Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unamwonaje Yesu?

Unamwonaje Yesu?

Unamwonaje Yesu?

Je, wewe humwona Yesu kama mtoto aliyetoka tu kuzaliwa, mwanamume anayekaribia kufa, au Mfalme aliyekwezwa?

Biblia inafunua kwamba Yesu ni Mfalme mwenye nguvu. Lakini jambo hilo linamaanisha nini kwako?

Wengi wanaamini kwamba Yesu alikufa kwa ajili yao. Hata hivyo, kifo cha mtu mmoja aliyekufa miaka 2,000 hivi iliyopita kinawezaje kuwasaidia wengine kupata uhai leo?

Unaalikwa kwa moyo mkunjufu kusikiliza maswali hayo yakijibiwa kupitia Maandiko. Habari hiyo itazungumziwa wakati Mashahidi wa Yehova watakapokutana kuadhimisha kifo cha Yesu. Mwaka huu mwadhimisho huo utafanywa Alhamisi, Aprili 5, baada ya jua kutua.

Tafadhali waulize Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu kuhusu wakati na mahali hususa.

Mwisho wa juma utakaofuata baada ya Ukumbusho huo wa kifo cha Yesu, Mashahidi wa Yehova watakuwa na hotuba yenye kuchochea na inayotegemea Biblia yenye kichwa “Je, Mwisho Uko Karibu Zaidi Kuliko Unavyofikiri?” Hotuba hiyo itakuwa tukio muhimu sana katika kazi ya ulimwenguni pote ya kuwasaidia wote wanaopenda ukweli na wanaotaka kujifunza mengi kumhusu Yesu. Unaalikwa kuhudhuria.