Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Miujiza Itakayofanyika Hivi Karibuni

Miujiza Itakayofanyika Hivi Karibuni

Miujiza Itakayofanyika Hivi Karibuni

IKIWA unajulishwa kama siku fulani ndiyo siku yako ya kupasuliwa na kwamba upasuaji huo utakuwa upasuaji mukubwa, sasa utajisikia namna gani ikiwa unajulishwa kama muganga huyo atakayekupasua hajafanya hata siku moja upasuaji wa namna hiyo? Kwa kweli, utakuwa na wasiwasi, sivyo? Lakini, unaweza kujisikia namna gani ikiwa unaambiwa kama muganga huyo hiyo ndio kazi yake na kama amekwisha kupasua watu wengi sana waliokuwa na ugonjwa kama wako na walipona? Utatumainia sana kama atakusaidia wewe pia, sivyo?

Dunia ambamo tunaishi leo ni yenye kugonjwa na inahitaji “upasuaji” mukubwa. Kupitia Neno lake, Biblia, Yehova Mungu ameahidi kama atairudisha Paradiso duniani. (2 Petro 3:13) Lakini ili ahadi hiyo itimie, watu wabaya wanapaswa kuondolewa kwanza, ni kusema, wataharibiwa kabisa. (Zaburi 37:9-11; Methali 2:21, 22) Hali zote zenye kuhuzunisha ambazo tunaona duniani leo zitakwisha na kisha paradiso itarudishwa. Itakuwa ni muujiza kabisa kuona jambo hilo linatimia!​—Ufunuo 21:4, 5.

Mashahidi wa Yehova wanaamini kama mabadiliko hayo makubwa yatafanyika hivi karibuni. Sababu gani wanaamini hivyo? Kwa sababu miujiza ambayo Yehova Mungu amekwisha kufanya inaonyesha kama yeye ana uwezo wa kutimiza ahadi zake. Ulinganishe miujiza sita tu kati ya miujiza inayozungumuziwa katika Biblia na ahadi ambazo Biblia inatoa juu ya wakati ujao.

Tunakutia moyo uendelee kujifunza juu ya ahadi za Biblia kuhusu wakati ujao. Imani yako ikiendelea kukomaa, tumaini lako pia litaendelea kukomaa, ni kusema, tumaini la kuishi wakati ambapo wewe pia utafaidika na miujiza ambayo Yehova atafanya.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 9, 10]

MUUJIZA:

YESU ALILISHA MAELFU YA WATU KWA MIKATE MICHACHE NA SAMAKI CHACHE.—MATHAYO 14:13-21; MARKO 8:1-9; YOHANA 6:1-14.

AHADI:

“Hakika dunia itatoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu atatubariki.”​—ZABURI 67:6.

YALE AMBAYO TUNAJIFUNZA:

HAKUNA MUTU ATAKAYESUMBULIWA TENA NA NJAA.

MUUJIZA:

YESU ALIFUNGUA MACHO YA VIPOFU.​—MATHAYO 9:27-31; MARKO 8:22-26.

AHADI:

“Macho ya vipofu yatafunguliwa.”​—ISAYA 35:5.

YALE AMBAYO TUNAJIFUNZA:

VIPOFU WOTE WATAONA.

MUUJIZA:

YESU ALIPONYESHA VILEMA.​—MATHAYO 11:5, 6; YOHANA 5:3-9.

AHADI:

“Kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya.”​—ISAYA 35:6.

YALE AMBAYO TUNAJIFUNZA:

VILEMA WOTE WATAPONYESHWA.

MUUJIZA:

YESU ALIPONYESHA MAGONJWA MBALIMBALI.​—MARKO 1:32-34; LUKA 4:40.

AHADI:

‘Hakuna mukaaji atakayesema: Mimi ni mugonjwa.’​—ISAYA 33:24.

YALE AMBAYO TUNAJIFUNZA:

MAGONJWA YOTE YATAKWISHA. TUTAKUWA NA AFYA KAMILIFU.

MUUJIZA:

YESU ALITULIZA UPEPO NA BAHARI.​—MATHAYO 8:23-27; LUKA 8:22-25.

AHADI:

“Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatafanya kazi ya bure.”​—ISAYA 65:21, 23.

“Utakuwa mbali sana na ukandamizaji​—kwa maana hutaogopa yeyote—na jambo lolote lenye kutia hofu, kwa maana halitakuja karibu nawe.”​—ISAYA 54:14.

YALE AMBAYO TUNAJIFUNZA:

MAMBO KAMA VILE MVUA NA UPEPO WA KUANGAMIZA HAYATAKUWA TENA.

MUUJIZA:

YESU ALIFUFUA WAFU.​—MATHAYO 9:18-26; LUKA 7:11-17.

AHADI:

“Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho . . . watatoka.”​—YOHANA 5:28, 29.

“Na bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi vikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake.”​—UFUNUO 20:13.

YALE AMBAYO TUNAJIFUNZA:

WATU TULIOPENDA AMBAO WAMEKUFA WATAFUFULIWA.