Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Kama Muko na Upendo Kati Yenu”

“Kama Muko na Upendo Kati Yenu”

“Kama Muko na Upendo Kati Yenu”

“Ninawapatia ninyi amri mupya, kwamba mupendane; kama vile nimewapenda ninyi, ninyi pia mupendane vilevile. Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.”​—YOHANA 13:34, 35.

Maana Yake Nini?: Yesu aliambia wanafunzi wake wapendane sawa vile yeye aliwapenda. Aliwapenda namna gani? Ile wakati, watu walikuwa na ubaguzi sana, lakini Yesu alipenda watu wa namna zote. (Yohana 4:7-10) Na juu Yesu alipenda sana watu, alitumia nguvu yake na wakati yake juu ya kusaidia wengine. (Marko 6:30-34) Ku mwisho, Yesu alionyesha upendo kwa njia kubwa zaidi. Alisema hivi: “Mimi ndiye muchungaji mwema; muchungaji mwema anatoa uzima wake kwa ajili ya kondoo.”​—Yohana 10:11.

Wakristo wa Kwanza-kwanza Walifanya Vile Namna Gani?: Wa kristo wa kwanza-kwanza walikuwa naitana “ndugu” ao “dada.” (Filemoni 1, 2) Wakristo walikaribisha watu wa namna zote mu kutaniko ya Kikristo juu waliamini kama “hakuna tofauti kati ya Muyahudi na Mugiriki. Kuko Bwana uleule juu ya wote.” (Waroma 10:11, 12) Kisha Pentekoste ya mwaka ya 33 kisha kuzaliwa kwa Yesu, wanafunzi katika Yerusalemu “walikuwa wanauzisha vitu vyao na mali zao na kugawia wote feza zenye walipata, kulingana na kile chenye kila mutu alikuwa nacho lazima.” Juu ya nini walifanya vile? Juu wale wote wenye walikuwa wametoka kubatizwa wabakie mu Yerusalemu na waendelee “kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume.” (Matendo 2:41-45) Nini njo iliwachochea wafanye vile? Miaka chini ya 200 kisha kifo ya mitume, Tertullian alirudilia maneno yenye watu walikuwa wanasema juu ya Wakristo, aliandika hivi: “Wanapendana sana . . . Na kila mumoja iko hata tayari kufa kwa ajili ya mwingine.”

Nani Njo Wako Nafanya Vile Leo?: Kitabu The History of the Decline and Fall of the Roman Empire (1837) inaonyesha kama kwa miaka mingi, wale wenye kujiita kuwa Wakristo “wametendeana bila huruma, kuliko hata vile wametendewa na wale wenye [hawaamini].” Uchunguzi wenye ulifanywa juzijuzi katika Amerika, umeonyesha kama watu wengi wenye kupenda mambo ya dini, zaidi sana wale wenye kujiita Wakristo, wako na ubaguzi wa rangi ya ngozi. Mara mingi, waamini wa inchi moja hawajue waamini wa ileile dini wenye kuwa mu inchi ingine. Njo maana hawawezi ao hawako tayari kusaidia waamini wenzao wakati wako na lazima ya musaada.

Mu mwaka wa 2004, kisha muji wa Florida kupigwa mara ine na upepo mukali mu kipindi ya miezi mbili, musimamizi wa halmashauri fulani ya kutoa misaada katika Florida, alifanya uchunguzi juu ya kuhakikisha kama misaada yenye ilitolewa ilikuwa natumiwa muzuri. Alisema kama hakuna kikundi ingine yenye ilikuwa napangwa muzuri sawa vile Mashahidi wa Yehova. Alisema tena kama iko tayari kutolea Mashahidi wa Yehova musaada wowote wenye wako nao lazima. Mwanzo-mwanzo wa mwaka wa 1997, kikundi ya Mashahidi wa Yehova ilienda mu inchi ya Congo juu ya kusaidia Wakristo wenzao na watu wengine. Waliwapelekea dawa, chakula, na nguo. Mashahidi wa Ulaya walikuwa wametoa misaada yenye ilifikia samani ya dola milioni moja.