Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Wakati Gani Yesu Alifanywa Kuwa Mufalme?

Ni Wakati Gani Yesu Alifanywa Kuwa Mufalme?

Neno la Mungu Linafundisha Nini?

Ni Wakati Gani Yesu Alifanywa Kuwa Mufalme?

Habari hii inazungumuzia maulizo fulani ambayo labda umekwisha kujiuliza na inaonyesha mahali ambapo unaweza kupata majibu katika Biblia. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia upate majibu ya maulizo hayo.

1. Yesu aliahidiwa kupewa Ufalme gani?

Mungu aliahidi kama muzao wa Mufalme Daudi angekaa juu ya kiti Chake cha Ufalme kwa wakati usio na kipimo. Muzao huyo aliyeahidiwa ni Yesu, na sasa yeye ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu na anatawala huko mbinguni.​—Soma Zaburi 89:4; Luka 1:32, 33.

Daudi alipokuwa angali kijana, Mungu alimuchagua ili awe mufalme juu ya watu wake, Israeli. Daudi alipokufa, Sulemani, aliyechaguliwa na Yehova, alikaa juu ya “kiti cha ufalme cha Yehova.” (1 Mambo ya Nyakati 28:4, 5; 29:23) Kisha kifo cha Sulemani, wafalme wengi walitawala huko Yerusalemu, lakini wengi kati yao hawakuwa waaminifu. Mwishowe, Yehova aliruhusu majeshi ya Babiloni yaharibu Yerusalemu na kumuondoa mufalme aliyekuwa akitawala. Jambo hilo lilitendeka katika mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Tangu wakati huo, hakuna mufalme wa uzao wa Daudi ambaye ametawala katika muji wa Yerusalemu.—Soma Ezekieli 21:27.

2. Ufalme wa Mungu uliowakilishwa na utawala wa Daudi huko Yerusalemu ulibaki bila mufalme kwa miaka ngapi?

Muda kidogo kisha kuharibiwa kwa muji wa Yerusalemu, Yehova alimuambia nabii wake Danieli kama atachagua mufalme ambaye atatawala akiwa mbinguni. Mufalme huyo alianza kutawala wakati gani?​—Soma Danieli 7:13, 14.

Danieli alifasiria ndoto fulani; katika ndoto hiyo Mungu aliamuru muti mukubwa ukatwe, kama vile tu alivyoamuru ufalme ukatizwe na kuharibiwa huko Yerusalemu. Lakini aliamuru kisiki cha muti huo kiachwe katika udongo ili kiote tena kisha “nyakati saba.” Biblia inaonyesha kama “nyakati” tatu na nusu ni siku 1 260. Kwa hiyo, “nyakati saba” ni siku 2 520. (Ufunuo 12:6, 14) Katika unabii wa Biblia, mara nyingi siku zinamaanisha miaka. (Hesabu 14:34) Kwa hiyo, Ufalme wa Mungu ungebaki bila mufalme kwa miaka 2 520.​—Soma Danieli 4:10-17.

3. Ni wakati gani Yesu alifanywa kuwa Mufalme?

Mungu alimufanya Yesu kuwa Mufalme huko mbinguni katika mwaka wa 1914, ni kusema, miaka 2 520 kisha kuharibiwa kwa Yerusalemu. Yesu alipofanywa kuwa Mufalme alifukuza Shetani na mashetani wake huko mbinguni, hilo ndilo tendo la kwanza ambalo Yesu alitimiza. (Ufunuo 12:7-10) Tukio hilo halikuonekana kwa macho ya wanadamu, lakini lililetea wanadamu matatizo yenye kuonekana. (Ufunuo 12:12) Mambo yenye kutendeka duniani tangu mwaka wa 1914 yanahakikisha kama Yesu alianza kutawala katika mwaka huo.​—Soma Mathayo 24:14; Luka 21:10, 11, 31.

4. Utawala wa Yesu utakufanyia nini?

Kutimizwa kwa unabii mbalimbali juu ya utawala wa Yesu kunahakikisha kama unaweza kutumainia yale Neno la Mungu linasema. Hivi karibuni, Yesu atatumia nguvu zake za kifalme ili kuondolea wanadamu mateso yote.​—Soma Zaburi 72:8, 12, 13; Danieli 2:44.

Ili kupata habari zingine, usome ukurasa wa 215-218 wa kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Muchoro kwenye ukurasa wa 16, 17]

(Ili kuona maelezo hayo, ona kitabu)

Mwezi wa 10 Mwezi wa 10

607 K.W.W. 1914 W.W.

← Miaka 2 520 →

1000 K.W.W. 1 K.W.W. 1 W.W. 1000 W.W. 2000 W.W.

← Miaka 606 na miezi 3 →← Miaka 1 913 na miezi 9 →

Ufalme Ufanye hesabu: Mungu anamufanya

uliharibiwa Miaka 606 na miezi 3 Yesu kuwa

huko + miaka 1 913 na miezi 9 Mufalme aliye

Yerusalemu = miaka 2 520 na nguvu

za kutawala

mataifa