Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Linda Moyo Wako!”

“Linda Moyo Wako!”

“Linda Moyo Wako!”

Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova

KICHWA CHA SIKU YA IJUMAA

“Yehova Huona Jinsi Moyo Ulivyo”​—1 SAMWELI 16:7.

KICHWA CHA SIKU YA JUMAMOSI

“Kinywa Kinasema Kutokana na Mambo Yaliyojaa Katika Moyo”​ —MATHAYO 12:34.

KICHWA CHA SIKU YA JUMAPILI

“Mtumikie Yehova kwa Moyo Kamili”​—1 MAMBO YA NYAKATI 28:9.

Biblia inataja moyo karibu mara elfu moja. Pindi nyingi kati ya hizo, Maandiko hayataji moyo halisi wa mwanadamu, badala yake moyo wa mfano. Moyo wa mfano ni nini? Neno moyo linaweza kumaanisha utu wa ndani kabisa, yaani, mambo ambayo mtu anafikiria, hisia zake, na mambo anayotamani.

Kwa nini tunapaswa kulinda moyo wetu wa mfano? Mungu alimwongoza Mfalme Sulemani kuandika maneno haya: “Linda moyo wako kuliko vitu vingine vyote vinavyopaswa kulindwa, kwa maana ndiko zinakotoka chemchemi za uzima.” (Methali 4:23) Hali ya moyo wetu wa mfano ndiyo inayoamua ikiwa tutakuwa na maisha bora sasa na tumaini letu la kupata uzima wa milele wakati ujao. Kwa nini? Kwa sababu Mungu anaona yale yaliyo ndani ya mioyo yetu. (1 Samweli 16:7) Kwa hiyo, maoni ya Mungu kutuelekea yanategemea jinsi tulivyo kwa ndani, yaani, sisi ni watu wa aina gani katika “mtu wa siri wa moyoni.”​—1 Petro 3:4.

Hata hivyo, tunawezaje kuulinda moyo wetu? Jibu la swali hilo litazungumziwa kwa undani zaidi katika Makusanyiko hayo ambayo Mashahidi wa Yehova watafanya ulimwenguni pote kuanzia mwezi huu. Unaalikwa kwa moyo mkunjufu kuhudhuria siku zote tatu za kusanyiko hilo. * Mambo utakayojifunza yatakusaidia kutenda kwa njia ambayo itafanya moyo wa Yehova Mungu ushangilie.​—Methali 27:11.

[Maelezo ya Chini]

^ Ili kufahamu kusanyiko lililo karibu nawe, tafadhali tembelea Tovuti ya www.pr418.com. Pia, unaweza kuwasiliana na Mashahidi wa Yehova walio katika eneo lenu au uwaandikie barua wachapishaji wa gazeti hili.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Photo on right: Aus dem Fundus der MÜNCHNER OLYMPIAPARK GMBH, München