Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Uzima wa Milele Ndio Huu”

“Uzima wa Milele Ndio Huu”

“Uzima wa Milele Ndio Huu”

“Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemutuma, Yesu Kristo.”​—YOHANA 17:3.

UJUZI unaweza kuokoa maisha. Huko Niger, Nouhou mutoto mwenye umri wa miezi kumi aligonjwa. Kwa sababu mama yake alikuwa na ujuzi fulani wa kiganga, alijua jambo la kufanya. Alitengeneza serum, ni kusema, alichanga sukari, chumvi, na maji safi na kumunywesha mutoto ili asiishiwe na maji mwilini. Kulingana na shirika la UNICEF, mutoto huyo alipona kwa sababu mama yake alitenda bila kukawia, na kwa sababu alikuwa na ujuzi fulani wa kiganga.”

Ujuzi wa Biblia unaweza pia kuokoa maisha. Musa, mwandikaji wa kwanza wa Biblia, alisema hivi: ‘Hilo si neno lisilo na samani kwenu, bali linamaanisha uhai wenu, na kwa neno hili munaweza kurefusha siku zenu.’ (Kumbukumbu la Torati 32:47) Je, kweli Biblia inaweza kutusaidia kurefusha siku zetu? Na tena, inamaanisha uhai ao uzima wetu katika njia gani?

Katika habari tano zilizotangulia za sehemu hii, tuliona kama Biblia ni kitabu ambacho hakiwezi kulinganishwa na vitabu vingine kwa sababu unabii ulio ndani haukose kutimia, ina habari zenye kupatana na historia na sayansi, vitabu vyote vilivyo ndani vinapatana, na kwa sababu kanuni zake ni zenye kufaa leo katika maisha. Mambo hayo yanaonyesha kama Biblia ni tofauti na vitabu vingine vyote. Basi, je, hauone kama ni jambo la lazima ujifunze Biblia kwa uangalifu kwa sababu inasema kama inaweza kutusaidia kurefusha siku zetu, maana yake, kutusaidia kupata uzima wa milele?

Tunakutia moyo ujifunze namna ujuzi sahihi wa Biblia unaweza kukusaidia upate amani ya akilini leo na pia furaha wakati ujao. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukuonyesha namna unaweza kupata ujuzi huo.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 9]

Tena, Biblia ni tofauti na vitabu vingine vyote kwa sababu ni Biblia tu inayotoa majibu yenye kufaa kwa maulizo ya lazima tunayojiuliza katika maisha. Kwa mufano inajibu maulizo haya:

• Sababu gani tupo hapa duniani?

• Sababu gani watu wanateseka sana?

• Je, kuna tumaini lolote kwa ajili ya watu tuliowapenda waliokufa?

Unaweza kupata majibu ya Biblia kwa maulizo hayo katika kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.