Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu

SABABU gani mwanaume aliyekomalia katika familia ya Wakatoliki wenye bidii sana na ambaye ana kazi yenye mushahara muzuri katika mambo ya sheria amekuwa Shahidi wa Yehova? Ni nini kilichomusukuma mutu aliyekuwa teroriste aache maisha yake ya jeuri na kuwa muhubiri wa habari njema? Soma mambo ambayo watu hao wanaeleza.

“Nilielewa vizuri kutofautisha mambo mema na mambo mabaya.”—SEBASTIÃO ALVES JUNQUEIRA

ALIZALIWA MWAKA WA 1946

ALIZALIWA KATIKA INCHI YA BRÉSIL

ALIKUWA MUKATOLIKI MWENYE BIDII SANA

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Wazazi wangu waliishi katika kijiji kilicho umbali wa kilometre 6 na muji wa Piquete; walikuwa na shamba ndogo, na shamba hilo ndilo lililotusaidia kuishi. Masomo yangu yalikuwa katika muji wa Piquete, kwa hiyo nilinunua kinga iliyokuwa imekwisha kutumiwa ili inisaidie kuenda kwenye masomo. Watu walikuwa masikini katika sehemu ambamo tuliishi, lakini muji ulikuwa safi na mauwaji hayakuwa mengi. Katika muji huo, wanaume wengi walikuwa wakitumika katika izine ya kutengeneza silaha.

Nilipenda sana kusoma na nilijikaza sana ili niingie kwenye masomo ya askari wanaotumia avion, masomo hayo hayakuwa mbali. Nilifanywa kuwa Sergent katika mwaka wa 1966. Kisha nikasoma masomo ya sheria na nikapata diplome. Baadaye, nikakuwa mukubwa wa polisi. Katika mwaka wa 1976, nilifanya mashindano yaliyotayarishwa na serikali ao guvernema, nikaweza na nikapewa kazi. Wakati fulani nilitumika kama musimamizi wa gereza. Wakati huo, Mashahidi wa Yehova walizoea kuja na kuniomba ruhusa ya kuhubiria wafungwa. Kila mara walinihubiria pia ujumbe wa Biblia. Nilikuwa nikimuheshimu sana Mungu. Nilishangaa sana kusikia kama jina la Mungu ni Yehova na kama tunaweza kufanya urafiki naye.

Polepole, niliendelea katika kazi yangu na nikapanda cheo katika mambo ya sheria. Katika mwaka wa 1981, nilifanya mashindano mengine yaliyotayarishwa na guvernema mbele ya kunipatia kazi ya muamuzi. Kisha, katika mwaka wa 2005, nilipewa cheo cha muamuzi mukubwa huko São Paulo.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Wakati mufupi tu kisha kupata diplome yangu ya masomo ya sheria, nilianza kusoma Biblia​—jambo hilo lilibadilisha kabisa mawazo yangu. Nilikuwa Mukatoliki mwenye bidii sana. Watu fulani wa jamaa yetu walikuwa mapadiri na mwengine alikuwa askofu, na wakati wa misa nilikuwa musaidizi wa padiri. Nilikuwa nikisoma sehemu fulani katika kitabu cha sala mbele padiri aanze kufundisha. Haikuwa jambo la kawaida kwa Wakatoliki kusoma Biblia. Mama yangu alikasirika sana aliposikia kama nimeanza kusoma Biblia. Alijaribu kunivunja moyo, akisema kama nitapatwa na wazimu. Hata hivyo, niliendelea kuisoma na sikupatwa na wazimu.

Ninafikiri kama ni tamaa yangu ya kutafuta kujua mambo ndiyo ilinichochea niendelee kusoma Biblia. Nilipenda kujua mambo mengi zaidi juu ya mapadiri na kazi yao katika kanisa. Nilianza pia kusoma vitabu vinavyozungumuzia mawazo ya chama fulani cha kanisa la Katoliki la Roma kinachotetea uhuru, lakini mawazo ya watetezi hao ni yenye makosa, na hayakunisaidia kuelewa jambo lolote.

Wakati huohuo, muganga wangu wa meno, ambaye alikuwa Buddhiste, alinipatia kitabu fulani ambacho yeye pia alipewa. Kitabu hicho ni L’homme est-il le produit de l’évolution ou de la création? * Nilikubali kitabu hicho kwa sababu niliwaza kama itakuwa vizuri kukisoma pamoja na kitabu cha Charles Darwin kinachoitwa L’origine des espèces ambacho kinazungumuzia chanzo cha uzima. Mawazo ya kitabu L’homme est-il le produit de l’évoulution ou de la création? yalikuwa yenye nguvu, yenye kutegemeka, na yenye kusadikisha. Niliona kabisa kama mafundisho ya mageuzi ni ya uongo na hayana musingi.

Tamaa yangu ya kujua mambo mengi zaidi iliongezeka sana niliposoma habari ya uumbaji. Nilitaka nipate vitabu vingine vilivyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kisha niliambiwa kama Shahidi wa Yehova mumoja ni mécanicien kwenye masomo ya kutengenezea avion. Nilizungumuza naye, na akanipatia vitabu fulani. Wakati huo, sikukubali kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Niliwaza kama ninaweza kujifunza Biblia mimi mwenyewe.

Nilipoanza kusoma Biblia, niliona kama ilikuwa vizuri kuisoma pamoja na familia yangu. Kila juma tulikuwa na funzo la familia na tulisoma Biblia pamoja. Kwa sababu tulikuwa Wakatoliki, tulizoeana sana na mapadiri na maaskofu. Lakini mambo niliyosoma katika andiko la Yohana 14:6 yalinigusa moyo sana. Andiko hilo linasema hivi: ‘Yesu akamuambia [mufuasi wake Tomasi]: Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu.’ Kisha kuchunguza habari hiyo kwa uangalifu, nilisadiki kama Yehova anatuokoa kupitia Yesu. Tulifundishwa uongo kama tutaokolewa kupitia mapadiri.

Maandiko mengine mawili yalibadilisha mawazo yangu juu ya Kanisa la Katoliki na mafundisho yake. Andiko la kwanza ni Methali 1:7, ambalo linasema hivi: ‘Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa ujuzi. Wapumbavu wamezarau hekima na nizamu.’ Na andiko la pili ni Yakobo 1:5, linalosema hivi: ‘Ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu; naye atapewa hiyo.’ Nilikuwa na kiu cha ujuzi na hekima, kiu ambacho kanisa langu halikumaliza. Kwa hiyo, nikaacha kuenda kwenye kanisa.

Bibi yangu alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa 1980. Kila mara nilipokuwa nyumbani, nilihuzuria kwenye funzo hilo. Kisha wakati fulani, nilikubali kujifunza Biblia. Lakini, mimi na bibi yangu tulifanya wakati murefu mbele ya kuamua kubatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Bibi yangu alibatizwa katika mwaka wa 1994, na mimi nikabatizwa katika mwaka wa 1998.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA: Watoto wetu wane wamefaidika sana kwa kufundishwa kanuni za Yehova tangu utoto. (Waefeso 6:4) Watoto wetu wawili wanaume wanatumika kwa bidii katika makutaniko yao. Na watoto wetu wawili wanawake ni wenye bidii katika kazi ya kuhubiria wengine. Kila mwezi bibi yangu anapitisha wakati mwingi ili kusaidia watu wengine kujifunza Biblia, na mimi niko muzee katika kutaniko letu.

Kisha kuwa Shahidi wa Yehova, nilielewa vizuri kutofautisha mambo mema na mambo mabaya. Kwa sababu mimi ni muamuzi, ninajikaza kuiga namna Yehova anavyotenda katika njia mbalimbali ninapoamua mambo kwenye tribinali. Ninachunguza hali zote, ninajikaza kuwa mwenye kiasi, na kuwa mwenye huruma kunapokuwa sababu zinazoweza kufanya mutu apate hukumu kali.

Nimeshugulikia hali nyingi zenye kuhusu jeuri, uvunjaji wa sheria, kuwatendea watoto vibaya kingono na makosa mengine mazito. Lakini, matendo hayo mabaya yananiumiza kabisa. Ninapotazama televizyo ao kusikiliza radio, ninachukizwa sana na mwenendo mupotovu unaoenea duniani. Mimi ni mwenye shukurani sana kwa Yehova kwa sababu amenisaidia nielewe sababu gani leo kuna ongezeko la uvunjaji wa sheria, na niko mwenye shukurani kwa sababu ya tumaini nzuri tunalo kwa ajili ya wakati ujao.

“Gereza halikunibadilisha.”​—KEITH WOODS

ALIZALIWA MWAKA WA 1961

ALIZALIWA KASKAZINI MWA IRLANDE

ALIKUWA TERORISTE

MAISHA YANGU YA ZAMANI: Nilizaliwa mwaka wa 1961 katika muji wa Portadown, kaskazini mwa Irlande; muji huo ulikuwa na watu wengi sana. Nilizaliwa katika familia ya Waprotestanti, na nilikomalia katika eneo ambamo Wakatoliki na Waprotestanti wanaishi pamoja. Familia nyingi zilikuwa masikini. Ilikuwa vigumu kupata feza, kwa hiyo familia nyingi zilichangana katika nyumba moja.

Nilikuwa na maisha mabaya. Katika mwaka wa 1974, nilijiingiza katika “misukosuko” iliyokuwa Kaskazini mwa Irlande. Wakati huo, hali iliharibika katika eneo letu. Kwa mufano, usiku fulani, baba yangu ambaye alikuwa musimamizi wa izine ya kutengeneza matapi, alikuwa kwenye kazi akiwazoeza vijana wawili Wakatoliki waliokuwa majirani wetu. Wakati huo, mutu mumoja alitupa bombe kupitia dirisha la salon ya nyumba ambamo vijana hao waliishi, bombe hiyo iliua baba yao, mama yao, na mudogo yao.

Hali ikaendelea kuharibika na vita ikaanza. Nyumba za Waprotestanti zilizokuwa katika eneo la Wakatoliki ziliunguzwa, na nyumba za Wakatoliki zilizokuwa katika eneo la Waprotestanti ziliunguzwa. Eneo letu likakuwa la Waprotestanti tu. Muda kidogo kisha hapo, mimi pia nilikamatwa na kufungwa kwa miaka mitatu kwa sababu nilijiingiza katika kazi ya kutupa mabombe.

Nilipokuwa katika gereza, nilifanya urafiki wa sana na mufungwa fulani aliyekuwa Muprotestanti na mwenye kujulikana sana kwa sababu alikuwa katika chama cha politike kinachotafuta kuunganisha Irlande ya Kaskazini na Royaume Uni. Mimi naye tulikuwa kama ndugu, na wakati alipooa alinifanya niwe musimamizi wa ndoa yake. Gereza halikunibadilisha mimi wala yeye. Wakati tuliachiliwa, tulirudilia tena maisha yetu ya politike, na kufanya matendo ya jeuri kwa njia kubwa. Kwa sababu ya matendo hayo, rafiki huyo alikamatwa tena na kufungwa. Alipokuwa katika gereza, aliuawa.

Mimi pia nilianza kutafutwa, na siku moja motokari yangu iliunguzwa kwa bombe. Lakini matukio hayo yalinifanya niwe mwenye bidii zaidi katika chama changu cha politike.

Muda huo, nilikuwa nikisaidia kupitisha kipindi fulani kwenye televizyo fulani ya Royaume Uni; kipindi kilichozungumuzia “Misukosuko” iliyokuwa katika inchi. Kupitisha kipindi hicho kuliniongezea magumu. Kwa mufano, usiku fulani niliporudi nyumbani nilikuta bibi yangu amekwisha kunikimbia. Kisha wakati fulani, watu waliochukizwa na kipindi hicho walimuiba mutoto wangu. Ninakumbuka wakati huo nilijiangalia katika kioo na kusema hivi: “Mungu ikiwa uko, tafazali unisaidie.”

Siku ya posho iliyofuata, nilikutana na mutu fulani niliyejuana naye anayeitwa Paul, ambaye alikuwa amekuwa Shahidi wa Yehova. Alianza kuzungumuza nami juu ya Biblia. Kisha siku mbili, Paul akanitumia Munara wa Mulinzi. Habari fulani katika gazeti hilo ilitaja maneno ya Yesu yanayopatikana katika andiko la Yohana 18:36. Alisema hivi: ‘Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini, kama ilivyo, ufalme wangu hautoke katika chanzo hiki.’ Maneno hayo yalinigusa moyo sana. Na tangu siku hiyo maisha yangu yakaanza kubadilika.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU: Paul alianza kujifunza Biblia pamoja nami. Kisha, niliendelea kujifunza na Shahidi wa Yehova mwengine aliyeitwa Bill. Ninajua kama nilikuwa mwanafunzi mugumu; nilikuwa na maulizo mengi sana! Nilianza pia kualika wakubwa wengi wa dini nyumbani ili wamuonyeshe Bill kama mambo anayofundisha ni ya uongo. Lakini ukweli wa Neno la Mungu ulikuwa wazi kabisa.

Siku moja nilimuambia Bill asikuje na motokari yake kwangu ili kujifunza nami kwa sababu kulikuwa vizuizi vingi barabarani na watu waliotia vizuizi hivyo wangeweza kumunyanganya motokari yake na kuiunguza. Hata hivyo, Bill alikuja ili kujifunza nami kama kawaida. Aliacha motokari nyumbani kwake na akatumia kinga. Hakuna mutu ambaye angetamani kumunyanganya kinga yake. Siku nyingine, tulipokuwa nyumbani mwangu tukijifunza na Bill, polisi na maaskari walifika ili kunifunga. Walipokuwa wakinipeleka, Bill alinilalamikia na kuniambia nimutumainie Yehova. Mambo hayo yalinigusa moyo sana.

Ninawaza kama siku ya kwanza nilipofika kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova niliuzi wamoja kati yao. Nilikuwa na nywele ndefu na vitu kwenye masikio, na nilivaa nguo iliyonitambulisha kuwa mutu wa chama fulani cha politike. Lakini, nilishangaa sana kuona namna walivyonitendea. Kwa kweli, wema wao ulinigusa moyo sana.

Ijapokuwa niliendelea kujifunza Biblia, sikuachana na marafiki wangu wa zamani. Mwishowe, mafundisho ya Biblia ambayo nilijifunza yakaanza kugusa moyo wangu sana. Nilielewa kama ikiwa ninapenda kumutumikia Yehova, ni lazima niachane na marafiki wangu wa zamani na niache kujiingiza katika mambo ya politike. Kwa kweli haikuwa vyepesi kufanya hivyo. Lakini, nilipoendelea kujifunza mengi juu ya Biblia, Yehova alinipatia nguvu, na hivi niliweza kufanya mabadiliko. Nilikata nywele zangu, niliondoa vitu vilivyokuwa kwenye masikio, na nikanunua veste. Mambo ambayo nilikuwa nikijifunza yalianza kunichochea nibadilishe pia namna yangu ya kuwatendea wengine.

FAIDA AMBAYO NIMEPATA: Nilikuwa teroriste na mutu mwenye kuvunja sheria ya serikali. Nilijulikana sana na polisi katika eneo letu. Lakini sasa mambo yamebadilika. Kwa mufano, nilipohuzuria kwa mara ya kwanza mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova uliofanyika katika muji wa Navan, Kaskazini mwa Irlande, wakubwa wa polisi walinisindikiza mupaka huko kwa sababu waliwaza kama nitaleta fujo kwenye mukusanyiko huo. Sasa, ninaenda kwenye mikusanyiko bila kusindikizwa na wakubwa wa polisi. Tena, ninahubiri kwa uhuru pamoja na Paul na Bill na Mashahidi wengine.

Maisha yangu yalipobadilika, nilianza kutumika kwa bidii katika kutaniko. Katika kutaniko hilo nilikutana na dada mumoja anayeitwa Louise; kisha wakati fulani tulioana naye. Baraka nyingine, nilimupata mutoto wangu ambaye maadui wangu waliiba.

Ninapokumbuka maisha yangu ya zamani, ninasikitika sana kwa sababu nilitesa watu wengine. Lakini ninaweza kusema kwa uhakika kama Biblia inaweza kubadilisha maisha ya watu kama mimi na kuwasaidia waache matendo mabaya na kuwa na kusudi na tumaini katika maisha yao.

[Maelezo ya chini]

^ Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova lakini hakichapishwe tena.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 12]

Mama yangu alikasirika sana aliposikia kama nimeanza kusoma Biblia