Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tunaweza Kupata Wapi Msaada wa Kupambana na Matatizo ya Leo?

Tunaweza Kupata Wapi Msaada wa Kupambana na Matatizo ya Leo?

Hotuba ya Pekee

Tunaweza Kupata Wapi Msaada wa Kupambana na Matatizo ya Leo?

Kuna mashauri mengi sana ulimwenguni leo. Vitabu na vipindi vya televisheni vinavyotoa mashauri kuhusu jinsi watu wanavyoweza kutatua matatizo yao wenyewe vinapendwa sana. Hata hivyo, bado watu wana matatizo. Huenda ukajiuliza, ‘Je, kuna mahali ambapo ninaweza kupata mwongozo wenye kuaminika?’ Jibu ni ndiyo!

Ingawa Biblia iliandikwa maelfu ya miaka iliyopita, ina kanuni zisizopitwa na wakati ambazo zinaweza kutusaidia kujibu maswali kama haya:

▪ Ninaweza kusuluhisha ugomvi jinsi gani na kufurahia uhusiano mzuri na watu wengine?

▪ Ninaweza kupata furaha jinsi gani?

▪ Ninaweza kukabiliana na matatizo ya kiuchumi jinsi gani?

▪ Ninaweza kupunguza mahangaiko jinsi gani?

Majibu ya maswali hayo yatazungumziwa kwenye hotuba ya watu wote yenye kichwa, “Kanuni za Biblia—Je, Zinaweza Kutusaidia Kukabiliana na Matatizo ya Leo?” Hotuba hiyo inayotegemea Biblia itatolewa duniani kote katika nchi zaidi ya 230. Katika sehemu nyingi, itatolewa kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova siku ya Jumapili (Siku ya Yenga), Mei 1, 2011 (1/5/2011).

Mashahidi katika eneo lenu watafurahi kukueleza mahali na wakati ambapo hotuba hiyo itatolewa. Unakaribishwa kwa uchangamfu uhudhurie.