea Masiya, Mukombozi mwenye alikuwa amechaguliwa na Mungu. Ule Masiya angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu wenye ungebadilisha ulimwengu. (Isaya 9:6, 7; Danieli 2:44) Ule Ufalme utatakasa jina ya Mungu kwa kuonyesha wazi uongo wa Shetani na kumuharibu Shetani na kuondoa mambo yote ya mubaya yenye ameleta. (Zaburi 46:9; 72:12-​16; Isaya 25:8; 33:24) Ile njo mambo yenye unaombaka itimie wakati unakuwaka unasali Ufalme wa Mungu ukuye.

“Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.”

Ile maneno ya Yesu inaonyesha kama mapenzi ya Mungu itafanyika ku dunia sawa vile iko inafanyika mbinguni, kwenye Mungu anaishi. Hakuna kitu yenye imezuia mapenzi ya Mungu kufanyika mbinguni; kule Mwana wa Mungu alipigana vita na Shetani na malaika zake, na akawatupa ku dunia. (Ufunuo 12:9-​12) Hii ombi ya tatu, sawa vile tu maombi mbili ya kwanza, inatusaidia tujue jambo ya maana zaidi yenye tunapaswa kutanguliza mu sala, ni kusema, mapenzi ya Mungu, hapana, mapenzi yetu. Ni wakati tu mapenzi ya Mungu inafanyika njo viumbe vyake vyote vinaweza kuwa mu hali ya muzuri. Njo maana, hata Yesu, mwanadamu mukamilifu, aliambiaka Baba yake hivi: “Lakini, mapenzi yako ndiyo yatendeke, hapana yangu.”​—Luka 22:42.

“Utupatie leo mukate wetu kwa ajili ya siku hii.”

Kisha, Yesu alionyesha kama haiko mubaya kumuambia Mungu mahitaji yetu. Kufanya vile kunatukumbusha kama Yehova njo “anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” (Matendo 17:25) Biblia inaonyesha kama yeye ni Baba mwenye upendo mwenye anafurahiaka kupatia watoto wake mambo yenye wako nayo lazima. Sawa vile baba muzuri, Yehova hawezi kutupatia mambo yenye haitatusaidia.

“Utusamehe madeni yetu.”

Uko kabisa na deni ya Mungu? Uko na lazima ya kusamehewa ile deni? Watu wengi leo hawaelewe zambi ni nini na hawajue uzito wa zambi. Lakini Biblia inafundisha kama magumu yetu inatokana na zambi, juu zambi njo imeletea wanadamu kifo. Tulizaliwa mu zambi, njo maana tunafanyaka makosa kila mara. Na juu tukuwe na tumaini ya kuishi milele, inaomba Mungu atusamehe. (Waroma 3:23; 5:12; 6:23) Biblia inatutuliza sana wakati inasema: “Wewe, Ee Yehova, uko mwema na uko tayari kusamehe.”​—Zaburi 86:5.

“Utukomboe na ule muovu.”

Unajua ni juu ya nini uko na lazima kabisa ya kulindwa na Mungu? Wengi wanakatala kuamini kama “ule muovu,” Shetani, iko kabisa. Lakini Yesu alifundisha kama Shetani iko kabisa, na hata alimuita “mutawala wa ulimwengu huu.” (Yohana 12:31; 16:11) Shetani amedanganya watu wengi mu hii dunia yenye iko anatawala. Na anapenda sana akudanganye juu usikuwe rafiki ya Baba yako, Yehova. (1 Petro 5:8) Lakini, Yehova iko na nguvu sana kuliko Shetani na anapenda sana kulinda wale wenye wanamupenda.

Hii mambo kidogo yenye tumezungumuzia juu ya sala yenye Yesu alifundisha, haionyeshe mambo yote yenye tunaweza kutia mu sala. Andiko ya 1 Yohana 5:14 inatuambia hivi juu ya Mungu: “Hata kama tunaomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye anatusikia.” Njo maana, usiwaze kama mambo yenye iko inakuhangaisha haiko ya maana na kama haupaswe kuiambia Mungu.​—1 Petro 5:7.

Sasa, tunapaswa kusali wakati gani na wapi? Ile nayo ni mambo yenye inaomba kufikiria.