Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Hii Habari Njema ya Ufalme Itahubiriwa”

“Hii Habari Njema ya Ufalme Itahubiriwa”

“Hii Habari Njema ya Ufalme Itahubiriwa”

“Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—MATAYO 24:14.

Maana Yake Nini?: Luka mwenye aliandika sehemu fulani ya Injili, alisema kama Yesu ‘alisafiri kutoka muji mupaka muji na kijiji mupaka kijiji, akihubiri na kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.’ (Luka 8:1) Yesu naye alisema hivi: “Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika miji ingine, kwa sababu nilitumwa ili kufanya vile.” (Luka 4:43) Alituma wanafunzi wake wahubiri habari njema mu miji na mu vijiji, na kisha akawapatia hii amri: “Mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”​—Matendo 1:8; Luka 10:1.

Wakristo wa Kwanza-kwanza Walifanya Vile Namna Gani?: Bila kukawia, wanafunzi wa Yesu walianza kufanya kazi yenye Yesu aliwapatia. Biblia inasema hivi: “Na kila siku katika hekalu na nyumba kwa nyumba wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Matendo 5:42) Wakristo wote walifanya kazi ya kuhubiri, haikukuwa tu kazi ya watu kidogo wenye kuheshimiwa. Mwanahistoria Neander alisema kama “Celsus, mwandikaji wa kwanza mwenye alikuwa napinga Wakristo, alichekelea wanafunzi wa Yesu kwa kusema kama wasuka-manyoa ya kondoo, washona-viatu, watengeneza-ngozi, watu wenye hawakusoma, na watu wa hali ya chini sana, wote walikuwa wahubiri wa habari njema wenye bidii.” Mu kitabu yake The Early Centuries of the Church, Jean Bernardi aliandika hivi: “[Wakristo] walikuwa naenda fasi yote na kuzungumuza na kila mutu. Mu barabara na mu miji, fasi za watu wengi, na mu manyumba. Wakaribishwe muzuri ao hapana, . . . walikuwa naenda mupaka sehemu za mwisho-mwisho za dunia.”

Nani Njo Wako Nafanya Vile Leo?: Padri Muanglikani mwenye kuitwa David Watson alisema hivi: “Sababu moja kati ya sababu zenye zinafanya watu wengi leo wasipende mambo ya Mungu, ni kwamba kanisa imeshindwa kukamata kwa uzito kazi ya kufundisha na kuhubiri.” Mu kitabu yake Why Are the Catholics Leaving? José Luis Pérez Guadalupe anaandika kuhusu kazi za Waevanjeliste, Waadvantiste na wengine. Anaandika hivi: “Hawaendake nyumba kwa nyumba.” Lakini anaandika hivi kuhusu Mashahidi wa Yehova: “Wanaendaka nyumba kwa nyumba bila kupita hata nyumba moja.”

Mu kitabu Cato Supreme Court Review, 2001-​2002 munapatikana hii maneno yenye kufurahisha yenye Jonatnan Turley alisema: “Kama unasema tu maneno Mashahidi wa Yehova, jambo yenye inakuyaka mu kichwa ya watu wengi ni wahubiri wenye wanatutembeleaka ku manyumba yetu saa yenye hatukuwaita. Mashahidi wa Yehova hawahubiriake tu mulango kwa mulango juu ya kuambia watu mambo yenye wanaamini, lakini kufanya vile ni sehemu ya maana ya imani yao.”

[Kisanduku kwenye ukurasa wa 9]

Umetambua Watu Wenye Wanatimiza ile Mambo Yote?

Kama unafikiria mambo yenye Biblia inasema yenye tumezungumuzia mu hizi habari, unawaza nani njo Wakristo wa kweli leo? Hata kama kuko dini za mingi sana zenye zinajiita kuwa za Kikristo, ukumbuke kama Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Haiko kila mutu mwenye kuniambia, ‘Bwana, Bwana,’ ndiye ataingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini ni ule tu mwenye kufanya mapenzi ya Baba yangu mwenye kuwa mbinguni ndiye ataingia.” (Matayo 7:21) Juu upate baraka za milele zenye Ufalme wa Mungu utaleta, unapaswa kutambua wale wenye wanafanya mapenzi ya Baba na kujiunga nao. Tunakutia moyo uombe Mashahidi wa Yehova, wenye walikuletea hii gazeti, wakufundishe mambo mingi zaidi juu ya Ufalme wa Mungu na baraka zenye utaleta.​—Luka 4:43.