Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ninapovuta tumbaku, je, Mungu anachukia?

Ninapovuta tumbaku, je, Mungu anachukia?

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Ninapovuta tumbaku, je, Mungu anachukia?

▪ Mutu mwenye nia nzuri anaweza kuuliza ulizo hilo, kwa sababu katika Biblia hakuna sheria inayozungumuzia tumbaku. Je, hilo linamaanisha kama ni vigumu kujua mawazo ya Mungu juu ya tumbaku? Hapana.

Biblia inasema kama “andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Katika Maandiko, muna kanuni na maneno yaliyo wazi yanayoonyesha kama Mungu anapenda tutunze afya yetu. Kwanza, tuone yale wachunguzi wamevumbua kuhusu matokeo mabaya ya tumbaku juu ya afya ya mutu. Kisha tutaona namna kanuni za Biblia zinavyopatana na mambo hayo.

Tumbaku inaharibu afya ya mutu anayeivuta na inatokeza kifo ambacho kingeepukwa. Kati ya watu 5 wanaokufa katika inchi ya Étas-Unis, mutu mumoja anakufa kwa sababu ya tumbaku. Shirika la États-Unis Linaloonyesha Hatari ya Kutumia Dawa za Kulewesha linaonyesha kama tumbaku inaua watu wengi zaidi kuliko “pombe, dawa za kulewesha, kuua watu, kujiua, aksida za motokari, na SIDA, vyote pamoja.”

Wale wanaovuta tumbaku wanaharibu afya ya wengine. Kupumua moshi wa sigareti kunaleta hatari. Watu wasiovuta wanaopumua moshi wa tumbaku wana hatari zaidi ya 30 % ya kupatwa na kansere ya mapafu na ugonjwa wa moyo. Katika miaka ya hivi karibuni, waganga wamevumbua hatari zingine. Wanasema kama sumu ya tumbaku inayobaki kwenye mavazi, kwenye tapi, na nafasi zingine inaweza kubaki muda murefu kisha moshi wa tumbaku kuisha. Sumu hiyo inaharibu zaidi sana afya ya watoto na inaweza kuchelewesha uwezo wao wa kujifunza.

Tumbaku inamufanya mutu awe mutumwa. Tumbaku inamufanya mutu anayeivuta awe mutumwa wa tabia hiyo inayoharibu afya. Juu ya hilo, wachunguzi wanaamini kama ni vigumu kuachana na tabia ya kuvuta tumbaku kwa sababu ya nikotini, sumu inayopatikana katika tumbaku.

Namna gani kanuni za Biblia zinaonyesha ukweli wa mambo hayo ambayo wachunguzi wamevumbua? Ona mambo yanayofuata:

Mungu anataka tuheshimu uzima. Katika Sheria ambayo Mungu aliwapatia Waisraeli, alionyesha kama wale wanaotaka kumupendeza wanapaswa kuheshimu uzima. (Kumbukumbu la Torati 5:17) Waisraeli walipaswa kujenga ukuta mufupi kando-kando ya dari ya juu ya nyumba. Sababu gani? Dari zilikuwa nafasi za wazi ambapo watu walikuwa wakikaa ili kuvuta hewa. Ukuta ulizuia watu wa familia na watu wengine kuanguka na kuumia ao kufa. (Kumbukumbu la Torati 22:8) Tena, Waisraeli walipaswa kulinda wanyama wao ili wasiumize watu wengine. (Kutoka 21:28, 29) Mutu anayevuta tumbaku anavunja kanuni zinazotegemezwa na sheria hizo kwa sababu anaharibu afya yake kimakusudi. Zaidi ya hilo, moshi anaotoa unahatarisha afya ya watu wengine wanaomuzunguka.

Mungu anataka tumupende na tupende jirani yetu. Yesu Kristo alisema kama wafuasi wake wanapaswa kutii amri hizi mbili kubwa. Wanapaswa kumupenda Mungu kwa moyo wao wote, kwa nafsi yao yote, kwa akili yao yote, na kwa nguvu zao zote na kumupenda jirani yao kama wanavyojipenda wenyewe. (Marko 12:28-31) Kwa sababu uzima ni zawadi ambayo Mungu alitupatia, mutu anayevuta tumbaku haheshimu kabisa zawadi hiyo na kwa hiyo, hamupende Mungu. (Matendo 17:26-28) Tabia mbaya ya mutu huyo inaweza kuhatarisha sana afya ya watu wengine. Kwa hiyo, hawezi kusema kama anamupenda jirani yake.

Mungu anataka tuepuke tabia zenye kutuchafua. Biblia inawaamuru Wakristo wajisafishe na “kila [uchafu] wa mwili na roho.” (2 Wakorintho 7:1) Hakika, tumbaku inamuchafua mutu. Wale wanaotaka kuachana na tabia ya kuvuta tumbaku ili kumupendeza Mungu wana tatizo ngumu. Lakini kwa musaada wa Mungu, wanaweza kuachana na tabia hiyo yenye kuchafua mutu.